Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 23 Water and Irrigation Maswali kwa Waziri Mkuu 3 2016-05-19

Name

Hassan Selemani Kaunje

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. KAUNJE:
Mheshimiwa Spika, nishukuru kupata nafasi ya kuuliza swali la moja kwa moja kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwanza tunafahamu kwamba maji ni uhai na Sera ya Taifa ya Maji inahitaji kila mwananchi kuweza kuyafikia maji ndani ya umbali wa mita 25. Je, Serikali ya Awamu ya Tano imejipangaje kuhakikisha maji haya yanawafikia wananchi especially
wananchi wa Mkoa wa Lindi ambao wanatatizo kubwa sana la maji?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kaunje, Mbunge wa Lindi Mjini kama ifuatavyo:-
Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Kaunje, amekuwa anafuatilia sana mwenendo wa maji na hasa alipoweka kule mwishoni hasa wananchi wa Mkoa wa Lindi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Sera ya Maji nchini imetamka wazi kwamba Serikali itasambaza maji kwa wananchi wake kote nchini mpaka ngazi za vijiji tena kwa umbali usiozidi mita 400 hiyo ndiyo sera na wakati wowote Wizara ya Maji inapofanya kazi yake inafanya kazi kuhakikisha kwamba sera hiyo inakamilika. Iko mipango mbalimbali na nadhani Wizara ya Maji itakuja na bajeti hapa ikiomba ridhaa yenu muipitishe Waheshimiwa Wabunge ili tukaendelee kutekeleza hiyo sera ya kusambaza maji, na mikakati yetu sisi, maji
lazima yawe yamefika kwenye ngazi za vijiji kwa asilimia mia moja ifikapo mwaka 2025 na ikiwezekana kufikia mwaka 2020 hapa kwa zaidi ya asilimia tisini huo ndiyo mkakati wetu. Mkakati huu utatokana tu kama tutaendelea kupata fedha nyingi Serikalini na kuzipeleka Wizara ya Maji ili Wizara ya Maji waendelee na mkakati ambao wanao.
Kwa hiyo, niseme tu kwamba kwa malengo haya tunakusudia kusambaza maji kwenye maeneo yote ya vijiji na maeneo ya miji ili wananchi wetu waweze kupata tija ya maji kwenye maeneo haya. Kwa miradi ambayo ipo, ambayo imeelezwa kwamba ipo inaendelea kutekelezwa, tunaamini miradi hiyo kwa watu wote ambao tumewapa kazi hiyo wataendelea kutekeleza kadri ambavyo tunawalipa fedha zao ili waweze kukamilisha.
Waliokamilisha wakamilishe miradi ambao hawajakamilisha tunaendelea kuwapelekea fedha ili waweze kukamilisha ili maji yaweze kutolewa na kila mwananchi aweze kunufaika na sera hiyo ya Serikali.

Additional Question(s) to Prime Minister

Name

Hassan Selemani Kaunje

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Question 1

MHE. HASSAN S. KAUNJE:
Mheshimiwa spika, ahsante sana. Mheshimiwa Waziri Mkuu, sababu zinazosababisha muda mwingine kutokupatikana maji ni pamoja na wakandarasi ambao wanakuwa wamelipwa lakini wanashindwa
kukamilisha miradi ya maji kwa wakati na sababu hizo ni pamoja na mradi wa Ng‟apa ambao uko Lindi. Je, ni hatua gani zinachukuliwa na Serikali dhidi ya wakandarasi wa aina hii ili maji yaweze kuwafikia wananchi?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la
Mheshimiwa Kaunje, Mbunge wa Lindi Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimeeleza kwenye jibu langu la
msingi, suala la wakandarasi wetu kwa sababu malengo ya Serikali tunawapa hizi kazi ili waweze kuzimaliza katika kipindi kifupi sasa kama inatokea mkandarasi hawezi kamaliza kazi kwa kipindi kifupi, ziko sababu mbalimbali ambazo pia tumezizoea maeneo mengine, malipo kutoka kwa kuchelewa nako kutokana na tatizo la fedha inawezekana mkandarasi hajamaliza. Lakini malengo yetu kama mkandarasi analipwa vizuri na kwahiyo basi anatakiwa akamilishe mradi huo kwa wakati uliokubalika. Lakini ikitokea mkandarasi
hajamaliza kama kuna tatizo la fedha hilo ni juu ya Serikali kupitia Wizara ya Fedha kukamilisha kulipa madeni ili mradi ukamilike. Kama mkandarasi amelipwa fedha zote au zaidi ya asilimia 90 na hajakamilisha kwa kipindi kinachotakiwa, zipo taratibu za kisheria za kufanya kwa sababu ameingia zabuni kisheria na kwa hiyo, tunaweza tukatumia utaratibu wa kisheria pia kwa kuadhibu mkandarasi ambaye hajamaliza kazi lakini pia amelipwa fedha.
Sasa sina uhakika na mradi wa Lindi uko katika sura gani na kama
ingekuwa session hii inaweza kumpa Waziri Mkuu nafasi ya kupata majibu sahihi ningweza kukupa jibu sahihi la mradi huo wa Ng‟apa.