Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 38 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 337 2022-06-06

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawasilisha Muswada wa Sheria unaozuia Polisi kukamata na kuwashikilia watuhumiwa kabla ya kukamilisha upelelezi?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Elibariki Immanuel Kingu, Mbunge wa Singida Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilifanya mabadiliko ya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura Na. 20 kupitia Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 1 ya mwaka 2022 mwezi Machi, 2022, ambapo kwa sasa Sheria imeweka masharti ya kutofungua mashtaka mpaka upelelezi utakapokamilika, isipokuwa kwa makosa makubwa tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)