Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 3 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 3 2017-11-09

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, naomba nimuulize swali Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu, ni sera ya Serikali kulinda raia na mali zao. Lakini mnamo tarehe 24 na tarehe 25, askari wa FFU katika Kambi ya Ukonga, Mombasa, walifunga barabara wakapiga akina mama, vijana na wazee na wakawatesa sana abiria na kuleta madhara makubwa.

Mheshimiwa Spika, sasa ninaomba nipate tu, na wananchi wangu wasikilize, Serikali inatoa kauli gani juu ya matukio kama haya ambayo yanafanywa na viongozi na vijana ambao kimsingi tunatakiwa tuishi kama ndugu na kushirikiana kwa ajili ya kulinda raia na mali zetu? Ahsante.

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Waitara, Mbunge wa Ukonga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tunazo taarifa kwamba pale Ukonga kulikuwa na mgongano mkubwa kati ya Jeshi letu la Polisi na raia, na mgongano huu umesababisha pia kuuawa kwa askari mmoja na watu wengi kupigwa, lakini hatua nzuri zimechukuliwa. Mkuu wetu wa Wilaya ya Ilala, Mheshimiwa Mjema, aliingilia kati na kuchukua hatua ya kuunda tume ambayo inafanya ufuatiliaji kuona chanzo na madhara yaliyojitokeza na wahusika katika jambo hili. Baada ya tume kumaliza kazi yake, ikibainika nani ametenda kosa hatua kali zitachukuliwa.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu wewe ni Mbunge wa eneo lile lazima utashirikishwa pia katika kupata taarifa za matokeo ya tume iliyoundwa na Mkuu wetu wa Wilaya ya Ilala, Mama Sophia Mjema.

Additional Question(s) to Prime Minister