Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 14 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 2 2023-04-27

Name

George Ranwell Mwenisongole

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kumuuliza swali Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu, kuna mifugo, mali nyingi za wananchi zilizokamatwa kwa kuingia hifadhini, na umesema kwamba ipo haja ya kuimarisha mahusiano kati ya wahifadhi na wananchi. Kwa nini usitoe kauli hapa Bungeni kuitaka mifugo yote, mali zote za wananchi zilizokamatwa kwa sababu ziliingia kwenye hifadhi ziachiwe ili kufungua ukurasa mpya tuanze moja? (Makofi)

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwenisongole, Mbunge wa Mbozi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa taarifa nimeitoa hapa leo na kutoa maelekezo kwa vyombo vyote vya Serikali kuchukua hatua hizi. Hatua zote za awali, taratibu, sheria na kanuni ambazo zipo ziendelee kufuatwa ili haki iweze kutendeka kwa haraka sana kama ambavyo nimesisitiza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, maelekezo yangu yamebaki, yamekuwa wazi na sahihi. Kwa hiyo, hatua hizo ziharakishwe ili wananchi waweze kutambua haki zao na upande wa Serikali uwajibike kutoa elimu kuanzia sasa na kuendelea. Ahsante.

Additional Question(s) to Prime Minister