Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 40 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 360 2022-06-08

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. JEREMIAH A. MRIMI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaweka alama za mipaka katika Hifadhi ya Serengeti na Pori la Akiba la Ikorongo ili kumaliza migogoro na vijiji jirani?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jeremiah Amsabi Mrimi, Mbunge wa Jimbo la Serengeti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kufanya tathmini ya mpaka wa Hifadhi ya Taifa Serengeti na vijiji imekamilika kwenye vijiji sita ambavyo ni Mbilikili, Gwikongo, Bisarara, Machochwe, Nyamakendo na Mbalibali. Zoezi linalofuata ni kuweka alama za kudumu kwenye mipaka ya Hifadhi ya Taifa Serengeti. Kazi hiyo itafanyika kwa njia shirikishi ili kuhakikisha kwamba kila upande unaridhika na zoezi hilo. Aidha, katika vijiji vya Robanda na Rwamchanga, Serikali iliweka mpaka wa Pori la Akiba Ikorongo kwa kuwashirikisha kikamilifu wananchi wa vijiji hivyo.