Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 47 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 415 2022-06-20

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE K.n.y MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha stakabadhi za mashine za EFD ili zisifutike baada ya muda mfupi?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kufutika kwa stakabadhi za mashine za EFD baada ya muda mfupi kumesababishwa na matumizi ya karatasi zenye ubora hafifu. Aidha, karatasi zinazopaswa kutumika ni zile zenye ubora wa "thermal paper".

Mheshimiwa Spika, baada ya kubaini changamoto hiyo, TBS kwa kushirikiana TRA imeshatengeneza viwango vya ubora wa karatasi hizo vinavyotakiwa na sasa wanaendelea na usimamizi kuhakikisha karatasi zote zinakidhi ubora unaotakiwa.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo TRA imeboresha mfumo wa usimamizi wa mashine za EFD kwa kuwezeshe kupokea taarifa zote za kila risiti inayotolewa na kuitunza katika saver zake na hivyo kuwezesha nakala ya risiti hizo kuweza kupatikana wakati wowote inapohitajika. Ahsante.