Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 34 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 7 2019-05-23

Name

Rose Cyprian Tweve

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Mheshimiwa Waziri Mkuu ni imani ya watanzania kuwa elimu bora ndiyo utakuwa msingi wa kuhakikisha vijana wa Taifa hili pale wanapohitimu wanakuwa na uwezo aidha wa kuajiriwa au kutumia knowledge na skills ambazo wamezipata shuleni kuweza kutambua fursa zilizopo ili waweze kujiajiri wenyewe. Sasa ni matumaini yangu Mheshimiwa Waziri Mkuu utakubaliana na mimi kuwa walimu bora ndiyo wenye uwezo wa ku-transfer au kuambukiza maarifa yaliyo bora kwa vijana wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa swali langu kwako Mheshimiwa Waziri Mkuu, nilitaka kujua mkakati wa Serikali kuhakikisha tunatumia vijana ambao wana division one na two ili wawe walimu ambao tunategemea wata-train wanafunzi ambao watakuwa competent either kutumika kwenye nchi yetu au waweze kutoka nje ya nchi kujitafutia fursa kwa ajili ya maisha yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tweve, Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, upo ukweli kwamba vijana wetu wakipata elimu bora wanaweza kuingia kwenye Sekta ya Ajira, ajira binafsi hata zile rasmi nje na ndani ya nchi. Na hii inatokana na uimara wa utoaji elimu tulionao nchini ambao pia tunaendelea kuuboresha kila siku ili tuweze kufikia hatua hiyo ya kuwawezesha kuona fursa na kuweza kuzitumia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, utaratibu ambao tumeuweka Serikalini ni kubainisha kati ya Wizara ya Elimu na TAMISEMI kwa usimamizi imara kwenye maeneo haya. Wizara ya Elimu kama msimamizi wa sera, yeye ndiye mwenye uwezo na ndiyo tumempa dhamana ya kuhakikisha kwamba tunaandaa walimu bora wenye uwezo kwa madaraja uliyoyataja na vigezo vinavyotumika kupeleka walimu ni vile ambavyo vimeshafafanuliwa. Tunao walimu wa shule za msingi, walimu wa sekondari lakini pia tuna walimu wa vyuo, maeneo yote yana sifa zake na wote hawa wanakwenda kama sifa zao zinavyoeleza.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, matokeo tunayoyapata sasa ni matokeo mazuri ya mipango ya Sera tuliyonayo lakini usimamizi wa utoaji elimu tumeipeleka TAMISEMI, wao ndiyo wanamiliki shule za msingi na sekondari kama elimu ya msingi kujihakikishia kwamba vijana wanaoandaliwa kwenda mpaka elimu ya juu ni vijana ambao walishapewa msingi imara wa kielimu. Kwa hiyo, kazi hii inaendelea kwa kuwa na walimu imara, bora lakini pia kuimarisha miundombinu na wote Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote ni mashahidi, tumepeleka fedha ya kutosha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa, nyumba za walimu, maabara na vyumba vingine pamoja na vifaa mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa mikakati hii yote inasababisha kuwa na elimu bora nchini na unapotoa elimu bora, unatoa matokeo yaliyo bora na vijana wanaopata matokeo hayo, sasa wanaweza kuziona fursa zao na kuweza kuzitumia. Kwa hiyo, mkakati wa Serikali unaendelea na tutaendelea kupokea ushauri wenu kuona naona nzuri ya kuboresha Sekta ya Elimu ili tuweze kufikia hatua nzuri, ahsante. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister