Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 8 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 1 2021-09-09

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ili niulize swali la kwanza kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Sera yetu ya Elimu hasa elimu ya msingi imeelekeza kwamba elimu ya msingi ni bure kuanzia ngazi ya msingi; na zoezi hili lilikuwa linafanyika vizuri sana, tunaipongeza sana Serikali kwa hatua hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu nilitaka kuufahamu, ni upi mkakati wa Serikali katika Sera ya Afya angalau sasa katika afya msingi kwa maana ya zahanati na vituo vya afya kuweka eneohili tupate huduma za afya bure?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shangazi, Mbunge wa Mlalo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali yetu imeandaa sera upande wa elimu na kuifanya elimu sasa ipatikane bure kuanzia elimu ya awali mpaka kiwango cha sekondari, kidato cha nne na mkakati huu unasaidia sana kuwapunguzia wazazi gharama za kumpeleka mtoto shule na huku tukiwa pia tumeweka ulazima wa kila mtoto wa Kitanzania kupata elimu ya msingi ambayo kwa sasa inaenda mpaka kidato cha nne.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anataka kujua nini mpango wa Serikali wa Sera aina ile ile ya elimu kuifanya pia kwenye sekta ya afya ili tuweze kutoa huduma za afya bure.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka tu kueleza kwamba tunaendelea kufanya mapitio ya sera zetu na hasa kwenye sekta ya huduma za jamii ili Serikali yetu iweze kutoa ikiwezekana unafuu mkubwa kwenye utoaji wa huduma za jamii kwa Watanzania ikiwemo na sekta ya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, pindi tutakapofanya mapitio haya na kukamilisha kuona uwezo wa kifedha wa kugharamia kwa upande mwingine, kwa maana ya kupata vifaa tiba, utafiti na maeneo mengine yote, Serikali itatoa tangazo wakati pale tutakapokuwa tumekamilisha utafiti huo ambao sasa hivi wataalam wetu wanaufanyia mapitio, ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister