Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 118 2024-02-07

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: -

Je, utaratibu gani unaotumika kwa Kamandi mbalimbali nchini kuanzisha miradi ya kibiashara katika maeneo ya Kamandi?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Jumah Soud, Mbunge wa Donge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, uendeshaji wa miradi ya kibiashara Jeshini ulianzishwa kupitia Mess and Institutes ambayo ilikua na jukumu la kusimamia mabwalo (Mess) ambayo yalikuwa yanauza vinywaji na kuendesha maduka katika vikosi vya Jeshi. Baadaye utaratibu huo ulifanyiwa maboresho kadhaa yaliyopelekea kubuni na kuendesha miradi ya kibiashara Jeshini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utaratibu wa sasa Kamandi, Brigedi, Vikosi na Shule zinapaswa kubuni na kuandaa andiko la mradi au biashara na kuwasilisha Makao Makuu ya Jeshi kwa ajili ya kibali. Makao Makuu ya Jeshi huchambua maandiko yaliyowasilishwa kujiridhisha endapo mradi au biashara hizo, hazitaathiri majukumu ya msingi ya Jeshi. Aidha, miradi hiyo huzingatia taratibu za uhifadhi wa mazingira, taratibu za usajili BRELA na taratibu za Mamlaka ya Mapato Nchini.