Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Dr. Thea Medard Ntara (28 total)

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020
MHE. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwanza kabisa namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kupata nafasi hii ya kuingia kwenye Bunge hili kwa mara ya kwanza. Pia nichukue nafasi hii kuwashukuru wanawake wa Mkoa wa Ruvuma na wanawake wa Taifa hili wale wajumbe wa Baraza Kuu ambao walinifanya mimi nikapita na nimeweza kuingia Bungeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, niende moja kwa moja katika kuchangiaspeech ya Rais. Najikita zaidi kwenye mikopo ya elimu ya juu. Bajeti ya mikopo bado ni ndogo sanana wanafunzi wengi sana wanakosa mkopo. Sasa ili tuweze kusaidia kuondoa manung’uniko kwenye suala la mikopo ningeshauri Serikali itoe fedha kwa wanafunzi wote angalau wote wapate flat rate kama ni asilimia 80 mpaka 85 itasaidia, lakini kama wengine wanapata asilimia 100 halafu wengine hawapati kabisa basi hili suala la mikopo litaendelea kuwa na manung’uniko mengi sana. Kwa hiyo cha kufanyika sasa hivi ni kuhakikisha kwamba watoto wote wenye vigezo vya kuingia Chuo Kikuu wapewe mikopo kwa rate ambayo itafanana wote.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine sasa hivi tuna wanafunzi wengi sana katika vyuo vikuu. Unaingia darasa lile kufundisha lina wanafunzi 1,000, Walimu ni wachache, wafanyakazi ni wachache. Miaka miwili iliyopita kila wakati wanasema Walimu wataongezeka, Wahadhiri wataongezeka, watendaji ndani ya vyuo vikuu wataongezeka lakini bado hawaongezeki. Hilo linasababisha hata ufundishaji ndani ya vyuo vyetu unakuwa sio ufundishaji wa kufundisha kama tunavyotegemea. Kwa hiyo napendekeza kwamba lazima idadi ya Wahadhiri iongezeke, vyuo vikuu waruhusiwe au wapewe dhamana ya kuajiri Wahadhiri wa kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine katika kuboresha maarifa na ujuzi. Sasa hivi tunalalamika kwamba wanafunzi wetu wakitoka vyuo vikuu hawana life skills, vocational skills lakini hii yote kwa sababu bado ile competence approach hata Wahadhiri bado hawaijui. Ningeishauri Serikali kwamba wajitahidi sana kuongeza bajeti kwa TAIili TAIwaweze kutoa seminar au waweze kutoa hayo masomo kwa Wahadhiri pia na wao waweze kufundisha vizuri inavyotakiwa kama vile ambavyo wanatoa semina au ujuzi wa Tutors. Kwa hiyo pia hata Wahadhiri wanatakiwa wapewe hizo semina ili wafundishe katika ubora unaotakiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, niipongeze Serikali. Kulikuwa na jambo limetokea katika vyuo vikuu kuhusu rushwa ya ngono. Mimi niwapongeze sana TAKUKURU kwa lile jambo walilolifanya, lakini niwaombe kama walifanya utafiti na kugundua kwamba kuna baadhi ya wahadhiri sio waaminifu wanatumia nafasi zao kupokea rushwa za ngono kutoka kwa wanafunzi wetu, basi tuwaombe hao wakuu wa vyuo pamoja na Wizara inayohusika wawachukulie hatua mara moja. Suala la ngono ni ngumu sana kupata ushahidi, lakini wengi wakikutaja wewe, watu 20 wanakutaja watu 50 wanakutaja, kwanini wasimtaje mtu mwingine? Viongozi wachukue hatua mara moja.Niwapongeze sana wale wakuu wa vyuo ambao wamechukua hatua ya kuwasimamisha kazi baadhi ya Wahadhiri wanaowatumia watoto wetu kuwageuza kuwa vyombo vya kustarehe.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, niwaombe TAKUKURU, baada ya kufanya tafiti zao, ile feedback waipeleke kwenye vyuo.Isibaki kwao. Ukishafanya tafiti lazima wewe ile ripoti uwape vyuo vikuu waone, wasome, kwamba ninyi mnafanya mambo hayana haya machafu. Sio ngono tu, watoto wetu wa kiume pia wanaombwa pesa. Kwa hiyo Serikali iingilie hilo na wasaidiane na TAKUKURU kuona kwamba sasa tunapata elimu bora na sio elimu ambayo imepitia huko kwenye rushwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, nikushukuru sana.(Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Msingi wa kujenga uchumi wa viwanda ni kuwa na technical schools au colleges, niipongeze Serikali kwa kuboresha baadhi ya vyuo hivyo, yaani sekondari za ufundi chache katika nchi hii, angalau wameboresha majengo. Sasa niombe licha ya kuboresha majengo hayo, waboreshe na vifaa vya ufundishaji na ujifunzaji, kwa sababu, majengo tu hayatasaidia.

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge wenzangu wanajua kwamba zile shule zilikuwa zinasikika sana; Ifunda, Iyunga, Mtwara, Moshi Technical, hizi sekondari sasa hivi hazisikiki kwa sababu ubora umepungua. Kwa hiyo, niwaombe sana Serikali waziangalie, majengo pamoja na vifaa vya ufundishaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia katika ufundishaji waboreshe kwa kutumia Taasisi ya Elimu ili waweze kuwapa mafunzo wale Walimu ya ufundishaji mahiri, tunaita competent base, tumeizungumza sana hiyo toka 2005, lakini ni practice bado Walimu wanafundisha kwa kuwajaza wanafunzi maarifa, wanawajaza, wanawajaza, lakini practical skills zimewekwa pembeni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nirudi kwa watendaji. Ni kweli kuna baadhi ya watendaji wetu wanatuangusha, lakini kuna baadhi ya Wakurugenzi wanafanya kazi vizuri, wakati wote tunaangalia wale wanaofanya vibaya, lakini wapo wazuri. Hivyo, nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, wapewe pongezi zao, wapewe recognition. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna Mkurugenzi alikuwa anafanya kazi pale Jiji, nitoe mfano, wakati anakuja pale, maegesho tu walikuwa wanapata milioni 84 kwa mwezi, lakini alipoingia yeye akakusanya bilioni 1.6 kwa mwezi. Wakurugenzi kama hao naomba wapewe recognition, Maslow’s hierarchy inasema binadamu siyo fedha tu, binadamu siyo mapenzi tu, binadamu siyo shughuli nyingine, binadamu hata kule kutambuliwa anaweza akafurahi zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa stendi ya Mbezi huyo Mkurugenzi aliweza kuokoa bilioni zaidi ya 12. Hizo zingepigwa, kwa hiyo, hapa nimesimama kuzungumzia kwamba Wakurugenzi wengine ni kweli siyo mahiri, lakini kuna wale wazuri tuwatambue na wapewe recognition. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwisho, nizungumze kwa watumishi; tunapozungumza ni watumishi na wengi zao ni Walimu, tunasema Walimu ndiyo wengi katika watumishi, kwa hiyo, tunapowatetea Walimu na mimi ni mwalimu, tunapowatetea siyo kwamba watumishi wengine tumewaacha pembeni.

Mheshimiwa Spika, Walimu wanafanya kazi nyingi mno na sisi ni mashahidi, tukija uchaguzi Walimu, tukija kwenye sensa tunategemea Walimu, watoto wetu tumewaacha mashuleni huko Walimu. Jana nilikuwa na Mheshimiwa mmoja akawa anasema jamani hawa Walimu wana kazi, sisi tuko huku watoto wako mashuleni huko. Kwa hiyo, tunapotetea wapandishwe mishahara, ni kwa sababu ndiyo kundi kubwa na limeshasemwa siku nyingi, lakini bado walimu mishahara yao hairidhishi, licha ya matatizo yao mengi ambayo wanakuwa nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nikushukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, suala la kuagiza nguzo nje wakati tuna miti ya kutosha na kuna Kiwanda Dar es Salaam cha nguzo za cement, hiyo italeta upigaji wa hali ya juu.
Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuruku, kwanza niungane na wenzangu kutoa pole sana kwa Watanzania kwa msiba mkubwa uliotupata wa kuondokewa na aliyekuwa Rais wa Tanzania. Lakini pili, nitoe pongezi kwa Mheshimiwa Rais na Makamu wake kwa kuapishwa kuwa viongozi wa juu wa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitajikita kwenye sekta ya elimu yenye vipengele vinne. Pamoja na ufundishaji na outreach universities pia ina kazi ya kufanya research. Azimio la AU inaitaka kila nchi itoe asilimia moja ya pato lake kwa mwaka kufadhili utafiti na maendeleo i.e RMD. Sasa kwa kufanya hivyo kutawezesha Vyuo Vikuu kufanya research na wakati mwingine tumelalamika kwamba havifanyi utafiti lakini inabidi Serikali ichangie asilimia ya pato hilo ili Vyuo Vikuu wafanye research. Mfano leo hii, kuna Chuo cha MUST wanafanya action research ya kutengeneza majokofu kwa ajili ya kuhifadhi matunda kama walivyosema wenzangu. Matunda tunayo mengi sasa wao wanataka kutengeneza majokofu ili yahifadhi hayo matunda throughout na majokofu hayo yawe ya bei nafuu kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Serikali ikitoa mchango, mimi nafikiri kama mikoa Tanga, Tabora na Tunduru wanaweza wakahifadhi matunda throughout the year na wakafanya biashara na wananchi wetu wakapata kipato. Hivyo, hilo nimuombe sana Mheshimiwa Dkt. Mwigulu na Profesa Ndalichako waliangalie hilo, watoe ile asilimia moja ili kuwezesha au ku-top-up fedha ambazo zinahitajika kwa ajili ya kufanya research. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya pili sasa hivi kuna upungufu mkubwa sana wa ajira, i.e lecturers na waendeshaji. Waziri Mheshimiwa Prof. Ndalichako analijua hilo kwamba Serikali ilikuwa na utaratibu zamani Vyuo Vikuu wanawabakiza pale vyuoni wanafunzi waliofanya vizuri sana wanakuwa ma-TA, Tutorial Assistant, halafu baadaye wanawajenga na kupeleka kuwasomesha wanakuwa baadaye Assistant Lecturers na baadaye wanakuwa PHd. Lakini leo hii utaratibu ule haupo, kwa hiyo, ndio maana tunapata shida katika kuwa na namba ya Wahazili wa kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niiombe Serikali, irudishe utaratibu ule wa zamani wahazili wale wabobezi wanaweza kutambua wanafunzi wazuri sana wakawabakiza pale na baadaye wanawakuza na baadaye tunakuwa na Wahazili angalu wakutosha katika vyuo vyetu. Tukiwaacha waondoke, inavyotokea sasa, wale best performance wakiondoka wakatoka kipindi kile wanamaliza masomo yao hatuwezi kuwapata tena wanaenda huko nje na wanachukuliwa. Lakini palepale waka-identify na wanarusiwa kuwabakiza pale basi tutapungua hilo tatizo la Wahazili katika Vyuo vikuu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, agizo la Baraza la Madaktari Afrika Mashariki, linawataka Vyuo Vikuu vyote vyenye taaluma ya Sayansi na Tiba viwe na hospitali za kufundishia tunaziita teaching hospitals. Kwa mfano UDOM inatakiwa iwe teaching hospital, MUHAS iwe na teaching hospital, UDSM iwe na teaching hospital kwasababu wana ile taaluma ya Sayansi na Tiba. Serikali iruhusu hizo teaching hospitals wapewe hawa, wapewe na wanaweza kuziendesha wakati mwingine tumekuwa tunawasiwasi hawataweza kuziendesha mbona vyuo wanaweza kuviendesha. Kwa hiyo, na zile teaching hospitals kwanza zinaweza kufanya vizuri kabisa na hivyo ndivyo wanavyofanya wenzetu katika nchi nyingine zilizoendelea. Watoto wanatoka wanaenda pale wanakuwa na hospitali yao lakini at the same time ile hospitali yao ndio inakuwa kama wanafanya pale practical’s na mara nyingi ndio zinafanya vizuri zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Suala la mikopo wenzangu wengi hapa wamelizungumza, nishauri, kwasababu kumekuwa na malalamiko mengi na Waheshimiwa Wabunge hapa wengi sana wamefuatwa na wanafunzi kuombwa pesa. Taasisi zinaenda wanafunzi wanakuwa kama ombaomba, kama wanafunzi wote hao wanastahili kupata mikopo na tunashindwa kuwapa ile asilimia, tufanye hivi tupunguze asilimia ile ili kila mwanafunzi apate ile mikopo turudi badala ya asilimia 100 wote wapate flat rate ya asilimia 70 ili kusiwe na malalamiko, tukiendelea hivi kila siku na namba ya wanafunzi inaongezeka kila mwaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tufanye hivyo ili angalau wanafunzi wote wapate mikopo na wengi wanaokosa mikopo ni watoto wa maskini. Kwasababu watoto wote wanaokosa mikopo ni watoto wa maskini ndio waliokosa mikopo, kwasababu mtoto kama hapa wa Mheshimiwa Dkt. Ntara lazima nitajipigapiga hapa nitamlipia lakini wa wale wa maskini hawawezi, ndio maana wamekuja hapa Dodoma. Nina mzigo mzito hapa nitamkabidhi, mzigo mzito wanasema mpe Mnyamwezi, nitamkabidhi hayo majina Mheshimiwa Prof. Ndalichako abebane nalo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hapo hapo kuna lile suala la penati, watoto tumeshindwa kuwaajiri au ajira hizi tunazijua hazipo. Mtoto anamaliza Chuo Kikuu ana kaa miaka sita unamwambia akipata ajira alipe penati, hilo mie naomba liondolewe kabisa. Yaani liondolewe, yaani hakuna ku- discuss sijui percentage nini, hili liondolewe hatuwatendei haki, sasa hivi wanahangaika wanajiajiri wenyewe, hii mikopo hata kidogo wanayopata watoto wote wanafanya umachinga badala ya kusoma sasa, hujikita kwenye kusoma, watoto wana vibanda vya chips, watoto wana pikipiki ndio maana unakuta sasa kunakuwa na vurugu tu. Ebu tuwasidie watoto tuwape asilimia inayofanana wote na baadaye wakimaliza mikopo hakuna mambo ya penati. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapozungumza mambo ya penati, leo hii niwaambie kitu kingine ambacho kinasikitisha. Kuna wanafunzi wa Vyuo Vikuu wanaofanya biomedical wanapokwenda kufanya field wanadaiwa walipe pesa. Ni jambo linalosikitisha sana, wanaenda kufanya field wanaambiwa walipe pesa kwa kutumia vile vifaa wanavyovikuta pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni sawasawa na mwanafunzi ambaye anakwenda teaching practice anafika pale kwenye shule anaambiwa wewe umekuja kufundisha hapa, enhee! utulipe pesa, anakwenda pale kutoa huduma halafu anaambiwa alipe. Hilo nalo naomba muliangalia Mheshimiwa Waziri wa Elimu pamoja na Mheshimiwa Waziri wa Afya. Tunahitaji Watoto hawa waende field wakafanye kazi, mikopo wamekosa halafu mnamdai tena pesa, hilo naomba mliangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo nakushukuru sana. (Makofi)Napenda kuunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kijiji cha Mdunduwalo, Kata ya Maposeni hawajawahi kupata maji toka wapate Uhuru. Kijiji hiki watu hutumia maji ya kisima na wana-share na vyura na mijusi. Naomba Serikali mwaka huu wamalize adha hiyo.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, suala la kutumia jembe la mkono halitaweza kuwasaidia wakulima wadogo wadogo. Ni muhimu sana Serikali sasa ipeleke matrekta kwenye vijiji kwa kuanzia na matatu kila kijiji. Tukiendelea kulima kwa mkono bado wakulima wadogo ambao ni wengi hawatafaidika na umaskini utabaki pale pale.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa vituo vya usambazaji mbolea tafadhali sana viwepo vijijini. Wakulima wanatapeliwa sana na wajanja ambao hutumia pikipiki kutoa kituo kikuu na kuongeza bei.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Nami nitumie nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Elimu ambaye ni mwalimu wangu wa Research Methodology ingawa ulinibania bania sana.

SPIKA: Mchoyo wa marks eeh!

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, nianze kwa neno moja halafu niendelee. Hilo neno atanisaidia kutafsiri baadaye Mheshimiwa Mwantumu Dau, linasema Iqra. Nami niseme kama walivyosema wenzangu. Mitaala yetu ya elimu ni mizuri, sio mibaya. Tatizo mitaala yetu ya elimu ni mikubwa (loaded) mno. Kwa hiyo, cha kufanya nimshauri tu Mheshimiwa Waziri aunde timu, wafanye in depth review ya program zote na hasa vyo vikuu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, unakuta leo hii ukianzisha chuo chochote kikuu, mtu anayazoa ma-program ya Chuo Kikuu fulani yote anayaweka kwenye chuo chake. Kwa hiyo, ni copy and paste. Kwa hiyo, tunakuwa na ma-program mengi. Mengine wakati mwingine ndiyo hayo ambayo mtoto akimaliza anakosa ajira. Kwa hiyo, hapa Mheshimiwa waziri ana kazi nzito. Watu wameongea sana kuhusu elimu. Inaonekana tayari kuna tatizo na wakati huu uliopo. Kwa hiyo, waka echini wa-review program ya elimu iwe reviewed in depth ili waje na zile special program ambazo tunazihitaji kwa wakati huu na wakati ujao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine nililizungumza lakini leo nizungumze kuhusu ku-post au kupata wahadhiri kutoka nje. Yaani tunatakiwa sasa tubadilike. Vyuo vikuu vyetu wahadhiri ni wale wa hapa Tanzania, hatukatai lakini tunatakiwa tuwe na angalau asilimia tano ya professors kutoka nje. Tukiwa na mchanganyiko wa professors wengine wakapata kibali cha kutangaza Internationally halafu tukapata wahadhiri kutoka nje kwanza itaongeza hadhi ya vyuo vyetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni jukumu sasa nimuombe Waziri watangaze kazi Internationally ili tupate maprofesa waweze kusaidiana na hao waliopo na hiyo itasaidia kuongeza exchange programs, itasaidia kuleta projects lakini pia hivi vyuo vyetu vitapanda hadhi. Tukiendelea tu kuwa wenyewe, local, local tu, laizma tufanye sisi wenyewe vile ambavyo leo kuna Watanzania Maprofesa wanaenda kufundisha South Africa, wengine wanaenda kufundisha Rwanda somo la Kiswahili. Kwa hiyo, na sisi lazima tujipange tuwe na wahadhiri kutoka nje. Na hapo ndiyo tutaleta maana ya neno University. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna hili suala la Sheria za Extension. Pale Chuo Kikuu ukichelewa kumaliza program za master’s au PHD unapewa extension na unalipa fine zaidi ya milioni moja. Sasa niombe, wanafunzi wanalalamika sana. Anayesababisha hawa wanafunzi mara nyingi kuchelewa ni yule supervisor. Kwa hiyo, kinachotakiwa hapa ile fine igawanywe. Mwanafunzi alipe nusu na yule supervisor nusu. Kwa kufanya hivyo, hawa ma-supervisor watakuwa wanasoma kazi za wanafunzi, wanamaliza kwa wakati, hakutakuwa na extension fine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wakishamaliza mwanafunzi yule anajulikana details zake zote. Siku anamaliza ana-graduate kupata cheti anaambiwa rudi Songea, au nenda Kagera uje baada ya wiki mbili. Hiyo nayo imekuwa inasumbua sana wanafunzi. Mheshimiwa Waziri asimamie. Akimaliza chuo, anapata cheti chake anaondoka. Lakini imekuwa ni usumbufu mno. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la mwisho niwaombe sana Wizara pamoja na halmashauri tumekuwa tukilalamika vyuo vikuu hawafanyi utafiti…

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Ntara.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: … aaah! Hivi ni kweli?

SPIKA: Haya, nakupa dakika mbili au tatu umalizie. (Kicheko)

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, sasa niwaombe sana Wizara na halmashauri tutumie vyuo vyetu kufanya kazi ndani ya halmashauri na wizara. Mfano mzuri ni Mheshimiwa Sajin alipokuwa RAS Simiyu. Alichukua wale wanafunzi kutoka ardhi Tabora kwenda kupima viwanja vyote kule Simiyu, wakammalizia kazi tena kwa bei ya chini. Kwa hiyo, tutumie vyuo vyetu. Tutumie TIA, IFM, Ardhi, tutumie University of Dar es Salaam, UDOM. Tuwatumie wakafanye kazi zetu. Ahsante sana. (Makofi)

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, Taarifa!

SPIKA: Mheshimiwa Thea Ntara, kuna Taarifa unapewa. Endelea nimekuruhusu.

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Nimekuruhusu, jitambulishe tu.

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, naitwa Cosato Chumi…

SPIKA: Cosato Chumi, nimekuona sasa.

T A A R I F A

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, naomba kumpa Taarifa Mheshimiwa Mbunge anayezungumza kwamba hata sisi Halmashauri ya Mji wa Mafinga tumetengeneza Master Plan kwa kutumia wanafunzi wa Chuo cha Ardhi kwa hiyo hoja yake ni ya msingi sana. (Makofi)

SPIKA: Unaipokea hiyo hoja Mheshimiwa Ntara?

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, nimeipokea halafu nawapongeza sana. Hiyo ndiyo namna tutakuza hawa watoto wetu waonekane wanafanya kazi.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo nikushukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, suala la ubovu wa majengo ya vyuo vikuu ni la muda mrefu. MUST, Mkwawa, UDOM ni baadhi ya vyuo vikongwe ambavyo vinahitaji maboresho kabla havijaharika zaidi.

Mheshimiwa Spika, viwanja vya Chuo cha Nelson Mandela viharakishwe kujengwa ili vitumike.

Mheshimiwa Spika, suala la mshahara wa wakuu wa vyuo vikuu lifanyiwe kazi na maelezo yatolewe kadri Mheshimiwa Waziri wa Elimu alivyoahidi katika Bunge la Kumi na Mbili kwa mwaka 2021/2022.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nami nichukue nafasi hii kuchangia katika maeneo kama matatu hivi. Kwanza kabisa, nitachangia kuhusu upandikizaji wa watoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la mwanamke au familia kukosa mtoto linaumiza sana. Mwanamke asipokuwa na mtoto anaumwa mno, na ni ugonjwa. Kisaikolojia na hata maisha kwa ujumla kwake hayana amani. Sasa kuna huu upandikizaji wa watoto nje ya nchi. Mtu hana mtoto, anajaribu kwa madaktari hapa, wanasema wewe lazima ukafanyiwe upandikizaji. Sasa hii ya upandikizaji inachukua fedha nyingi mno. Wanawake hawawezi kwenda China wala South Africa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali kupitia Wizara ya Afya, hebu tuwasaidie wanawake kama tunavyosaidia magonjwa ya moyo na figo, watu wanasaidiwa, wanakwenda nje. Basi hata kama ni shilingi milioni 20, Serikali ichangie angalau nusu na yule mtu aambiwe na wewe saidia ongeza kiasi. Kwa kufanya hivyo, tutasaidia wanawake wengi sana.

Pia Serikali ianze kujipanga. Tutakwenda kutafuta watoto huko nje mpaka lini? Ndiyo maana kunatokea maneno kwamba unajuaje kama zile mbegu ni za mume wako? Kwa sababu unaenda kupandikizwa kule nje, labda watachukua mbegu nyingine, wataweka ili mradi mtu arudi na mtoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Serikali ianze kujipanga katika utaalam huo, tuwe na maabara hapa Tanzania, nasi tuanze test tube babies, tuianze wenyewe hapa Tanzania. Haya mambo ya kwenda nje yatatuletea matatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, naipongeza sana Serikali, ilipofanya zoezi la tohara hasa kwa watani zangu kule Tabora, Mwanza, nasikia hata huko Sumbawanga, hili jambo lilikuwa ni zuri kwa manufaa ya afya na hasa katika kupungiza maambukizi ya Ukimwi. Sasa wamefanya hiyo kazi ya tohara ya wanaume vizuri sana, naomba sana Serikali ijipange kumaliza kabisa tatizo la ukeketaji wa wanawake katika mikoa ambayo bado ukeketaji unaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimepata ushahidi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, anasema licha ya juhudi zile zote; seminars na workshops bado watoto wanakeketwa. Sasa Mheshimiwa Ummy alifanya, alijitahidi sana, mimi leo nawaomba na wanaume mtusaidie kupiga kampeni kwamba msichana au mwanamke aliyekeketwa hataolewa. Mkianza ninyi, itasaidia kwa sababu asili ya mwanamke kukeketwa ilitokana na wanaume kutaka kuwagandamiza wanawake wasipate hisia katika tendo la ndoa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kidogo nieleze, tunaliona hili jambo ni rahisi sana au la kawaida. Nimefanya utafiti, hawa wanawake waliokeketwa ukiongea nao inasikitisha. Kwanza wana madhara yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mwanamke aliyekeketwa anapewa ulemavu makusudi. Unamkata mtu kidole hiki cha mwisho makusudi tu, hawezi kufa lakini hawezi kushika ugali vizuri. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sina nia ya kuwachekesha lakini nasema ukweli kisayansi. Imagine mtu akikukata ulimi hapa mbele, hutakufa lakini huwezi kuonja. Kwa hiyo, wanawake hao kwanza wanapata ulemavu, kwa sababu wanaondolewa kiungo ambacho akipaswi kuondolewa. Yaani ile ni kama kufyeka; na sehemu nyingine wanafyeka mpaka zile labia minora sasa hilo ni tatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, maumivu makali, ulemavu, halafu wanawake hao wakiingia katika kuolewa, wanabakwa kwa sababu hawasikii kabisa, nisemeje kwa Kiswahili? Hawasikii hisia na hawafikii orgasm. Sasa huyo mwanamke anaishi maisha yote. Mmoja aliniambia, nimezaa watoto watano mwanangu, sijui mnachosema eti kuna raha na furaha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo ni shida sana. Wengi hupata ulemavu, maumivu makali wakati wa kujifungua, wakati mwingine lile kovu sasa linaweza likachanika. Hawa wanaweza kupata Ukimwi, kwa sababu vile visu siyo kwamba wanabadilisha. Sijui wanatumia visu au mapanga, mimi sijui. (Kicheko/Makofi)

MBUNGE FULANI: Eeh! (Kicheko)

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, wengine wanapata Ukimwi, tetanus na magonjwa mengine. Halafu waki-bleed sana lazima watakuwa anemic. Kwa hiyo, hayo ni madhara. Naiomba sana Serikali sasa hivi itoe tamko, Wizara ya Afya pamoja na Katiba na Sheria, mtoe tamko la kutokomeza kabisa kama tulivyoweza kutokomeza wale waliokuwa wanawachinja albino. Wale wanaowaita mangariba, bado wapo na huo ukeketaji umehama kwenye ile mikoa huko mpaka Dar es salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu wengi mnajua kuna kundi lile ambalo linatoka Mara, liko Ukonga na Segerea. Kuna watoto kule walitoroka; nina uhakika na nina Ushahidi kwamba watoto wawili walitoroka kukimbia kukeketwa. Kwa hiyo, naliomba sasa ulibebe Waziri wa Afya tufanye kampeni, tuandike andiko zuri kutumia hata celebrity wetu, hilo litapotea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine, Kituo cha Afya, Mkwawa University kinahudumia watu zaidi ya 50,000. Namwomba sasa Waziri, ikiwezekana tuongozane akaangalie pale. Kinatakiwa kipandishwe sasa kiwe Hospitali kwa sababu kinahudumia watu wengi. Hiyo itasaidia sana kupunguza msongamano kwenye ile hospitali ya mkoa pamoja na Hospitali ya Rufaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho tiba asili zinatusaidia, tiba mbadala zinatusaidia, lakini sasa hivi hizo dawa ni ghali mno. Mtu akishindwa kupata dawa hospitali, akaenda kule anaambiwa shilingi 50,000, au shilingi 100,000. Kwa hiyo, naomba Wizara hapo ikae vizuri na hao watu wa tiba asili hizi ambazo mmezitambua, bei zao zishuke. Maana yake mtu anakubali kwenda kule ili aishi. Sasa bei yao ni kubwa sana kuliko hata bei ya dawa za hospitali ya kawaida.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana, naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nami nichukue nafasi hii kuchangia katika maeneo kama matatu hivi. Kwanza kabisa, nitachangia kuhusu upandikizaji wa watoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la mwanamke au familia kukosa mtoto linaumiza sana. Mwanamke asipokuwa na mtoto anaumwa mno, na ni ugonjwa. Kisaikolojia na hata maisha kwa ujumla kwake hayana amani. Sasa kuna huu upandikizaji wa watoto nje ya nchi. Mtu hana mtoto, anajaribu kwa madaktari hapa, wanasema wewe lazima ukafanyiwe upandikizaji. Sasa hii ya upandikizaji inachukua fedha nyingi mno. Wanawake hawawezi kwenda China wala South Africa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali kupitia Wizara ya Afya, hebu tuwasaidie wanawake kama tunavyosaidia magonjwa ya moyo na figo, watu wanasaidiwa, wanakwenda nje. Basi hata kama ni shilingi milioni 20, Serikali ichangie angalau nusu na yule mtu aambiwe na wewe saidia ongeza kiasi. Kwa kufanya hivyo, tutasaidia wanawake wengi sana. Pia Serikali ianze kujipanga. Tutakwenda kutafuta watoto huko nje mpaka lini? Ndiyo maana kunatokea maneno kwamba unajuaje kama zile mbegu ni za mume wako? Kwa sababu unaenda kupandikizwa kule nje, labda watachukua mbegu nyingine, wataweka ili mradi mtu arudi na mtoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Serikali ianze kujipanga katika utaalam huo, tuwe na maabara hapa Tanzania, nasi tuanze test tube babies, tuianze wenyewe hapa Tanzania. Haya mambo ya kwenda nje yatatuletea matatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, naipongeza sana Serikali, ilipofanya zoezi la tohara hasa kwa watani zangu kule Tabora, Mwanza, nasikia hata huko Sumbawanga, hili jambo lilikuwa ni zuri kwa manufaa ya afya na hasa katika kupungiza maambukizi ya Ukimwi. Sasa wamefanya hiyo kazi ya tohara ya wanaume vizuri sana, naomba sana Serikali ijipange kumaliza kabisa tatizo la ukeketaji wa wanawake katika mikoa ambayo bado ukeketaji unaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimepata ushahidi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, anasema licha ya juhudi zile zote; seminars na workshops bado watoto wanakeketwa. Sasa Mheshimiwa Ummy alifanya, alijitahidi sana, mimi leo nawaomba na wanaume mtusaidie kupiga kampeni kwamba msichana au mwanamke aliyekeketwa hataolewa. Mkianza ninyi, itasaidia kwa sababu asili ya mwanamke kukeketwa ilitokana na wanaume kutaka kuwagandamiza wanawake wasipate hisia katika tendo la ndoa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kidogo nieleze, tunaliona hili jambo ni rahisi sana au la kawaida. Nimefanya utafiti, hawa wanawake waliokeketwa ukiongea nao inasikitisha. Kwanza wana madhara yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mwanamke aliyekeketwa anapewa ulemavu makusudi. Unamkata mtu kidole hiki cha mwisho makusudi tu, hawezi kufa lakini hawezi kushika ugali vizuri. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sina nia ya kuwachekesha lakini nasema ukweli kisayansi. Imagine mtu akikukata ulimi hapa mbele, hutakufa lakini huwezi kuonja. Kwa hiyo, wanawake hao kwanza wanapata ulemavu, kwa sababu wanaondolewa kiungo ambacho akipaswi kuondolewa. Yaani ile ni kama kufyeka; na sehemu nyingine wanafyeka mpaka zile labia minora sasa hilo ni tatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, maumivu makali, ulemavu, halafu wanawake hao wakiingia katika kuolewa, wanabakwa kwa sababu hawasikii kabisa, nisemeje kwa Kiswahili? Hawasikii hisia na hawafikii orgasm. Sasa huyo mwanamke anaishi maisha yote. Mmoja aliniambia, nimezaa watoto watano mwanangu, sijui mnachosema eti kuna raha na furaha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo ni shida sana. Wengi hupata ulemavu, maumivu makali wakati wa kujifungua, wakati mwingine lile kovu sasa linaweza likachanika. Hawa wanaweza kupata Ukimwi, kwa sababu vile visu siyo kwamba wanabadilisha. Sijui wanatumia visu au mapanga, mimi sijui. (Kicheko/Makofi)

MBUNGE FULANI: Eeh! (Kicheko)

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, wengine wanapata Ukimwi, tetanus na magonjwa mengine. Halafu waki-bleed sana lazima watakuwa anemic. Kwa hiyo, hayo ni madhara. Naiomba sana Serikali sasa hivi itoe tamko, Wizara ya Afya pamoja na Katiba na Sheria, mtoe tamko la kutokomeza kabisa kama tulivyoweza kutokomeza wale waliokuwa wanawachinja albino. Wale wanaowaita mangariba, bado wapo na huo ukeketaji umehama kwenye ile mikoa huko mpaka Dar es salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu wengi mnajua kuna kundi lile ambalo linatoka Mara, liko Ukonga na Segerea. Kuna watoto kule walitoroka; nina uhakika na nina Ushahidi kwamba watoto wawili walitoroka kukimbia kukeketwa. Kwa hiyo, naliomba sasa ulibebe Waziri wa Afya tufanye kampeni, tuandike andiko zuri kutumia hata celebrity wetu, hilo litapotea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine, Kituo cha Afya, Mkwawa University kinahudumia watu zaidi ya 50,000. Namwomba sasa Waziri, ikiwezekana tuongozane akaangalie pale. Kinatakiwa kipandishwe sasa kiwe Hospitali kwa sababu kinahudumia watu wengi. Hiyo itasaidia sana kupunguza msongamano kwenye ile hospitali ya mkoa pamoja na Hospitali ya Rufaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho tiba asili zinatusaidia, tiba mbadala zinatusaidia, lakini sasa hivi hizo dawa ni ghali mno. Mtu akishindwa kupata dawa hospitali, akaenda kule anaambiwa shilingi 50,000, au shilingi 100,000. Kwa hiyo, naomba Wizara hapo ikae vizuri na hao watu wa tiba asili hizi ambazo mmezitambua, bei zao zishuke. Maana yake mtu anakubali kwenda kule ili aishi. Sasa bei yao ni kubwa sana kuliko hata bei ya dawa za hospitali ya kawaida.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana, naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, niungane na wenzangu wasemaji waliopita kama Mheshimiwa Mpina aliongea jana na Mheshimiwa Aida na huyu wa leo kwamba inabidi bajeti ya kilimo iongezeke na tufuate kabisa ile Maputo Declaration ambayo ilizitaka nchi za Afrika zitumie angalau asilimia 10 ielekezwe kwenye kilimo. Sasa ikielekezwa huko kwenye kilimo fungu hili likiongezeka Wizara itaweza kukuza kilimo lakini pia itaweza kupata mbegu bora kupitia seed science and research. Bila hivyo tutaendelea kununua mbegu nje, kulima karanga Dodoma halafu mnasema hazioti; hili tatizo ni kwamba fedha Wizara ya Kilimo hazitoshi.

Mheshimiwa Spika, Waziri wa Fedha atafute fedha ndiyo kazi yake, atafute fedha na zikipatikana ndiyo tunaweza kufanya vitu katika hii Wizara ya Kilimo. Haya mambo ya kuchukua mbegu kutoka nje au kutegemea nje maana yake ni kweli hatuna wanasayansi. Kuna Profesa anaitwa Susanne Nchimbi alitengeneza mbegu nzuri sana za maharage pale SIA na zikasambaa Tanzania. Kwa nini tusitumie hao wanasayansi wetu ili tupate mbegu ambazo hazitaleta utata zinavyooteshwa sehemu mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia ni wakati sasa wa ku- intensify, kukuza na kupanua kitu kinachoitwa commercial farming; tusipokuwa na commercial farming hatuwezi kufanya biashara za kilimo. Tukifanya commercial farming ina maana kwamba hata hawa vijana wetu tutafanikisha hata hicho tunachosema irrigation schemes lakini kutegemea hizi mvua za misimu bado hatutaweza kuwa ni nchi inayoweza kuzalisha kwa ajili ya kuuza. Tukifanya commercial farming ina maana tutakuwa na mazao bora lakini pia tutaweza kutoa mafunzo (practical skills) kwa wanafunzi wetu wanaotoka katika vyuo vya kilimo lakini pia wanaotoka katika vyuo vingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo hii tunasema hakuna ajira lakini hao Watoto wakiweza kwenda kujifunza kwenye hizo commercial farms itatusaidia hata wao kutengeneza vikundi na Serikali ndiyo hapo itapeleka fedha kwa hivi vikundi. Tunaweza kuwa na hivi vikundi kwenye mikao yote 26; wengine wakawa na kikundi wanalima karanga, wengine maparachichi Njombe, kikundi kingine cha hawa vijana ambao ni wasomi watapewa mikopo waweze kulima mahindi Ruvuma na wengine michikichi huko sijui Kigoma. Kwa hiyo, tukifanya hivyo tunaweza tukaendelea, watafute fedha.

Mheshimiwa Spika, kama World Bank inaweza/ imejipanga kufanya investment kwenye nchi za Afrika, dola bilioni 150 na Tanzania kwanini tukose hizo fedha. Waziri wa Fedha akatafute fedha, IFAD wanatoa mikopo tena ya bei nafuu, wakatafute fedha ili iongezwe kwenye Wizara ya Kilimo. Tukiendelea hiki kilimo cha kijungujiko hatufiki. Sasa hivi inatakiwa tuwe na mashamba makubwa ndiyo tutaweza kuwapa hao vijana mikopo waweze kufanya ukulima wa kisasa na wenye tija. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimalize kwa kusema nawashukuru Wizara wameleta wanunuzi wa zao la soya huko Ruvuma lakini Ruvuma wanalima ufuta pia na mikoa mingine. Watafute na wanunuzi sio wanunuzi hawa wa kusema ulete sijui stakabadhi ghalani, tunataka mtu akipeleka zao anapata pesa yake palepale, wakulima ndiyo wanapenda hivyo. Lakini haya mambo ya kusema unaleta zao kama yalivyokuwa kule mambo ya tumbaku ndiyo yanaleta shida, upigaji unakuwepo mwingi sana hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa kule Tabora najua shida ya AMCOS, mtu akitoka kule ameiba hela ya wakulima anatoka pale ana pesa nyingi halafu anaingia mara Diwani, mara Mbunge. Walikuwa wanawaibia wakulima fedha siwasemi hawa wakina Mheshimiwa Gulamali lakini ndiyo kilichokuwa kinatokea kule Tabora. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, ninakushukuru sana, naunga mkono hoja. (Makofi)
Hoja ya Dharura kuhusu Mikopo ya Elimu ya Juu Nchini
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Nami nipongeze hoja iliyotolewa na Mheshimiwa Ezra. Ni kweli kwamba, Serikali kuna sera ya wanafunzi wote wanaostahili kupata mikopo wapate mikopo. Kwanza hiyo ni sera kabisa kwenye elimu, wanastahili kupata mikopo wale wote wanaotimiza vigezo.

Mheshimiwa Spika, niliongea katika Bunge lililopita, nikasema kwamba kama tunashindwa kuwapa wote asilimia 100, basi afadhali wote wapate flat rate. Hivi unampa mtoto mkopo wa asilimia 30 wakati mnajua hawa watoto wanatakiwa kufanya research, wanatakiwa kulipa hiyo tuition, wanatakiwa kula vizuri; asilimia 30 inatosha nini? Nilishauri basi ikiwezekana watoto wote wapate flat rate ili idadi kubwa ya wanafunzi waweze kupata mkopo.

Mheshimiwa Spika, na hii ya kuwabagua watoto wengine wasipate mkopo eti kwa sababu wamesoma private si haki na si sawa. Kwa sababu mtoto anaposoma sekondari mkataba ni kati ya mzazi na shule, kwa hiyo pale mzazi anahitajika alipe ada, ule ni mkataba wa shule na mzazi. Lakini mtoto anapoingia chuo kikuu ni mkataba kati ya yule mwanafunzi wa chuo kikuu na chuo au na Serikali. Kwa hiyo hatuna haja ya kuweka ubaguzi, eti amesoma private asipate mkopo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na watoto wengi walioniletea mimi maombi, eti wananiletea mimi maombi kama mwakilishi, wengi wametoka private, hasa huko KCMC aliposema Mheshimiwa Ezra. Wanaomba mikopo; SAUT wanaomba mikopo, Teofilo Kisanji wanakosa mikopo, na mara nyingi wakati wako karibu na mitihani.

Mheshimiwa Spika, hili jambo nimefurahi sana leo limeingia hapa. Umenisaidia sana Mheshimiwa Ezra; I salute you. Kwa hiyo tuangalie namna gani sasa tutajipanga, na vigezo vile ambavyo havileti haki viondolewe. Tutafute fedha ili sasa hivi watoto wote hao wapate stahiki zao ili waweze kusoma.

Mheshimiwa Spika, leo tunalalamika kwamba watoto wakimaliza vyuo vikuu hawafanyi kazi nzuri kwenye field. Ni kwa sababu sasa hivi watoto hawana hela za kufanya research, kwa hiyo hakuna ubunifu. Hawa watoto wana-copy tu vitu. Tunapata watoto wamemaliza vyuo vikuu lakini hawana ubunifu, ni kwa sababu ya hapa.

Mheshimiwa Spika, tuwekeze fedha kama walivyofanya Thailand, wamewekeza fedha kwenye elimu. Thailand ilikuwa ni nchi ya kawaida, maskini, leo Thailand inatupiga, Singapore inatupiga. Wamewekeza fedha kwenye elimu kuanzia kindergarten. Kwa hiyo tubadilike tuwekeze fedha kwenye elimu ili iwakomboe watoto wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, niungane na wenzangu wasemaji waliopita kama Mheshimiwa Mpina aliongea jana na Mheshimiwa Aida na huyu wa leo kwamba inabidi bajeti ya kilimo iongezeke na tufuate kabisa ile Maputo Declaration ambayo ilizitaka nchi za Afrika zitumie angalau asilimia 10 ielekezwe kwenye kilimo. Sasa ikielekezwa huko kwenye kilimo fungu hili likiongezeka Wizara itaweza kukuza kilimo lakini pia itaweza kupata mbegu bora kupitia seed science and research. Bila hivyo tutaendelea kununua mbegu nje, kulima karanga Dodoma halafu mnasema hazioti; hili tatizo ni kwamba fedha Wizara ya Kilimo hazitoshi.

Mheshimiwa Spika, Waziri wa Fedha atafute fedha ndiyo kazi yake, atafute fedha na zikipatikana ndiyo tunaweza kufanya vitu katika hii Wizara ya Kilimo. Haya mambo ya kuchukua mbegu kutoka nje au kutegemea nje maana yake ni kweli hatuna wanasayansi. Kuna Profesa anaitwa Susanne Nchimbi alitengeneza mbegu nzuri sana za maharage pale SIA na zikasambaa Tanzania. Kwa nini tusitumie hao wanasayansi wetu ili tupate mbegu ambazo hazitaleta utata zinavyooteshwa sehemu mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia ni wakati sasa wa ku- intensify, kukuza na kupanua kitu kinachoitwa commercial farming; tusipokuwa na commercial farming hatuwezi kufanya biashara za kilimo. Tukifanya commercial farming ina maana kwamba hata hawa vijana wetu tutafanikisha hata hicho tunachosema irrigation schemes lakini kutegemea hizi mvua za misimu bado hatutaweza kuwa ni nchi inayoweza kuzalisha kwa ajili ya kuuza. Tukifanya commercial farming ina maana tutakuwa na mazao bora lakini pia tutaweza kutoa mafunzo (practical skills) kwa wanafunzi wetu wanaotoka katika vyuo vya kilimo lakini pia wanaotoka katika vyuo vingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo hii tunasema hakuna ajira lakini hao Watoto wakiweza kwenda kujifunza kwenye hizo commercial farms itatusaidia hata wao kutengeneza vikundi na Serikali ndiyo hapo itapeleka fedha kwa hivi vikundi. Tunaweza kuwa na hivi vikundi kwenye mikao yote 26; wengine wakawa na kikundi wanalima karanga, wengine maparachichi Njombe, kikundi kingine cha hawa vijana ambao ni wasomi watapewa mikopo waweze kulima mahindi Ruvuma na wengine michikichi huko sijui Kigoma. Kwa hiyo, tukifanya hivyo tunaweza tukaendelea, watafute fedha.

Mheshimiwa Spika, kama World Bank inaweza/ imejipanga kufanya investment kwenye nchi za Afrika, dola bilioni 150 na Tanzania kwanini tukose hizo fedha. Waziri wa Fedha akatafute fedha, IFAD wanatoa mikopo tena ya bei nafuu, wakatafute fedha ili iongezwe kwenye Wizara ya Kilimo. Tukiendelea hiki kilimo cha kijungujiko hatufiki. Sasa hivi inatakiwa tuwe na mashamba makubwa ndiyo tutaweza kuwapa hao vijana mikopo waweze kufanya ukulima wa kisasa na wenye tija. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimalize kwa kusema nawashukuru Wizara wameleta wanunuzi wa zao la soya huko Ruvuma lakini Ruvuma wanalima ufuta pia na mikoa mingine. Watafute na wanunuzi sio wanunuzi hawa wa kusema ulete sijui stakabadhi ghalani, tunataka mtu akipeleka zao anapata pesa yake palepale, wakulima ndiyo wanapenda hivyo. Lakini haya mambo ya kusema unaleta zao kama yalivyokuwa kule mambo ya tumbaku ndiyo yanaleta shida, upigaji unakuwepo mwingi sana hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa kule Tabora najua shida ya AMCOS, mtu akitoka kule ameiba hela ya wakulima anatoka pale ana pesa nyingi halafu anaingia mara Diwani, mara Mbunge. Walikuwa wanawaibia wakulima fedha siwasemi hawa wakina Mheshimiwa Gulamali lakini ndiyo kilichokuwa kinatokea kule Tabora. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, ninakushukuru sana, naunga mkono hoja. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, nami nikushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nianze kwa kusema, hili suala la ukosefu wa ajira kwa vijana wetu limekuwa ni changamoto. Sasa kutokana na hilo, naipongeza sana sana Wizara ya Kilimo kwa kuanza mpango wa kupokea vijana wanatuma application, wanawa-enroll ili baadaye hao vijana wote wawapatie skills au mafunzo ya kilimo, nafikiri ni kilimo cha umwagiliaji, halafu baadaye wawape vifaa, yaani matrekta na pembejeo ili waanze vile vitu mnavyoita block farms.

Mheshimiwa Spika, sasa naiomba Wizara, hii link mnayoituma ili hao wanafunzi au hao vijana watume application, nafikiri vijana waliopo mijini watafaidika sana. Sasa nilikuwa nawaza kwamba ni vizuri ili vijana wote walioko katika wilaya zetu wapate hii taarifa, basi hizi taarifa au link ipelekwe mawilayani. Wakuu wa Wilaya au Wakurugenzi wajue kuzituma katika Wilaya zao ili vijana wote wafanye hiyo application. Kwa sababu idadi hii mliyoipata ya karibu wanafunzi 16,000 inaweza ikaongezeka. Kwa hiyo, hilo litasaidia sana pia kupunguza hilo tulilosema la ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, niseme hivi, kama Wizara ya Kilimo imeweza kufanya hilo jambo, kwa nini Wizara nyingine hizi mbili ambazo nazo zinafanya kazi ya production wasifanye kama Wizara ya Kilimo? Mfano, hii Wizara ya Mifugo, kwa nini na ninyi msifanye hivyo ili tuwe na hizo blocks za mifugo? Wizara ya Viwanda na Biashara kwa nini na ninyi msifanye hivyo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Viwanda na Biashara mkichukua wanafunzi 10,000, Wizara ya Mifugo nayo ikachukua wanafunzi 10,000, kwa kufanya hivyo Wizara hizi tatu zinaweza zikasaidia sana sana kupunguza hili wimbi au manung’uniko ya changamoto ya ajira. Kwa hiyo, naomba hizi Wizara mbili zifanye kama wanavyofanya hawa Wizara ya Kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine ni kuhusu mbolea. Kuna wakati nimesikia kwamba mbolea hizo zitakwenda kwenye maeneo, na centers za kusaidia kupeleka mbolea zitaongezeka. Niseme tu, hata mkiweka hizo centers Wizara ya Kilimo kwa sababu tunaleta Kilimo cha Umwagiliaji, naomba sana hiyo mbolea ipatikane throughout. Tukisubiri tu wakati wa msimu ule wa mvua, ndiyo maana kunakuwa na changamoto ya wakulima kunyanyasika, kuibiwa pesa zao na mbolea yenyewe kuuzwa kwa namna ambayo haipendezi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni vizuri sasa mbolea ikawa inapatikana wakati wote, tusisubiri tu wakati wa msimu wa kilimo. Kwa sababu tunatengemea kuanzisha Kilimo cha umwagiliagi, basi hiyo mbolea ipatikane wakati wote na hiyo itapunguza sana changamoto za upatikanaji wa mbolea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Kwanza kabisa nami niungane na wenzangu kuipongeza sana Serikali. Ni mara ya kwanza kuingia katika Bunge hili Tukufu lakini kwa yaliyotokea kwenye hii bajeti kwakweli yanafurahisha sana. Na kwa upande nimpongeze Waziri wa Fedha nimpongeze mwenyekiti wa Kamati na Wajumbe wote wa Kamati ile ya bajeti, mmejitahidi sana angalau kujibu yale ambayo tuliyokuwa tunayazungumza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimefurahishwa kwanza kuhusu lile suala la mikopo, nimefurashishwa mno. Kuondoa zile sijui retention zile adhabu kwenye mikopo, nimepigiwa simu yaani nifuraha nifuraha huko vyuo vikuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kuongeza mikopo kutoka bilioni 464 mpaka 500, niwapongeze Serikali. Na kama Mheshimiwa Waziri wa Fedha alivyoahidi, amesema watoto wote wenye vigezo watapata mikopo kupitia ule mradi wa HIT.

Mimi ninaamini kutakuwa na mabadiliko makubwa sana, si kwa vyuo vikuu tu lakini na kwa wale wanaomaliza. Na ndiyo kutokana na hii miradi nafikiri sasa fedha za research itapatikana. Niipongeze sana Serikali yangu, kwakweli I just love you people.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nije kwenye suala moja, Mheshimiwa Waziri wa Fedha naomba kwenye hili unisikilize vizuri sana nashauri, kuna ulipaji wa madeni wazabuni na wakandarasi, na niiombe sana Serikali haya madeni mnayolipa mzingatie na lile suala la Nelson Mandela kuna tatizo kubwa sana kwenye kile chuo Wizara ya fedha pamoja na Kampuni inayoitwa PPL walichukua mkopo wa mabilioni ya fedha takriban bilioni 38.7 kwa ajili ya ujenzi wa kile chuo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, walipochukua ule mkopo wakaipa ile kampuni PPL wao pia wakaingiza kampuni nyingine na kugawana kazi na wakampa mzabuni anayeitwa ELERA Construction, yeye ashughulikie na viwanja vya michezo. Sasa huyu hajamaliza vile viwanja vya michezo na anadai ile fedha, takriban milioni mia nne na kitu, ambayo ni retention. Sasa wale wamesema hawaweze kumlipa kwa sababu hajamaliza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nikuombe Mheshimiwa Waziri, kuna vurugu pale, wanashindana je, nani amlipe huyu na nani ambaye hataki kumlipa. Kwa hiyo kuna vurugu kati ya Wizara ya Fedha, Ardhi pamoja na Wizara ya Elimu, na Ardhi nafikiri inahusika. Sasa nimuombe Waziri alimalize hilo, na nikimaliza kuzungumza hapa Mheshimiwa Waziri nina document nitakupa uandike umalize lile tatizo la Nelson Mandela kwa sababu huyu mtu anataka retention lakini kazi hajamaliza, wewe ukimsimamia najua hilo litakwisha nafikiri umenielewa hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jingine nije kwenye ujenzi wa miundombinu. Mimi nakushukuru, kwenye elimu mmetoa bilioni 406 kwa ajili ya kuangalia miundombinu katika elimu. Niiombe sana Serikali na hasa Waziri wa Fedha pamoja na Waziri wa Elimu, kaeni pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niombe majengo yaliyojengwa UDOM, Waheshimiwa wenzangu mtakumbuka, UDOM ile ilijengwa kwa speed kali mno ili kuwaokowa watoto wengi waingie vyuo vikuu; wazo lilikuwa zuri na ni jema, lakini niwaambie kitu, yale majengo yalijengwa mengine kwa speed ya ajabu kiasi kwamba si imara. Kuna nyufa na tiles zimebanduka. Niwaombe Waziri wa Fedha na Waziri wa Elimu nendeni mkatembelee pale UDOM mtasikitika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tufanya ukarabati kabla hali haijawa mbaya. Nendeni UDOM, lakini si huko tu kuna sehemu nyingi majengo yamechakaa; ukienda MUST ni balaa majengo yamechakaa, ukienda Hombolo barabara haifai na hizo ni barabara zote zinazoingia vyuo vikuu. Jamani mbona tumeviweka nyuma ebu wasaidieni ili nao waonekane kweli ni vyuo vikuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hawa Hombolo wamepata eneo pale palikuwa kwa Mkuu wa Mkoa (RS); sasa muwasaidie, wanataka kutoa structure nzuri mno pale, nyinyi muwasaidie kwa kuwa-top-up ili waweze kujenga jengo zuri lenye tija. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nirudi kuzungumzia fedha mlizotenga kwa ajili ya sensa. Mimi nimefurahi mmetenga fedha za kutosha, bilioni 328 sio mchezo. Hata hivyo naomba sana m-develop device za kuweza kugundua watoto wenye ulemavu wanaofichwa wakati wa sensa ili tupate idadi kamili ya watu waliopo; sasa wale wanaofichwa ndani mtawagunduaje? Ninyi mtumie teknolojia, mtengeneze devices wakati wa sensa ili tupate idadi hata ya wale watoto wanaofichwa ili waweze kusaidiwa na Serikali yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho niipongeze Serikali kwa kuingia kwenye hizi blocks. Nakumbuka Mheshimiwa Naibu Spika alisema nini Kiswahili chake, nimejaribu kutafuta hili neno blocks sijui ni vipande. Nipongeze kwa kuwa kwenye hizo blocks; tuna PAP tuna IPU maziwa makuu na SADC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo SADC yenye ina nchi kama 15. Sasa unaona tukishakuwa blocks nyingi kiasi hiki mimi ninaamini kwanza tutaleta mahusiano mazuri na vilevile tutaondoa na vikwazo visivyo vya kikodi. Wazungu wale waliotoka Songea wanasema none tariff barriers zitaondoka (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kwa kufanya hivyo, na pia kwa kujikita huko mimi ninaamini tunaweza kufungua masoko vizuri na kuwa na urafiki wa kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi baada ya kusema hayo nikushukuru sana, ahsante sana. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Niende moja kwa moja kwenye kuchangia, mimi nitakwenda kwenye kilimo. Sasa kwenye Mpango, wenzetu wamesema kwamba wataimarisha mashamba makubwa yawe kitovu cha teknolojia kwa wakulima wadogo wadogo. Najiuliza haya mashamba makubwa makubwa yapo wapi, mangapi, halafu yapo wapi? Lakini nilifikiri katika Mpango, tunaongea hapa Mheshimiwa Nape amezungumza kuhusu kilimo na wewe mwenyewe umeongea. Hivi kwa nini tusiweke kwenye mpango sasa hivi, mashamba makubwa yaanzishwe na hawa vijana tunaosema hawana ajira nilizungumza, tuna vijana wengi hawana ajira Vyuo Vikuu hebu tuanze hilo kwa nini tunaogopa? Tufanye kama pilot hata katika mikoa miwili au mitatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya kuna hayo mabailiko ya hali ya hewa, kuna Covid, hivi wakati mwingine nawaza tutapata shida ya chakula na tungekuwa na mashamba haya makubwa je, si yangetusaidia. Kwa nini tusiwekeze huko tunaogopa nini? Iwe kwenye Mpango tuwasaidie hawa vijana, watafanya production wao wenyewe watafanya processing halafu baadaye mambo ya sales. Ni kiasi tu chakuwekeza kuwapa matrekta na pembejeo, hebu tuanze sasa kuwa hizo commercial farms tunazungumza lakini tunazo ngapi? Tunazo ngapi?

