Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 3 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 1 2024-02-01

Name

Janejelly Ntate James

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza naipongeza Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi inavyojitahidi kuboresha elimu nchini, hongereni sana. Nina swali dogo tu, Serikali sasa mtuambie mna mkakati gani wa kuweza kutosheleza walimu wenye weledi kufundisha masomo haya ya amali ukichukulia tuna upungufu wa walimu nchini?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Janejelly Ntate, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakiri kwamba tunao upungufu wa Walimu kwenye shule zetu kwa ngazi mbalimbali na hii inatokana na kuwepo kwa Walimu wanaostaafu, wanaotangulia mbele za haki na wagonjwa ambapo tunajua yapo mapengo ya ufundishaji hasa kwenye eneo hili la elimu ya amali.

Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali kwenye mpango huu ni kuhakikisha kwanza, tunaendelea kupokea vibali vya ajira kama ambavyo Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan anavyotoa vibali vya kuajiri walimu, miongoni mwa Walimu ambao tunawaajiri hasa tunaangalia zaidi kwenye eneo hili la elimu ya amali ili kuwezesha utekelezwaji mzuri wa Sera hii mpya inayogusa kwenye maeneo ya amali ili kuwezesha ufundishaji na wanafunzi waweze kupata elimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mkakati wetu ni kuongeza ajira kwenye sekta ya elimu ili kuwa na walimu wa kutosha, ahsante. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister