Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 47 Energy and Minerals Wizara ya Madini 418 2022-06-20

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: -

Je, uchimbaji wa madini kando ya mito na maziwa ni chanzo cha upungufu wa samaki?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Anyigulile Jumbe Mlaghila, Mbunge wa Jimbo la Kyela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunafahamu kuwa uchimbaji wa madini umegawanyika katika aina kuu mbili, uchimbaji juu ya ardhi na ule wa chini ya ardhi (surface and underground mining) na unafuata Sheria ya Madini, Sura 123 ambayo hairuhusu uchimbaji wa madini katika vyanzo vya mito na maziwa. Endapo shughuli za uchimbaji zitafanyika kando ya mito au maziwa, zitafanyika umbali wa mita 60 kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Na. 20 ya Mwaka 2004.

Mheshimiwa Spika, aidha, kabla ya shughuli za uchimbaji wa madini kufanyika katika eneo husika tathmini ya mazingira hufanyika na kutathmini athari za kimazingira ikiwemo viumbe hai pamoja na vyanzo vya maji. Hivyo, hakuna uhusiano wa moja kwa moja kwa uchimbaji wa madini na upungufu wa samaki katika mito na maziwa. Ahsante sana.