Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 3 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 2 2020-01-30

Name

Munde Abdallah Tambwe

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii na mimi niweze kuuliza swali kwa Waziri Mkuu. Mheshimiwa Waziri Mkuu Tanzania ni nchi ambayo inaendelea kwa kasi kubwa katika uchumi wa viwanda hususan Serikali ya Rais Joseph John Pombe Magufuli; ambayo imejikita sana kwenye uchumi wa viwanda mpaka ambapo muda huu tunaviwanda zaidi ya 3,700; si jambo dogo. Lakini maendeleo haya ya kasi kubwa ya uchumi yanabidi yaendane na maendeleo ya wananchi. Je Mheshimiwa Waziri Mkuu mnamkakati gani kama Serikali kuhakikisha maendeleo ya kasi kubwa ya uchumi wa viwanda na kuhakikisha maendeleo ya watu vinakwenda sambamba?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Munde Mbunge wa Mkoa wa Tabora kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali yetu inayoongozwa na Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli imeelekeza kuboresha uchumi wake kupitia viwanda pia. Viwanda hivi baada ya kufanya study ya kuweza kuwafikia Watanzania na kuwapatia maendeleo; tunajua mchango wa viwanda popote palipo na kiwanda lazima kitumie mali ghafi na malighafi hizi ziko kwenye sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi, maliasili pia hata madini. Kwa hiyo panapokuwa na kiwanda kinachohitaji malighafi hiyo obvious malighafi hiyo na wale wote wanaozalisha malighafi hiyo watakuwa wameboreshewa uchumi wao kwasababu tayari wanauhakika wa soko pale kwenye kiwanda. Ule uhakika wa soko tayari tunapeleka tunaunganisha manufaa ya uwepo wa kiwanda na hali na maisha ya wananchi wanaopata huduma hiyo kwenye kiwanda hicho.

Lakini viwanda hivi navyo vinavyofaida nyingine nyingi ambazo pia tunaunganisha na maendeleo ya mtu mmoja mmoja. Leo mgogoro wetu wa kukosekana kwa ajira, Rais weru alikuwa na muono wa mbali sana. Viwanda hivi sasa vinaajiri Watanzania kwenye maeneo kilimo; na wote mnajua kwamba hata kwenye ajira tumeweka tumebana kidogo mianya ya watu wengi kutoka nje kuajiriwa badala yake tumefungua milango kuajiriwa kwa Watanzania wenyewe. Kwahiyo viwanda vingi vinaajiri Watanzania kwahiyo angalau tumepunguza mgogoro wa kutokuwepo kwa ajira.

Lakini mbili kwa uwepo wa viwanda hivi tunapata kodi, kodi hizi ndizo ambazo zinatuwezesha leo kujenga zahanati, kujenga shule, kujenga miundombinu ya barabara na maeneo mengine. Kwahiyo tunaufanya uchumi wa viwanda tunaupeleka pia kwa jamii. Hatujaishia hapo tu viwanda hivi sasa vinazalisha malighafi ambazo leo tunakuwa na uhakika nazo kwa uzalishaji wake na ubora wake, lakini pia kwa gharama nafuu na upatikanaji wa karibu kuliko kuagiza vitu kutoka nje zaidi. Kwahiyo tumetengeneza uwepo wa soko la ndani la uhakika ambako sasa uchumi huu tunaupeleka sasa kwa wananchi. Kwahiyo kufungamanisha kwa viwanda na uchumi wa mtu mmoja mmoja hasa kumejikita kwenye maeneo hayo, namna ambavyo viwanda vinaleta tija kwa uwepo wake na kwa wananchi walioko jirani na kwa Tanzania nzima. Tunaendelea kuhamasisha ujenzi wa viwanda ili watanzania waweze kunufaika na uwepo wa viwanda hivyo.

Mheshimiwa Spika, nataka niwahakikishie Watanzania, tunaendelea kuhamasisha na kuita wawekezaji kutoka nje na ndani ya nchi tuendelee kuwekeza kwenye viwanda ili tuboreshe pia uzalishaji na kupata masoko wa malighafi inayotakiwa viwandani. Ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister