Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 130 2023-11-09

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:-

Je, lini barabara ya Makofia - Mlandizi itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Muharami Shabani Mkenge, Mbunge wa Bagamoyo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza maandalizi kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Makofia - Mlandizi, kilomita 35 ambapo kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina imekamilika. Katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali imepanga kujenga daraja dogo (box culvert) katika eneo la Mbwawa. Aidha, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara hii, ahsante.