Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 39 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 352 2022-06-07

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa katika Kata za Qameyu, Madunga na Kiru Babati Vijijini?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Sillo Baran, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kata ya Qameyu ina jumla ya vijiji vinne ambavyo ni Endaw, Qameyu, Gawal na Merri. Kati ya vijiji hivyo, vijiji vitatu vya Endaw, Qameyu na Gawal tayari vimepatiwa umeme. Kijiji kimoja cha Merri ndio hakijapata umeme na kipo kwenye mradi wa REA III Mzunguko wa Pili ambapo mkandarasi anaendelea na kazi ya kuchimba mashimo na kusimika nguzo katika kijiji hicho. Kazi za mradi katika Kijiji hicho cha Merri zinatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, 2022.

Mheshimiwa Spika, Kata ya Madunga ina vijiji vitatu ambavyo ni Madunga, Utwari na Gidng’war. Vijiji vyote vitatu tayari vimeshafikiwa na huduma ya umeme. Kata ya Kiru ina jumla ya vijiji sita ambapo kijiji kimoja cha Kiru Six tayari kimeshapata huduma ya umeme. Vijiji vyote vitano visivyokuwa na umeme vya Kiru Dick, Kimara, Kokomay, Kiru Ndogo na Erri vinapatiwa umeme katika mradi wa REA III Mzunguko wa Pili unaoendelea. Mkandarasi anaendelea na kazi za kuchimba mashimo na kusimika nguzo katika vijiji hivyo. Kazi za mradi zinatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2022.