Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 41 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 363 2022-06-09

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: -

Je, ni kiasi gani Halmashauri zinahakikisha 30% ya fedha za manunuzi zinakwenda kwenye kampuni za wanawake?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anastazia James Wambura, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2011 inaekeleza taasisi nunuzi zote kutenga asilimia 30 ya bajeti inayotengwa katika manunuzi kwa ajili ya makundi maalum ambayo ni makundi ya vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Spika, mpaka kufikia Mei, 2022 jumla ya Halmashauri 24 kati ya 184 zimekwishavitambua na kuwezesha usajili wa vikundi 88 katika Mamlaka ya Kudhibiti Manunuzi ya Umma (PPRA) ikiwa ni kigezo cha lazima cha kisheria cha kuwezesha kundi hilo maalum kupata zabuni za ununuzi.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuzielekeza Halmashauri zote nchini kuhamasisha vikundi kujisajili na kutenga kiwango cha asilimia 30 ya bajeti ya manunuzi kwa vikundi hivyo vikiwemo vikundi vya wanawake. (Makofi)