Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to Primary Questions by Hon. Selemani Moshi Kakoso (1 total)

MHE. MOSHI S. KAKOSO (K.n.y. MHE. JUMA S. NKAMIA) aliuliza:-
Wilaya ya Chemba haina hospitali jambo linalowalazimu wananchi wake zaidi ya laki tatu kwenda kupata huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Kondoa.
Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuhakikisha Wilaya hiyo inapata hospitali?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juma Selemani Nkamia, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Chemba imetenga kwa kupima eneo la ekari 23.7 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa hospitali ya Wilaya. Katika mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri imeomba maombi maalum ya shilingi bilioni mbili ili kuanza ujenzi wa hospitali hiyo. Aidha, upo mpango wa kukopa kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ili kufanikisha ujenzi wa hospitali hiyo kwa awamu. Ofisi ya Rais - TAMISEMI itashirikiana na Halmashauri ya Chemba ili kuhakikisha mipango ya ujenzi wa hospitali hiyo unafanikiwa. (Makofi)