Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 3 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 37 2023-11-02

Name

Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga miundombinu ya umwagiliaji katika mabonde ya mpunga ya Kwamgumi na Kwamsisi - Korogwe?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa Niaba ya Waziri wa Kilimo, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alfred James Kimea, Mbunge wa Korogwe Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Korogwe ina zaidi ya skimu 64 zilizoendelezwa na ambazo hazijaendelezwa ikiwemo Skimu ya Kwamgumi inayokadiriwa kuwa na ukubwa wa hekta 210 na Kwamsisi yenye ukubwa unaokadiriwa kufika hekta 1,500.

Mheshimiwa Spika, katika skimu ya Kwamgumi Serikali imefanya uwekezaji wa awali kwa kufanya ujenzi wa mfereji mkuu wenye urefu wa kilomita tatu. Aidha, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imefanya ukaguzi na tathmini ya awali kwa ajili ya kufanya ukarabati na uendelezaji wa miundombinu ya umwagiliaji katika skimu hii, ikiwemo usakafiaji wa mifereji ya kupitisha maji kwa ajili ya umwagiliaji. Hivyo basi, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Skimu ya Kwamgumi utaingizwa katika mpango na bajeti ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika mwaka wa fedha 2024/2025.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ina mpango wa kujenga miundombinu katika Skimu ya Kwamsisi. Aidha, mchakato wa manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa kufanya ujenzi katika skimu hii umeanza.