Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 14 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 1 2023-04-27

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, naomba niseme kwa niaba ya wananchi wa Tarime Vijijini kwamba Mheshimiwa Waziri Mkuu ni Waziri Mkuu wa viwango; hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, nataka nikwambie kwamba hotuba uliyotoa hapa Waheshimiwa Mawaziri na viongozi wakiifanyia kazi Wabunge hawa watafurahi sana na wananchi wetu watafurahi, ume-cover karibu kila eneo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ombi langu; pamoja na hotuba nzuri uliyotoa hapa, ninataka uwasaidie wananchi wa Tarime Vijijini, Serengeti, Bunda; ni lini hawa Mawaziri watakwenda kuwasikiliza wananchi wale ili kutoa elimu na kutambua ile GN ya mwaka 1968 ambayo kimsingi ndiyo kilio cha watu wangu? Ahsante. (Makofi)

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru Mheshimiwa Mbunge kutambua jitihada za Serikali katika kufanya utatuzi wa migogoro iliyopo kwenye Wilaya yake, Jimbo lake kule Traime Vijijini, Mkoani Mara, kwamba hatua iliyofikiwa sasa kwenye eneo lile ni kukutana kwa Mawaziri na wananchi ili kuwaelimisha, hayo ndiyo mahitaji makubwa ya wananchi wale, ili waweze kutambua kikamilifu mipaka iko wapi na wananchi wapate nafasi pia ya kuweza kuwasilisha hoja zao, mahitaji yao ili Serikali ifanyie kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa nilishawaagiza waende haraka, na ilikuwa ndani ya mwezi huu, lakini kutokana na majukumu tuliyonayo ndani ya Serikali na Mawaziri hawa kuwajibika kikamilifu, nataka nikuahidi, kuanzia tarehe 02 Mei baada ya sherehe za Mei Mosi ambazo wao pia watashiriki kule Morogoro, wataanza safari kwenda Tarime. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nina uhakika kwamba kati ya tarehe 03 na 04 watakuwa Tarime. Na tukualike wewe, tuwaalike Wabunge wa Bunda wanaoguswa na eneo lile la mipaka pamoja na Serengeti kushiriki vikao hivyo kwa sababu hoja zitakazotolewa na Mawaziri zitakuwa zinagusa kwenye maeneo hayo, ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister