Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 38 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 338 2022-06-06

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupitia sheria zinazokinzana na Sheria Namba 4 na 5 juu ya umiliki wa ardhi kwa wanawake?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema Kichiki Lugangira, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Ibara ya 24 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inampatia kila mtu bila kujali jinsia yake, haki ya kumiliki mali ikiwemo ardhi na haki ya kuhifadhi kwa mali yake aliyonayo kwa mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, kama kuna Sheria inayokinzana na Katiba na Sheria za Ardhi Na. 4 na Na. 5 ya mwaka 1999 kuhusu umiliki wa ardhi kati ya mwanaume na mwanamke, Serikali itaanzisha mchakato wa kuzifanyia mabadiliko Sheria hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu umiliki wa ardhi kwa watoto chini ya miaka 18 wanaweza kumiliki ardhi kwa kupitia waangalizi wao kwa mujibu wa sheria.