Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 3 Education, Science,Technology and Vocational Training, Maswali kwa Waziri Mkuu 3 2023-11-02

Name

Joseph George Kakunda

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Ningependa kumuuliza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwamba hatimaye imehuishwa Sera ya Elimu ambayo ilizinduliwa kwa mara ya kwanza mwaka 2014 lakini mpaka inahuishwa tena haikuwahi kutekelezwa kwa sababu ilikosa nguvu ya sheria. Sasa kwa mahuisho haya yaliyofanyika sasa hivi, je, Serikali imejipanga lini kuleta Sheria ya Elimu mpya Bungeni ili kuyapa nguvu haya mahuisho ambayo yamefanyika?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kakunda, Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli hata Sera ya mwanzo tulipokuwa tunatekeleza tulikuwa na Sheria inasaidia, inaongoza utekelezaji wake, lakini kutokana na mabadiliko haya tumegusa maeneo yanayohitaji mabadiliko ya kisheria pia ili Sera hii iweze kutekelezeka; na kwa kuwa tunaelekea kwenda kuizindua na Wizara ya Elimu inaendelea na mchakato wa kusimamia maboresho ya Sera hii mpaka kuzinduliwa na utekelezaji wake, tutaendelea kubaini maeneo muhimu ya kubadilisha Sheria ili tuweze kutunga Kanuni ili ziweze kuwezesha urahisi wa utekelezaji wa Sera hii. Kwa hiyo Wizara ya Elimu imejipanga, inaendelea na mchakato na nimetoa wito hapa na nimeeleza kwamba, bado tunaendelea kutoa elimu kwa njia mbalimbali, kushirikisha wadau wote. Kwa hiyo hii hatua tunayoendelea nayo ya kila hatua itakuwa inabaini kadiri ya mahitaji ya mabadiliko ya sheria na kutengenezea kanuni za usimamizi wa utekelezaji wa sera hiyo, ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister