Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 131 2023-11-09

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:-

Je, nini mkakati wa Serikali kuboresha miundombinu ya barabara na kuinua maendeleo mikoa ya Lindi na Mtwara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tecla Mohamedi Ungele, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifautavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa Mkoa wa Mtwara, Serikali inaendelea na ujenzi wa barabara ya Mtwara – Nanyamba – Tandahimba – Newala – Masasi yenye urefu wa kilometa 210, ambapo sehemu ya Mtwara – Mnivata kilometa 50 ujenzi umekamilika na sehemu iliyobaki ya Mnivata – Newala – Masasi kilometa 160 pamoja na Daraja la Mwiti ujenzi umeanza na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2026. Aidha, Serikali imepanga kuifanyia ukarabati barabara ya Mtwara – Mingoyo – Masasi kilometa 200 ambapo maandalizi ya kutangaza zabuni za ukarabati wa barabara hii yako katika hatua za mwisho.

Mheshimwia Spika, kwa upande wa Mkoa wa Lindi, Serikali inaendelea na ujenzi wa barabara ya Nanganga – Ruangwa kilometa 53.2 ambapo umefikia asilimia 74 na ujenzi wa barabara ya Nachingwea – Ruangwa kilometa 52.8 upo hatua za mwisho za manunuzi. Aidha, ujenzi wa barabara ya Masasi – Nachingwea – Liwale kilometa 175 utatekelezwa kwa utaratibu wa EPC + F na tayari mkataba wa ujenzi umesainiwa, ahsante.