Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 3 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 5 2020-01-30

Name

Leah Jeremiah Komanya

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kumuuliza Mheshimiwa Waziru Mkuu.

Mheshimiwa Spika, ni ukweli usiopingika kwambaSerikali ya Chama cha Mapinduzi imefanya kazi kubwa katika sekta ya elimu na wananchi wameunga juhudi hizo kwa kuchangia ujenzi wa madarasa. Hata hivyo kuna maelfu ya wanafunzi waliofaulu kujiunga kidato cha kwanza hadi leo hawajaripoti shuleni kwaajili ya upungufu wa madarasa

Mheshimiwa Spika, nilitaka kujuwa ni nini kauli ya Serikali?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Komanya kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, sasa tunayo idadi nzuri na kubwa ya wanafunzi wanaofaulu darasa la saba kwenda Sekondari. Serikali msimamo wake ni kuwapeleka wanafunzi wote waliofaulu kwenda Sekondari kwa asilimia mia. Serikali imetoa maelekezo kwa mamlaka ya Serikali za Mitaa kuhakikisha kwanza unafanya sense kupitia mfumo wa elimu ambao unaweza kuutabiri halmashauri hii inaweza kutoa wanafunzi wangapi kwenda Sekondari na kujipanga katika kuboresha katika miundombinu tayari kwa kuwapokea vijana hawa.

Kazi hiyo inafanywa kila halmashauri kwa usimamizi wake na wanapofaulu tunataka wote waende waanze kidato cha kwanza kwa wakati. Hata mwezi wa Disemba nilitoa kauli nikiwa mkoani Lindi kwamba kila halmashauri ihakikishe wanafunzi wote wanaenda awamu moja badala ya kuwaweka awamu mbili kwa sababu awamu mbili wale awamu ya pili wanakosa baadhi ya topics za kusoma na kwahiyo syllabus hawawezi kwenda pamoja; na kwamba kila Halmshauri isimamie hilo. Kwahiyo, usimamizi huu ni lazima uzingatiwe

Mheshimiwa Spika, na tumewapa deadline kufikia tarehe 31 mwezi huu wa kwanza wanafunzi wote wawe wamekwenda shule. Kwahiyo tufanye subira mpaka tarehe 31 tupate taarifa, inawezekana pia kuna wasiwasi wa awali, kwamba wanafunzi wengi hawajaenda lakini kutokana na maelekezo tuliyoyatoa, na muda tuliowapa mpaka tarehe 31 unaweza ukawa umekamilika; kwahiyo baada ya tarehe 31 tutatoa taarifa na swali lako litapata majibu mazuri. Kwa sasa msimamo wa serikali ni kuwapeleka wanafunzi wetu wote wanaosajiliwa. Awe anakwenda chekechea, anaingia darasa la kwanza, anaingia kidato cha kwanza, anaingia kidato cha tano, wote lazima waingie darasani kwa wakati na waanze kusoma kadiri syllabus inavyoeleza. Ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister