Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 8 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 3 2017-11-16

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kumuuliza swali Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Waziri Mkuu hapa nchini tunazo Sera za Ugatuaji wa Madaraka. Hii Sera ya Ugatuaji wa Madaraka lengo ilikuwa ni kufikisha huduma hizi kwa jamii kwa karibu zaidi na usimamizi wa karibu wa miradi yetu ya maendeleo inayoibuliwa katika Halmashauri zetu na vijiji.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, ili sera hii iweze kutekelezwa ni kwamba Serikali inapeleka pesa nyingi kwenye Halmashauri zetu ili kuweza kutekeleza miradi hiyo na kutoa hizo huduma. Hata hivyo, kada hii, wasimamizi wakubwa wa kwanza kabisa wa fedha hizi ambazo Serikali tunapeleka ni Watendaji wetu wa Vijiji na Watendaji wa Kata.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, sasa hivi nchi yetu inakumbwa na tatizo kubwa sana katika Halmashauri zetu kutokana na uhaba wa Watendaji wa Kata na Watendaji wa Vijiji wakati hao ndiyo tunaowategemea kwamba ndiyo wangekuwa wasimamizi wa kwanza wa fedha hizi.

wali langu ni kwamba mkakati wa Serikali ya Awamu ta Tano unasema nini katika kutatua tatizo hili ambalo limekuwa sugu, linasababisha Halmashauri zetu kupata hati isiyo salama?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kuchauka ambalo limezunguka zunguka lakini msingi wake ni Serikali inatumia utaratibu gani kuhakikisha kwamba kunakuwepo na rasilimali watu ambao pia wataweza kudhibiti rasilimali fedha kama ambavyo nimekuelewa kwa mzunguko mzima wa swali lako.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali imeweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba tunakuwa na watumishi wa kutosha kwenye kada zote. Kwa sasa tunaendelea kushuhudia kupungua kwa rasilimali watu kwenye sekta zetu na hatimaye kusababisha rasilimali fedha hizo kutotunzwa/ kutosimamiwa vizuri. Kwa Serikali ya Awamu ya Tano, jambo hilo linaweza kuwa limetokana na mazoezi mawili ambayo tumeyaendesha; ya kubaini watumishi hewa na watumishi wenye vyeti ambao hawana stahili sahihi ya kufanya kazi walioajiriwa. Sasa zoezi hili limepunguza idadi ya watumishi na ni kweli kwamba tunaweza tukawa tunapeleka fedha halafu zisipate watu wa kuzisimamia vizuri.

Mheshimiwa Spika, kwenye eno hili, Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli ametupa nafasi za ajira zaidi ya 52,000 na tumeanza kuajiri kwa sababu anatupa vibali kadiri tunavyohitaji na tunaendelea kuhakiki kwamba wanaokwenda ni watumishi wenyewe na wamefika vituoni wanafanya kazi yao. Kama ambavyo mmeshuhudia tumeajiri kwenye Sekta ya Elimu, Afya na juzi Majeshi na tunaendelea kuajiri.

Mheshimiwa Spika, sasa kada hizi za Watendaji wa Kata na Vijiji hizi ni kada ambazo pia tumezipa mamlaka halmashauri zenyewe kuajiri pale ambapo wanaona kuna upungufu ili kuziba mapengo haya. Kwa hiyo ni halmashauri yako na Mheshimiwa Mbunge wewe pia ni Mjumbe wa Baraza la Madiwnai pale, kwa hiyo unayo fursa ya kupata takwimu za Watendaji wa Kata na Vijiji waliopo na kujua wangapi wamepungua ili muamue na muweze kuziba ninyi wenyewe pale kwa lengo la kuweza kudhibiti fedha zilizopo na zilizopelekwa kwa ajili ya miradi kwenye ngazi hizo za vijiji.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Additional Question(s) to Prime Minister