Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 37 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 326 2022-06-03

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza: -

Je, ni Halmashauri na Manispaa ngapi nchini zinatekeleza ununuzi na ugawaji wa mafuta ya ngozi kwa watu wenye ulemavu wa ngozi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Alex Ikupa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, huduma kwa watu wenye ulemavu zimeendelea kuboreshwa kote nchini, ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya watu wenye ulemavu 138,468 kati yao wanawake 68,401 na wanaume 70,067 wametambuliwa. Aidha, katika kipindi hicho, watu wenye ulemavu wapatao 15,596 wamehudumiwa kwa gharama ya shilingi bilioni 1.3.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuwakinga watu wenye ualbino dhidi ya maradhi ya ngozi kutokana na jua, kati ya mwaka 2020 hadi 2022 jumla ya Halmashauri 102 kwenye mikoa 20 imetekeleza ununuzi na ugawaji wa mafuta ya ngozi (sun-screen cream) kwa kushirikiana na wadau. Jumla ya wanufaika 3,389 walipata huduma hiyo. Ahsante.