MWENYEKITI: Mheshimiwa Thea huwezi kuwa na commercial farms kama huna mabwawa makubwa, ili pale mvua haijanyesha wewe una supplement kwa kumwagilia, mvua ikinyesha mnakwenda namna hiyo.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, vivyo hivyo unavyosema.

MWENYEKITI: Nakuunga mkono lakini, endelea tu.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Eheee! Mmmh!

MWENYEKITI: Taarifa, endelea nimekuona Mheshimiwa Tabasam.

T A A R I F A

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba katika hili nataka kumwambia Mheshimiwa Mpango huu upo Misri, wenzetu wa Misri kwa kutumia maji haya haya yanayotoka katika Ziwa Victoria, kule kwao wamechimba bwawa, wanafunzi wanaotoka katika Vyuo Vikuu vya Kilimo wanakopeshwa kila kitu kwenda kufanya kazi hiyo. Nafikiri Tanzania na sisi tunaweza kwenda kujifunza kule tukaleta habari hiyo Tanzania.

MWENYEKITI: Taarifa hiyo Mheshimiwa Ntara.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani naipokea sana, nafikiri wewe ni Dokta. Tufanye hivyo, nafiriki tusisubiri wakati mwingine tunasubiri tamko lakini hebu tujipange tuone kwamba kila Kanda au kila mkoa. Wakati tupo Kahama tuliwaomba Kahama kwa sababu wale wanadiriki, wanathubutu, hebu waanzishe hilo. Tutamaliza au kupunguza hizi kelele za ajira. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu ya pili niende kwenye elimu. Suala lililozungumzwa nyuma kwamba tuboreshe mitaala, mitaala yetu ya elimu haijakaa vizuri, tatizo ni moja kwenye Mpango sijaona sehemu wamesema watawekeza ili hawa watu wa TARI waweze kuboresha. Hawana fedha kabisa hivi watakaaje chini waanze kuboresha mitaala. Serikali iangalie ile mitaala ili iboreshwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimeona kuna ujanzi wa Chuo VETA kikubwa Dodoma, sioni wivu lakini nilitegemea kutakuwa na mpango wa kuimarisha ile branch ya SUA iliyoko Tunduru. Hayo ni maneno tu, kule Tunduru wanasema kuna branch ya SUA, siku moja niliongea hapa Naibu Waziri wa Elimu ananiamba tutaongozana, mambo ya kuongozana siyataki, kwa nini tuongozane? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, SUA mmesema mmeanzisha branch Tunduru nilitegemea hapa angesema kwamba, tunaimarisha mpango wa SUA na nikuambie jambo moja wakiimarisha ile branch pale Tunduru itapanda baadaye kinaweza kikawa Chuo chenye program nyingi tu. Kuna korosho kule kwa hiyo, tutakuwa na program ya chemical engineering, tutakuwa na program ya mambo ya crops, tutakuwa na program ya fisheries inatoka kule Lake Nyasa. Lakini ile branch iko pale sijui ni jina tu hakuna kinachoendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, katika mpango wahakikishe kwamba watu wa Ruvuma, watu wa Lindi na Mtwara kunakuwa na Chuo. Tunalalamika hapa kwenye Vyuo tukisema Kusini hakuna Vyuo tunaambiwa eti hivi Vyuo vilivyopo ni vya Kitaifa. Kama vya Kitaifa basi vijengwe kwenye Mkoa mmoja vyote vije Dodoma au vyote viende Dar es Salaam. Tunaomba kuwe na Chuo mtusaidie ile SUA pale Tunduru inyanyuke. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine la mwisho. Nimeona kuna mpango kama alivyosema mwenzangu mmoja, huu mpango wa reli kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay nimeusikia toka enzi hizo nikiwa Mwalimu nafundisha nasikia mpango, enzi za Mtwara Corridor nilikuwa namsikia Marehemu Profesa Mbilinyi nimeusikia, nimeusikia, nimeusikia! Sasa hivi kule Ruvuma wanangoja wanasema na sisi tutaona treni? kwanza hawaijui! Nafikiri siku itakayopita watafikiri sijui ni bomu linapita sijui ni dudu gani? Sasa huo mpango uwe kweli waanze hata kwa kitu tuone tu wanafukua fukua matuta kule angalau, lakini isiwe mpango kwenye maandishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nakushukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, na mimi nikushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nitakwenda moja kwa moja, na nitachangia sana kwenye eneo la elimu.

Mheshimiwa Spika, eneo lolote au sehemu yoyote ambayo kuna vyuo vikuu hata watu wake katika eneo lile wanakuwa na maendeleo ya kiuchumi, maendeleo ya kisiasa na maendeleo ya kijamii.

Mheshimiwa Spika, Mikoa ya Kusini kwa muda mrefu imekuwa nyuma sana katika maendeleo kwa nyanja zote. Mikoa ya Kusini wakati tumekuwa wote tukisema jamani sisi watu wa Kusini tuko nyuma. Leo hii kama Mikoa ya Kusini ya Lindi, Mtwara pamoja na Ruvuma kukiwa na Chuo Kikuu cha Serikali mambo ya uchumi yatafunguka na watu wa eneo lile wote watakuwa wanapata elimu kutoka vyuo vikuu na mambo yao yatabadilika kama ilivyo kwenye Mkoa wa Dodoma. Wagogo tulikuwa tunawasema watani zangu; zamani ukisema Mgogo wengine wanaona aibu hata kusema mimi ni Mgogo, lakini sasa hii ukisema unatoka Dodoma Mheshimiwa Mavunde anafurahi, kwa sababu Dodoma imefunguka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na mpango wa kujenga Chuo Kikuu kishiriki cha Mkwawa, Matogoro, Songea na Mtwara, wakati ule Mheshimiwa Waziri alikuwa Prof. Msola, nimpongeze sana alikuwa mwerevu na mjanja; kikawekwa Chuo Kikuu pale Mkwawa ambacho ndicho Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu. Hata hivyo, wazo la Mtwara likafa kimya mpaka leo ikawa hatujui kinachoendelea, Matogoro – Songea nayo ikafa na hatujui kinachoendelea. Hizi sehemu tatu zilikuwa katika mpango wa kufanya haya maeneo yawe ni vyuo vikuu vishiriki, lakini mipango hiyo ikafa na hatujui kwa nini ilikufa.

Mheshimiwa Spika, niseme tu, kwamba Kusini tunahitaji a Public University full flagged. Mimi ningeomba Serikali jamani sasa hivi ijipange angalau kwa kipindi hiki waache legacy kama iliyoachwa hapa UDOM basi tuache legacy huko Kusini, kijengwe chuo kikuu ili watu wa Kusini nao waanze kufunguka. Tutafanya maendeleo mengine yote; tutajitahidi kilimo na mengineyo lakini bila elimu bado Kusini kule tunaonekana hatujatoka.

Mheshimiwa Spika, nije kwenye suala la pili ambalo naona nilisemee hapa ndani, ni suala hili la watoto wadogo wa chekechea. Hawa watoto wadodo nafikiri na Mawaziri waliangalie. Watoto wadogo wa chekechea wanaamshwa saa kumi usiku, saa kumi na moja magari yanawapitia, wanafika kwenye gari wanazunguka mpaka wafike shuleni labda ni saa mbili.

Mheshimiwa Spika, tunajiangalia sisi kwa sababu tayari tumeshakomaa na tayari tumeshapata elimu vizuri, lakini mimi naangalia, hivi hawa watoto wadogo wanaoamshwa saa kumi wanaandaliwa kwenda shuleni is it fair? Hiyo cognitive development ya hawa watoto kweli inaenda vizuri? Kwa sababu wanasinzia mpaka wakifika kule shuleni, na wakati wa kurudi wanazungushwa mpaka wanafika nyumbani kule yule wa kwanza anakuwa wa mwisho. Wakati mwingine tunasikia mambo yanayotokea ndani ya hayo mabasi wanayozungushwa.

Mheshimiwa Spika, sikatai kwamba tunafanya biashara, lakini sasa wanazungushwa na wakati mwingine wale wanaowazungusha kwenye magari mnasikia wanachowafanyia hao watoto. Sasa hilo nalo tuliangalie, kwamba hivi hii trend ni sawa? Wenzangu wataalam wa Saikoloji na wataalam wa Development ya hiyo brain, je, hicho kinachotendeka ni sawa?

Mheshimiwa Spika, niunganishe na moja linalotokea sasa hivi, mimi naona ni janga la Kitaifa. Kuanzia primary mpaka vyuo vikuu dawa za kulevya zimekuwa ni kawaida, bangi zimekuwa ni kawaida, michezo michafu inayofanywa na watoto wa kiume kwa wakiume imekuwa ni ya kawaida. Serikali tunasema nini? Tunajenga taifa la namna gani?

Mheshimiwa Spika, kuna siku moja kuna mzazi akanipigia simu akasema alienda huko beach, mnaita beach, sijui kwa Kiswahili tunaitaje, ufukweni; kwenda kule amekuta wasichana na wavulana wanafanya vitu vya ajabu vya waziwazi huko kwenye beach. Sizitaji shule maana tunasema tutaharibu biashara za watu; hivi tunaharibu biashara za watu ama tunaharibu Watoto? Mambo yanayofanyika sasa hivi ni ya ajabu, Wizara ya Elimu mpo, Wizara ya Afya mpo, Wizara ya Ustawi wa Jamii upo, Mambo ya Ndani mpo mpaka Utumishi. Tunalipeka hili Taifa wapi? Hivi baada ya miaka kumi au ishirini tutakuwa na watoto au tutaongeza vituo vya Mirembe? Hilo jambo linaniumiza na ni janga la Kitaifa, ni janga. Tutakuwa na watoto wa namna gani ikiwa hata watoto wa primary wanazijua bangi ni za kawaida? Je, tumehalalisha hii bangi? that a thing I want to know.

Mheshimiwa Spika, nije kwenye ukarabati wa vyuo vikuu. Niliongea kipindi kilichopita mpaka nikawa nawaza, hii UDOM niliizungumzia. Waende hao Mawaziri wakaangalie kule. Niliwaza nikasema hiki chuo ninachokizungumzia kingekuwa kipo Sumbawanga au kiko kule Newala labda wangekwenda, lakini kipo hapa karibu, hivi kwa nini hawaendi? Nelson Mandela ule mgogoro wa ujenzi wa kiwanja mpaka leo unaendelea, hawaendi.

Mheshimiwa Spika, ninawatahadharisha tu, ikija hiyo bajeti yao Elimu mimi yaani Shilingi hiyo nimeshandaa na watanifuata mpaka Ruvuma kuja kuichukua. Nelson Mandela, UDOM hapo kuna vyuo vya Afya vya kati, nilisema kule Songea hali ni mbaya, hebu nendeni mkazunguke kule muangalie. Nilisema wakati ule ulipokuwa Mwalimu wangu Ndalichako nilifiki umenielewa lakini ukani-put off kabisa, yaani sijui ulini-neglect kwa sababu ni mwanafunzi wako? I don’t know. Sasa amechukua mwingine, Professor Mkenda sitaki kuja kuniambia tuongozane, mimi sitaki kuongozana tukutane hukohuko, kuongozana sitaki. (Makofi/Vicheko)

Mheshimiwa Spika, jambo jingine nilizungumze kuhusu fedha za research katika vyuo. Nishukuru sana Serikali ni kweli sasa hivi watoto wengi wanapata mikopo, lakini kutokana na idadi kubwa ya watoto wanaopata mikopo fedha za research zikapungua sana.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Mtanisamehe sana leo sauti sio nzuri kama ile mliyoizoea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali ya Awamu ya Sita, kitendo cha kutoa trilioni 1.3 ziende kwenye miundombinu, imesaidia sana sana kwa madarasa na sasa tunaamini kweli watoto wakiingia kwenye madarasa yetu yapo na yamekaa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo niombe Waziri wa Fedha kwenye Mpango tuone sasa tunaongeza bajeti kwenye research. Kwenye ile mikopo ya wanafunzi tusipoongeza fedha, research zetu zitakuwa za kulipua. Pia tuongeze bajeti kwenye COSTECH wafanye research za uhakika. Nalisema hilo leo nalirudia ni mara ya nne; elimu ni rearch, afya ni rearch, uvuvi ni research na kadhalika. Haya yote tunayozungumza humu ndani bila kujikita kwenye research za uhakika na kutoa
facilities za uhakika kwenye research itakuwa ni kazi bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi juzi mlimsikia Mheshimiwa Rais akizungumzia suala la family planning. Alizungumzia suala la family planning na kusema sasa twende na family planning tupunguze lile zoezi ili tusiwe tunaongezeka kwa mtindo ambao hautasaidia kuleta maendeleo. Alilisema hivyo kwa sababu gani? Tayari takwimu za research ndizo zilisaidia Mheshimiwa Rais akaona kwamba huko tunakokwenda ni kubaya. Kwa hiyo ushauri huo aliutoa kwa sababu ya ripoti hizo za research. Ndio maana nasema research ni muhimu katika kila nyanja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu kila Wizara hapa wana zile basic research yaani kila Wizara ina kaeneo ka research wana basic research, lakini niwaombe washirikiane na Vyuo Vikuu ili wafanye research za uhakika, ziwe research effective.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nachangia kwenye eneo la kilimo. Narudia kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Sita kwamba anaendeleza ule mpango wa kuwapeleka Makatibu Wakuu pamoja na watendaji wengine wa Wizara Japan katika kusoma ile Program ya Local Government Reforms. Sasa kwenye hiyo program wenzetu kule wanaangalia namna gani kila eneo linaweza likawa na jambo moja la kuwaletea uchumi wananchi mmoja mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna program ile inaitwa OVOP, one village one product, sisi tujipange kwenye one district one product au one region one product. Mwekezaji au mfanyabiashara akija Tanzania akisema nataka asali nzuri unamwelekeza sehemu. Vile vile sio asali nzuri mwingine anasema nenda Lindi, nenda Singida, nenda Tabora hiyo haitawezekana. Kwa hiyo tukiwa na program ile tukai-develop hapa kwetu, tukai- copy, ndio italeta ufanisi na yale mafunzo yetu tunayokwenda huko yatakuwa yanaleta tumaini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna mazao hapa wenzangu walishaongea, unakwenda mahali ujue kabisa hapa nakwenda kwa ajili ya kahawa, nakwenda mkoa huu kwa ajili ya alizeti, nakwenda mkoa huu kwa ajili ya mahindi, lakini sitapenda kuzungumza nakwenda mkoa huu kwa ajili ya tumbaku. Hilo nimemwambia Mheshimiwa Waziri wa Kilimo, hilo hapana. Kwa hiyo tujipange hivyo, twende na ile program ili tusaidie. Wawawezeshe sasa, wamerudi kwenye mpango Mheshimiwa Waziri awawezeshe sasa tu-practice ile ili kwa kweli tuwe na zao moja, sio lazima zao la kupanda hata madini mbalimbali, mwekezaji au mfanyabiashara akija ajue nakwenda mahali fulani napata kitu fulani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, katika kufanya hivyo niombe katika Mpango, hivi ni lini wakulima hawa wataendelea kulima kwa jembe la mkono? Niombe Mheshimiwa Rais anapotafuta fedha hizi nyingi na zinapoingia katika Mawizara tunakuja hapa tunalalamika fedha nyingi zinapigwa. Hebu tujipange sasa hizo fedha zisipigwe, tuone kama tunaweza kufanya pilot study kwenye mikoa michache, vijiji vinunuliwe matrekta, kijiji kimoja matrekta matatu, tutakuwa tunafanya kitu cha maana. Tunataka uchumi wa mtu mmoja mmoja, lakini hili jembe la mkono Mheshimiwa Waziri wa Kilimo na Mheshimiwa Mwigulu hatufiki mbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tujaribu, hivi hatuwezi kila kijiji kikapata trekta tatu? Kwani trekta tatu ni bei gani? Waweke kwenye mpango kwani hawalielewi hili? Hebu waweke kwenye mpango jamani tubadilishe hiki kilimo. Yaani hii mipango tutaiongea lakini itakapokuja wakati wa utendaji kama mtindo ni ule ule wa jembe la mkono, nakwambieni tutakuwa na mipango lakini utekelezaji wake ni zero. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kama nilivyosema, tuone kabisa kwamba sasa kwenye mpango huko zao la tumbaku Waziri asiliweke, kama wanataka kuendelea kulima tumbaku, wawachague wale wakulima wakubwa wanaofaidika, wa-deal na hao wakulima wakubwa, wakulima wadogo wa tumbaku hawapati faida yoyote, Mheshimiwa Bashe analijua hilo, hawapati faida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wale verifiers usipowapa pesa, usipowahonga, tumbaku yako kila siku itakuwa grade ya chini, sasa kuna faida gani? Wawawezeshe wakulima walime mazao yale yanayoweza kuwapa faida, mazao mbadala, tumbaku tuipige vita, tumbaku haiwasaidii wakulima wa chini.

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Taarifa.

T A A R I F A

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe mzungumzaji taarifa, ni kweli faida inakuwa ndogo kwa sababu hata kwenye masoko kumekuwa na utaratibu wa kufanya central market ambazo zinafanyika mjini badala ya masoko kufanyika kwa wakulima walioko kwenye maghala yao vijijini.

SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara unapokea taarifa hiyo?

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea kwa mikono miwili na namwomba anisaidie tuendelee na kampeni ya kuliondoa na kulipunguza kabisa hili zao la tumbaku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Na mimi niungane na wezangu kuwapongeza sana Mawaziri, ndugu yangu dada yangu Jenista pamoja na Naibu wake; jina lake la Kigogo ni gumu samahani sana. Niwapongeze kwa kazi nzuri nipo kwenye hiyo Kamati, kwa hiyo niwapengeze kwanza…

SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara, anaitwa Deogratius Ndejembi; kwa hiyo unaweza ukamwita Deo.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nikupongeze sana Mheshimiwa Deo kwa kazi nzuri unayofanya kwa kusaidiana na Mheshimiwa Jenista. Kwanza niwapongeze hasa kwa usikivu tukiwa kwenye Kamati. Ni Mawaziri wasikivu sana, maoni yetu mengi waliyachukua kwa uzito waliostahili.

Mheshimiwa Spika, mimi nianze na suala moja ambalo tulizungumza kwenye Kamati na mlitoa ahadi; kuhusu harmonization ya mishahara kati ya wahadhiri na waendeshaji.

Mheshimiwa Spika, Katibu Mkuu alitoa ushahidi kwamba hilo suala tayari wanalifanyia kazi. Sasa mimi niseme tu, liamenza muda mrefu, na mnasema hao watu walikuja kuwaona; hebu niombe sasa mlifanyie kazi ili huko kwenye vyuo watu wafanya kazi kwa upendo. Nililisema, maana unakuta mhadhiri ana master na mwendeshaji ana masters lakini mishahara yao inakuwa tofauti mno kiasi kwamba ikapelekea watu kudharahuliana au kujengeana chuki. Kwa hiyo ni vizuri mkaangalia hilo suala lifike wakati sasa liishe.

Mheshimiwa Spika, Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya hawa ni watumishi. Kwa muda mrefu wamekuwa wakipata political fund ya milioni tano ambayo ni ndogo sana. Mimi nilikuwa Mkuu wa Wilaya, hiyo milioni tano nilikuwa ninaiona; na Wakuu wa Mikoa milioni 20. Sasa ni muda mrefu Mkuu wa Wilaya au Mkuu wa Mkoa anakwenda na hicho kiwango.

