Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Maswali kwa Waziri Mkuu 1 2016-11-03

Name

Munde Abdallah Tambwe

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii nami niweze kuuliza swali kwa Waziri Mkuu. Kwa kuwa Serikali ina mifumo, sheria, miongozo na taratibu ya upelekaji wa fedha za maendeleo katika Halmashauri zetu mara tu baada ya bajeti ya Serikali kwisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni wazi kuwa sheria hizi na miongozo hii haifuatwi na kupelekea Halmashauri zetu kupelekewa robo tu ya fedha au nusu tu ya fedha zikiwemo Halmashauri zangu za Mkoa wa Tabora ambazo zote saba hazijawahi kupata fedha kamili. Hii inaleta taharuki kubwa ndani ya Halmashauri zetu. Je, Mheshimiwa Waziri Mkuu unatoa kauli gani kuhusu ucheleweshwaji wa fedha za bajeti kwenda kwenye Halmashauri zetu kwa wakati muafaka?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabla sijaanza kujibu swali, uridhie kuwakumbusha Watanzania kwamba leo hii Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatimiza siku ya 365 kwa maana ya mwaka mmoja. Naamini Watanzania wote tumeona utendaji wake na hasa mwelekeo wake wa kuiongoza Serikali hii kwa mafanikio. Jukumu letu ni kumwombea Mheshimiwa Rais aweze kuendelea vizuri na kuiongoza nchi yetu na wananchi wote tuungane pamoja kila mmoja kwa dhehebu lake kuiombea Serikali hii iweze kupata mafanikio makubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba nianze kujibu swali la Mheshimiwa Munde kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali yetu baada ya bajeti inawajibika kutekeleza maamuzi ya Bunge letu hasa katika kupeleka fedha za bajeti zilizopangwa. Hata hivyo, Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote mnajua kwamba baada ya Bunge kuridhia na kutoa mamlaka ya matumizi ya fedha, Serikali hii tulianza na majukumu muhimu; moja, ilikuwa kwanza kujiridhisha kuwepo kwa mifumo sahihi ya makusanyo ya mapato na matumizi yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, mbili kwa upya wake tulianza kupeleka watumishi watakaosimamia shughuli za usimamizi wa ukusanyaji wa mapato na matumizi yake kwenye Halmashauri zote nchini. Kazi kubwa ya tatu ilikuwa ni kuratibu na kutathmini miradi yote iliyokuwa imeanza halafu ilikuwa haijaendelezwa na ile miradi mipya ili tuweze kutambua pamoja na thamani zake. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuwa tumejiridhisha sasa tumeanza kupeleka fedha kwenye Halmashauri zote nchini. Kwa mujibu wa kumbukumbu kutoka Hazina ambazo wakati wote tunapewa taarifa; ofisini kwangu pia napewa taarifa; kufikia mwezi Oktoba tumeshapeleka zaidi ya shilingi bilioni 177 za miradi ya maendeleo kwenye Halmashauri zetu nchini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge watabaini wiki hizi tatu tumeanza kuona kwenye magazeti yetu mengi matangazo mengi ya zabuni kutoka kwenye Halmashauri mbalimbali. Hii ina maana kwamba tayari miradi ile ambayo ilikuwepo na ile ambayo inaendelea na mipya imeshaanza kutengewa fedha na kuanza kutangazwa kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo. Kwa hiyo, nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote kwamba sasa Serikali itaendelea na upelekaji wa fedha kwenye Halmashauri kwa ajili ya shughuli zetu za maendeleo kwenye Halmashauri zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, bado msisitizo umebaki pale pale kwamba Halmashauri ziendelee kukusanya mapato ya ndani ili kuongezea bajeti kwa fedha za Serikali ambazo tunazipeleka na tumesisitiza ukusanyaji huo uwe ni wa mfumo wa kielektroniki ili kudhibiti mapato ambayo tunayapata. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, tumeendelea kusisitiza matumizi sahihi ya fedha ambazo tunazipeleka kwenye Halmashauri kwamba fedha hizi ni lazima zitumike kadiri ilivyokusudiwa kwa miradi iliyoandaliwa kwenye Halmashauri zenyewe.
Waheshimiwa Wabunge, sisi wenyewe ni Wajumbe wa Baraza letu la Madiwani kwenye Halmashauri zetu; niendelee kuwasihi kusimamia na kufuatilia matumizi ya fedha tunazopeleka kwenye Halmashauri ili ziweze kutekeleza miradi ile kikamilifu. Serikali itaendelea kutuma fedha kwenye Halmashauri zetu kadri miradi ile ilivyoweza kuratibiwa. Ahsante.

Additional Question(s) to Prime Minister

Name

Munde Abdallah Tambwe

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Question 1

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, mimi binafsi na Watanzania wote wana imani na Rais Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Waziri Mkuu wetu na tuna imani haya yote aliyoyasema hapa kwa Serikali hii ya Awamu ya Tano yatatekelezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimuulize swali dogo tu la nyongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu. Atakuwa tayari sasa kuzifuatilia Halmashauri zote ziwe zinapokea pesa kwa kutumia mashine za kielektroniki?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

yote, tumeendelea kuwaagiza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na watendaji wa Halmashauri wakiwemo Wakurugenzi kuhakikisha kwamba moja ya majukumu yao waliyonayo ni kuhakikisha na kujiridhisha kwamba kila eneo la makusanyo, vifaa vya kielektroniki vinatumika na kwa hiyo, wajibu wangu ni kusimamia kuona kwamba matumizi ya vifaa hivi yanafanyika na yanaendelea. Ahsante sana.