Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Eng. Isack Aloyce Kamwelwe (1 total)

MHE. ENG. ISACK A. KAMWELWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Namuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, kwenye jibu lake la msingi la swali la Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Mjini Mpanda amezungumzia chanzo cha maji cha Bwawa la Milala. Bwawa la Milala linaweza likatoa maji kwa muda wa miezi minne tu.

Je, haoni kwamba, itakuwa ni kupoteza pesa kuwekeza katika chanzo ambacho kitatumika kwa muda wa miezi minne tu badala ya kwenda moja kwa moja kuchukua maji kwenye Ziwa Tanganyika? (Makofi)
WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nakushukuru, lakini nimpongeze sana sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa namna anavyojibu maswali vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu ina rasilimali toshelevu zaidi ya bilioni 126 mita za ujazo. Sasa mkakati wa Wizara ni kutumia rasilimali toshelevu kuhakikisha Watanzania wanapata huduma ya majisafi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ambaye ni Waziri wangu ambaye amenifunza mpaka leo nipo hapa, hili jambo tunalizingatia katika kuhakikisha kwamba wananchi hawa tunaenda kuwaondolea tatizo hili. Ahsante sana. (Makofi)