Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 3 Youth, Disabled, Labor and Employment Maswali kwa Waziri Mkuu 4 2016-11-03

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Nina swali moja kwa Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tangu napata ufahamu kulikuwa na sera katika nchi yetu ya wataalam, wafanyakazi wale wa nje, zamani walikuwa wanaitwa ma-TX. Wafanyakazi wa nje, kulikuwa na sera kwamba wanafanya kazi kwa kupata kibali kutoka uhamiaji cha miaka miwili, wakitegemewa kwamba kipindi hicho wana-recruit Mtanzania kwenye kampuni au kwenye kiwanda hicho na baada ya miaka miwili tunatarajia kwamba yule TX atakuwa ameshamhitimisha yule kijana au yule mfanyakazi atakuwa amehitimu na kibali chake kitakoma. Kama huo ujuzi utakuwa bado unahitajika, yaani hapana mtu aliyehitimu, ataongezewa tena miaka miwili kutimiza miaka minne. Je, Mheshimiwa Waziri Mkuu, hiyo sera bado ipo? Kama ipo, bado inatekelezwa?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niseme kwamba, sera ile bado ipo na Serikali tunaisimamia. Msingi wa jambo hili wa kuwapa muda mfupi hawa watalaam wenye ufundi maalum nchini kwetu katika sekta za kazi, ilikuwa ni kujenga wigo mpana kwa Watanzania kupata ajira na kuweza kusimamia maeneo haya ambayo yanahitaji pia utalaam.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumefanya hili kutoa nafasi kwa watumishi wa nchi za nje kuja nchini Tanzania kufanya kazi ambazo hapa ndani tunakosa utalaam; ndiyo tunapofuata utaratibu huo. Tunawapa miaka miwili ya kwanza, tukiamini kwamba Watanzania waambata watakuwa wameshajifunza utalaam ule na baada ya miaka miwili wanaweza kuondoka. Pale ambapo inaonekana kuna uhitaji zaidi, sheria inawaruhusu kuwaongezea miaka miwili ili tuendelee, lakini mwisho tunaweza kumwongezea mwaka mmoja na kufanya miaka mitano ya mwisho. Baada ya hapo, tunaamini Watanzania watakuwa wameshaweza kupata ile taaluma na kusimamia sekta za kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninachotaka niwahakikishie, mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kwamba tunafungua milango ya ajira kwenye sekta zote ikiwemo na utaalam, tutaendelea kuusimamia utaratibu huu wa kupokea watalaam kutoka nje wenye utalaam ambao nchini kwetu haupo ili kutoa nafasi kwa Watanzania kujifunza na baada ya miaka miwili tutataka wale wa kutoka nje warudi nchini kwao ili nafasi zile ziendelee kushikiliwa na Watanzania. Tutaendelea kusimamia Mheshimiwa Mbunge.

Additional Question(s) to Prime Minister

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu ya Waziri Mkuu kuonesha kwamba hiyo sera bado ipo. Kwa uzoefu wangu, utekelezaji wa sera hiyo haupo. Nina mifano, nchi za jirani anapokuja mwekezaji kuwekeza katika nchi hiyo huwa anaruhusiwa kuja na watu watano tu kutoka nchini kwake, tofauti na ilivyo hapa nchini kwetu. Wawekezaji wa kwetu hawana hiyo sera; hawana limit ya kuweka wafanyakazi kutoka nchini kwao. Ndiyo hiyo inayosababisha sasa hivi viwanda vingi vinaendeshwa na wageni wakati sisi wenyewe Watanzania tunapoteza ajira.
Mheshimiwa Naibu Spika, ushahidi huo ninao kwa sababu nimefanya kazi kwenye sekta ya watu binafsi siyo chini ya miaka 30 mpaka naingia hapa Bungeni. Tumeshaona wafanyakazi wengi wako zaidi ya miaka 20 wafanyakazi wa nchi za nje. Ukiwauliza vibali vyao havieleweki na wengine kama wanakuja Wakaguzi, wanafungiwa kwenye ma-godown, huo ushahidi ninao.
Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu, nipe kauli yako, ni lini Serikali yetu itaweza kufuatilia hili suala ili kuzalisha ajira kwa watu wetu? Lini itaweka sheria kwa wawekezaji kwamba wanahitajika walete wafanyakazi wangapi kutoka kwenye nchi wanazotoka?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nataka nimhakikishie kwamba jambo hili tunalisimamia tena kwa ukaribu zaidi. Sera aliyoitaja ya nchi za nje ndiyo sera yetu nchini kwamba mwekezaji yeyote anayekuja kuwekeza nchini iwe ni kiwanda au sekta ambayo inahitaji utalaam, tumeruhusu watumishi watano, ndio ambao wanaruhusiwa kuingia kufanya kazi nchini. Sekta zote ambazo zinaweza kufanywa na Watanzania, tumeweka utaratibu na tunasimamia kwamba sekta zote hizo zitafanya kazi na Watanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kama kuna eneo ambalo linalalamikiwa, basi Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane, kwa sababu sekta ya kazi iko ofisi kwangu. Nina Naibu Waziri anayeshughulikia ajira na kazi na nina Katibu Mkuu. Kwa hiyo, ni rahisi pia kufuatilia maeneo hayo ili tuone kwamba tunafungua nafasi hizo kwa Watanzania badala ya kuwa tunajaza raia kutoka nje ya nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, bado Serikali hii haizuii mashirika ya nje au wawekezaji kutoka nje kuja kuwekeza nchini, lakini lazima wanapofika Tanzania wataendelea kufuata sheria na sisi Serikali tutasimamia sheria hiyo kuwa inatumika ili kufungua nafasi kwa Watanzania.