Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 38 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 342 2022-06-06

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE K.n.y. MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: -

Je, ni lini Mradi wa REA II wenye vijiji 25 na REA III wenye vijiji 33 utakamilika katika Jimbo la Rungwe?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anton Albert Mwantona, Mbunge wa Rungwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji takribani 25 vilivyokuwa vinatekelezwa chini ya Mradi wa REA II vimeshafanyiwa uhakiki ili kujua upungufu ambao haujafanyiwa kazi. Marekebisho ya upungufu uliobainika katika vijiji hivyo utarekebishwa ndani ya miezi mitatu kuanzia mwezi Julai, 2022. Kazi hizo zitatekelezwa na Mkandarasi M/S ETDCO.

Mheshimiwa Naibu S[pika, Mradi wa REA III Mzunguko wa II ambao unapeleka umeme katika vijiji 33 vya Wilaya ya Rungwe unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba, 2022. Kwa sasa, Mkandarasi M/S Electrical Transmission and Distribution Construction and Maintenance Co. LTD anaendelea na kazi ya kupeleka umeme katika vijiji hivyo.