Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 39 Water and Irrigation Wizara ya Maji 347 2022-06-07

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: -

Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji Kata ya Iwawa Makete Mjini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Festo Richard Sanga, Mbunge wa Jimbo la Makete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa maji wa kuhudumia Kata ya Iwawa kwa kutumia chanzo cha Mto Isapulano. Mradi huu unahusisha ujenzi wa chanzo, ulazaji wa bomba kuu umbali wa kilometa 12.5, ulazaji wa mabomba na usambazaji umbali wa kilometa 39 na ujenzi wa matanki matatu yenye ujazo wa lita 450,000. Utekelezaji wa mradi huo unatarajiwa kukamilika katika mwaka wa fedha 2022/2023.