Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Eng. Dr. Leonard Madaraka Chamuriho (1 total)

MHE. ENG. DKT. LEONARD M. CHAMURIHO: Mheshimiwa
Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia fursa hii ya kuuliza swali. Kijiji cha Kyabakari kimekosa huduma ya maji kwa muda wa miezi mitatu sasa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba kijiji hicho kinapata maji japo kuwa kuna mradi mkubwa wa maji? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Leonard Chamuriho kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kijiji ambacho kinaweza kikakosa maji miezi mitatu na tayari kina miundombinu ya maji ni suala la kufuatilia changamoto ilipo. Naomba nilichukue tutahakikisha maji yanarejea kwa wananchi ili kuondokana na kero ambayo wanaipata kwa sasa.