Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 3 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 1 2023-02-02

Name

Ally Mohamed Kassinge

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali moja kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu kutokana na taarifa iliyowasilishwa. Kwa mujibu wa waraka ambao unaelekeza adhabu za viboko kwa wanafunzi wenye utovu wa nidhamu, viboko visizidi vinne na ameidhinishwa Mwalimu Mkuu au Mkuu wa Shule au atakayeidhinishwa na wakuu hao kutoa adhabu hiyo. Kutokana na usimamizi au udhibiti ambao hauko sawa, imebainika taharuki kama ambavyo imejiri hivi karibuni.

Je, kwanini Serikali isirekebishe waraka huu na kuongeza kwamba wakati aliyeidhinishwa kama ni Mkuu wa Shule au mwingine aliyeidhinishwa anatoa adhabu kukawa na Kamati maalum ya usimamizi na kubariki adhabu hiyo ili kuondokana na taharuki kama hizi? Ahsante.

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli waraka wetu wa elimu umetoa maelezo thabiti ya namna ya utoaji wa adhabu shuleni, kama nilivyosema kwenye maelezo yangu, adhabu ya viboko ni moja kati ya adhabu zinazotumika katika kumjenga mtoto na kumfanya aweze kutii sheria za shuleni na viboko visizidi vinne. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa uundwaji wa Kamati Shule zote za Msingi zina Kamati ya Shule, na Shule zote za Sekondari zina Bodi ya Shule. Pale ambako mwanafunzi hufanya kosa kubwa kuliko haya makosa madogo madogo basi mtoto huyo, kwanza hatua inayochukuliwa mzazi kuitwa kujulishwa tabia na mwenendo wa mtoto huyo ili sasa kumshirikisha mzazi katika kumjenga mtoto kinidhamu. Mbili, pale ambako adhabu hiyo inahitaji kumfukuza shule unashirikisha sasa Kamati ya Shule. Kwa hiyo, utaratibu wa utoaji adhabu umewekwa vizuri kabisa na ndiyo ambao unafuatwa mashuleni. Hili ambalo limejitokeza hivi karibuni ni tatizo la mmoja kati ya watumishi wengi kutenda bila kufuata utaratibu lakini siyo utaratibu ambao umewekwa na siyo ambao unatumika kwenye maeneo mengi. Ahsante sana.

Additional Question(s) to Prime Minister