Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 8 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 6 2021-11-11

Name

Rose Cyprian Tweve

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, kila mwaka Serikali imekuwa ikiongeza bajeti ya kupeleka kwenye Vyuo Vikuu ili watoto wasiokuwa na uwezo waweze kupata mkopo na kujikimu na mahitaji yao ya chuo. Utakubaliana na mimi kama Taifa tuna uhitaji mkubwa sana wa Watanzania hasa vijana wenye ujuzi hasa ujuzi wa kati ili sasa twende kuboresha na kupanua huduma muhimu kama vile afya, elimu, nishati na miundombinu vijijini. Sasa changamoto kubwa ya hawa vijana ambao tunawahitaji ambao wako kwenye vyuo vya kati hawana access ya hii mikopo na wao hawana uwezo wa kujilipia ada hizi.

Mheshimiwa Spika, sasa nataka kujua mkakati wa Serikali wa kuhakikisha hawa vijana ambao tunawahitaji ambao wako kwenye vyuo vya kati wanakuwa na access ya kupata hii mikopo kama ambavyo tunafanya vijana wa elimu ya juu? Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tweve, Mbunge wa Iringa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, anachosema Mheshimiwa Mbunge ni sahihi kwamba tuna kada ya elimu ya kati hawajaingia kwenye mkopo kama ambavyo mkopo huu unaendelea. Hii inatokana na sheria tuliyoiweka na ndiyo kwa sababu Bodi inaitwa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu. Sheria iliyoanzisha Bodi hii ilianza kwa kuelekeza elimu ya juu na ndiyo ambayo sasa tunayo. Toka tulipoanza mpaka sasa tumegundua kwamba mahitaji ni mapana mno, lakini upana huu wa mahitaji utategemea pia na uwezo wa kifedha wa Serikali. Tukiwa tunaendelea kuwanufaisha Watanzania kupitia elimu ya juu kwa vyuo tu vya elimu ya juu, bado tuna mafanikio lakini tuna changamoto zake, tunaendelea nazo. Tumegundua tuna uhitaji pia wa elimu ya kati ambayo ni kada ambayo inafanya kazi kubwa sana kwenye sekta mbalimbali mpaka viwandani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo kadiri tunavyokwenda Serikali tutaleta Muswada ndani ya Bunge kama pia uwezo wa kifedha nao ukiwa mzuri na tutashiriki pamoja kujadili uwezekano wake ili kufungua mlango kwa vijana wa kada ya kati wa elimu ya kati ili na wao waweze kunufaika na mikopo hii. Kwa hiyo kadri tutakavyokuwa tunapata fedha, tutakuwa tunaendelea kuboresha kupanua wigo, tukifika elimu ya kati tutashuka mpaka elimu ya juu ya kawaida huku chini kwa maana ya sekondari kadiri tutavyopata fedha. Hiyo tutaileta Bungeni, tutajadili Waheshimiwa Wabunge na Mheshimiwa Tweve najua utakuwepo. Ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister