Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 47 Water and Irrigation Wizara ya Maji 413 2022-06-20

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaharakisha na kumaliza upembuzi yakinifu kwa ajili ya mradi wa maji katika vijiji 46 Wilaya ya Rungwe?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge Viti Maalum, Mkoa wa Mbeya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 utekelezaji wa miradi ya maji unaendelea katika vijiji 15 na kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwa wastani wa asilimia 70. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 kazi za usanifu kwa vijiji 31 itakamilika na kuanza ujenzi wa miradi, matarajio ni kuhakikisha wananchi wa vijiji 155 Wilaya ya Rungwe wanapata maji kwa lengo la kufikia asilimia 85 ifikapo mwaka 2025.