Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 8 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 4 2021-09-09

Name

Aleksia Asia Kamguna

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo mengi yana maeneo makubwa ya kiutawala nchini kwetu; kwa mfano, Mikoa ya Tabora, Tanga na Morogoro. Mkoa wa Morogoro una hususan wa square meter 73,000 ambazo ni kubwa sana. Sasa zile zinafanya kwamba ule mkoa ushindwe kutimiza adhma yake ya kuhudumia watu wake kikamilifu. Kwa mfano, kuna baadhi ya maeno hayafikiki kabisa huduma za afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa maeneo haya hayafikiki na huduma zinakuwa ni hafifu.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kugawa haya maeneo hatimaye huduma za jamii ziweze kufika kila eneo kwa urahisi? (Makofi)

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kamguna, Mbunge kama ifuatavyo, samahani kama nimekosea jina.

Mheshimiwa Naibu Spika, upo ukweli kwamba tulikuwa na nia ya kugawa maeneo mapya ya utawala, hasa baada ya kugundua kwamba kuna maeneo makubwa sana kuliko huduma ambazo zinatolewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Morogoro, Tanga na Tabora ni miongoni mwa mikoa mikubwa sana ambayo pia tumepata taarifa kwa maandishi lakini pia kupitia vikao mbalimbali wakiomba kuyatenga tena maeneo hayo na kuongeza maeneo ya utawala kwa lengo la kurahisisha utoaji huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tulisitisha kidogo kutoa maeneo mapya ya utawala na kutaka kuimarisha maeneo yale ambayo tumeikabidhi mamlaka hiyo, kwa maana ya vijiji, kata, wilaya hata halmashauri na mikoa mipya ili iwe na miundombinu ya kutosha na kuwapeleka watumishi wa kutosha kuweza kuhudumia maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nini mpango wa Serikali kwa sasa, tunasubiri sensa hii inayokuja mwakani ya mwaka 2022 iweze kutupa takwimu halisi ya idadi za idadi ya wakazi ili pia tuone idadi ya watumishi ambao tumewapeleka kuwahudumia na miundombinu tuliyoipeleka kuhudumia wananchi hao halafu tutafanya maamuzi kulingana na ukubwa huo na vigezo hivyo ambavyo tutavitumia kuweza kutoa maeneo haya mamlaka mpya. Hii ndiyo sababu kwa sasa hatujaruhusu tena kutoa mamlaka mpya kwenye maeneo mengine mapya kwa sababu hiyo. Kwa hiyo, baada ya sensa Serikali itafanya maamuzi ya kuona umuhimu wa kugawa maeneo hayo kulingana na vigezo vile ambavyo tumeamua kuvitumia, ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister