Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe (24 total)

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ili na mimi niweze kuchangia hoja ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Kwanza, napenda niwashukuru wananchi wangu wa Jimbo la Kavuu, kwa kuniamini na mimi nawaambia sitawaangusha tuko pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze na hotuba ya Waziri Mkuu ukurasa wa 15, uwezeshaji wananchi kiuchumi. Katika hili, napenda kwanza niishukuru Serikali yangu kwa kuweza kuanzisha VICOBA na SACCOS ambazo zimekuwa na mchango mkubwa katika kuinua pato la wananchi. Pia napenda nishukuru Chama changu cha Mapinduzi katika Ilani yake ilipokuwa inajinadi kuanzisha mfuko wa shilingi milioni 50 katika kila kijiji. Katika hela hizi kutokana na namna tulivyokuwa tunajinadi, basi ziende zikatumike hivyo, kwa makundi mbalimbali ndani ya kila kijiji ambavyo vitakuwa vimesajiliwa na Halmashauri na kutambuliwa kisheria. Kwa sababu tunaelewa katika makundi ya vijana na akina mama tuna asilimia 10 ya kila mapato ya Halmashauri. Kwa Halmashauri ambazo hazifanyi hivyo basi Serikali isimamie.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende ukurasa wa 25 kuhusu Hifadhi ya Mifuko ya Jamii. Mifuko hii imekuwa na michango mikubwa katika shughuli za maendeleo katika kuendeleza Taifa letu kiuchumi. Niwaombe na niiombe Serikali, kwa sababu tumekuwa tunawahimiza wananchi wajiunge na Mifuko ya Bima ya Afya na kwa sababu hii Mifuko ya Bima ya Afya inachangia katika maendeleo ikajenge zahanati kwenye vijiji, ikatusaidie hata kupata vifaa tiba katika zahanati zetu na vituo vya afya. Kwa nini natamka hivyo? Hii itatusaidia kujenga imani kati ya wananchi na hii mifuko na hivyo itakuwa rahisi kwa wananchi kujiunga na mifuko hii kwa sababu wataona wananufaika, wataona faida yake na watajiunga kwa urahisi. Kwa hiyo, niwaombe NHIF watusaidie kuwekeza katika zahanati zetu na vituo vya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee suala la mifugo hususani suala la migogoro, nafikiri Serikali imepokea malalamiko mbalimbali kutoka katika kila Jimbo kuhusiana na migogoro ya ardhi. Naongelea katika Jimbo langu kuhusiana na migogoro inayojitokeza kati ya wafugaji na mipaka ya Hifadhi ya Taifa hususani Hifadhi ya Katavi. Migogoro imekuwa ikiwasilishwa mara kwa mara. Serikali hii nafahamu ni makini kweli kweli na inafanya kazi kweli kweli na Mbunge mwenyewe Kikwembe anafanya kazi kweli kweli, kutokana na namna tulivyojipangia kutatua hii migogoro, niombe sasa baada ya Bunge hili, baada ya Bajeti, Serikali ikaanze kutatua migogoro kati ya wakulima na wafugaji, kati ya wananchi wanaoishi mipakani na Hifadhi za Taifa, tuondokane na kero hii ili tuweze kufanya shughuli za maendeleo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba niongelee suala la uwekezaji kwa wananchi. Tunakuwa na uwekezaji mzuri ambao unalenga kukuza pato la mwananchi. Napenda niongelee uwekezaji katika masuala la mawasiliano. Mawasiliano ni kitu cha msingi sana, napenda niishukuru Serikali yangu kutoka awamu iliyopita mpaka hii tuliyonayo kwa kuwezesha mawasiliano vijijini kupitia mtandao wa Halotel, Mkoa wa Katavi sasa hivi tuna 100% ya mawasiliano. Ninachopenda kusema tumekuwa na migogoro kati ya wawekezaji hasa wanapokwenda kuweka minara. Nafahamu Halotel imekuja kutatua tatizo ambalo makampuni mengine yalishindwa kwa sababu yanajiendesha kibiashara zaidi lakini Halotel wamefanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, niiombe Serikali kupunguza matatizo ambayo yanajitokeza hivi sasa kati ya wawekezaji hawa wa Halotel na wananchi katika maeneo husika, waweze kuangalia namna watakavyoweza kutoa zile tozo. Siamini kabisa kwamba hawa Halotel wanatoa huduma bure na sisi tunalipia hizo huduma.
Kwa hiyo, huu mpango wa kusema shilingi 30,000 kwa mwezi katika eneo husika, kwa kweli bado si sahihi, naomba Serikali waliangalie hilo. Pamoja na kwamba wametusaidia kiasi cha kutosha na nawapongeza sana Serikali kwa kuwaleta hawa Wavietnam ambao wamekuwa mkombozi katika mawasiliano vijijini lakini naomba tuangalie upya hizo tozo kuondoa migongano kati yao na wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee upande wa barabara. Naishukuru Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi, Bunge lililopita Mheshimiwa Rais alikuwa Waziri wa Ujenzi. Amejitahidi kwa kadiri ya uwezo wake, tumepata pesa ya kutengeneza barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mpanda – Tabora. Wananchi wa Katavi, Tabora na Kigoma kwa ujumla tunasema ahsante.
Kama ilivyokuwa kwenye mipango ya Serikali iliyopita ya kutengeneza barabara ya lami kutoka Majimoto - Inyonga naomba iwemo ndani ya bajeti kwani sijaiona na Daraja la Kavuu sijaliona na liko kwenye mpango. Kwa hiyo, niombe sana wazingatie kuweka kwenye bajeti hii mipango iliyokuwepo kipindi kilichopita. Si kwa Jimbo la Kavuu tu ambalo ni jipya, niombe katika Majimbo yote mapya, tuwekeeni hata barabara za vumbi ambazo zinapitika kwa kuanzia si haba tofauti na ambavyo hatuna barabara kabisa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie suala la reli. Lengo la Serikali ni kutandika reli mpya na nzito zaidi kwa kiwango cha standard gauge. Huu wimbo umekuwa ni wa muda mrefu si chini ya miaka saba iliyopita. Kwa sababu Serikali yetu ni ya hapa kazi tu tunachohitaji ni vitendo. Let us put our ideas into action. Tumechoka na huu wimbo kwenye reli ya kati, tunataka tuone reli ya kati inatengenezwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee suala la maji. Tarehe 20 Aprili nilipata majibu mazuri kutoka Serikalini kwamba kuna pesa imetengwa kwenye kata zangu kwa ajili ya suala hili. Hizo pesa ni za bajeti iliyopita, bajeti itaisha tarehe 30 Juni, niombe pesa hizo zitoke kabla ya bajeti mpya ili tuanze shughuli za kujipatia maji safi na salama.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende ukurasa wa 47, aya ya mwisho inaongelea umeme Gridi ya Taifa. Mkoa wa Katavi ulikuwa kwenye mpango wa kupita Gridi ya Taifa kutoka Biharamulo sijaona kwenye mpango huu. Kwa vile kwenye bajeti iliyopita tulitenga naomba iendelee kuwepo na itekelezwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwenye bajeti iliyopita kulikuwa na suala la generator mbili zilizokuwa zinatoka Belgium kwenye bajeti iliyopita hazijafika Katavi mpaka leo na hivyo kuifanya Mpanda na Katavi kwa ujumla kutokuwa na umeme wa uhakika, na kushusha mapato ya Mkoa. Kwa hiyo, tunaomba kabisa hilo suala la generator hizo mbili nalo lipatiwe majibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru Serikali yangu katika sekta ya elimu kwa kubana matumizi katika shughuli za Bunge lakini isibane tu katika shughuli za Bunge ibane hata kwenye baadhi ya vifungu ambavyo vinasemekana viko kisheria kwenye mafungu ya bajeti mtayaona, kwenye masuala ya simu, magazeti, nyumba, umeme, haitavumilika, haiwezekani milioni nane, milioni 10, milioni 20 zinakwenda kule zirudishwe. Wote tunafunga mikanda, hakuna atakayesema nalipiwa simu kisheria, tunafunga mikanda. Kwa hiyo, wote tufunge mikanda tuiweke pesa kwenye maendeleo ya maji, tupeleke elimu, tupeleke kwenye barabara na tupeleke afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee suala la Ustawishwaji Makao Makuu Dodoma. Hili suala limekuwa ni tatizo kwa wananchi wote wanaokaa Dodoma, ni shida, ni taabu, ni kero isiyokuwa na majibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, CDA wana mambo yao, Manispaa wana mambo yao, mwananchi unalipa kodi zaidi ya mara mbili, kunakuwa na mgongano wa kazi kati ya Manispaa na CDA. CDA wanapandisha kodi, una kiwanja ulikuwa unalipa shilingi 97,000 leo unalipia ile kodi mara nne yake, si sahihi. Lazima iletwe sheria kwa niaba ya wananchi wa Tanzania tuweze kujadili hili suala. (Makofi)
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa muda wako umekwisha.
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru na naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ili niweze kuchangia katika hotuba hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende moja kwa moja kuwashukuru waandaaji, maana yake kuandaa hizi taarifa nayo ni shughuli. Kwa hiyo, wameweza kutuandalia vitu ambavyo na sisi tumeweza kuviperuzi na sasa tunaweza tukatoa michango yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, napenda niwashukuru wananchi wangu wa Jimbo la Kavuu kwa uvumilivu wao na ushirikiano wao wanaonipatia mimi Mbunge wao wa Jimbo la Kavuu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaendelea na hotuba, naomba niwaombe wafugaji wangu wa Kata ya Ikuba, Kijiji cha Kikulwe na Ikulwe (Maji Moto), wawe na uvumilivu wa kuhamisha mifugo yao vizuri pindi watakapooneshwa maeneo ya kupeleka mifugo hiyo. Niiombe Serikali kupitia tangazo lake la kuwaambia watoke mita 500 kwenye vyanzo vya maji, niliomba kuchangia katika Wizara ya Kilimo na Mifugo, nikawaambia waende wakatengeneze malambo, ni ahadi ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakatengeneze malambo kule ili wafugaji wale wa Kata ya Ikuba wasiweze kwenda kwenye ule mto wanaowaambia waondoke mita 500 na wanawafukuza bila kuwapa mbadala wa maeneo ya kwenda. Wizara na Serikali wanasema wametenga maeneo Katavi, sasa wanawaondoa hawajawapeleka kule, leo wakikataa kutoka kule watasema wanaleta vurugu, hapana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hawatawaonesha maeneo ya kwenda kuweka mifugo yao maana yake ni nini? Sasa hivi wakulima wanavuna, maana yake watatoka pale walipo wanaenda kuongeza shughuli na vita nyingine na wakulima. Wamenitatulia tatizo lile lakini sasa wameongeza tatizo lingine jana. Leo hii ninavyoongea hapa wakulima na wafugaji kule ni shughuli kubwa, ni vita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Profesa Maghembe akitoka hapo saa saba kapige simu kule uwaeleze waache vurugu zile. Mkuu wa Mkoa na Serikali ya Mkoa imetoa tamko kule kuwa-disturb wafugaji lakini wakulima hawajatoa mazao yao shambani, kwa hiyo leo wanataka kuleta fujo juu ya fujo, jambo ambalo sitalikubali. Tumesema hapa, tunataka kutatua matatizo na si kuongeza matatizo. Haya ni matatizo ambayo yanatokana na mbuga ya Katavi pamoja na hiki kijiji ninachokisema Kata ya Ikuba pamoja na Kata ya Chamalendi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hizo mita 500 mkulima wa kawaida, mfugaji wa kawaida anazipimaje? Waende wakaweke alama, wakachimbe malambo waache kwenda kwenye ule mto, hakuna maji, kila siku hapa ni kilio na tunapiga kelele hapa Wabunge wote wanazungumzia tatizo hili la maji. Sasa kama hawana maji wakanyweshe wapi mifugo yao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakiingia pale kunywesha askari wa TANAPA wanawaswaga wale ng‟ombe kuwapeleka ndani ya mbuga na kuwaua. Jambo ambalo wanawasababishia umaskini wafugaji na wakulima hawa na sisi lengo letu tunasema watu hawa waende kwenye uchumi wa kima cha kati. Tunafikaje kule kama leo sisi wenyewe tunakuwa ndani ya sheria zetu tunakinzana namna ya kuzitekeleza. Naomba waka-harmonize hizo sheria zao na waangalie ni namna gani wanatekeleza hayo majukumu na kwa wakati gani na kama eneo lile limetengwa wawapeleke wale wafugaji kule. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja katika suala lingine na naomba Mheshimiwa Waziri anielewe ni suala la utalii. Kwanza kabisa napenda nimpongeze Mheshimiwa Lucy Owenya jana amechangia vizuri sana kwenye suala zima la utalii, hakuwa bias na upande wao. Utalii imeonekana sasa ni Kaskazini tu, jamani kila siku nasema Mbuga ya Katavi ina wanyama wakubwa kuliko wanyama wote Tanzania. Anayebisha hapa leo aende lakini haitangazwi hata kidogo. Tuna twiga mazeruzeru kule, hakuna mbuga yoyote utawapata, tuna viboko wakubwa hakuna popote utawapata Tanzania nzima. Kwa nini hawatangazi mbuga zingine tumekazana tu na Serengeti, Ngorongoro, Manyara, sana sana tukisema tunakuja kusema hii hapa ya Iringa, kwa nini hatuvuki kwenye mbunga nyingine? Tunapoteza mapato kwa ajili tu ya utangazaji. Naomba hilo suala waliangalie. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, narudi kwenye suala la wahanga katika Operesheni Tokomeza Ujangili. Katika Bunge lililopita Bunge lilitoa maazimio hapa mambo gani yakafanyiwe kazi, mojawapo ikiwa ni pamoja na kuwalipa wahanga ambao kwa namna moja au nyingine hawakuwa majangili bali walikuwa katika utekelezaji wao wa majukumu mbalimbali wakiwemo Watendaji wa Kata na Vijiji na baadhi ya Waheshimiwa Madiwani. Tuliwahi kusema hapa, wapo waliopigwa mpaka kupoteza viungo vyao na tulitoa maazimio wakasema watawalipa fidia. Nataka kujua fidia hiyo imekwenda wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri asiniambie ndiyo kwanza anaingia ofisini, ofisi ipo na shughuli ziko mezani, ukifika ni kuperuzi tu na kuendelea na utaratibu wa kazi. Kwa hiyo, tunaomba hili nalo alitolee ufafanuzi ili wahanga hawa ambao wengine waliweza hata kupoteza watoto wao bila sababu za msingi kutokana na kazi kufanyika bila kufanya utafiti wa kutosha. Kwa hiyo, watu wengi waliumizwa kwa namna moja ama nyingine na tulitoa maamuzi hapa na maazimio kwamba wapatiwe fidia. Kwa hiyo, tunaomba wale wote walioingia katika zoezi hilo bila wao wenyewe kuwa majangili wapatiwe fidia zao na Serikali itupe hapa majibu kwamba wanafanyaje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, narudi kwenye suala langu la Ikuba na Chamalendi, tafadhali sana Mheshimiwa Waziri mpaka saa nane mchana naomba awe amekwishaongea na Serikali ya Mkoa waangalie wale wafugaji wanawapeleka wapi. Sitaki niende kule nikute watu wamechapwa fimbo, watu wameuawa na kwetu kule unajua wakianza kupigana, ni mapanga na fimbo, hatutaki tusababishe vita kati ya wakulima na wafugaji. Tumeoana na tumeingiliana katika familia, hatutaki sasa tuanze kuwa na demarcation kati ya mkulima na mfugaji. Sisi wote ni wamoja, tuna namna tunavyoishi kule, mkianza kuleta vurugu zile mkulima hatakubali mwingine aingize ng‟ombe mle wala mwenye ng‟ombe hatakubali ng‟ombe wake wauawe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nachelea kusema majipu yapo ndani ya TANAPA, maaskari wale wa mbugani wana mipango fulani. Haiwezekani askari anaajiriwa ndani ya mwezi mmoja ni milionea, ndani ya miezi miwili siyo mwenzio, lazima kuna namna inayofanyika kule, naomba wafanye utafiti. Haiwezekani hata kidogo mtu mmoja kapigiwa ng‟ombe 80, ng‟ombe 70, ng‟ombe 200 kwa kosa lipi? Sheria haisemi hivyo, sheria inasema hata kama wale ng‟ombe wamewakamata basi walipishwe faini. Kama faini zao wanaona ndogo walete sheria hapa tufanye marekebisho, tuone tunafanya nini kupata mapato na kuongeza uchumi katika Halmashauri zetu lakini kuwaonea wafugaji, kuwaonea wakulima kwa kweli ni kosa la jinai.
Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ili niweze kuchangia hoja iliyoko mbele yetu. Kwanza kabisa napenda kuishukuru Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna ambavyo amekuwa akitekeleza majukumu ambayo yamekuwa yakitatua shida mbalimbali zinazowagusa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili napenda niishukuru Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa namna ya kipekee ambayo imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na mimi Mbunge wa Jimbo la Kavuu kwa namna ambavyo wamekuwa wakijaribu kutatua matatizo ya wananchi wangu. Napenda kabisa niishukuru Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya TAMISEMI kwa kuweza kunipatia ambulance ambayo inaweza ikafanya shunting kati ya vituo viwili vya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua jiografia ya Jimbo langu bado siyo nzuri, kwa hiyo, nikuombe Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI uniongezee ambulance itakayofanana na miundombinu ambayo nimepata. Hata hivyo, nashukuru sana kwa kile nilichokipata ambacho ni ambulance ambayo itanisaidia kutoka kituo cha afya cha Kibaoni kwenda kituo cha afya cha Mamba. (Makofi)

Mheshimiwa wenyekiti, napenda niendelee kushukuru kwa kuwa wameweza kuniwezesha kituo changu cha afya cha Kibaoni ambacho sasa kinaelekea kwisha lakini niwaombe katika Jimbo langu la Kavuu nina vituo vya afya vitatu; nina kituo cha afya cha Mamba na kingine cha Mwamapuli ambacho wananchi wameanza kujitolea namna ambavyo ya kuweza kutatua matatizo ya afya kutokana na jiografia ilivyokaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Waziri atuongezee nguvu katika vituo hivi. Nimshukuru kwa namna ya pekee Dkt. Zainab ambaye aliweza kutupa mawazo akishirikiana na Katibu Mkuu Engineer Iyombe namna ambavyo tunaweza tukaanzisha hospitali ya Halmashauri ya Wilaya katika Jimbo la Kavuu na niwashukuru Wizara hii wametupatia kibali na sasa tunakwenda kujenga hospitali ya Wilaya. Ahsanteni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee lingine limekuwa likiongelewa sana na limeongelewa na baadhi ya Wabunge hata jana kuhusu mchango wa chakula mashuleni. Ni kweli kwamba chakula mashuleni kinapunguza utoro, ni kweli kwamba chakula mashuleni kinasaidia wanafunzi kuwepo mashuleni na kinaongeza kiwango cha ufaulu. Kwa hiyo, niwaombe Waheshimiwa Wabunge tuendelee kuwaomba wananchi wetu waendelee kuchangia kwa maana ya kwamba ni jambo lenye tija katika kizazi chetu kijacho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano tu; Mbunge wao wananchi wangu wa Jimbo la kavuu nimeweza kuchangia karibu hekari 30 kwa maana kwamba kila shule inapata hekari moja ya chakula na sasa tumeanza kuvuna. Kwa hiyo ni mchango wangu kwa chakula kwa maana naelewa umuhimu wa chakula mashuleni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishukuru Serikali na niishukuru halmashauri yangu, Halmashauri ya Mpingwe imekuwa ni halmashauri ya pili kati ya halmashauri 185 ambayo imekuwa ikifanya vizuri katika kutenga asilimia 10 kwa maana kwamba asilimia tano ya akinamama na asilimia tano ya vijana. Kwa hiyo, niwaombe, niko vizuri na Mkurugenzi wangu na nafanya naye kazi vizuri sana na anasimamia miradi vizuri mno.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba, kama watafanya reshuffle mimi Mkurugenzi wangu waniachie pale, yuko vizuri. Kama kuna Wakurugenzi wengine hawako vizuri mimi wa kwangu yuko vizuri, anasimamia miradi vizuri, milioni 400 walizonipa kituo cha Kibaoni pale cha afya zimesimamiwa vizuri, pesa za Jimbo zinasimamiwa vizuri. Kwa hiyo, kazi inakwenda na maendeleo tunayaona na Jimbo la Kavuu sasa linaonesha mabadiliko chini ya Dkt. Pudenciana Kikwembe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishukuru Serikali kwa namna ya pekee ilivyoondoa riba katika ule mkopo wa asilimia 10 kwa akinamama na vijana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nirudi kwa TARURA. TARURA ni chombo ambacho kwa malengo yake ni mazuri sana, lakini naomba kiongezewe pesa, kiongezewe watalaam. Kutokana na mvua hizi zinazonyesha nilikwenda ofisini kwa Mheshimiwa Waziri na nikapeleka maombi yangu binafsi, maombi rasmi, maombi special kwa namna ambavyo sasa Jimboni kwangu hakuna hata njia moja inayopitika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemwomba pesa ya kutengeneza box culvert ya Mwamapuli-Majimoto ambayo inagharimu karibu milioni 160, nimeomba Majimoto daraja jipya la Msadya ambalo kwa wale wanaongalia vyombo vya habari waliniona nikienda kulitembelea. Sasa hivi kwa hela waliyotupatia nashukuru limeanza kupitika angalau wagonjwa wanaweza kwenda kutibiwa kituo cha afya kingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pesa takribani bilioni 1.7 kwa ajili ya kujenga daraja lingine, kwa sababu daraja lile linahudumia karibu Kata tano kwa ajili ya akinamama na watoto wanaokwenda hospitali. Kwa hiyo, ni maombi rasmi, naomba niyalete kwako hapa na kwa sababu nilishayaleta kwa maandishi naomba mnisaidie kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba drift mbili kati ya Ntibili na Kikonko ambako kumepata mafuriko na hivi ninavyoongea mvua bado zinaendelea, zimenyesha karibu siku nne mfululizo. Naomba pia box culvert kati ya Kata ya Mamba na Makuyugu ambayo inaweza kugharimu pia milioni 160.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia culvert ya Kibaoni-Chamalendi ambako pia barabara imekatika ambayo ni barabara moja hiyo hiyo inayoungnisha kwenda kwenye kituo cha afya cha Kibaoni. Naomba pia culvert lingine la Mabambasi kupitia Mwamapuli ambalo pia linaunganisha barabara hiyo hiyo kwenda kwenye Kata ya Kibaoni ambayo inakwenda kwenye kituo cha afya ambacho watu wanatumia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee suala la watumishi, watumishi wamekuwa wengi wakistaafu hawapati haki zao, kwa mfano, tuna wastaafu wa Magereza na Mahakama wapatao karibu 200 waliostaafu tarehe 1 Julai, mpaka leo hawjaalipwa haki zao kwa hiyo tulikuwa tunaomba walipwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwa watumishi Walimu; Walimu wamekuwa kama ni wanyanyaswaji kwa sababu hawapandishwi vyeo vyao, hawalipwi pesa zao wanapokwenda likizo, hawalipwi pesa zao wanapohamishwa. Kwa hiyo, naomba malipo yao kwa kweli kwa mwaka huu yatiliwe mkazo. Walimu wetu ni wachache katika vituo vyetu, sasa tunapozidi kuwadidimiza, tunawapunguzia morally ya kazi kwa kweli naomba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee lingine; Mwalimu anapotaka kuhama tunasema atafute nafasi eneo mbadala ili aweze kuhamishwa. Sasa unakuta kuna mwingine kaolewa ama mwingine kaoa kule mnakompeleka hana mume, hana mke, mnachotarajia nini? Kwa hiyo, niwaombe kama mume anataka kumfuata mkewe au mke anataka kumfuata mume wake basi waruhusiwe kwa sababu tunajua maambukizi mapya ya UKIMWI sasa hivi ni mengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunapowaachanisha vile inakuwa ni rahisi kuwaweka kwenye mitego ambayo wanaweza wakapata maambukizi. Kwa hiyo, tunaomba muwalipe malipo yao ya uhamisho na mambo yao mengine ambayo wamekuwa wakidai hasa wanapokuwa pia wanakwenda kwenye matibabu ambayo yako nje ya utaratibu wa bima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba sana suala la Walimu, kwa kweli ni tatizo. Mimi ni Mwalimu pamoja na kwamba ni Mbunge, lakini ninapokwenda Jimboni kwangu mimi naingia darasani kufundisha. Nafundisha kwa sababu ya uhaba wa Walimu. Kwa hiyo niwaombe sana, katika kasma ijayo ya waajiriwa mtupatie watumishi wa sekta ya afya pamoja na sekta ya ualimu, ni vitu ambavyo tunavihitaji sana hasa katika kuhudumia wagonjwa wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, nahitaji zaidi Madaktari badala ya Makatibu wa Vituo vya Afya. Makatibu wanakaa ofisini na computer, nikipata nurse pale clinic atanisaidia zaidi kuliko Katibu wa Afya. Kwa hiyo, naomba hata tunapofanya allocation ya watumishi, tuangalie; Kituo changu cha Kibaoni kina Makatibu wa Afya watatu wa nini?

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naunga mkono hoja kwa asilimia zote.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ili nami niweze kuchangia katika hoja hii iliyoko hapa mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, napenda nianze na dhima ya Wizara. Dhima ya Wizara ni pamoja na kuendeleza utalii kwa manufaa ya Taifa. Naomba nianzie hapa hapa kwenye kuendeleza utalii kwa manufaa ya Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mradi wa kuendeleza utalii Kanda ya Kusini ambao unajumuisha Udzungwa, Ruaha, Mikumi, Selou na uligunduliwa pale Iringa. Naomba Serikali na Wizara inijibu, Katavi ipo wapi? Kwa nini haiko kwenye mradi huu? Katavi tuna kiwanja cha ndege suala ni kuongeza, zimebaki kilomita mbili pia na kuweka taa ili tuweze kukuza uchumi wa kule. Katavi National Park iko wapi? Nataka kujua ina mradi gani ili na sisi tuweze kufaidika na hii hela ya REGROW ambapo imetolewa karibu dola milioni 150 kwa ajili ya kuendeleza utalii Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia niungane na maoni ya Kamati hasa kwenye sera ya ujirani mwema kuhusu huduma za kijamii. Nakumbuka niliwahi kuuliza swali hapa kuhusiana na vijiji vyangu vinavyopakana na mbuga ya National Park pamoja reserve ya Rukwa Rekwati. Vijiji hivi vimepakana na mto ambao wanautumia lakini watendaji wengine ambao si waaminifu wamekuwa wakitumia advantage ya kuwaumiza wananchi kutokana na mto huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nikaomba katika Kata yangu ama Kijiji changu cha Luchima kilichopo Kata ya Majimoto ambako kuna Vitongoji vya Luchima, Masangano, Ilunda, King’anda, Kawanga na Kiwanjani vyenye wananchi wapatao 7,571 wapatiwe visima vya maji kama ambavyo Kamati imeshauri ili tuweze kuondoa hiyo migogoro. Baada ya kufanya hivyo tuone ni askari wa TANAPA ama hawa TAWA ndio wenye matatizo na wananchi ama wananchi ndiyo wenye matatizo wanaoingia ndani ya reserve.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Kijiji cha Ikulwe ambako kuna Kitongoji cha Ikulwe A, Ikulwe B, Madulu, Isimba na Mgoroka na kuna wananchi wapatao 5,562. Kwa hiyo, niombe sana tufanye kama Kamati ilivyoshauri ili tuweze kuondoa migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza ambapo wananchi wamekuwa wakipigwa na kuumizwa bila sababu wakati mnakuja kuwapa kifuta jasho ambacho hakifanani wala hakilingani na kiungo chake cha mwili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini naomba niongelee kuhusu suala hilo hilo la watendaji ambapo wamekuwa wakiwaumiza wananchi. Nina mwananchi wangu nimewaambia kesi wapeleke polisi na mahakamani, ameuawa au amepotea maana haonekani katika Reserve ya Rukwa Rukwati. Kati ya tarehe 15-16 Aprili, alipotea na nguo zake zikapatikana kisa ng’ombe zilikwenda kunywa maji pale na hawa watu wa TAWA nafikiri wanalifahamu hili suala vizuri sana. Mwingine alipigwa risasi kwenye paja. Huyu mtu ambaye amepotea anaitwa Seme Mahila. Kwa hiyo, tunaomba kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Ndani tujue ukweli uko wapi kuhusiana na tatizo hili ambalo limejitokeza katika Kata ya Mwamapuli, Kijiji cha Ukingwaminzi. Kwa hiyo, naomba sana huyu mtu tupate taarifa zake na Serikali iingilie kati ili tuweze kujua watu gani wenye makosa, ni watendaji ama ni wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee suala lingine ambalo limekuwa likilikumba Jimbo langu la Kavuu. Katika Jimbo langu la Kavuu sehemu tunayoweza kuchimba kifusi ni ndani ya National Park. Kwa hiyo, niwaombe sana kwa maendeleo ya wananchi wangu na jimbo langu ambalo ni jipya, hawa watu wa TANAPA na Wizara hii ya Maliasili washirikiane na halmashauri ili tuweze kupata vifusi kwa ajili ya kuweza kutengeneza barabara zetu. Tumekuwa na tatizo la kupata kifusi na sehemu tunayoweza kupata ni ndani ya National Park eneo la Kibaoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwaombe sana mnaweza kushirikiana na halmashauri kwa karibu ili tuweze kutengeneza barabara zetu angalau ziwe za kwiango cha changarawe tuweze kupita ama udongo kwa sababu barabara zangu hazipitiki. Najua ni sheria, huruhusiwi kuingia ndani ya National Park au kwenye reserve area lakini naomba kwa kutumia vigezo hivyo hivyo kwamba Serikali ni moja basi tushirikiane tuone tunatatua vipi matatizo ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nije katika sekta ya wanyamapori. Katika sekta hii ukisoma hotuba na hata ripoti ya Kamati wanazungumzia kuwalinda wanyama ambao wako hatarini kupotea kama faru na tembo. Naomba nitoe mfano wa tembo, tunasema wako hatarini kupotea lakini kila siku tunalalamika tembo wanavamia mashamba. Kwangu hivi vijiji vyote nilivyovitaja saa hizi sina mahindi, tembo wamevamia na wako wengi, mimi nasema wako wengi ndiyo maana wanakwenda kule. Je, kwa nini tusifanye uratatibu wa kuwavuna na hiyo nyama ikaliwa na wananchi ili tuwapunguze badala ya kusema tuweke pilipili, hivi nani ataweka mwanzo wa Jimbo mpaka mwisho? Hiyo pilipili unaiagiza kutoka wapi? Tunaanza kuilima lini ili huyo tembo akimbie? Je, wananchi wote sasa tuache kulima tufuge nyuki pembeni ya reserve areas? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kuna mbadala ambao hata zamani wazee wetu walikuwa wakiutumia badala ya haya mambo ya vitalu mnayobadilisha sheria kila siku na matamko, tulisema hapa vitalu viondolewe ndiyo chanzo cha ujangili lakini tena mmerudisha. Wananchi zamani walikuwa wanapewa leseni wanawinda na wakawa na mapenzi mema na mbuga zao. Sasa leo mnawapa watu wachache ambao hao hao kwa kushirikiana na watendaji ambao si waaminifu ndiyo wanaopiga wananchi wetu na wanavuta wale ng’ombe kwa makubaliano wanaziingiza katika mbuga zao na kuanza kuzipiga risasi na kuwadai wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi naomba tutafute njia mbadala, hatuwezi miaka yote tukawaweka tembo, tutashindana nao, tutaishi nao vipi? Hatuwezi kuishi nao kwenye vijiji ambavyo tunapakana navyo. Kwa hiyo, niwaombeni sana taratibu zilikuwepo na wanyama walikuwepo na tulikuwa tunaishi nao, sasa kwa nini tunaanza kuja na vitu ambavyo vinaanza kutuletea shida. Wananchi wanaweza kabisa wakavuna tembo kwa utaratibu ambao mmejiwekea wenyewe kama Serikali. Nyama ile ikaliwa na wale tembo wakapungua wasilete tabu kwenye maeneo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, mimi napenda kuishukuru Serikali yangu kwa kuendelea kuagiza ndege, naamini zitatumika katika kutangaza utalii wetu. Kwa hiyo, naomba sasa hizo ndege zinazoagizwa na Katavi zifike ili ziweze kuufungua mkoa ule pamoja na Mikoa
ya Kigoma, Iringa na huko Ruvuma, itaweza kutuunganisha vizuri sana. Kwa hiyo, mimi niwaombe Kiwanja cha Ndege cha Mpanda kitatusaidia sana kama mtakifungua ili kuweza kukuza utalii katika Mbuga yetu ya Katavi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilishawaambia kwamba ile mbuga ni very unique, ina wanyama unique kama watu wake wenyewe walivyo unique. Kwa hiyo, niwaombe sana muitangaze mbuga hii. Tuna twiga zeruzeru tunamwita Wamweru, nyie mlishaona twiga zeruzeru? Hakuna, hayupo mbuga yote tembea utamkuta Katavi na ukimuona una bahati sana. Kwa hiyo, naomba Kiwanja kile cha Ndege cha Mpanda kianze kutumika, kimetumia pesa nyingi sana kutengenezwa, kinapokaa bure haitusaidii tunapoteza mapato, tunapoteza pesa nyingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwaombe sana Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kupitia Wizara hii pamoja na Wizara ya Ujenzi muangalie namna gani kile kiwanja sasa kitaanza kufanya kazi na kuleta watalii katika mbuga yetu ili na sisi tuweze kunufaika na angalau na sisi tuwashangae hata Wazungu maana hatujawahi kuwaona. Tangu Mjerumani na Mrusi walivyoondoka hatujawaona tena. Kwa hiyo, wakianza kuja kule na sisi tutawashangaa kidogo inaweza kutusaidia na sisi tukaji-socialize na tukabadilika. Kwa hiyo, niwaombe sana sana, lazima tuangalie namna ya kukitumia kiwanja hicho na hizi ndege zinazoletwa ili tuweze kuongeza pato la Taifa maana mnasema mbuga za Kusini lakini sijaiona Katavi National Park. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naishukuru Serikali yangu kwa namna ambavyo inavyofanya kazi kuhakikisha inatatua matatizo ya wananchi. Pamoja na kwamba bajeti hii ni ndogo lakini naamini Wizara mnaweza mkafanya yale ambayo mmejipangia. Nawaombeni sana, sana vijiji vyangu nilivyovitaja vipatiwe visima vya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja.
Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi hii ili nami niweze kuchangia Hotuba ya Rais ambayo inalenga moja kwa moja kutatua matatizo ya wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa napenda nitoe shukrani zangu za dhati kwa wananchi wangu wa Jimbo la Kavuu kwa imani kubwa waliyonipatia mpaka nikaweza kufika hapa nilipo, ni kutokana na uchapaji wangu wa kazi hawakuona kwa nini watoe kiongozi kutoka upinzani, wakaona wanipe mimi mwanamama, jimbo jipya, Mbunge mpya mwanamke. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa naomba nianze moja kwa moja kujielekeza kwenye suala la elimu. Huu mpango wa elimu bure naomba niishauri Serikali yangu kwamba mpaka sasa bado una mkanganyiko, haueleweki kwa wazazi, walimu, wakurugenzi na wale wote wanaopaswa kuuelezea huu ukoje mpango, hata leo katika mijadala ya Maswali na Majibu limejitokeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi niombe Serikali ifanye jitihada za makusudi ikauelezee mpango huu vizuri ili wazazi, wananchi waelewe majukumu yao ni yapi na nini kinatakiwa kufanyika mashuleni. Kwa sababu mmeshasema kuna changamoto na upungufu umeonekana basi mimi naamini Serikali itafanya kazi haraka iwezekanavyo kwa sababu tayari shule zimeshafunguliwa ili ziweze kuendelea vizuri na masomo. Naomba suala la elimu bure lifafanuliwe vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hili niliwaahidi wananchi wangu wa Jimbo la Kavuu kwamba nitachangia chakula mashuleni. Nawaomba wale wote wanaopeleka propaganda hizi kwamba niliomba kwa sababu ya kupata Ubunge si kweli. Mimi ni mwalimu na najua maana ya elimu na nawahakikishia Wanakavuu ahadi zangu zote nitatekeleza kwa sababu ziko ndani ya uwezo wangu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende katika hotuba ya Mheshimiwa Rais ukurasa wa 11 inapoongelea kuunganisha barabara, Miji Mikuu ya Wilaya na Mikoa. Ukanda wa kwetu kule Rukwa, Katavi, Kigoma, Tabora bado barabara zetu hazijakaa vizuri. Barabara za ndani kati ya wilaya na wilaya bado hazijakaa vizuri. Naliongea hili na naomba Waziri wa Ujenzi kama yupo, nimeambiwa amekwenda kwenye dharura Kilombero lakini Serikali ipo, naomba ichukue hatua za dharura.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo langu hakuna mawasiliano kati ya Kata ya Ikuba, Chamalendi, Majimoto mpaka Mbede. Hivi ninavyoongea hakuna mawasiliano yoyote na ni eneo kubwa ambalo lina wananchi wa kutosha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba Serikali ichukue hatua za dharura, waende wakaangalie, sina madaraja pale, madaraja manne yameporomoka kwa hiyo wananchi hawana mawasiliano.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu limetamkwa ndani ya Ilani na ndani ya mpango wa kutatua matatizo ya wananchi, naomba basi Serikali ijitahidi kwa kadri inavyoweza kuunganisha barabara za Mikoa, za Wilaya na maeneo mengine muhimu ya biashara. Nilishachangia katika Bunge lililopita, tutakapoweza kuunganisha barabara mpaka Kahama tutaweza kuuza mpunga na mahindi yetu sisi watu wa Katavi mpaka Darfur wanakopigana vita, hatutakuwa na shida tena ya soko la mazao yetu. Kwa hiyo, niwaombe kabisa mlichukulie kwa undani wake suala hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuipongeza Serikali yangu kwa namna ya pekee ambavyo imejitahidi kusambaza umeme vijijini. Niiombe tu sasa, kasoro ndogo ndogo zipo hasa kwenye nguzo. Nguzo zile ni nyembamba sana, nyingine jamani hata mguu wangu ni mnene. Zile nguzi nyingine hazina hata kamba za ku-support hivyo nyingi zimelala, mradi ni mzuri sana. Mheshimiwa Waziri Muhongo najua uko hapa, tumekuwa tukishirikana mara nyingi katika kubadilishana mawazo, kule kwetu mvua ni nyingi mno, naomba mtuletee nguzo nzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo ni uwekaji wa nguzo zile, kijiji kinakuwa mbali nguzo inakuwa sehemu nyingine. Naomba wale mawakala wa REA kupitia kurugenzi husika ndani ya Wizara wafanye utafiti, waonane na watendaji wa maeneo husika kabla ya kuanza kuweka zile nguzo. Najua unakuja tu umeelekezwa, sasa sisi siyo robot, lazima tufanye mawasiliano na tuone hiki tunachokifanya hatupotezi pesa sanasana kinakwenda kulenga wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naongea hilo kwa sababu kwangu mimi kutoka Milumba mpaka Manga kwenda Kibaoni nguzo zimewekwa karibu na Mbuga ya Katavi ambako wananchi hawaruhusiwi kwenda kule na kijiji kiko upande wa pili. Kwa hiyo, naomba kama hilo linawezekana muongee na mkandarasi aliyepo kule aweze kuzihamisha nguzo hizo. Najua itakuwa ni gharama kwa sababu alipewa ushauri akawa mjeuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la migogoro ya ardhi limeongelewa. Naomba Wizara ya Ardhi na Maliasili wafike kule kwangu kwani zaidi ya kata sita zinapakana na Mbuga ya Katavi na misitu ya hifadhi. Ndugu zangu wa Kavuu ni wafugaji na wakulima, wana ng‟ombe wengi ambao wanapitiliza wanakwenda mpaka mbugani. Nakumbuka Mheshimiwa Rais alipofungua kampeni kwangu alianzia Majimoto, alitamka, kama TANAPA ama askari wa TANAPA wanakamata ng‟ombe wale hawaruhusiwi kuwapiga risasi. Tunapowaua wale ng‟ombe tunawatia hasara wale wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, niiombe Serikali sasa, kama ile sheria ya kutoza faini labda imekuwa ni ndogo basi bora tukaongeza faini lakini wale ng‟ombe wakamatwe wakiwa wazima tuwatoze faini ili itusaidie sisi kufanya kazi. Utakamata ng‟ombe 70 unaua ng‟ombe 70 au mwenye ng‟ombe anaweza kuja akakwambia ng‟ombe wangu ni 500, sasa ukiwakamata wakiwa wazima ni rahisi kuwaangalia na kuwa-identify ukajua ni ng‟ombe wangapi wamekamatwa na wakatozwa faini. Pia tunaendelea kutoa elimu kwa ndugu zetu wasiingie katika mipaka ya mbuga lakini haya ni matatizo ambapo Bunge lililopita Kamati iliundwa kwa ajili ya kuyashughulikia. Nimuombe Mheshimiwa Rais ashughulikie migogoro hii haraka iwezekanavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja kwenye suala la afya hasa katika kuwahamasisha wananchi kukata bima za afya. Tuna mifuko ya aina mbalimbali, tuna ule mfuko wa CHF ambao tunawahamasisha wananchi wajiunge. Kitu kinachojitokeza na changamoto iliyopo katika mfuko huu ni kwamba kama nimejiandikisha Kata ya Majimoto siwezi kutibiwa Kata ya Usevya, kama nimejiandikisha Usevya siwezi kutibiwa Kata ya Mamba, kwa maana mfuko ule unakubana pale ulipojiandikishia tu na ugonjwa hauwezi kukuambia utakupata pale ulipo. Mimi naweza kuwa nimetoka Mamba nimekwenda Mpanda Mjini nimeugua, ama nimepata referral kwenda Mpanda Mjini, siwezi kutumia ile kadi. Naomba hili nalo Wizara mliangalie kwa undani tuone tunatatuaje tatizo hili, ni sugu na lina-embarrass wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia naomba niongelee Mfuko wa Jimbo ambao umeongelewa katika hotuba ya Rais ukurasa wa kumi kwamba mfuko huo sasa pesa itapatikana kwa wakati. Naomba Serikali ama Wizara husika isianze kuwa na kigugumizi, tutekeleze hili haraka iwezekanavyo ili tuweze kuwahudumia wananchi wetu kwa wakati muafaka kwa sababu tumesema „Hapa ni Kazi tu‟ na tufanye kazi kweli. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee suala la hati miliki za kimila, naomba Serikali iharakishe kuzitoa kwa wale wanaomiliki mashamba kihalali ili waweze kukopa na wajikwamue kutoka kwenye umaskini, japokuwa baadhi ya benki imekuwa hazizitambui.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niwaombe sana, aidha mtuelekeze ni wapi wananchi wenye zile hati za kimila wanaweza wakapata mikopo ili waweze kujiendeleza badala ya kwenda benki unaambiwa sisi hiki hatukitambui, unataka kuweka dhamana ndugu yako kakamatwa, haitambuliki. Kwa hiyo, niiombe sana Serikali yangu, kwa spirit tuliyonayo mimi naamini tutashinda na naamini tutavuka malengo katika kutatua matatizo ya wananchi, la msingi ni ushirikiano.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu zangu wa Kata ya Usevya, najua hamtaniona sasa hivi lakini baadaye mtaniona, niwaombe sana wazazi wangu wa Kata ya Usevya, hao wazazi wanaowaambia msichangie, mmojawapo anaitwa Bulimba, mwingine Emma Godfrey, najua wanatoka upande gani wa chama, ni walewale wasiotaka kuchangia maendeleo …
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha
kwa muda wa Mzungumzaji)
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba muda kidogo. Wazazi wangu wa Usevya, naomba mtumie busara katika kuchangia suala la elimu.
NAIBU SPIKA: Samahani Mheshimiwa muda wako umekwisha, naomba ukae.
MHE. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipo, ahsante kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kuchangia katika hotuba hii.
Kwanza kabisa napenda niwapongeze walioandaa hotuba hii, na sisi kuweza kutupatia nafasi kuweza kuchangia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nianze na viwanja vya ndege. Ni kweli Serikali imejitahidi kupanga bajeti kwa ajili ya viwanja vya ndege, na tunaomba basi, kwa namna ambavyo mmeweza kupanga, muweze kuvitekeleza, tumekuwa na mipango mingi ambayo hatuiwezi. Napenda kuishukuru Serikali kwa kuweza kutenga kiasi fulani cha fedha kwa kiwanja cha ndege cha Mpanda, mmetenga karibu shilingi milioni 700. Sasa hizi shilingi milioni 700 sijajua zinaenda kutengeneza visima vya mafuta, kuweka taa, ama extension ya zile kilometa mbili. Kwa hiyo, nilikuwa napenda Mheshimiwa Waziri, utakapo kuja uweze kunipatia majibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini naomba niende kwenye suala moja la daraja langu la Kavuu kwenye Jimbo la Kavuu. Sipendi sana kulaumu napenda niseme litekelezwe. Daraja hili la Kavuu si chini ya miaka nane linapangiwa bajeti. Kila bajeti nikisoma ni shilingi bilioni mbili ambazo sijaziona, kila mwaka naona shilingi bilioni mbili ambazo sijui zinapelekwa wapi. Ninaomba Waziri uniambie daraja hili linakwisha lini? Na ningependa liishe mwaka huu na ninapenda pesa hizo zitakapotoka uniambie ili nizifuatilie daraja hilo niweze kulisimamia mwenyewe naona Serikali imeshindwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ninaomba kabisa Waziri pesa hizo pindi zinapotoka uniambie ili niweze kuzifuatilia na wakandarasi wa nchini wapo wanaoweza kufanya kazi nzuri, tunaweza tukakuelekeza; wengine wako Mbeya na Sumbawanga, wanafanya kazi vizuri sana, hasa katika mkoa wa Katavi ambao wanaufahamu na udongo wa kule wanaufahamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo napenda pia nijue kiwango cha lami kitajengwa lini kutoka barabara ya Kibaoni mpaka Kilamatumu kupitia Inyonga, kutoka Inyonga mpaka Ilunde. Ninaongea haya akina mama, watoto, wagonjwa wana teseka kweli kweli; hawafiki maeneo ya matibabu kutokana na ubovu wa barabara. Hakuna magari kwa sababu maeneo yale karibu eneo kubwa ni mbuga na ni hatari kwa kina mama kwa kupanda pikipiki na magari kwa sababu tu ya barabara.
Ninaomba barabara hizo zitengenezwe ili wananchi wa maeneo hayo nao waweze kupata ahueni hasa katika suala zima la kufuata matibabu; ukizingatia kwamba mkoa wetu bado ni mpya na hauna hospitali ya Mkoa wala ya Rufaa, ni lazima twende Bugando, Tabora ama Mbeya. Kwa hiyo lazima tupite hizo barabara na tunapita kwa shida.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunaomba sana ili na sisi tuweze kupata matunda ya nchi yetu kwa sababu tunalipa kodi kama watu wengine wanavyoishi mijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nije kwenye suala la bandari, naongelea gati la Karema. Gati hili limekuwa ni wimbo, meli ya MV Liemba imetoka kuongelewa hapa, katika bajeti iliyopita ukurasa wa 38 wa kitabu kile mmeongelea ile meli sasa inawekwa kwenye makumbusho, lakini leo humu ninasoma mnasema mmekubaliana na Ujerumani kwamba mnakuja kuitengeneza. Kipi ni kipi wananchi wale wachukue, kwamba meli ile ni nzima ama ni mbovu inafanyiwa marekebisho ama inawekwa makumbusho inaletwa meli nyingine?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini tuweke maisha ya Wananchi wa Ikola, Karema, Kala, Kirando, Kabwe mpaka Kigoma tuyaweke rehani kwa ajili ya meli hii? Kama ni mbovu meli hiyo wekeni, leteni meli mpya wananchi wanataka maendeleo. Ile ni corridor ya biashara, tunaenda Congo, Burundi, Zambia, kama mnaona tatizo kwamba meli kutoka Mpanda mpaka Karema inashindikana, tukarabati barabara/tutengeneze barabara ya kwenda Kasesha, Karema mpaka Kasanga Port ili tuweze kupata na kufanya biashara na wananchi wa mkoa wa Katavi na Rukwa waweze kuuza mazao yao kwa urahisi, ili waweze kujiongezea kipato na waweze kukuza uchumi wao kama Serikali inavyosema, kutoka kima cha chini kwenda kima cha kati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyoMheshimiwa Waziri nafikiri unanisikia, unanielewa, umetoka Katavi juzi na umeona hali halisi ya kule naomba utekeleze hilo hasa daraja la Kavuu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja barabara ya kutoka Kibaoni – Kasansa – Buze – Kiliamatundu na ya Majimoto – Inyonga mpaka Ilunde, ninaomba majibu ya barabara hizo. Tumekuwa tukisema kila siku, na ninapenda nirudie kama wenzangu waliokwishatangulia kusema kuwa hatuna sababu ya kusema tunasubiri barabara fulani ipandishwe daraja, tunapadisha daraja kutoka lipi kwenda lipi? Wananchi ni wale wale, wa level ile ile, haki yao ni sawa. Wote tuna haki ya kupata barabara bora, maji salama na huduma za msingi kwa wakati mmoja bila kujali huyu ni wa kijijini au wa mjini.
Ninaomba sasa kama Sheria hiyo ya Bodi ya Barabara au ya kwenu, inaleta matatizo tunaomba muilete hapa, ile siyo msahafu wala biblia kwamba haibadiliki. Leteni hapa tutafanyia marekebisho watu waweze kuapata maendeleo sawa kwa sawa na mgawanyo uwe sawa kwa sawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja barabara ya kutoka Kawajense – Ugala – Kaliua mpaka Kahama. Barabara hii tumekuwa tukiiongelea sana sambamba na ujenzi wa daraja la Ugala, tumekuwa tukiiongelea sana, itamsaidia mwananchi kutoa mazao yake kutoka Mbeya, Sumbawanga, Katavi, Kahama na hatimaye kwenda Musoma na na hata kwenda Darfur wanakopigana kila siku hawana chakula. Tumekuwa tukiongelea umuhimu wa barabara hii; na barabara hii ilikuwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi toka mwaka 2005 na haijatengewa hata hela ya upembuzi yakinifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli sipendi sana kuilaumu Serikali lakini tufike mahali tuwe realistic, kila siku tunaongea hapa haipendezi mtu kila siku ukalisema neon moja, ukisema neno moja kila siku unaumia. Sasa tusianze kupeana pressure humu maisha ni mazuri hata kama magumu. Lakini tunahitaji tunapoongea tunajua tunaongea na Serikali ni watu wazima, wenye akili timamu, tusikilize shida za wananchi na zitekelezwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliongelea suala la reli ya kati, reli ya kati imeongelewa sana, kwa kweli itakuwa ni aibu kama kila siku tutakuwa tunaongelea suala hili ifike mahali tuchukue maamuzi tufanye kwa vitendo sasa. Matokeo makubwa sasa si pesa, ni pale unapokuwa na tatizo na ukali-solve tatizo mara moja, hayo ndiyo matokeo makubwa na si pesa kutoka sehemu nyingine. Niwaombeni sana tatizo la reli tunalo, sasa ni wakati muafaka wa kulitatua. Tutakapo litatua ndipo tutakapokuwa tumefika kwenye matokeo makubwa sasa.
Kwa hiyo, niwaombe kabisa na Serikali inisikilize na standard gauge iwe ni kipaumbele, si suala la kung‟oa mataruma ya reli ya Tura mkayapeleka Katumba ama mkapeleka Mpanda hapana, tunataka reli sawa sawa na maendeleo ya sehemu nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliongelea suala la kurudisha, vinaitwa nini vile?
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Not viberenge, magenge. Tulisema yale magenge yatasaidia sana katika kulinda reli zetu na pia katika kuongeza ajira. Sasa mimi sielewi kwa nini yaliondolewa. Ndiyo maana mnaona kila wakati yale mataruma yanang‟olewa na wananchi kwenda kuuza chuma chakavu, tunaona kwenye tv magari yanavyobeba. Ni vyema sasa mkafikiria mahali na mkafika wakati wa kurudisha; sambamba na kwenye barabara tuliposema kwamba turudishe Public Work Department kwa ajili ya matengenezo ya kila mara ya barabara, kwa ajili ya kuhakikisha barabara zetu zinapitika wakati wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niongelee suala la mitandao au suala la mawasiliano. Ninashukuru sana Serikali yangu kwa kutupatia mitandao hasa vijijini kupitia Halotel, hawa ndugu zetu wa Vietnam, wanafanya vizuri nashukuru. Tatizo langu kubwa na hawa watu ni namna wanavyotoza zile tozo…
Haiwezekani wakatoa kwenye mnara shilingi 30,000 kwa mwezi…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kengele ya kwanza. Mimi hilo nalikataa ninaomba kabisa Serikali iangalie namna itakavyo toza hizo tozo tozo hizo…
Haiwezekani shilingi 30,000 kwa mwezi huo ni uonevu na ni wizi hata kama wanapewa huduma wanafanya biashara...
Wapewe hela kufuatana na huduma wanayotoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kuchangia hoja hii katika haya yafuatayo:-

(i) Katika mgawanyo wa vitabu vya History, Geography na English Book One kwa kidato cha kwanza, Halmashauri ya Mpimbwe haijapata vitabu hivyo.

(ii) Madai na madaraja ya walimu yashughulikiwe kwa haraka sana.

(iii) Walimu wasaidiwe vifaa vya kufundishia kama
computers.

(iv) Vitabu vya kidato cha sita, vitabu vya English ni vitano tu.

(v) Suala la uhamisho kwa walimu ni vema likaangaliwa upya na ikiwezekana wapangiwe maeneo yao kwa manufaa ya familia zao.

(vi) Fedha zilizotolewa kama motisha kwa Halmashauri katika Mpango wa P4R, Halmashauri ya Mpimbwe, Jimbo la Kavuu haijapata fedha hizo.

(vii) Mtaala wa elimu uangaliwe upya ili uwezeshe jamii kuendana na mabadiliko ya maendeleo duniani.

(viii) Nakumbusha maombi yangu maalum niliyompatia Mheshimiwa Waziri. Naomba tusaidiwe wananchi wa Jimbo la Kavuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika haya yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ukarabati wa mikakati ya kupunguza umaskini katika aya ya 26 limeongelewa suala na mafunzo kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii, je nini tofauti ya kada hizi? Kwa nini isijumuishwe ikawa kada moja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu taasisi za mafunzo aya ya 165, Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP); pamoja na kuongeza udahili wa wanafunzi kutoka 5,852 hadi 6,500 bado idadi hiyo ni ndogo ukilinganisha na idadi ya wanafunzi wanaoomba nafasi katika Chuo hicho na hivyo wakati mwingine kupunguza mapato na kufanya Chuo hicho kushindwa kujiendesha. Je, Serikali inasema nini kuhusu suala hilo? Je, Serikali inasema nini kuhusu kupeleka OC kwa wakati ili vyuo hivyo viweze kujiendesha na kufanya kazi zake za kutoa taaluma kikamilifu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la road licence ni vema sasa Serikali ikaangalia upya mpango huu hasa kwa yale magari ambayo hayatembei. Ili kuondoa malalamiko kwa wananchi ni vema sasa tozo hii ikahamishwa kwenye mafuta ili mtumia chombo cha usafiri aweze kulipia tozo hiyo kwa chombo kinachotembea na yale yasiyopo barabarani yaachwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia katika haya yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuzungumzia kuhusu uharibifu wa barabara katika Mkoa wa Katavi hususani katika Jimbo la Kavuu. Kwa kuwa barabara ya Tabora - Mpanda imeharibika sana na imefungwa kwa muda; je, Serikali haiwezi kuongeza mabehewa kwa njia ya reli kutoka Tabora - Mpanda ili kuweza kuwapunguzia adha wananchi wa Katavi kwani mabehewa ni machache? Kwa hiyo, ni vyema yaongezwe kwa madaraja yote, yaani kwa maana ya mabehewa ya daraja la kwanza, la pili na la tatu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha na ninaunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, mwandiko wa kuunganisha herufi. Katika hili, Serikali inabidi iangalie upya mpango huu kwani umekuwa ukileta mkanganyiko kwa wanafunzi wa madarasa ya chini yaani awali mpaka darasa la nne kwa namna ambavyo imekuwa ikiwaletea taabu wanafunzi katika utambuzi wa herufi na namna ya kuanza kuzitambua na hivyo kuwa na mwandiko mbaya. Hivyo basi, Serikali kupitia Wizara hii iangalie namna nzuri ya uumbaji wa herufi toka wanafunzi wakiwa katika hatua za awali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, maabara za shule za sekondari. Ni vema sasa Serikali ikaelekeza nguvu ili kumalizia maabara za shule zote nchini na kuhakikisha zinanza kufanya kazi kwani tunakwenda kwenye uchumi wa viwanda. Hivyo, ni vema maabara ziboreshwe na kumalizika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, maktaba. Serikali sasa ni lazima itambue umuhimu wa maktaba kwani ndiyo chanzo cha kufanya rejea ya mambo mbalimbali ambayo wanafunzi wanakuwa wanafundishwa darasani kwa muda mfupi. Hivyo basi, Serikali iharakishe ujenzi wa maktaba katika shule zote za msingi na sekondari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, nilileta ombi la Shule ya Sekondari Mpanda ianzie Form I – VI badala ya ilivyo sasa form four - six. Je, ombi hilo limefikia wapi na limeshughulikiwa kwa kiasi gani?
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipatia nafasi hii niweze na mimi kuchangia katika hoja hii muhimu inayogusa maisha ya kila mwananchi katika nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, napenda niishukuru Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi chini ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna ambavyo katika hii Awamu ya Tano tumeshuhudia mapinduzi makubwa ambayo na yeye pia amekuwa kiongozi shujaa katika kutatua matatizo ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la tatu, napenda niwashukuru Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu na wasaidizi wao kwa ujumla katika Wizara ya Maji kwa namna ambavyo wamekuwa wakichapa kazi kwa bidii na pindi wanaposikia matatizo wamekuwa mstari wa mbele kwenda kuangalia kuna matatizo gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nianze kuchangia kabla sijasahau, la kwanza kabisa katika Mfuko wa Maji. Katika hali ya kawaida, mimi nafikiri hata Mheshimiwa Rais anatambua namna gani tulivyo na shida ya maji hasa tunaotoka vijijini. Anatambua kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba kwa Serikali hii iliyo sikivu tusiwe na kigugumizi, Waheshimiwa Wabunge wengi hapa wamechangia kwa namna ya pekee, walivyoona umuhimu wa maji, sitaki kurudia michango yao. Naomba Serikali ichukue suala hili na ikalifanyie kazi ili tuone kwa namna yoyote ile ni mahali gani wanapata vyanzo vya mapato ili tuweze kupata maji ya uhakika hasa katika maeneo ya vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo, napenda kuishukuru Wizara hii kwa bajeti iliyopita waliweza kunitengea katika Kata yangu ya Ikuba, Vijiji vya Kashishi, Itula ambavyo vyote sasa hivi vina maji. Sasa naomba, Kata hiyo tu ya Ikuba, Kata ya Usevya na Kibaoni ndizo zenye vyanzo vizuri vya maji na wanapata angalau maji safi na salama. Naomba katika Kata ya Chamalendi sina maji kabisa katika vijiji vya Maimba, Mkwajuni na Chamalendi yenyewe, na Mwamapuli katika vijiji vya Lunguya, Centre Pinda na Centre Clara. Mheshimiwa Kalobelo kama yuko hapa, vijiji vyote hivyo ninavyovitaja anavifahamu kwa sababu aliwahi kuwa Mkurugenzi wangu kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nawaombeni sana, sana, naomba Chamalendi mnipatie maji ya kutosha na visima. Sina maji kabisa kule, watu wanatumia maji yanayoporomoka katika Mto Msabya na yanayotoka katika Mto Kavuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nawaombeni sana, tupunguze matatizo ya wananchi wangu wa Kata ya Chamalendi, Mwamapuli ambao kila siku wamekuwa wakipigizana kelele na Askari wa TANAPA. Kwa hiyo, nawaomba sana, sana, tuondoe hiyo adha ya wananchi wale kugombana na TANAPA. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, nikirudi katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri katika ukurasa wa 23, mmeongelea uamuzi wa ujenzi wa mabwawa ya kimkakati. Niliwahi kuuliza hapa masuala ya umwagiliaji yako wapi? Hayaongelewi siku hizi huku. Nina umwagiliaji Kirida, nina umwagiliaji Mwamapuli, ambapo Mwamapuli mwaka 2017 mlitutengea hela ya upembuzi yakinifu kupitia Wizara ya Maji, lakini mpaka sasa sioni kinachoendelea. Ni mradi mkubwa na mradi wa Mwamapuli mliuondoa kwenye Halmashauri mkaupeleka kwenye mikakati ya Kitaifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nakuomba sana Mheshimiwa Naibu Waziri na Mheshimiwa wangu Waziri wa Nchi uko hapa, wananchi wangu wale wana mashine na mitambo mikubwa ambayo takribani ina miaka saba haifanyi kazi kwa sababu hatuwezi kuendelea na kilimo kwa ajili ya mvua zilizoharibu ile mitambo. Nimesema ni umwagiliaji Kirida pamoja na Mwamapuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaongea hivyo najua utanijibu hicho kilimo, lakini ni masuala mtambuka; na utanijibu hicho kilimo kwa kunikwepa tu, lakini katika ukurasa wa 23 mmeandika kilimo cha umwagiliaji na uzalishaji umeme. Katika kilimo cha umwagiliaji ndiyo nimeweka mradi wa Mwamapuli pamoja na wa Kirida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikirudi kwenye uzalishaji umeme, nilimwomba Mheshimiwa Prof. Mbarawa aweze kukutana na Mheshimiwa Dkt. Kalemani waangalie ni namna gani tunaweza tukazalisha umeme katika Kata ya Majimoto, kwenye chanzo chetu cha Majimoto pale. Kwa hiyo, naomba pamoja na hii mipango mlioyoiandika humu, basi na Majimoto mpafikirie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nirudi katika mradi wa kutoa maji katika Ziwa Tanganyika. Nimeona kabisa kwamba upembuzi yakinifu na tathmini ya athari za kimazingira na kijamii imeshafanyika. Tunasubiri nini sasa kuanza kufanya usanifu wa kina ili tupeleke fedha kule? Kwa sababu haya maji ninaamini yanakuja mpaka kwenye Halmashauri yangu ya Mpimbwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, wananchi wangu wa kule tatuwapunguzia adha ya kupata haya maji. Kwa hiyo, naomba tu, ni lini mtaanza kufanya huo usanifu wa kina ili tuweze kuanza mara moja namna ya kutafuta fedha kwa ajili ya kutoa maji Tanganyika kupita Karema, Mpanda, Kavuu na kufika Mpimbwe kabisa kule Jimboni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo yote, naomba niongelee suala lingine. Pamoja na kwamba nimeshaongea mambo ya Jimboni kwangu sasa naomba niongee kama mwananchi ninayetoka Mkoa wa Katavi. Naomba niongelee kuboresha mfumo wa maji katika Mji wa Mpanda, nimeona kuna fedha pale imetengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na mradi wa Ikorongo, una miaka kadhaa, maji Mpanda ni tatizo. Ni mji pale, ni tatizo, ni tatizo ni tatizo, naomba litatuliwe. Wananchi wamekuwa hawataki kulipa bill kwa sababu tu maji wanapata mara moja kwa wiki; kwa sababu tu maji yanatoka mara moja kwa wiki. Huyo mtu akifanya mahesabu yake kwa bill na lita alizotumia, lazima atakukatalia kulipa bill. Mtaanza kuwakatia maji, mtagombana bila sababu za msingi. Kwa hiyo, naomba hilo pia mliangalie vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee suala moja ambalo kwa mimi binafsi naona kama ni kero; ankara kutolewa kwa njia ya kielektroniki, yaani kwenye simu. Kwanini tusitoe karatasi pamoja na meseji kwenye simu? Kama mimi mwenye simu nimesafiri, basi nyumbani pale inabaki karatasi wale watu wanalipa bill, na siyo muda wote mtu atakuwa na simu mkononi kuangalia bill yangu imeingia ya maji ya mwezi huu, kwa hiyo lazima niende nikalipie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilikuwa naowaomba mfanye utaratibu; na hizi ni Kanuni, siyo kwamba ni amri za Mungu. Hizi ni Kanuni tu tunatunga. Kwa hiyo, huo utaratibu mimi nimeona una malalamiko na una matatizo. Kwa hiyo, ni vema sasa mkatoa karatasi na pia mkatumia hiyo njia ya kielektroniki. Siyo muda wote watu wana simu kama hizo na nimekuwa nikisema kila wakati, kwa hiyo, nilikuwa nawaomba pia mwangalie hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hili suala la Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Oman ambayo imeleta mradi wa kuchimba visima 100 kwa shule za sekondari. Mimi kwangu sijaona hata shule moja. Sasa nikuombe Mheshimiwa Waziri, nipatie sekondari hata mbili tu; au shule za msingi hata tano tu ili wale watoto kule wapate maji. Sina maji katika shule hizi. Sina maji katika shule za msingi wala za sekondari. Kwa hiyo, nawaomba, nipatieni hata visima viwili tu vya sekondari, vitano nipe vya shule ya msingi; vingine nitakuwa naomba pole pole angalau wanafunzi wangu wapate kusoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi mwenyewe ni mwalimu, nikienda naingia darasani kufundisha. Nikitoka natafuta kidumu cha mwanafunzi kiko wapi ndiyo ninawe maji chaki. Sasa hii siyo nzuri, naomba tupate angalau usawa. Kwa nini maeneo mengine yapelekewe hivi visima, maeneo mengine hayapati? Nataka tujue, mtakapokuja nawaomba kabisa katika hili mwangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la miundombinu. Wakandarasi wamekuwa wakinunua vifaa ambavyo siyo vizuri ni vibovu. Mpira badala ya class C, sijui mnatuletea mpira gani. Mwananchi au Mwenyekiti wa Kamati ya Maji Kijijini anajua huu mpira ni class C? Hiyo nayo iangaliwe.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Malizia, malizia Mheshimiwa.

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Maombi yangu naomba yachukuliwe kama nilivyoyaleta kwako Mheshimiwa Waziri na ninaunga mkono hoja ili nipate maji. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia katika suala la Ziwa Rukwa, kulikuwa na fununu ya upatikanaji wa gesi ya helium katika Ziwa Rukwa, je, hali ya utafiti mpaka sasa Serikali inasemaje. Je, kuwepo kwa gesi hiyo katika Ziwa Rukwa hakuna athari za kiafya kwa wananchi na watumiaji wa ziwa hilo. Serikali ina mpango gani wa kuweza kuvuna gesi hiyo na kuitumia?
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipatia nafasi nami niweze kuchangia katika hii Wizara. Kwanza kabisa napenda niungane na wananchi wangu wa Jimbo la Kavuu ambao wamepata athari kubwa sana kutokana na mvua ambazo zinakaribia kuisha, athari ambazo zimesababisha watu karibu saba hivi kupoteza maisha yao.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, napenda niishukuru Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu ambao baada ya kusikia tatizo hilo, wameweza kufika mahali pale na kuweza kufanya tathmini na kutoa huduma ya kwanza kwa wale walioathirika, takribani nyumba 200 hawana makazi mpaka sasa. Nawaomba wananchi wangu wa Jimbo la Kavuu, Mwenyezi Mungu atupe wepesi wa kuvumilia na tatizo hili ninalishughulikia na niko pamoja na ninyi katika matatizo haya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naomba niishukuru sasa Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi, chini ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, ambayo imeanza kutekeleza ilani yake. Unajua waswahili wanasema, mti wenye matunda hauishi kupigwa mawe. Ukiona mti haupigwi mawe, ujue una kasoro. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa wetu ni mti wenye matunda na sasa tunatekeleza na haya ndiyo
tunayotekeleza. Amesaini mikataba mingi ambayo Mheshimiwa amekwishaongea, sitaki kurudia, lakini ni ukweli na uwazi ambao unaonekana kwa juhudi ya Serikali ya Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli, namna ambavyo inafanya kazi kwa bidii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende moja kwa moja sasa katika utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Napenda niishukuru Serikali kupitia Wizara hii, nimekuwa na kilio cha muda mrefu sana kuhusu daraja langu la Kavuu ambalo ni kiungo cha barabara ya kutoka Majimoto mpaka Inyonga. Daraja hili ninavyosema, katika ufunguzi wa Mbio za Mwenge zilizofanyika Mkoa wa Katavi lilipitika. Aaah, nilitaka kusema CCM oyee! Mheshimiwa Naibu Spika, samahani!
Mheshimiwa Naibu Spika, ninasema napongeza sana. Kelele zangu na juhudi zangu zimezaa matunda daraja lile linapitika. Namuomba Mheshimiwa Waziri, sasa zile kilometa kumi zinazounganisha Majimoto kupitia daraja hilo kwenda Inyonga, sasa ziishe na daraja lile wananchi waweze kulitumia kwa ukamilifu kwa sababu, limetumia pesa nyingi ambazo ni kodi za wananchi. Kuliacha hivi hivi kwa kutokuwa na barabara tutakuwa hatuwatendei haki wananchi wa Jimbo la Kavuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninasema hivyo kwa maana kwamba Hospitali ya Wilaya iko Inyonga, wananchi wanalazimika kwenda Hospitali ya Mpanda ambako ni mbali. Sasa ni vema tukamaliza ile barabara tuwasaidie akina mama, watoto na wananchi kwa ujumla ambao wanaenda kupata matibabu mbali.
Pili, litatusaidia pia kuwasaidia wananchi wale kuweza kufanya biashara zao kati ya Mkoa wa Tabora na Mkoa wa Katavi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa barabara yangu ya Starike - Mpanda imekamilika; lakini naomba barabara ya kutoka Kizi – Kibaoni yenye kilometa 76.6 imalizike. Barabara ile kupitia upande wa pili wa Mlima wa Lyamba Lya Mfipa, imekuwa ni tatizo na kisababishi kikubwa cha ajali kwa sababu, hakijamalizika pale. Kwa hiyo, magari mengi yanakuwa yanatumbukia kule chini kiasi ambacho siyo rahisi kuokoa na imekuwa ikisababisha vifo vya watu wengi. Naomba barabara ile ikamilike.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba barabara inaishia pale Kibaoni, barabara hii ya kutoka kibaoni ambayo imekuwa ikiulizwa humu na maswali mengi ambayo yamekuwa na majibu yasiyotosheleza, barabara ya kutoka Kibaoni kupita Muze mpaka Kilyamatundu ambayo inaenda kupita Daraja la Momba, naomba Mheshimiwa Waziri katika hotuba yako utakapohitimisha, tunahitaji majibu ya uhakika. Hatuhitaji kurudia maswali, tunataka leo tupate majibu ya uhakika, ni lini barabara hii itafanyiwa usanifu na ni lini itaanza kuwekewa lami? Kwa sababu, ni miaka kumi imepita tukiiongelea hii barabara ya kutoka Kibaoni mpaka Kilyamatundu kupitia Muze.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nije kwenye aya ya 50 inayoongelea barabara ya Mpanda – Tabora – Ipole mpaka Sikonge. Barabara hii nashukuru imetengewa pesa na angalau tuna kilometa 30 kutoka Tabora Mjini mpaka Sikonge, sawa. Mahali pabaya ni kutoka Sikonge kupita Koga mpaka Mpanda. Sielewi kigugumizi kiko wapi hapa?
Mheshimiwa Naibu Spika, hii barabara Mheshimiwa Rais alipokuwa Waziri wa Ujenzi alinihakikishia na alinishirikisha maongezi na Mwakilishi Mkazi wa ADB pamoja na World Bank na wakakubali na pesa zilikuwa zimeshatoka. Ukisoma kwenye hii aya, wanakwambia pesa zilikuwa zimetoka, sasa ina maana zimeenda kufanya kazi zipi? Ama zinaendelea kufanya kazi ipi? Ni vema tukajua status ya hii barabara. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hii barabara tumekuwa tukiipigia kelele kila siku. Kwa kweli, Serikali yangu naipenda,
inafanya kazi vizuri na ni sikivu. Naomba barabara hii sasa tuipe kipaumbele ili wananchi wa kule nao waweze kuondoa mazao kule. Mazao yako kule na mvua zimenyesha, mazao yameharibika, hawana pa kuyapeleka kwa sababu ya barabara mbovu. Tunaondokaje na umaskini na sisi tunataka twende kwenye kima cha kati? Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri, Profesa, nafikiri unanielewa ninapoongelea hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, natoa pongezi za dhati kwa Serikali kuonesha nia ya kujenga reli ya kati. Napenda niseme, reli ya kati haiishii Mwanza, ina matawi yake aliyojenga Mjerumani ambayo inakwenda mpaka Mpanda mpaka Kigoma.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niungane na Mheshimiwa Nsanzugwanko, aliongea vizuri sana kuielewesha jamii ya Tanzania pamoja na Serikali kwa ujumla reli ya kati maana yake ni nini?
Kwa hiyo, pamoja na kwamba tunaenda kwa vipande, naomba basi vile vipande vinavyobakia vingine visiishie Mwanza. Raha ya reli ya kati ifike Mpanda. Nashukuru kwamba mnatoka Mpanda mnaenda mpaka Karema, Karema mnajenga bandari pale mpaka Kalemii, tunashukuru sana. Sasa itoke pia Tabora – Urambo mpaka Kigoma. Hapo tutakuwa tumeweza kuwaunganisha wananchi wa huku kwetu pamoja na Ukanda wa Kongo, Burundi, Rwanda na Zambia kwa ajili ya biashara. Tunaweza tukainua uchumi kwa haraka sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee suala la viwanja vya ndege. Nimeona katika kiwanja cha ndege cha Mpanda ambapo pesa imetengwa kwa ajili ya kumlipa mkandarasi. Sasa tukishamlipa yule mkandarasi sijaona mwendelezo kwamba nini kitafanyika pale. Ule uwanja umejengwa, hautumiki. Ni kiungo kikubwa kwa kukuza uchumi kupitia maliasili zetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tuna Katavi National Park pale, kila siku nasema jamani, ile mbuga ina wanyama wakubwa hakuna mfano. Kuna twiga mrefu hakuna mfano, kuna twiga chotara ambaye hutampata Tanzania kokote. Naomba kile kiwanja; kitatuunganisha sisi na mbuga za Kigoma, tunaunganishwa na mbuga zinazotoka huko Kaskazini, watu watapenda kutembea sehemu mbalimbali za Tanzania. Tusisubiri mpaka sijui Clouds nini wale, wafanye utalii ndiyo na sisi tuamke, hapana. Naomba kabisa kwa dhati kile kiwanja mkiendeleze. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa kule kutokana na ubovu wa barabara, msifikiri hawana uwezo wa kupanda ndege, uwezo huo tunao. Sisi tunalisha karibu nusu ya Tanzania, tushindwe kupanda ndege!
Kwa hiyo, tunaomba kabisa kile kiwanja sasa kifikie mahali tuone ndege zinatua, zinaondoka na watalii wanashuka pale, ili tuone ni kwa namna gani ambavyo tunaweza kukuza uchumi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa kwa mara nyingine, pamoja na kwamba…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Nitaleta maombi binafsi kwa Mheshimiwa Waziri, kuhusu barabara zangu za Katavi. Ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizari ya Maji na Umwagiliaji
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kuchangia katika hotuba ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji ambayo ni muhimu sana katika maendeleo ya binadamu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa naomba niwaaminishe ndugu zangu wa Kambi ya Upinzani kwamba CCM haijachoka kubeba mzigo, CCM ni kama tembo, tembo hachoki kubeba mkonga wake na wale wanaofikiri itatoka madarakani ni ndoto za mchana. Sasa niwaombe tu kwamba tuwe wavumilivu na Serikali hii makini inayotekeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili naomba niendele kuwaomba ndugu zangu wa Kata ya Kasansa na Mamba wawe wavumilivu kwa mvua zinazoendelea na pili waweze kuchukua tahadhari kwa ajili ya kujinusuru na maafa yanayoweza kutokana na mafuriko; na mafuriko yale niliwahidi nayashughulikia na niko mbioni kukamilisha ili nikawatembelee.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niishukuru Serikali yangu na niishukuru Wizara hii ya Maji, katika bajeti ya mwaka uliopita imeweza kunisaidia angalau nusu ya jimbo langu kupata maji. Vijiji vya Kashishi, Chamalendi, Mwamapulu, Ukigwamizi, Msadya, Maimba, Ikulwe, Kaunyala, Minyoso, Ntompola, Mkwajuni, Lichima, Kibaoni, Nyambwe, Lunguya, Ilalangulu, Mawiti karibu kote huko nimepata visima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo nililonalo gari la kuchimbia liko moja, kwa hiyo, naomba mniongezee magari angalau mawili ili tuweze kumaliza tatizo hili mara moja. Nirudi pale pale kwenye kata yangu ya Kibaoni, tuna mradi mkubwa na kisima kikubwa pale cha maji. Niliomba mnitafutie wataalam kuja kuangalia kisima pale tatizo ni nini sijapata taarifa, naomba nipate taarifa na nijue status ya pale kwa sababu kile kisima ndicho kinachosambaza maji katika kata ya Kibaoni nzima.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niungane na wenzangu wote waliotanguliza kusema sasa tuongeze tozo kutoka ile shilingi 50 tupate shilingi 100 na ikiwezekana 150 ili wananchi vijijini wapate maji safi na salama, maji ya kutosha na yawe endelevu isiwe kwamba yakifika kipindi cha kiangazi maji yanakuwa yanakauka hapana, tunaomba namna ambavyo tutafanya miradi yetu hii iwe endelevu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nirudi tena kwenye mradi wangu wa umwagiliaji wa kata ya Mwamapuli, humu sijaona umetengewa fedha yoyote. Skimu ya Mwamapuli naomba nipate status yake. Katika bajeti iliyopita mliniambia mmenitengea karibu shilingi bilioni moja kwa ajili ya upembuzi yakinifu.

Kwa hiyo, ninaomba sasa kama upembuzi yakinifu mmeshafanya mniambie, kama ni pesa mtanipa kutoka kwenye hiyo asilimia tutakayoongeza ndiyo yenye uhakika zaidi naomba mnifikirie katika mradi huu, ni mradi wa Kitaifa kwa hiyo naomba muutafutie pesa ili tuweze kupata.

Mheshimiwa Naibu Spika, pale tumeshakufungua maghala manne na tuna mashine ya kisasa ya kuchambulia Mpunga. Sasa ile mashine inakaa bure pamoja na yale maghala yanakaa pale bure. Sasa naomba mradi huu uanze mara moja ili wananchi wanufaike na kazi walizojitolea za asilimia 20 za kuchangia maendeleo katika kujenga miradi ile. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba niseme neno moja. Wapo wenzangu waliotangulia kuzungumza kwa kusema kwamba tupunguze tutoe hela kwenye REA, hapana. Si vijiji vyote vimekwishapata umeme, naomba ile tozo ya kwenye REA ibaki vilevile, tuhakikishe vijiji vinapata umeme. Nimekuwa nikilia kila siku na Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini, kata zote zilizoko Jimbo la Kavuu pamoja na kata zote zilizoko Jimbo la Kwela kwa Mheshimiwa Malocha hakuna umeme hata kijiji kimoja. Jimbo la Kavuu lina umeme kata ya Kibaoni na Usevya center tu, Usevya ni nyumba kumi.

Kwa hiyo, ninaomba sana kwa sisi tunaotoka majimbo ya vijijini hii hela tusikubali ipunguzwe. Lazima tuhakikishe inapatikana tena kwa wingi na wananchi kule vijijini wana enjoy haya matunda ndugu zangu. Tusiwe wachoyo watu wa mjini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vijijini ndio kwenye nguvu kazi kubwa, ndiko tunakotoa chakula na nimewaomba hata ndugu zangu wa Jimbo la Kavuu, tukivuna mazao yetu hakuna kupunguza bei, tulinunua kwa shilingi 25,000 kwa debe na wao wauze shilingi 25,000 na kuendelea ili mjini yapande zaidi na wakulima waone sasa wanapata chochote kidogo na kukuza maisha yao kwa sababu pembejeo walijinunulia wenyewe. Leo tunataka tuanze ooh, chakula kule kimefanya hivi, hapana, tuwaache wauze kwa bei zile zile walizonunua ili na wao waweze kubadilisha maisha yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba niongelee mradi wangu wa umwagiliaji wa Kilida. Mradi huu ulikula hela nyingi sana na ni mkubwa, umeharibika kutokana na mvua na mafuriko yaliyopita pale. Sasa sababu mvua bado zinaendelea niiombe sasa Wizara na nimekwishaleta maombi yangu maalum, mabanio na mifereji na magati pale yavunjika. Kwa hiyo, zile mvua zinavyoendelea maji yale sasa yanahama kwenye ile kata yanaenda kujaa kwenye Mto Msadya ambao umefurika sasa kwenye kata ya Usevya. Kwa hiyo, niwaombe mshughulikie lile banio, Naibu Katibu Mkuu yupo hapa ananifahamu na hilo banio analifahamu, Mr. Kalobelo unalifahamu vizuri. Naomba mlisimamie sasa ili ile scheme irudi kwenye miundo yake ili tuokoe kata zingine zisipate mafuriko. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naishukuru sana Serikali yangu, nawashukuru sana Wizara ninaomba magari mawili ya nyongeza yaje kunisaidia kuchimba vile visima, tena nashukuru ni visima virefu vitakaa muda wa mwaka mzima ili wananchi wangu wapate maji safi na salama, na shule zangu zote za msingi na sekondari zipate maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi na ninaunga mkono hoja ninaomba ile tozo iongezewe asante sana.
Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi niweze kutoa maoni yangu kuhusiana na hotuba ya Mheshimiwa ambayo imeletwa kwa ajili ya mapendekezo ya maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda nitoe pole kwa ndugu zetu walemavu waliopata rapture pale Dar es Salaam, ni sawa inawezekana ni katika kutekeleza sheria, lakini ni vema sasa hata utekelezaji wa hizi sheria tukaangalia ni namna gani, nimuombe Mheshimiwa, ndugu yangu, dada yangu Mheshimiwa Jenista, dada ambaye unasikiliza na unasimamia masuala haya hasa mambo ya Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu nina kuamini utalishughulikia suala hili kwa kushirikiana na mamlaka husika ili tuweze kuona ni namna gani wale walemavu wameweza kutendewa ndivyo sivyo, kwa kweli si jambo jema kwa kupiga walemavu hata kama tunatekeleza sheria. (Makofi)

Kwa hiyo nikuombe ndugu yangu kwa umahiri wako dada yangu Jenista ulionao ninaamini suala hili utalishughulikia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia vilevile masuala yaliyotokea Tabora kwenye michezo tunasema michezo inadumisha amani, upendo, utulivu. Wamecheza kule pamoja na Jeshi la Wananchi sasa sielewi matokeo yalikuwaje, matokeo yake MP’s wakaingia uwanjani na kuanza kupiga wachezaji na wananchi, hilo nalo naomba Waziri anayehusika alishughulikie hili tujue sasa nini maana ya michezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo naomba nipongeze sasa bajeti hii iliyoko hapa mbele yetu inayopendekezwa. Bajeti hii kwa kweli imeweza kulenga maeneo mbalimbali na lengo lake kubwa tunaona ilikuwa ni kupunguza kodi ili kuweza kuwasaidia wananchi kufikia uchumi wa kati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti hii imeweza kutoa misamaha mingi ya kodi ambazo nyingi zilikuwa ni kama kero kwa wananchi, kwa mfano naweza kusema katika jimbo langu la Kavuu kata ya Majimoto na kata ya Usevya wamekuwa wakilalamikia sana kodi ya majengo, kodi ya guest house, kwa kweli kuwaondolea kule kutawawezesha na wao angalau kusonga mbele, kwa sababu kule sisi tunategemea siku za mnada tu, kwa hiyo hata tulivyokuwa tukitoa zile kodi kwa kweli ilikuwa inawaumiza wananchi na wako huko najua wananisikia, mitandao iko mingi tu wananisikia wanajua nawakilisha mawazo yao hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Lakini naomba niende katika suala zima ambalo limekuwa likiongelewa la shilingi 40. Katika hii shilingi 40 tunaelewa lengo ni jema na ni zuri kwa Serikali, lakini ukiangalia kwa ndani hii pesa imeongezwa kwenye mafuta, bidhaa za mafuta ikiwemo na mafuta ya taa. Bidhaa hizi za mafuta ya taa na wananchi wetu vijijini hasa katika jimbo langu ambalo halina umeme, wanatumia mafuta ya taa kwa maana kwamba watachangia hii shilingi 40, sasa kwa msingi huo huo wa wao kuchangia hii shilingi 40 nimuombe Mheshimiwa Waziri usiwe na kigugumizi kwa kuitoa hii shilingi 40 katika ku-cover deni la Serikali la shilingi milioni 28 hii shilingi 40 ipeleke kwenye maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Lazima iende kwenye maji, usiwe na kigugumizi Mheshimiwa Waziri katika hili kwa kweli ukifanya hivyo ndipo utakapokuwa bajeti yako sasa umeinogesha ipasavyo, pale tutakapoweza kuiweka hii pesa kwenye maji kwa sababu lengo lako ni kukusanya hii shilingi milioni 28 ili iende ika-cover lile deni lenu Hazina, sawa hatukatai ni pesa ya maendeleo, sasa tutakaposema kwamba ile shilingi 40 isiende kwenye maji vyanzo wewe vya kupata hii milioni 28; unayo shilingi bilioni 28 unavyo vyanzo? Itafute kwenye vyanzo vingine na hii shilingi 40 uliyoongeza kwenye bidhaa za mafuta ambazo wote itatugusa mpaka wananchi wa kijijini iende kwenye maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine namba niongee kuhusu ahadi ya shilingi milioni 50, katika hotuba ya Kambi ya Upinzani ukurasa sita wameongelea ahadi ya milioni 50. Ahadi hii ni ahadi ya Chama cha Mapinduzi, tumuache Mheshimiwa aliyepita kila kijiji kuomba kura na kuitoa ahadi hii haitekeleze, tukianza kudandia gari kwa mbele, tutapata kugongwa. Muachieni Mheshimiwa aitekeleze ahadi yake, maana yake imeshakuwa ni nini tumeshapewa maelekezo hapa na Serikali namna gani pesa hii itatoka lakini nashangaa kwenye ukurasa wa sita ndio ajenda kuu ya bajeti ya ndugu zangu pale, tuachieni tuka-organize wananchi wajiunge waweze kupata pesa hizi kwa utaratibu maalum na msiseme ni ajenda yenu, maana kazi yenu kudandia mbele magari. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee kodi ya majengo tumesema itaanza kwa shilingi 10,000 nyumba za kawaida na shilingi 50,000 kwa ghorofa, nikuombe Mheshimiwa Waziri katika hili utunyumbulishie ni nyumba gani italipa shilingi 10,000 ni ghorofa gani italipa shilingi 50,000. Maana ukiniambia nyumba kwangu jamani nina tembe, sasa yule mwenye tembe kadi ya bima tu ile ya CHF hana, leo ukamwambie atoe shilingi 10,000 inawezekana? Sasa utuambie ni nyumba ya aina gani itakayoanzia shilingi 10,000 na ni nyumba gani itakayoanzia shilingi 50,000 . (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake huwezi kuniambia ghorofa kama lile LAPF pale ama Kilimanjaro Hotel itafanana na nyumba ya kuishi ya mtu mwenye ghorofa moja ama huwezi kuniambia nyumba ya vyumba viwili vya kulala hapo ukifika Mwitikila hapo itafanana na nyumba ya vyumba vitano self ya kulala.

Kwa hiyo, naomba mtuambie vigezo. Maana utakapoweka hivi wale ndugu zangu watoza ushuru na watoza kodi wao wataenda kutoza kama lilivyo hawataweza kusema huyu anafaa, huyu hafai, wao wataenda kutoza kama mlivyolielekeza na wengine wanaweza kusema kwamba sasa nyumba yangu ghorofa saba silipi, tumeambiwa ya ghorofa ni shilingi shilingi 50,000. Sasa lazima mueleze hapo kwamba ni nini mnakusudia katika kupata haya majengo na haya majengo yako kivipi? Huwezi ukaenda mtu mwenye nyumba sita ukamwambia akalipa shilingi 10,000 sawa na yule mwenye nyumba ya chumba kimoja ambacho labda ni chumba, sebule na choo haiwezekani…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niunge mkono hoja na ninaungana na Waheshimiwa wote na wananchi wote wa Tanzania kwa ujumla.
Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ili niweze kuchangia hoja iliyoko mbele yetu. Kwanza kabisa napenda kuishukuru Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna ambavyo amekuwa akitekeleza majukumu ambayo yamekuwa yakitatua shida mbalimbali zinazowagusa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili napenda niishukuru Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa namna ya kipekee ambayo imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na mimi Mbunge wa Jimbo la Kavuu kwa namna ambavyo wamekuwa wakijaribu kutatua matatizo ya wananchi wangu. Napenda kabisa niishukuru Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya TAMISEMI kwa kuweza kunipatia ambulance ambayo inaweza ikafanya shunting kati ya vituo viwili vya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua jiografia ya Jimbo langu bado siyo nzuri, kwa hiyo, nikuombe Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI uniongezee ambulance itakayofanana na miundombinu ambayo nimepata. Hata hivyo, nashukuru sana kwa kile nilichokipata ambacho ni ambulance ambayo itanisaidia kutoka kituo cha afya cha Kibaoni kwenda kituo cha afya cha Mamba. (Makofi)

Mheshimiwa wenyekiti, napenda niendelee kushukuru kwa kuwa wameweza kuniwezesha kituo changu cha afya cha Kibaoni ambacho sasa kinaelekea kwisha lakini niwaombe katika Jimbo langu la Kavuu nina vituo vya afya vitatu; nina kituo cha afya cha Mamba na kingine cha Mwamapuli ambacho wananchi wameanza kujitolea namna ambavyo ya kuweza kutatua matatizo ya afya kutokana na jiografia ilivyokaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Waziri atuongezee nguvu katika vituo hivi. Nimshukuru kwa namna ya pekee Dkt. Zainab ambaye aliweza kutupa mawazo akishirikiana na Katibu Mkuu Engineer Iyombe namna ambavyo tunaweza tukaanzisha hospitali ya Halmashauri ya Wilaya katika Jimbo la Kavuu na niwashukuru Wizara hii wametupatia kibali na sasa tunakwenda kujenga hospitali ya Wilaya. Ahsanteni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee lingine limekuwa likiongelewa sana na limeongelewa na baadhi ya Wabunge hata jana kuhusu mchango wa chakula mashuleni. Ni kweli kwamba chakula mashuleni kinapunguza utoro, ni kweli kwamba chakula mashuleni kinasaidia wanafunzi kuwepo mashuleni na kinaongeza kiwango cha ufaulu. Kwa hiyo, niwaombe Waheshimiwa Wabunge tuendelee kuwaomba wananchi wetu waendelee kuchangia kwa maana ya kwamba ni jambo lenye tija katika kizazi chetu kijacho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano tu; Mbunge wao wananchi wangu wa Jimbo la kavuu nimeweza kuchangia karibu hekari 30 kwa maana kwamba kila shule inapata hekari moja ya chakula na sasa tumeanza kuvuna. Kwa hiyo ni mchango wangu kwa chakula kwa maana naelewa umuhimu wa chakula mashuleni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishukuru Serikali na niishukuru halmashauri yangu, Halmashauri ya Mpingwe imekuwa ni halmashauri ya pili kati ya halmashauri 185 ambayo imekuwa ikifanya vizuri katika kutenga asilimia 10 kwa maana kwamba asilimia tano ya akinamama na asilimia tano ya vijana. Kwa hiyo, niwaombe, niko vizuri na Mkurugenzi wangu na nafanya naye kazi vizuri sana na anasimamia miradi vizuri mno.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba, kama watafanya reshuffle mimi Mkurugenzi wangu waniachie pale, yuko vizuri. Kama kuna Wakurugenzi wengine hawako vizuri mimi wa kwangu yuko vizuri, anasimamia miradi vizuri, milioni 400 walizonipa kituo cha Kibaoni pale cha afya zimesimamiwa vizuri, pesa za Jimbo zinasimamiwa vizuri. Kwa hiyo, kazi inakwenda na maendeleo tunayaona na Jimbo la Kavuu sasa linaonesha mabadiliko chini ya Dkt. Pudenciana Kikwembe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishukuru Serikali kwa namna ya pekee ilivyoondoa riba katika ule mkopo wa asilimia 10 kwa akinamama na vijana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nirudi kwa TARURA. TARURA ni chombo ambacho kwa malengo yake ni mazuri sana, lakini naomba kiongezewe pesa, kiongezewe watalaam. Kutokana na mvua hizi zinazonyesha nilikwenda ofisini kwa Mheshimiwa Waziri na nikapeleka maombi yangu binafsi, maombi rasmi, maombi special kwa namna ambavyo sasa Jimboni kwangu hakuna hata njia moja inayopitika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemwomba pesa ya kutengeneza box culvert ya Mwamapuli-Majimoto ambayo inagharimu karibu milioni 160, nimeomba Majimoto daraja jipya la Msadya ambalo kwa wale wanaongalia vyombo vya habari waliniona nikienda kulitembelea. Sasa hivi kwa hela waliyotupatia nashukuru limeanza kupitika angalau wagonjwa wanaweza kwenda kutibiwa kituo cha afya kingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pesa takribani bilioni 1.7 kwa ajili ya kujenga daraja lingine, kwa sababu daraja lile linahudumia karibu Kata tano kwa ajili ya akinamama na watoto wanaokwenda hospitali. Kwa hiyo, ni maombi rasmi, naomba niyalete kwako hapa na kwa sababu nilishayaleta kwa maandishi naomba mnisaidie kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba drift mbili kati ya Ntibili na Kikonko ambako kumepata mafuriko na hivi ninavyoongea mvua bado zinaendelea, zimenyesha karibu siku nne mfululizo. Naomba pia box culvert kati ya Kata ya Mamba na Makuyugu ambayo inaweza kugharimu pia milioni 160.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia culvert ya Kibaoni-Chamalendi ambako pia barabara imekatika ambayo ni barabara moja hiyo hiyo inayoungnisha kwenda kwenye kituo cha afya cha Kibaoni. Naomba pia culvert lingine la Mabambasi kupitia Mwamapuli ambalo pia linaunganisha barabara hiyo hiyo kwenda kwenye Kata ya Kibaoni ambayo inakwenda kwenye kituo cha afya ambacho watu wanatumia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee suala la watumishi, watumishi wamekuwa wengi wakistaafu hawapati haki zao, kwa mfano, tuna wastaafu wa Magereza na Mahakama wapatao karibu 200 waliostaafu tarehe 1 Julai, mpaka leo hawjaalipwa haki zao kwa hiyo tulikuwa tunaomba walipwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwa watumishi Walimu; Walimu wamekuwa kama ni wanyanyaswaji kwa sababu hawapandishwi vyeo vyao, hawalipwi pesa zao wanapokwenda likizo, hawalipwi pesa zao wanapohamishwa. Kwa hiyo, naomba malipo yao kwa kweli kwa mwaka huu yatiliwe mkazo. Walimu wetu ni wachache katika vituo vyetu, sasa tunapozidi kuwadidimiza, tunawapunguzia morally ya kazi kwa kweli naomba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee lingine; Mwalimu anapotaka kuhama tunasema atafute nafasi eneo mbadala ili aweze kuhamishwa. Sasa unakuta kuna mwingine kaolewa ama mwingine kaoa kule mnakompeleka hana mume, hana mke, mnachotarajia nini? Kwa hiyo, niwaombe kama mume anataka kumfuata mkewe au mke anataka kumfuata mume wake basi waruhusiwe kwa sababu tunajua maambukizi mapya ya UKIMWI sasa hivi ni mengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunapowaachanisha vile inakuwa ni rahisi kuwaweka kwenye mitego ambayo wanaweza wakapata maambukizi. Kwa hiyo, tunaomba muwalipe malipo yao ya uhamisho na mambo yao mengine ambayo wamekuwa wakidai hasa wanapokuwa pia wanakwenda kwenye matibabu ambayo yako nje ya utaratibu wa bima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba sana suala la Walimu, kwa kweli ni tatizo. Mimi ni Mwalimu pamoja na kwamba ni Mbunge, lakini ninapokwenda Jimboni kwangu mimi naingia darasani kufundisha. Nafundisha kwa sababu ya uhaba wa Walimu. Kwa hiyo niwaombe sana, katika kasma ijayo ya waajiriwa mtupatie watumishi wa sekta ya afya pamoja na sekta ya ualimu, ni vitu ambavyo tunavihitaji sana hasa katika kuhudumia wagonjwa wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, nahitaji zaidi Madaktari badala ya Makatibu wa Vituo vya Afya. Makatibu wanakaa ofisini na computer, nikipata nurse pale clinic atanisaidia zaidi kuliko Katibu wa Afya. Kwa hiyo, naomba hata tunapofanya allocation ya watumishi, tuangalie; Kituo changu cha Kibaoni kina Makatibu wa Afya watatu wa nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naunga mkono hoja kwa asilimia zote.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda niishukuru Serikali yangu pamoja na Wizara kwa ujumla kwa namna ya pekee ambavyo wamekuwa wakifanya kazi kwa bidii na kuhakikisha kwamba wanachanganua changamoto ambazo zinatupelekea kupata maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napenda nimshukuru Mheshimiwa Waziri na Serikali katika kutupatia pesa ya maendeleo ya barabara; milioni karibu mia tisa katika Mkoa wa Katavi, lakini bado ni chache. Naomba wafikirie namna ya kuongeza kutokana na namna ambavyo barabara zimeharibika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudi katika jimbo langu; napenda kuongelea Daraja la Kavuu. Daraja la Kavuu lilikwisha, lakini pamoja na kwamba ni la muda naomba sasa barabara ya Majimoto-Inyonga ambayo wamenitengea karibu milioni mia moja sabini, sidhani kama zitatosha kutengeneza zile kilomita mia mbili na kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba sasa ili daraja lile liweze kupitika niombe Mheshimiwa Waziri wanisimamie na waniongezee pesa katika barabara hii ya Majimoto-Inyonga ili tuweze kutumia lile daraja na tuweze kuwarahisishia wananchi kutoka katika Jimbo la Kavuu kufika Inyonga na hatimaye kuweza kufika Tabora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niwashukuru wameweza kunipatia hela ya matengenezo ya barabara ya Mamba- Kasansa ambayo ni karibu milioni tisini. Pia niwashukuru kwa kunipatia pesa kwa ajili Kibaoni-Majimoto-Kasansa ambayo ni milioni takriban mia moja hamsini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri asinichoke ninapokwenda kuendelea kuomba kuhusu maendeleo ya Jimbo langu la Kavuu kwa sababu mvua ni nyingi na hivi ninavyoongea bado zinaendelea kunyesha na barabara na madaraja mengi na makalavati mengi yameharibika. Kwa hiyo, naomba washirikiane na TARURA kwa karibu na najua pesa yao ni ndogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niungane na Wabunge wengine, kama vile tunavyosema tuwaongezee pesa angalau sasa ifike asilimia 50 kwa sababu wamekuwa wakifanya kazi nyingi bila uwezo wa kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee daraja langu ya Mwamapuli-Chamalendi ambalo TARURA wameweza kunipa pesa ya dharura na sasa hivi linapitika na wananchi wangu wanaweza kupita kwenda kwenye matibabu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sasa yale maombi yangu ya dharura niliyoleta TANROAD ambayo nataka kujenga daraja la kudumu basi wayafikirie ili tuweze kurahisisha wananchi wa Kata kuanzia ya Majimoto, Mbede, Chamalendi, Mwamapuli, Ikuba, wote waweze kufika katika hospitali ama Kituo cha Afya cha Usevya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee kuongelea suala la Mradi wa Kokoto wa Kongoro. Mradi huu kwa kweli kama tutausimamia vizuri tunaweza tukaingiza pesa za kutosha. Inawezekana tatizo ni makubaliano kati ya TAZARA upande wa Zambia na upande wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe Mheshimiwa Waziri aunde tume basi ambayo itaweza kusimamia na kuangalia mkataba huo ili huu mradi uweze kujiendesha kibiashara na Watanzania wengi waweze kufaidika katika mradi huo ili tuweze kuona ni namna gani wanaweza wakachangia maendeleo katika nchi ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba niongelee Gati la Karema. Gati la Karema limeshafanyiwa upembuzi yakinifu, lakini katika bajeti iliyopita walituambia kwamba Karema hakutajengwa tena gati patajengwa bandari. Sasa tulikuwa tunaomba tupate ufafanuzi ni gati litakalojengwa ama ni bandari ili wananchi waweze kuelewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba wameshafanya upembuzi yakinifu tunataka tujue maendeleo ya Bandari hiyo ya Karema ikoje, kwa sababu ndio kiungo kinachotusaidia sisi kutoka Kavuu kuja Mpanda Mjini mpaka Karema kuvuka mpaka Congo ambako tunaweza kupeleka mazao kwa urahisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia niongelee kuhusu Kiwanja cha Ndege cha Mpanda. Kiwanja cha Ndege cha Mpanda ni kizuri na kimekwisha. Naomba ule upungufu uliobaki, Mheshimiwa Waziri mwaka jana nimemweleza na naomba tena na narudia, ili kiweze kufanya kazi tuweze kupata na sisi watalii wanaoweza kuja katika Mbuga ya Katavi ili tuweze kuongeza uchumi, kwa sababu Mbuga ile ya Katavi ina wanyama ambao ni unique. Tuna Twiga ambao ni machotara ambao hawapatikani kokote, ni warefu kuliko kama wengine, ni wanyama walioshiba. Tuki- promote na sisi mbuga yetu upande wa kule angalau tunaweza tukaongeza kipato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nirudi pia katika suala la mawasiliano, kwa ndugu yangu Mzee Kamwele Ilunde, bado mawasiliano ni shida katika Kata ya Inyonga- Ilunde. Niwaombe basi tuweze kuwasaidia ndugu zetu wa Ilunde ili waweze kupata mawasiliano hatimaye waweze kuongeza vipato vyao kwa sababu wako karibu na Tabora na wako karibu na Kavuu, kwa hiyo inaweza kuturahisishia sisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watakapokuwa na mawasiliano mazuri wanaweza wakafika mpaka Mbeya na wakarudi wakaingia mpaka Tunduma, Zambia kuweza kufanya shughuli zao ambazo zinaweza kuwaletea vipato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba niongelee kuhusu TBA. TBA wamekuwa wakifanya kazi nzuri sana; tatizo ni kwamba inawezekana hawana mtaji. Kwa hiyo naomba Serikali iangalie namna ya kuwatumia TBA katika miradi mbalimbali ya ujenzi inayoendelea nchini ili waweze na wao kuweza kwenda mbele katika kuongeza pato la Taifa. Kwa hiyo lengo ni kwamba wawaongezee hawa watu ili waweze kupata nanii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mheshimiwa Waziri naomba niulize, katika maziwa makuu yanayotajwa sijasikia Ziwa Rukwa. Sasa nataka kujua Ziwa Rukwa wana mpango gani nalo, maana yake wavuvi wako kule; lakini nasikia Ziwa Tanganyika, Victoria na Ziwa Nyasa, lakini sijasikia Ziwa Rukwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa, kama walikuwa hawajaliweka katika mpango wa Maziwa Makuu, naomba wafahamu kwamba lile ziwa nalo lipo na naomba liingizwe katika mpango wa maendeleo namna ambavyo wataweza kulishughulikia tuone namna gani ambavyo wavuvi wa upande wa kule nao wanafaidika kutokana na miradi ambayo wanakuwa wameiweka kwenye Maziwa Makuu ambayo Ziwa Rukwa hawajaliweka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na yote hayo naomba nikumbushe barabara yangu ya Kibaoni kupita mpaka Muze mpaka Kilyamatundu ambayo waliahidi kwamba itajengwa kwa kiwango cha lami, lakini ipo kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi tangu awamu iliyopita mpaka leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka tupate majibu, je, barabara hii itajengwa lini na itaanza lini na itakwisha lini? Kwa sababu ni zaidi ya miaka 15 ipo kwenye maandishi ambayo haijaweza kufanyiwa lolote. Ni kutoka Kibaoni kupita Majimoto–Kasansa-Mfinga- Muze mpaka Kilyamatundu. Kwa hiyo tunaomba kabisa tutake kujua hatma ya barabara hiyo ikoje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo napenda tu niwapongeze Wizara kwa namna ambavyo wamekuwa wasikivu, hasa Mheshimiwa Waziri ni msikivu sana tunaposema shida zetu anatusikiliza na Serikali ya Chama cha Mapinduzi ni sikivu, Rais wetu ni msikivu, napenda tu niwatie moyo, naomba wasikate tamaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua changamoto za hali ya hewa ni nyingi sana, tuangalie, tushirikiane na Ma-engineer kama walivyosema na watu wa hali ya hewa tuone tunajenga barabara za aina gani ili tuweze kukabiliana na majanga yanayotokana na hali ya hewa hasa mafuriko yanayoendelea hivi sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja. Ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia katika sekta hii ya elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mtu amesema nakuja kupongeza ni kweli napongeza na ninaanza kupongeza kwa kusema kwamba naishukuru Serikali yangu kwa namna ya pekee ambavyo imeweza kuanzisha mpango wa elimu bure ambayo imeweza kusaidia watoto wengi kuingia shuleni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nasema naipongeza Serikali kwa sababu hata wazazi wamejitokeza na wameweza kuchangia na kuongeza madarasa, naongelea katika Jimbo langu la Kavuu ambalo Mheshimiwa Ndalichako nilikwishakuja nikakuambia tayari nina maboma 69 katika kuongezea katika idadi ya wanafunzi walioingia, kwa hiyo naomba unisaidie tu shilingi milioni 48 kwa ajili ya kuezeka maboma hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, napenda kuishukuru Serikali yangu, tayari katika Jimbo langu la Kavuu nimeweza kutatua tatizo la madawati, nilikuwa na upungufu wa madawati 1,000 na nimeyatatua na sasa hivi nayagawa shuleni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende moja kwa moja katika Vyuo vya Maendelo ya Wananchi. Vyuo vya Maendeleo vya Wananchi vinatuchanganya na kozi ambazo zimekuwa zikitolewa na VETA, niombe sana hili liangaliwe na wakati mwingine tunashindwa kuelewa ama viko chini ya Wizara ya Afya kwenye Maendeleo ya Wananchi ama viko Wizara ya Elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, chuo kilichopo Mkoa wa Katavi cha Maendeleo ya Wananchi, Chuo cha Msanginya bado hakijaanza kufanya lolote na miundombinu yake siyo. Naomba ukiangalie kwa hali ya kipekee ili tuweze kupeleka watoto wetu pale hasa wa kike ambao hawafiki form four waweze kujifunza maarifa mbalimbali ambayo yanaweza kuwasaidia kutatua matatizo yao katika maisha yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine naomba niongelee kuhusu malipo na madai mbalimbali ya walimu. Kimekuwa ni kilio cha muda mrefu. Mimi ni mwalimu, nimeanza kufundisha Chuo cha Ualimu Sumbawanga kama first appointment yangu pale, ninafahamu matatizo ya walimu. Nimefundisha Mpanda Girls ambapo niliomba ni shule iliyokuwa na form one mpaka form four na ilijengwa kwa msaada wa DANIDA. Kwa hiyo ninaomba kwa sababu sasa hivi mmeiweka kama form five na form six naomba ianze form one boarding mpaka form six ili na sisi Mkoa wa Katavi watoto wetu wapate nafasi ya kuweza kusoma katika ile shule ambayo ni moja ya shule kongwe ambazo zilijengwa kwa ajili ya kuwasaidia watoto wa kike pale Mpanda Girls. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee suaa la TEHAMA, suala hili naomba uliangalie vizuri. Katika shule zangu za msingi, nimefanya ziara katika shule zangu za msingi Jimbo zima, TEHAMA shuleni wanasoma kwa nadharia. Kwa hiyo ninaomba computer, Serikali ifanye utaratibu wa kupeleka madarasa ya computer pamoja na computer kwa ajili ya walimu wa shule za msingi na wanafunzi wa shule ya msingi angalau kila shule moja iwe na darasa moja na upendeleo uanze na Jimbo la Kavuu ili tuweze kufanya maendeleo kwa sababu ni Jimbo ambalo liko vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee hili suala la kuhamisha walimu kuwatoa sekondari kuwapeleka shule za msingi. Kwa kweli halijapokelewa vizuri, kwa mwalimu linaonekana kama ni adhabu, basi naomba wapelekwe special course kwa ajili ya kufundisha shule za msingi kwa sababu wao walifundishwa methodology shuleni kwa ajili ya kufundisha shule za sekondari.

Kwa hiyo, tunaomba sasa kama mnawapeleka kule, muwapeleke na special course kwa ajili ya kujielekeza katika masomo ya shule za msingi bila kuathiri madaraja yao pamoja na vyeo vyao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda niongelee suala la asilimia mbili ambayo walimu wamekuwa wakikatwa kwenye mshahara. Tunaelewa kuna kipindi Bunge lililopita tuliongea hapa tukasema kuwe na mikataba, wanaopenda wasaini wakatwe na wasiopenda wasikatwe. Tunajua ni jambo la kisheria lakini sheria inaweza ikaletwa hapa na pia ikafanyiwa kazi ili tuone walimu tunawasaidiaje. Tunawakata asilimia mbili katika mshahara wao kila mwezi na Chama cha Walimu, Chama cha Walimu kina ghorofa pale ni mtaji lakini walimu bado wanashindwa kukopeshwa kwa ajili ya maendeleo ya maisha yao. Wanashindwa kukopa katika mshahara ambao wanakatwa waweze kujenga maisha yao yawe vizuri hasa kwenye nyumba zao wanazotakiwa kuishi. Kwa hiyo, niombe sana hili mlifikirie na mliangaie. Walimu wengi wamekuwa wakilalamika kuhusu hii asilimia mbili ambayo na mimi nilikwishakatwa na ninaidai kwa sababu siko huko tena, kwa hiyo napenda irudishwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee usawa wa elimu. Tunajua elimu ni haki ya kila mwanafunzi. Naongelea shule za private na shule za Serikali. Kwa kuwa matokeo ya ufaulu yanaonesha bado ni tatizo na shule nyingi za Serikali ziko vijijini, mwanafunzi wa kijijini anatembea umbali mrefu. Kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha mwanafunzi wa Serikali asifanye vizuri hasa aliyeko kijijini. Ninaomba muangalie namna mtakavyokuwa mnaandaa mitihani sasa kwa ajili ya watoto hawa wanaoenda na magari, wanaokula shuleni na wale wanaotembea kwa miguu ili usaili wao uwe tofauti, usiwe unaofanana kwa sababu wako katika mazingira tofauti ili tuweze kuona tatizo liko wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee shule yangu Maalum ya Majimoto. Nina shule pale ya Majimoto Mheshimiwa Profesa Ndalichako. Ninaomba kama utaweza kutuma wasaidizi wako wakafika katika ile shule, Halmashauri yangu imejitahidi imejenga miundombinu mizuri, tuna mabweni lakini bado tuna mambo machache ambayo tunahitaji Serikali Kuu itusaidie na tunaomba shule hiyo sasa irudi Serikali Kuu itoke Halmashauri ili iweze kuwasaidia watoto wote wenye mahitaji maalum. Ni shule nzuri tumejitahidi kuitengeneza pale, naomba Profesa kwa jicho la pekee utume watalaam yako ije iangalie ile shule tuweze kuona tunaweza kuifanyaje ili iweze kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum hasa wale wenye ulemavu na wengineo ni shule ambayo tayari tuna mabweni matatu tumekwishajenga, tuna madarasa manne na tuna vyoo ambavyo tumetengeneza miundombinu kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali. Kwa hiyo, nakuomba sana shule yangu hii kama kawaida yangu nitakuletea special request na mahitaji yake ili muweze kuona mnatusaidiaje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda niishukuru Serikali yangu na naipongeza kwa namna pekee ambavyo imekuwa ikifanya kazi chini ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Napenda niwashukuru Wizara ya Elimu, Mawaziri wote wa Serikali hii kwa sababu wamekuwa ni wasikivu. Ndugu yangu Joyce Ndalichako ni msikivu sana, ni mwalimu wangu wa statistics wakati nikiwa chuo kwa sababu mimi nilisoma elimu ya MEMKWA mpaka nimepata Udaktari na hivi naenda kupata Uprofesa. So lazima nijipongeze. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nakuomba sana Mheshimiwa suala la elimu tuliwekee mkazo ili na sisi kule watoto wetu kule vijijini wawe maprofesa, wawe wahandisi, tunajua tunaenda kwenye mfumo wa viwanda lazima turekebishe mfumo wetu wa elimu. Lazima tuone kwenye sayansi na teknolojia kuanzia kwenye vyuo vya ufundi, kwenye VETA ambao wakati mwingine tunaweza tukawa tunawadharau lakini hawa ndio watu wazuri ambao wanaweza wakatufanyia miradi yetu mizuri sana katika uchumi unaokuja na viwanda ambavyo tunatarajia kufunguliwa na Serikali yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakuomba sana Mheshimiwa Joyce Ndalichako, suala la elimu sawa naomba muangalie na mitaala pamoja na mitihani mtakayoweza kuwa mnaitunga kwa differences ya mazingira kati ya wanafunzi hasa wa vijijini na wale wanaokwenda na mabasi ya Martin Luther, Ignatius na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kabisa kwa namna ya pekee uweze kuliweka hili suala ili uweze kuona ni namna gani ambavyo tunaweza kuwasaidia watoto wetu.

Kwa hiyo, naomba kabisa suala hili Serikali mlitilie mkazo. Ni mawazo yangu binafsi ambayo baada ya kutembelea hali halisi na kuiona shuleni ni mawazo yangu binafsi ninayowasilisha Bungeni kama Mbunge kuishauri Serikali.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi niweze kuchangia katika bajeti hii iliyoko hapa mbele yetu. Kwanza kabisa, napenda niishukuru Serikali yangu kwa namna ambavyo imekuwa ikijitahidi kwa namna pekee kutatua matatizo ya wananchi japo kuna changamto mbalimbali hasa katika ukusanyaji wa pesa.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda niwashukuru Mawaziri, viongozi na watumishi wa Wizara hii kwa namna ambavyo wameweza kuyapokea baadhi ya maoni ambayo tuliweza kuyatoa katika bajeti ya mwaka 2016/2017 ambayo ni pamoja na kuondoa baadhi ya kodi kwenye bidhaa mbalimbali zikiwemo taulo za kike kwa ajili ya watoto wetu wa kike, nashukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili, nimwombe Mheshimiwa Mpango ashirikiane na sekta zingine kwa ajili ya kudhibiti ubora wa hizi bidhaa ambazo mmeziondolea kodi. Kwa sababu wakati mwingine zitakuwa zinamnufaisha yule mfanyabiashara mkubwa na siyo mtumiaji. Kwa hiyo, tunategemea sana hizi bidhaa zitashuka bei. Naomba sana muangalie hilo na uwe ni uangalizi wa hali ya juu kwa sababu mara nyingine tutajikuta tunamsaidia tu yule mfanyabiashara mkubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nije kwenye mapato ya ndani na naomba niongelee ukwepaji wa kodi.

Si kwamba wananchi hawapendi kulipa kodi, wananchi wetu wakipata elimu ya kodi wako tayari kulipa kodi na waelimishwe ni kodi zipi wanapaswa kulipa. Kumekuwa na mlolongo wa kodi nyingi mno ndizo hizo zinamfanya mtu aone kwamba kwa nini kodi zimekuwa nyingi, leo una hii, kesho hii na hii. Ndiyo maana unakuta wananchi wakati mwingine wanaona maafisa wa TRA wanatoweka, siyo kwamba hawapendi, wapeni elimu ili wananchi waweze kulipa kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilishampa Waziri maombi yangu aniletee wataalam wa TRA wa kodi waje jimboni kwangu, wawafundishe wananchi haya mambo waweze kuzijua hizo kodi mbalimbali wanazotakiwa kulipa. Zipo kodi zenye kero mpaka leo kama hotel and service levy katika baadhi ya halmashauri. Naomba mliangalie upya na muweze kulichanganua wananchi walielewe hata kwa kutumia vyombo vya habari. Naomba wananchi wapewe elimu wanapaswa kulipa nini kwenye hii hotel and service levy hasa kwenye zile guest house ndogo za vijijini ambazo zinasubiri siku ya mnada wale wauza ng’ombe waende wakalale pale, naomba mziangalie sana. Kwenye halmashauri zingine hasa ya kwangu wananchi bado wanateseka na hawazielewi lakini halmashauri wanalazimika kukusanya kutokana na miongozo waliyopelekewa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine naomba niongelee kodi za zimamoto. Kodi za zimamoto ni kero. Leo ukienda kununua kiwanja lazima utaambiwa ulipe kodi ya zimamoto, ni mchimbaji mdogo mdogo utalipa shilingi milioni mbili ama tatu, hazina kiwango, hazieleweki, unaanza ujenzi unatakiwa kulipa kodi ya zimamoto. Sasa zimamoto hiyo huduma iko wapi mpaka mtu unamchaji hiyo kodi ya zimamoto? Kwa mfano, kwangu Kavuu, hiyo zimamoto iko wapi? Wanatoka Mpanda Mjini wanaenda kulala kule kwa ajili tu ya ku-harass wafanyabiashara wadogo wadogo wenye guest houses kwa ajili ya hizi kodi za zimamoto. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeshampelekea Waziri malalamiko haya ya wananchi wangu naomba suala hili alisughulikie. Waziri alinipa Kamishna wa Kodi akaniletea bundle la sheria, mimi sio mwanasheria. Kwa hiyo, naomba sana tunapoleta concern zetu zinazotoka kwa wananchi mzishughulikie. Naomba hili la zimamoto lishughulikiwe specifically katika Jimbo langu la Kavuu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee suala lingine la ulimbikizaji wa madai mbalimbali ambayo bado wanaendelea kuhakiki. Uhakiki umeanza muda mrefu, sasa ifike mahali tuumalize huo uhakiki tuwalipe stahiki zao watumishi hasa katika sekta ya afya na sekta ya elimu. Naomba tufike mahali uhakiki sasa uishe na tuendelee mbele. Mheshimiwa Chenge ametoka kusema hapa tusipende kwenda mbele na kurudi nyuma, naomba twende mbele. Tukitembea haturudi nyuma hatua zinakwenda mbele na sisi tunataka twende, mbele ndiyo maendeleo. Kwa hiyo, naomba sasa tufike mahali tuwe na ukomo wa huu uhakiki, twende mbele ili tuone tunataka kuwasaidiaje watumishi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nije kwenye vipaumbele katika bajeti hii, nianze na kilimo. Kwa kweli bado hatufanyi vizuri, naomba tukiri ukweli katika sekta ya kilimo, uvuvi na mifugo. Hata leo tukiangalia bajeti yao, ukiijumlisha sidhani kama inafika shilingi bilioni 100 kwa sekta zote tatu. Sasa hivi tumejikita kwenye miundombinu, reli hizo zinajengwa najua itafika mpaka Karema kwetu kule ili tuvushe mizigo mpaka Kalemii (Kongo) lakini tutasafirisha nini? Kama kwenye production hatutaki kwenda sambamba na uwekezaji katika miundombinu, haya mazao hayapo, miundombinu ipo sidhani kama inakaa vizuri. Kwa hiyo, kama kweli tuna nia ya dhati, naomba tuwe na ulinganisho kati ya production na hizi means za usafirishaji. Kwa maana kwamba mazao yetu sasa ndiyo yatabebwa na hizo reli ili yaweze kusafirishwa tupate kurudisha pesa ambayo tutakuwa tumeitumia katika kujenga reli hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia upatikanaji wa pembejeo bado ni tatizo. Mwaka jana katika bajeti hii niliongea, nikasema nawaomba muangalie jiografia na hali ya hewa ya maeneo mbalimbali. Kwa mfano, Mikoa ya Kusini Magharibi mvua zake zinaanza mapema, sasa mvua zinaanza mwezi wa tisa unapeleka pembejeo mwezi wa kumi au kumi na moja, unategemea nini kwa mkulima?

Mheshimiwa Naibu Spika, pia angalia katika msimu wa mwaka huu kilimo cha mahindi imekuwa ni kilio kila sehemu na huyo mdudu mnayesema ametoka America sijui alikuja na nini, hata sijui? Kutoka America mpaka Tanzania tena Tanzania yenyewe Kavuu ambako sina hata barabara sasa sijui huyo mdudu alikujaje, ninyi wataalam mnajua. Naomba sana myaangalie haya mambo pindi mnapokuwa mnaleta vitu hivi hasa pembejeo kwa wakulima. Kama mnafanyia utafiti wa kutosha ni vyema mkaleta kule lakini ni vyema pia zikawahi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuangalie pia kwenye uvuvi na mifugo. Leo hii gumzo ni kupima samaki kwa rula, jamani! Hebu tufike mahali tuone tunafanyaje kazi, tusikurupuke.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nije kwenye huduma za jamii hasa upatikanaji wa maji. Tulipendekeza kwenye bajeti iliyopita kwamba iongezeke tozo ya Sh.50. Sasa hivi tuna tozo ya Sh.50, tukapendekeza iongezeke Sh.50. Leo umekuwa shahidi maswali ya maji yaliyokuwa yakiulizwa ni upatikanaji wa maji kwenye shule za msingi, sekondari, A- Level. Siyo hivyo tu, akinamama wanabakwa na wanauawa kwa imani za kichawi wanapokwenda kutafuta maji na mama sasa hivi hawezi kutembea peke yake. Nayaongea hayo wenzangu wa Shinyanga mnayafahamu, jimboni kwangu yanatokea, wanawake hawawezi kwenda kuchota maji sasa hivi kutokana na umbali mrefu kuogopa imani za kichawi za kunyongwa na kutupwa hovyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Waziri aongeze tozo hii ili maji yaweze kutosha tuwe na tozo ya Sh.100 katika Mfuko wa Maji. Nina uhakika tutayatatua haya matatizo na tutawaondolea vifo ambayo si vya lazima akina mama. Kwa sababu sasa hawaendi mabombani kwa kuogopa kunyongwa, ni mbali. Hebu ongezeni hii pesa ifike Sh.100. Tumepunguza bei ya hizi pads kwa nini sasa tusiwawekee maji shuleni? Unakuta mtoto ana fagio, dumu na begi anaenda shuleni. Naomba sana ongezeni tozo ya Sh.50 ili tuwe na uhakika wa kupata maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kwenye elimu na afya, naomba muongeze pesa na iweze kutoka kwa wakati. Halmashauri hazina pesa za kutosha kutekeleza miradi, naomba Serikai yangu sasa ule ucheleweshaji wa kupeleka pesa kwa ajili ya miradi kwenye halmashauri na wenyewe ufikie ukomo. Pindi tunapopitisha bajeti, pesa ziende kwa wakati na miradi itatekelezwa kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, mengine nitaandika kwa maandishi lakini naunga mkono hoja. Ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi asubuhi hii nami niweze kuchangia katika Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa napenda niishukuru Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kupitia Wizara hii imeweza kufanya mambo makubwa katika Sekta zote hizi za Uchukuzi, Mawasiliano na Ujenzi, hasa katika ununuzi wa ndege, upanuzi wa viwanja vya ndege, ujenzi wa reli ya kisasa na mengineyo. Kwa ujumla naomba niwashukuru na niwapongeze viongozi wote wa Wizara kuanzia Waziri na Watendaji wake ambao siyo rahisi kuwataja mmoja mmoja, lakini kwa umoja wao wameweza kufanya kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze na suala la barabara ya Tabora mpaka Mpanda. Naiongelea hii barabara kwa sababu imeanza kusemwa toka mwaka 2005 mpaka leo hii. Nami nafahamu kwamba Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli akiwa Waziri wa Ujenzi, alishaiombea fedha kupitia Benki ya Afrika. Sasa sielewi kunasuasua nini? Kwa sababu ukiangalia kila kipande kipande kina viasilimia; kuna asilimia 12 Kasinde - Mpanda, kuna asilimia 18; Urila kuna asilimia 15.9.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hizi asilimia hatujui tunazipimaje na hatuelewi hii barabara pamoja na kwamba ilishapata fedha, itakwisha lini ili iweze kuwasaidia wananchi wa Mkoa wa Katavi, Tabora, Rukwa, Mbeya na wote watakaopita ile njia pamoja na wananchi wangu wa Jimbo la Katavi, Jimbo la Kavuu, (samahani Jimbo la Katavi ni la Mheshimiwa Waziri), Jimbo la Kavuu na Wajimbo la Katavi wenyewe kupitia Inyonga ili waweze kupita kwenda mpaka Mwanza, mpaka Kahama waweze kufanya biashara zao? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia, naomba niongelee suala la Mfuko wa USCAF. Napenda niwashukuru mfuko huu wameweza kufanya kazi kwa uwazi na kwa namna ambavyo wananchi wameweza kuuelewa sasa, kwa sababu mwanzo walikuwa hawauelewi lakini leo wananchi wanaelewa chini ya Eng. Ulanga na wengineo wote wanaofanya nao kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama kawaida yangu ndani ya Jimbo la Kavuu, lazima niombe masuala yote yanayohusu maendeleo. Kupitia Mfuko huu wa USCAF naomba Kata nzima ya Maji Moto na vitongoji vyake na vijiji vyake iweze kupata mawasiliano ya uhakika. Naomba Kijiji cha Mawiti, Kabunde, Mainda, Lunguya, Ikupa, Luchima, Kanindi, Minyoso, Kwamsisi, kote naomba niweze kupata mawasiliano. Ni vijiji ambavyo havina mawasiliano. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri Watendaji wako hapa na Mheshimiwa unapafahamu huko kote, naomba wananchi hawa wapate mawasiliano ili tueweze na sisi kwenda kisasa, tuweze kufanya biashara za kupitia mitandao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nirudi kwenye suala la Shirika la Reli. kwenye suala la Shirika la Reli, mimi toka nimeingia humu nimekuwa nikiongelea Shirika la Reli hasa kwa usafiri wa kutoka Mpanda – Tabora, Tabora – Dodoma, mpaka Dar es Salaam. Jamani, kuna kipindi alikuwa Mheshimiwa Waziri Mwakyembe, nikamwambia kule siyo mabehewa ya kukaa binadamu. Nilishaongea mwaka 2017 kwamba basi waangalie namna bora ya kubadilisha hata mabehewa, wananchi wale waweze kuingia kwenye mabehewa safi na salama. Mabehewa yale ni machafu, yemechoka. Kwa nini yaletwe Mpanda? Kama yamechoka, yakawekwe Morogoro, mtuletee mabehewa mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongee kuhusu mpango wa anuani za makazi wa Post Card; mpango huu ni mzuri sana. Tumetenga fedha nyingi sana. Nawaomba Watendaji tufanye vizuri. Leo ukitoka hapo nje ukienda Chuo cha CBE, ile tuliyoweka pale imeshang’oka. Sasa tuweke imara zaidi. Ni mpango mzuri unaoweza kutambulisha nchi yetu vizuri na ni kwa utaratibu wa maendeleo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niwaombe, hebu tuongeze ile value for money katika huu mradi kwa sababu hauna impact, hata ukitembea hapa kwenda hapo stand Kimbinyiko. Bado haijakaa vizuri. Kwa hiyo, naomba sana tuboreshe hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nirudi katika barabara ya Kibaoni – Maji Moto – Inyonga, bado inafanyiwa upembuzi yakinifu na nini. Naomba Mheshimiwa Waziri aje na majibu. Hii pia ni ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kutoka Maji Moto mpaka Inyonga kwa kiwango cha lami, lakini pia kutoka Kibaoni; siyo Kibaoni tu mpaka Inyonga, mpaka Kansansa, Klyamatundu.

Mheshimiwa Naibu Spika, najua tumejenga daraja la Momba, Serikali yangu imefanya vizuri, nashukuru tunaipongeza, lakini hii barabara pia lazima tuifungue ili wananchi hawa wa Jimbo langu la Kavuu waweze kutoka Kansansa ama Maji Moto, ama Kibaoni mpaka waweze kufika Mbeya, Mbeya waweze kwenda Kalambo, Kalambo waweze kwenda Kasesha, Kasesha waweze kwenda Mpulungu, waingie Zambia, waingie Mozambique waweze kufanya biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kila siku naliongea hili. Lazima tuangalie sasa ni namna gani tutatanua wigo wa kutoka Tunduma na wa kutoka Kalambo ili tuingie mpaka Mozambique. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nirudi niongelee sasa daraja langu la Msadya. Daraja hili naomba Waziri anisikilize vizuri, nimekwishapeleka maombi, najua linahudumiwa na Ofisi ya TAMISEMI kupitia TARURA, lakini TARURA hawa ni Wizara hii ndiyo wanawapatia pesa. Leo ni mwaka wa tatu wananchi wangu wa Kata ya Mbebe, Mwamapuli, Chamalendi mpaka wanaotoka Kibaoni hawawezi kufika Usevya ambako kuna kituo cha afya nilichosimamia mwenyewe na Mkurugenzi wangu cha mfano! Pia Mheshimiwa Ummy alishafika pale akakiangalia, ni cha mfano, niwaombe sana wanitengee pesa kwa ajili ya hili daraja ili wananchi wangu waweze kupata huduma pale. Hawapati huduma mpaka sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee suala la barabara ya Mpanda mpaka Kahama…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa, kengele ya pili imeshagonga. Ahsante sana.

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja na naomba yote haya niliyoyaeleza yachukuliwe kwa umuhimu wake. Ahsante. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi nami niweze kuchangia katika hotuba hii. Kwa sababu muda ni mchache, naomba niende moja kwa moja kwenye mchango wangu.

Mheshimiwa Spika, naomba niende kwenye Fungu 05 - Tume ya Umwagiliaji ambapo katika maelezo ya hotuba inaelezea kujenga na kuboresha na kukarabati skimu za umwagiliaji. Nakuja kwenye Mkoa wa Katavi, Serikali katika hotuba yake imesema itakarabati skimu 16 na nyingine kujenga tano, nafikiri hii ni Tanzania nzima kama sikosei, maana hawajaielezea vizuri. Hata hivyo, ukirudi katika Mkoa wa Katavi skimu ambazo hazifanyi kazi ni skimu sita, skimu ambayo inafanya kazi ni skimu moja na hii skimu nafikiri ni ile ya Urwira, iko katika Kata ya Urwira, Jimbo la Nsimbo ambayo nafikiri inafanya kazi kwa sababu tu iko chini ya usimamizi wa Kanisa Katoliki.

Mheshimiwa Spika, narudi ambazo hazijajengewa miundombinu ziko 84, ambazo zimejengwa baadhi ya miundombinu ziko 35, jumla ya skimu Mkoa wa Katavi ni 126 na inafanya kazi moja. Je, kweli, tuna nia ya dhati katika kuleta mapinduzi ya kilimo ambayo mazao yake ndio sasa yanayoenda kutumika katika viwanda ambayo tunasema uchumi wa viwanda, naomba tuwe serious katika hili ndugu zangu.

Mheshimiwa Spika, narudi sasa mimi, katika skimu hizo hizo naona zisizofanya kazi Skimu za Mwamapuli na Skimu ya Kilida hazimo kabisa. Skimu ya Mwamapuli katika bajeti ya mwaka juzi iliwekwa kwenye mpango mkakati wa Serikali, wa Taifa. Sasa nauliza na hela ile ilitengwa karibu bilioni mbili, sasa sielewi zilikwenda wapi?

Mheshimiwa Spika, huu mradi ninaosema Skimu ya Mwamapuli katika Kata ya Mwamapuli, Jimbo la Kavuu, nauongelea huu mradi kwa heshima kubwa ya Mheshimiwa Mstaafu Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mizengo Pinda. Alitujengea pale mradi mkubwa wa kinu kikubwa cha kuchambulia mchele kwa kutegemea kwamba, hii skimu sasa ingelisha kwenye hiki kinu, lakini mpaka leo hii, kile kinu kinaoza, hakifanyi kazi yoyote, wakulima wamejiandaa pale, tuna mbuga kubwa sana pale na skimu hiyo ni kubwa. Nashangaa kwa nini, na kwenye Wizara ya Maji nimeiongelea, nashangaa kwa nini haichukuliwi hatua? Naomba Serikali sasa inipatie majibu kwa nini skimu hii imeachwa haimo kwenye bajeti kabisa? Skimu ya Mwamapuli na Skimu ya Kilida. Skimu ya Kilida ni matengenezo tu inahitaji, lakini na yenyewe hawajaiweka kabisa. Kwa hiyo, naomba sasa watakapokuja waje na majibu wanieleze kwa nini skimu hizi mbili hawajaziweka kabisa? Pia kwa nini Mkoa wa Katavi iko skimu moja tu wakati tuna skimu 126, skimu moja tu ndio inayofanya kazi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niwaombe sana, narudi kwenye Jimbo langu la Kavuu, nataka wanieleze kwa nini Mradi wa Skimu ya Mwamapuli pamoja na Kilida haumo kwenye bajeti? Je, hauna umuhimu kwa wananchi? Je, ilikuwa haifanyi kazi? Miradi yote hii ilikuwa inafanya kazi. Sasa naomba waniambie kwa nini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niongelee suala la pembjeo, hasa kwenye upande wa mbegu. Nataka nijiulize, nimekaa nikijiuliza sana kwani ni lazima kila mwaka mwananchi anunue mbegu? Je, katika zile mbegu wanazokuwa wamezileta mwaka huu, je, mkulima amelima, mimi nakumbuka zamani tulikuwa tukilima, mnachagua mahindi ambayo ni mazuri mnayahifadhi kwa mbegu; je, hizo mbegu zikihifadhiwa zikatumika kwa mwaka unaofuata hazifai? Naomba niulize swali hili kwa sababu, tumekuwa na ucheleweshaji wa mbegu ambazo sasa wakulima wanakuwa hawapati. Nilikwishasema maeneo mbalimbali yana mvua tofauti, kwa mfano katika Jimbo langu la Kavuu mimi kuanzia mwezi wa 11 mvua zinaanza kunyesha, pembejeo wanaanza kuleta mwezi wa Tatu, sasa je, mtu akihifadhi mbegu alizolima mwaka huu akahifadhi akapanda mwaka kesho, hizo mbegu hazifanyi kazi? Nawauliza kupitia kitengo chao cha utafiti? Maana tunataka kujua kwa sababu, hata hizo wanazoleta kila mwaka bado hazioti na hazifanyi vizuri. Kwa hiyo, naomba watufafanulie katika hayo.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Wananchi wangu wamenisikia. Nakushukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia katika haya yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ilipanga na imepanga kuendelea kujenga Mabwawa na malambo kwa ajili ya kunyweshea wanyama (Mifugo). Je, ni lini sasa mabwawa na malambo hayo yatajengwa katika Jimbo la Kavuu Halmashauri ya Mpimbwe Mkoa wa Katavi?

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango gani wa kuhamisha ufugaji wa kuku wa kienyeji katika maeneo ya kijijini hasa katika maeneo ya vijijini kama maeneo ya Jimbo la Kavuu?

Mheshimiwa Spika, kupitia Wizara hii kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Wanyamapori iainishe mipaka kati ya hifadhi na matumizi ya mifugo.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipatia niweze kuchangia katika hotuba hii ya Maliasili na Utalii. Kwanza kabisa napenda niwapongeze Mawaziri wote na viongozi wote wa Wizara chini ya Serikali ya Awamu ya Tano kwa namna ambavyo mmekuwa mkifanya kazi kwa bidii.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende moja kwa moja katika Sheria ambayo inaongelea mazao ya misitu ambayo ni Sheria ambayo inasema kwamba ni The Forest Act Cap 323 ni Sheria ya TFS agency ambayo schedule yake namba 8 na 14 zilizofanywa marekebisho kwa mwaka 2017.

Mheshimia Naibu Spika, naomba niende moja kwa moja kwenye fees na loyalty for forest product and services. Nimesimama hapa kutokana na malalamiko ya wananchi ambao Sheria hii imekuwa kwao ni kandamizi, imekuwa kwao ikiwaonea na kama ilikuwa ikifanya kazi kipindi kile kwa sasa hivi nafikiri haiko sawa sawa. Kwa hiyo ni vyema sasa niiombe Wizara waweze kuileta hii Sheria tuweze kuifanyia marekebisho iende na wakati kutokana na kwamba Mheshimiwa Rais amekwishatamka tozo zozote na fees zozote tunazoona kwamba zinawakandamiza wananchi tuzirekebishe ili tuweze kuendelea kupata mapato kwa urahisi na kwa wingi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano ninaongea nini shatter ya milango kwa one piece shatter ya mlango, kutoka Mpanda Mjini kwenda Jimboni kwangu Kavuu halmashauri moja kwenda halmashauri nyingine wanatozwa per piece one shatter shilingi 50,500. Fremu moja ya mlango ama dirisha moja kutoka Mpanda Mjini kwenda Jimboni kwangu Kavuu shilingi 51,800, wakati shatter ya mlango pale Mpanda ataitengeneza kwa shilingi 22,000, mnamtoza 50,000 bado hajasafirisha kwenye gari kutoka Mpanda kwenda wapi kwenda Kavuu. Hii maana yake nini, maana yake mnawaambia wananchi wangu wa Kavuu hawapaswi kutoka kwenye umaskini kwenda kwenye kima cha kati, kwa maana kwamba lengo tunataka kujenga uchumi wa kima cha kati.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ni lazima sasa hizi fees tuziangalie, lakini utakuta kuna kitanda shilingi 20,000, uyoga shilingi 200, sasa yaani unashindwa kuelewa, kiti ama stuli shilingi 17,250, dawati la shule mzazi ametengeneza dawati anapeleka kule Kavuu shilingi 17,250 kutoka halmashauri kwenda halmashauri yaani inamaana hizi ni fees ndani ya Mkoa mmoja. Kitu ambacho nafikiri ilikuwa imewekwa kwa ajili ya ku-discourage labda wale wafanyabiashara wakubwa wanaosafirisha mininga labda kutoka Inyonga kule kupeleka Mkoa mwingine na kwamba Mkoa mwingine unazilipia hizo fees.

Kwa hiyo, nilikuwa naomba sana mfano mkeka ama kikapu unaambiwa ulipe shilingi 1,700, vitu vidogo vidogo vinavyotokana na mbao nikimaanisha labda mwiko, kijiko kwamba shilingi 1,700. Sasa nashindwa kuelewa, kama tunaona hizi zimekuwa ni kero naomba tuziondoshe kama Rais anavyoelekeza ili wananchi waweze kulipa vizuri na tuweze kuongeza mapato kwa wingi kwa sababu haiwezekani ndani ya Mkoa uka-charge hivi vitu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna mila na desturi, binti anapoolewa anapewa kitanda, anapewa sofa, atapewa godoro hivyo vitu vyote lazima alipie sasa inakuwa kwa kweli haileti maana kabisa hata kidogo. Ukizingatia kwangu ni halmashauri mpya sitarajii na wala hatutarajii kuwe mafundi wengi wa kusema kwamba kule watajitosheleza wasiweze kusafisha, kwanza Mininga sasa hivi hakuna ndiyo tunaanza kusubiria ianze kuota upya kwahiyo naomba sana muangalie.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba nikumbushie tena kuhusu suala langu katika Kata ya Mwamapuli, Kata Luchima, Kata ya Majimoto Kijiji cha Luchima; pale tuliwaomba na TANAPA wamekwishaanza kutengeneza kisima kile. Naomba kisima kile kimaliziwe ili tuondoe mgogoro kati ya wananchi wanaotumia maji katika ule mto unaopakana na mbuga. Wananchi wamekuwa wakipigwa sana na Askari wa TANAPA na nimekwishaongea na wamekwishaanza kwanini hawamalizii kile kisima ili tuondoe migogoro inayotokea kati ya Wannachi pamoja na hao watu wa TANAPA.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba niulize na naomba tena niongelee suala lingine; Askari wa TANAPA kati ya mwaka juzi na mwaka jana katika Kata ya Kibaoni walimgonga Mama mmoja pale na kwa bahati nzuri nafikiri nilikuwepo Jimboni yule Mama alifariki pale pale. Sasa naomba nielewe ni fidia ili mtampa yule Baba, huyo ni Mzee pale anaitwa Mzee Lusambo mke wake ndiye aliyegongwa na gari na wale TANAPA hawakusimama walipitiliza walichofanya ni kusaidia tu maziko. Kwa hiyo, nilikuwa naomba ni namna gani huyu Mzee Lusambo sasa kupitia kifo cha mke wake mtampa fidia ili naye aweze kuona kwamba angalau Serikali imeweza kumjali kwa sababu wanapita kwa speed kali kiasi kwamba inabidi muwe waangalifu na kuangalia namna ambavyo mtavuka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nirejee katika kisima change cha Luchima, naomba kikamilike na ikiwezekana kikamilike mapema iwezekanavyo, Mheshimiwa Naibu Waziri uliniambia kwamba umekwishaongea na watu wa TANAPA na najua wako hapa, Mkurugenzi Kijazi yuko hapa, naomba sasa umuelekeze kile kisima kiishe haraka iwezekanavyo kabla ya Septemba kiwe kimekwisha na Wananchi waanze kutumia maji yale kuepuka vurugu ambazo wanazipata kutokana na Askari wa TANAPA.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo sina mengi zaidi ya kuiomba Serikali ilete hiyo Sheria ili tuweze kuifanyia marekebisho Wananchi waweze kunufaika na mazao na vitu vyao wanavyosafirisha. Meza imekwishatumika una sababu gani ya kum-charge mtu wakati ana hama kutoka halmashauri moja kwenda halmashauri nyingine? Na siyo kitu kipya na wala hakijazidi hata tani moja kwanini um- charge? Kwa hiyo, hizo ndiyo kero ambazo naziwakilisha kutoka kwa Wananchi wangu wa Jimbo la Kavuu ambao wamekuwa wakilalamika kila siku namna wanavyo hapa kutoka Mpanda Mjini kwenda Kavuu kwa ajili ya kufanya shughuli zao za maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kunipatia nafasi hii, naunga mkono hoja, naomba Serikali mzingatie haya yote niliyokwisha waeleza, ahsante sana, naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi nami niweze kuchangia katika hotuba hii muhimu ya Nishati. Kwanza kabisa napenda niwapongeze viongozi wa Wizara hii wakiongozwa na Dkt. Kalemeni pamoja na watendaji wengine Wizara.

Mheshimiwa Spika, naomba niende moja kwa moja katika ukurasa wa 44 katika hotuba ya Waziri ambao unaongelea mradi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa KV 400, mradi ambao unaanzia Iringa unakuja kufika mpaka Nyakananzi na unatekelezwa kwa awamu tatu. Niwashukuru kwamba mradi huu umeweza kuwekwa hata kwenye mpango na katika kazi zilizofanyika 2018/2019 ni pamoja na upembuzi yakinifu kati ya Mbeya na Sumbawanga na uthamini wa mali kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, sasa nimwombe Mheshimiwa Waziri kwa kuwa mradi huu umeshafanyiwa uthamini na upembuzi yakinifu, basi ni vema sasa wakatafuta huyo mkandarasi wa kuweza kuratibu mradi huu ili uweze kufanya kazi. Kwa nini nasema hivyo? Kwa sababu umeme wanaotumia hasa kutoka tunduma mpaka Sumbawanga umeme ule mwingi unatoka Zambia na umekuwa ukikatika mara kwa mara. Sasa tuondoshe hii adha ya wananchi wa maeneo haya ambao ni pamoja na Jimboni kwangu Kavuu katika Kata ya Kibaoni ambapo pia wanatumia umeme huu ambao umekuwa ukikatika mara kwa mara na hivyo kuwafanya wananchi ambao wamejiajiri kupitia sekta hii kutoweza kufanya maendeleo yao vizuri.

Mheshimiwa Spika, naomba nirudi katika Kata yangu ya Kibaoni katika Jimbo la Kavuu. Naomba niongelee transformer ya Kijiji cha Mirumba, transformer hii imekuwa ni tatizo, kila leo nimekuwa nikisema. Kwa hiyo naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja anieleze tatizo lipo wapi katika transformer katika Kijiji cha Mirumba ambayo inapokea umeme kutoka Sumbawanga kupeleka pale Kibaoni ambapo umekuwa ukikatika karibu kila siku, kila siku kwa kisingio cha transformer. Kwa hiyo niombe kama transformer hiyo ni mbovu naomba mbadilishe transformer pale ili wananchi waendelee na shughuli zao za utekelezaji wa shughuli zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nije katika Mradi wa REA awamu hii, naishukuru sana Serikali kwa sababu wameweza sasa na sasa hivi ninavyoongea wakandarasi wapo kule jimboni kwangu katika Kata ya Majimoto na Kasaka wakiendelea na kuweka nguzo. Kwa hiyo niombe sasa katika vijiji vilivyorukwa katika Kata ya Kasansa, ambavyo nasema ni Iziwasungu, Majimoto kuna Kijiji cha Luchima ukija Mbede kuna Kijiji cha Kansisi ukija Mbede hapo hapo kuna kijiji cha Nyambwe ukija Kata ya Majimoto kuna Kijiji cha Lunguya; naomba vijiji hivi viingizwe kwenye mradi kwa sababu vimerukwa na vipo kwenye mradi. Waziri alipokuja tulipoenda Majimoto aliongea kwamba ni lazima vijiji vyote viingizwe na vitongoji vyake kwenye njia hii ya umeme wa REA, awamu ya tatu ili wananchi na sisi kule tupate kuona umeme, kwa sababu nitoka uhuru hatujaona mwanga wa taa.

Mheshimiwa Spika, tunaomba sasa na kazi ya huyo mkandarasi iwe kubwa kiasi kwamba wananchi wana hamu ya kuwekeza. Mheshimiwa amefika Majimoto, yeye mwenyewe anapapenda na anataka awekeze pale, kwa hiyo namwomba sasa, kasi pale ya kusambaza huo umeme wa REA iwe kwa kasi kubwa ili tuweze kuendelea na shughuli zetu za maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niliwahi kuongelea suala la nguzo zinazowekwa na TANESCO. Unaenda kuomba kuwekewa umeme, TANESCO wanakuletea nguzo unalipia laki tatu mpaka laki tano, lakini kuna mwingine jirani atataka naye kuunganishwa umeme atatumia ile nguzo, zimekuwa zikileta matatizo hasa kwa wananchi huku kwenye maeneo ambapo naye anataka kuunganishiwa kwenye ile nguzo, kwa nini? Kwa sababu yule aliyeweka mwanzo naye anataka arudishiwe gharama.

Mheshimiwa Spika, nashauri kwa sababu tunalipa umeme kila mwezi, kwa nini nguzo hizi ziwekwe bure ili wananchi waweze kupata na kuweka umeme kwa urahisi, kwa sababu hata hapa Dodoma wapo wanaoshindwa kuweka umeme kwa sababu tu ya gharama za nguzo. Kwa hiyo, niombe kama kweli tuna nia ya dhati na wananchi wetu wapate umeme basi wananchi nguzo ziwekwe bure kwa sababu tunalipia umeme. Kwa hiyo kama tunalipia naomba hizo nguzo ziwekwe bure.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa muda ni mchache, nakushukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)