Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 8 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 5 2021-09-09

Name

Esther Nicholus Matiko

Gender

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kumekuwepo na uhaba wa rasilimali watu kwenye taasisi za idara mbalimbali za Serikali, mathalani kada ya walimu, watumishi wa afya na kwenye majeshi yetu; Jeshi la Polisi, Magereza na JWTZ kitu ambacho kinapunguza ufanisi katika kutoa huduma kwa wananchi. Hata jana Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani alikiri kabisa kwamba kuna upungufu ambao unapelekea hata kufunga vituo vya polisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imechukua hatua kwa kutangaza ajira 3,000 kwenye Jeshi la Polisi lakini kuna masharti ambayo yameambatana, kwanza wamesema ni ambao wamemaliza JKT na JKU lakini sharti namba tano na sita linaeleza kwamba ni wale vijana waliomaliza form four na form six kati ya mwaka 2017 na 2020.

Mheshimiwa Naibu Spika, sote tunatambua kwamba ajira zilisitishwa tangu mwaka 2015 na kuna vijana ambao wamemaliza form four na form six kati yam waka 2015/2016 na wameenda JKT na JKU na zaidi wamejenga Taifa letu kwa mfano Oparesheni Magufuli, Operesheni Makao Makuu na Operasheni Mererani.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kwa nini sasa Serikali isifanye rejea kwenye tangazo lao la ajira ambalo lina-limit vijana hawa wa 2015/2016 ili liweze kuwa-accommodate na wao? Kwa nini wasiseme kwamba ajira inatolewa kwa vijana wote wenye sifa kuanzia waliomaliza form four na six 2015 mpaka 2020? Mfano Iringa na Mbeya wamewakataa walivyoenda kwenye usaili. (Makofi)

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali inaendelea na zoezi la kuajiri watumishi wa sekta mbalimbali hapa nchini ikiwemo na hayo matangazo aliyoyasema ya Jeshi la Polisi. Sina uhakika na vigezo hivyo na wito walioutoa kwamba wanataka waajiri vijana kuanzia mwaka gani lakini tuichukue hiyo kama ushauri kwa Wizara ya Mambo ya Ndani ambayo sasa inasimamia ajira hiyo ili waanze kufanya mapitio ya ajira hiyo na vigezo ili pia hawa waliomaliza jeshi kuanzia mwaka 2015 nao waingie halafu wachujwe wote tupate vigezo na tuweze kuwapata wale ambao wana sifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, natambua pia tulikuwa na hilo kundi la Operesheni Magufuli na Operesheni Mererani na wote waliahidiwa kuingia kwenye orodha ya ajira na kama miongoni mwa hao walianza mwaka 2015 na kumaliza 2016 na hao walioanza kuchukuliwa 2017 mpaka sasa basi Wizara naona itatimiza wajibu wake kuwaita wote halafu iwachuje waweze kupata ajira pia. Kwa hiyo, tunaupokea ushauri wako na Waziri wa Mambo ya Ndani yuko hapa atalichukua hilo kwa ajili ya kulifanyia kazi. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister