Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 41 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 367 2022-06-09

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wenye viwanda vilivyokufa au havifanyi kazi kwa sababu mbalimbali ikiwemo kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Famili kilichopo Salasala katika Jimbo la Kawe?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Askofu Josephat Mathias Gwajima, Mbunge wa Jimbo la Kawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali kupitia utekelezaji wa blue print ni kuhakikisha changamoto zote zilizokuwa zinavikabili viwanda visivyofanyakazi zinatatuliwa ili kuwezesha viwanda hivyo kufanya kazi ikiwemo kiwanda cha mafuta ya kupikia cha Famili. Nakushukuru sana. (Makofi)