Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 3 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 31 2023-11-02

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga Wodi ya Akinamama, Watoto na Wanaume katika Vituo vya Afya Lukungu - Lamadi na Kiloleli?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Jimbo la Busega, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Vituo vya Afya vya Lukungu na Kiloleli ni miongoni mwa vituo vilivyosajiliwa na kuanza kutoa huduma vikiwa na upungufu wa miundombinu ikiwemo Wodi ya Wazazi, Jengo la Upasuaji na Maabara.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa awamu kwa ajili ya ukarabati na upanuzi wa miundombinu inayopungua kwenye vituo vya afya kote nchini vikiwemo Vituo vya Afya vya Lukungu na Kiloleli, ahsante.