Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 3 Education, Science,Technology and Vocational Training, Maswali kwa Waziri Mkuu 4 2023-11-02

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Gender

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kumuuliza Waziri Mkuu swali la nyongeza.

Mheshimiwa Waziri mmefanya kazi kubwa sana kupunguza miaka kutoka 11 sasa na kuwa 10 kwa maana ya miaka sita na miaka ile minne ya lazima, lakini kuna mzigo mkubwa sana wa masomo mengi kwa watoto wa shule za awali. Je, kuna utaratibu gani ambao Serikali imeuona wa kupunguza idadi ya masomo lakini quality ikabaki palepale? Ahsante.

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, Mbunge wa Mbeya, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Elimu ilipokuwa inatekeleza Sera hii ambayo tunaimalizia muda wake iliaandaa masomo kulingana na uhitaji. Sasa mabadiliko ya sera hii nayo yataangalia mzigo huo na kwa kuwa wadau walishapata nafasi ya kuchangia tunaamini hili nalo walishalisema na Wizara ya Elimu imechukua maoni yote yaliyotolewa na wadau katika kuhakikisha kuwa mzigo huu unapungua na utaratibu ambao upo kwa madarasa ya awali yanayomwandaa mwanafunzi kuingia darasa la kwanza wale masomo yao ni kusoma, kuhesabu na kuandika.

Mheshimiwa Spika, walikuwa wanaandaliwa hivyo kwa kipindi chote cha mwaka mmoja au miwili kulingana na umri wa mtoto. Wanamwandaa kujua kuandika, kusoma na kuhesabu ili aingie darasa la kwanza akiwa anajua kuhesabu, kuandika na kusoma na anapoingia kwa darasa la kwanza, la pili anaanza sasa kuingia masomo ya shule za msingi. Hapa sasa sera na michango ya wadau watakuwa wameshapitia hayo na ushauri upo Wizara ya Elimu, kuona ni masomo yapi yafundishwe kutoka darasa la kwanza mpaka la sita na pia yataangalia uzito na umuhimu.

Mheshimiwa Spika, baada ya kuwa sasa tunawaandaa kwa ajili ya kuingia kwenye mafunzo ya sekondari, lazima watafanya mapitio tena ya masomo haya ili kutoa idadi ya masomo ambayo yataweza kubebwa na kijana huyu wa umri huu ambaye anasoma mpaka darasa la sita ili kumfanya awe na uelewa mpana na wa haraka zaidi, ahsante. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister