Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 113 2024-02-07

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaweka utaratibu wa mbolea kuwekwa kwenye vifungashio vya kilo tano, kumi, 15, 25 na 50?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua kuwa mahitaji ya mbolea kwa wakulima yanatofautiana hususan kwa wakulima wa mazao ya bustani na mazao mengine ya nafaka. Uhitaji wa mbolea ya mazao ya bustani ni wa kiasi kidogo ikilinganishwa na mazao mengine ikiwemo nafaka na mizizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kukidhi mahitaji ya aina hiyo na matakwa ya Sheria na Kanuni ya 32(4) ya Kanuni za Mbolea za Mwaka 2011, Wizara ya Kilimo kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea (TFRA) imeelekeza waingizaji, wazalishaji na wasambazaji wa mbolea nchini kuanza kufungasha mbolea katika ujazo unao tofautiana kuanzia kilo 5, 10, 25 na 50 ili kuwawezesha wakulima kupata mbolea kulingana na mahitaji yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika msimu wa 2023/2024,,Kampuni tatu zimeshaanza kufungasha mbolea, kampuni hizo ni (ETG Inputs Limited, Yara Tanzania Limited na Minjingu Mines and Fertilizers Limited) hata hivyo Serikali inaendelea kuhimiza Kampuni za Mbolea nchini kufungasha katika ujazo tofauti ili kukidhi mahitaji ya wakulima, kuongeza matumizi ya mbolea na kupunguza vitendo vya baadhi ya mawakala kufungua mifuko.