Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 39 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 344 2022-06-07

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa stendi ya kisasa ya mabasi katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni imekwishaandaa wazo mradi (concept note) kwa ajili ya ujenzi wa Mradi wa kimkakati wa stand ya mabasi. Kazi inayoendelea kwa sasa ni kutafuta msanifu wa mradi kwa ajili ya kuandaa michoro ambayo itawezesha kujua gharama halisi za mradi huo. Kazi hii ya usanifu inatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 30 Juni, 2022.

Mheshimiwa Spika, baada ya kupata gharama halisi za mradi huo na kukidhi vigezo vya mradi wa kimkakati, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuutekeleza. Ahsante.