Mheshimiwa Spika, mimi niwaombe wakae pamoja na TAMISEMI kuangalia kiwango cha huyu mtumishi kiwe angalau kipande. Mkuu wa Wilaya anakwenda mahali kwenye harambee huku hana hela, unakuta anatoa mia tano, mia tatu; na hiyo inawafanya wanaonekana wanyonge. Mkuu wa Mkoa anakwenda mahali anashindwa hata kutoa milioni moja. Sasa sijui Waheshimiwa Mawaziri political fund yao ni kiasi gani; lakini ningeomba hili litazamwe mkishirikiana pamoja na TAMISEMI kuona kwamba kwamba ifikie wakati sasa kile kwango kiongezeke. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kingine nipongeze sana kazi waliyoifanya wala CAG kama alivyosema Prof. Mkumbo. CAG walifanya kazi nzuri sana kuangalia idadi ya watumishi katika shule za msingi. Sasa ile asilimia 41 ya upungufu ni kubwa mno. Kwa hiyo, cha kufanya hapa sasa ni kuangalia namna gani hao CAG nao waende kwenye vyuo, na wakifika kwenye vyuo nako watoe hizi takwimu za upungufu wa watumishi. Sasa CAG akienda kwenye vyuo yeye anangaalia tu mambo ya consultancy; ajue vyuo na shule kazi yao ni ufundishaji na kujifunza. Kwa hiyo a-base kwenye kukagua vitu vinavyohusiana na ufundishaji na kujifunza. Kwa mfano anaenda pale Ardhi ili tujue watumishi wa pale ardhi wamepungua wangapi? Anacheki workshops zao zikoje, anacheki maabara; hivyo ndiyo vitu anatakiwa CAG atuambie ili tujue kabisa upungufu wa vituo hivyo katika vyuo vikuu na vyuo vya kati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine, niwaombe Ofisi ya Utumishi kule Hai Mkoani Kilimanjaro tayari wametenga eneo la kujenga Chuo cha Utumishi wa Umma na wametenga muda mrefu. Sasa, niwaombe Ofisi ya Utumishi, lichukueni hilo Mheshimiwa Waziri ili muone kama mnaweza kuanza angalau na zile process za mwanzo, kwasababu ni muda mrefu hilo eneo limetengwa. Bahati nzuri kwenye kamati tuliwaambia mimi naona ingependeza kama mtalichukua hilo na kuona kwamba tunaongeza idadi ya vyuo vya utumishi kwa kuwasaidia watumishi kupata elimu na pia kuongeza vyuo vya aina hiyo katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, mimi baada ya hapo nikushukuru sana kwa leo naishia hapo. Ahsante sana. (Makofi)
Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa miongoni mwa viongozi wenye ushawishi mkubwa Duniani na kupewa Tuzo ya mafanikio ya ujenzi wa miundombinu
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, na mimi nichukue nafasi hii kuwaomba Wabunge wote kabisa tumpongeze Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, kwanza kabisa ametuheshimisha sana wanawake wa Tanzania na wanawake wa Afrika. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Spika, kwanza hata katika teuzi ametuheshimisha, yaani ni kiongozi ambaye amesimama na kuona kwamba binadamu wote, wanaume na wanawake tunaweza tukafanyakazi. Pia tuangalie katika suala la miundombinu, miundombinu hii itawasaidia sana wanawake katika suala la uchumi. Kwa hiyo, ametuheshimisha kuona kwamba miundombinu yetu sasa inaendelea kukua vizuri na inaendelea kuboreshwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine ambao Mheshimiwa Rais anastahili pongezi ni suala linalohusiana na eneo la afya. Mheshimiwa Rais amejipambanua sana kuona kwamba katika hospitali zetu, hasa maeneo ya wanawake kujifungua na watoto wadogo kupata huduma, amehakikisha kwamba zanahati zetu na vituo vya afya sasa hivi maeneo yote ukienda lazima yawe na sehemu ya wanawake kujifungua salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mimi nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri sana anayoifanya upande wa miundombinu, afya na hata elimu. Kwa hiyo, anastahili pongezi na niwaombe Wabunge wote tuendelee kumtia moyo Mheshimiwa Rais, tumpongeze ili aendele kuboresha maeneo haya yote kwa manufaa ya wanawake na wanaume wote wa Tanzania, ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nichukue nafasi hii kupongeza Serikali na hasa Wizara ya Elimu kwa kazi nzuri ambayo wameifanya toka wamekabidhiwa ofisi hiyo na hasa kwa kipindi hiki ambacho wamekaa wanaboresha mitaala na wanaboresha sera katika elimu. Nitakwenda moja kwa moja kwenye point, kwanza nitazungumzia kuhusu ajira kwa Wahadhiri.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeongea mara nyingi kwamba Wahadhiri hawatoshi, wameajiriwa 2017 mpaka 2018 ndiyo kulikuwa na ajira. Kuanzia hapo wanasema ajira zimeongezeka, lakini siyo ajira mpya yaani ni ajira mbadala, labda mtu ame-retire au mtu bahati mbaya amefariki, ndiyo kunakuwa na replacement.

Kwa hiyo ajira zimekuwa ni shida na madarasa yale tunajua ya Vyuo Vikuu makubwa wanafunzi ni wengi bado ajira haitoshi kabisa. Hata leo ukiwauliza hapo mbele wanasema tumeajiri, wanipe data wameajiri Wahadhiri wangapi katika kila chou, waje na majibu wameajiri Wahadhiri wangapi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hapo hapo tuliomba, kwa sababu kuna shida hii ya ajira, hebu tuongeze retirement age ya maprofesa. Leo tumesomewa hapa idadi ya maprofesa waliokuja pale, bado wana nguvu ya kuweza kutoa msaada katika vyuo. mfano juzi tulikuwa na profesa Ishumi, mawazo aliyokuwa ananipa pale mimi mwenyewe nilishangaa akina Profesa Maboko bado akili zao zinafanya kazi safi, kwa hiyo tuongeze retirement age.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Naibu Waziri alinijibu siku moja akasema hilo tumelichukua. Haya majibu ya kusema hilo tumelichukua sijui wanayachukua wanayapeleka wapi? Sisi tunataka utekelezaji ndiyo unafaa, unalichukua unalibeba unalipeleka wapi? Wazo limetolewa kama linawezekana lifanyiwe kazi, waongeze muda wa maprofesa, miaka 65 bado wadogo sana. Wizara imeona maprofesa walivyo wadogo na wanavyofanya kazi; akina Profesa Ndekidemi bado anafanya kazi ya kutosha. Profesa Muhongo yuko hapa, wanafanya kazi nzuri. Naomba Wizara iongeze age ya retirement kwenye vyuo vikuu ili hawa watu watusaidie kwenye vyuo vyetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwenye mshahara pia. Hawa Ma-VC, nilizungumza. Ma-VC hawana mishahara, yaani wamepewa vile vyeo hawana mishahara. Wakati mwingine inalingana kabisa na wale Wahadhiri wa kawaida. Hivi kutakuwa na heshima kweli katika kufanya kazi? Mtu ni mkuu wa Chuo mshahara wake unalinga na na lecture wa kawaida. Hebu Waziri wa Elimu libebe hilo, wewe ni Profesa, unafahamu kazi za maprofesa wenzako huko vyuoni, libebe hilo ukalifanyie kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine katika vyuo vikuu, ipo haya ya kuruhusu freedom katika academics. Tuwaachie uhuru vyuo vikuu kwenye suala la taaluma lisiingiliane na watu wa Utumishi. Zamani kulikuwa na utaratibu, wale wanaofanya vizuri tunawabakiza pale na wanachaguliwa na wetu wenyewe pale pale vyuo vikuu. Anabaki pale kama tutorial assistant baadaye analelewa, anafanyiwa mentoring, anapanda, anaenda kusoma mpaka anakuwa na Ph.D; lakini tukiliondoa hilo kwenye upande wa taaluma, yaani University hazina freedom kabisa. Hiyo lazima tuiangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hata katika kuajiri, tunaposema tuongeze retirement age pia tuhakikishe sasa hivi Universities ziwe kweli universal, tuwaruhusu walete maprofesa kutoka nje ya nchi. University zetu kweli jamani zimekuwa local; very local. Tuwaruhusu walete maprofesa kutoka nje ili kweli tuweze kupata elimu mchanganyiko inayokidhi haja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwenye hizi suala za fedha za HIT. Fedha za HIT ni mkopo na mikopo huwa inalipwa na wote, na vyuo vyote. Naomba mgawanyo wa fedha uende kwenye Private Universities na Public Universities. Siyo unanijibu hapa siku moja Mheshimiwa Waziri unaniambia kwamba na wale private watapata kamgao as if wao hawastahili. Inapokuja mikopo hapa, tunalipa wote na sehemu zote zinalipa mikopo sawa kupitia kodi. Kwa hiyo, naomba Wizara ihakikishe ije na majibu mazuri kwenye ule mgao wa HIT; Private Universities wanapata vipi na Public wanapata vipi? Kwa sababu hawa watoto wanaosoma ni watoto wetu sote. Kwa hiyo, hata yale manufaa ya mkopo wayapate wote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, nipongeze kwenye…

(Hapa kengele iliilia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Ni kengele ya ngapi? Mheshimiwa Naibu Spika, kazi zinazofanywa na TET; hawa TET (Taasisi ya Elimu) kazi yao ni kuandaa mitaala, kufuatilia na kutoa mafunzo. Mwaka 2005 wakati imekuja hiyo programu ya ufundishaji mahiri (competence base) walimu hawakupewa training ndiyo maana leo hii tunalalamika hapa, walimu hawajui kufundisha, wanawafundisha watoto hawawezi wakawa na skills kwa sababu hii programu walimu hawakupata mafunzo na kama walipata, walipata wachache mno.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naiomba Wizara, kwa sababu mmekaa mnaandaa hii mitaala na tumeipigia kelele sana hapa Bungeni, inapokuja kwenye kutoa mafunzo, tuwape fedha za kutosha hii taasisi ili watoe hayo mafunzo, lakini niwaombe hawa wanaotengeneza mitaala, waangalie ule mfumo wa chakula, nami nipo tayari kwenda kusaidia hata bila posho; mfumo ule wa chakula na mfumo wa uzazi wauangalie vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye mfumo wa uzazi toka mwanzo tunafundisha tohara ni muhimu. Sasa kwenye mfumo wa uzazi waanze kuingiza ukeketaji ni haramu, waweke kwenye mfumo wa uzazi. Watoto wakianza kujengeka toka mwanzo kwenye ile reproduction kwamba ukeketaji haufai, itawajengea hiyo kuelewa na huo ukeketaji tunaoupigia kelele unaweza ukapungua. Ukeketaji ni ukatili, wekeni ndani ya mfumo wa uzazi mnapokwenda kurekebisha hiyo mitaala. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia angalieni mfumo wa chakula. Kwenye ule mfumo wa chakula andikeni umuhimu wa chakula; umuhimu wa chakula kwa watoto wa kike na watoto wa kiume. Sasa hivi huu mfumo wa chakula unaambatana na uzazi. Leo hapa tunalalamika vijana wengi hawana nguvu za kiume. Inaanzia kwenye mfumo wa chakula. Kwa hiyo, watu wa mitaala andikeni pale, vijana wale chakula gani? Wewe… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante Daktari.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nianze moja kwa moja kwa kuipongeza Serikali ya Awamu ya Sita hasa kwa eneo kubwa kabisa la suala la mikopo. Sasa hivi hali imetulia, wanafunzi wametulia, angalau zile Message za mikopo zimepungua. Jambo kubwa sana limefanyika na Serikali hii, lakini bado niombe Serikali hao wanafunzi wa vyuo vya kati, naomba Serikali wajipange safari hii, hatutaki kelele za hao wanafunzi wa vyuo vya kati nikiwa na maana vyuo vya ufundi, maeneo ya afya na maendeleo ya jamii, hata wao waweze kupata mikopo. Tukifanya hivyo tutawasaidia sana watoto wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwenye suala la maadili. Leo kwa mara ya kwanza nimefurahi sana kuona baadhi ya Wabunge hasa wanaume akiwemo Mheshimiwa Sanga na Saashisha wanalizungumzia suala hili la maadili na hasa katika maeneo ya kuona watoto wetu na hasa wa kiume wanafanyiwa mambo ambayo hayafai.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ifike wakati Serikali ilete Muswada hapa ili kuweza kuwa na sheria kali na sheria kali hizi hatutakuwa sisi wa kwanza. Tunaogopa, mtu akinyongwa tunasema haki za binadamu, lakini huyu mtoto anayelawitiwa hana haki? Tulete sheria niwaombe Wabunge jamani tusimame wote kwa umoja wetu, Serikali walete Muswada hapa wa Sheria hawa watu wanaofanya hivyo wahasiwe au wawekewe dawa wawe wanapata vifafa, yaani mtu akipata kifafa hata zile nguvu zinakuwa hakuna. Nimwombe sana Waziri wa Afya, wao wnajua hayo mambo ya chemicals, watafute dawa hawa watu tuwa-fix, kama hatutaki kuwahasi basi tuwape wadudu wale wa kupata kifafa, waendelee kuanguka na kifafa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivyo kwa sababu gani Waheshimiwa Wabunge? Hiki kizazi ni cha laana, haya mambo wanayofanya ni laana, tukiendekeza kuwaacha nawaambieni wote hapa tutapata laana. Tuondoe hicho kizazi waondoke kabisa na dawa ya kuwaondoa hawa ni kuwahasi tu wasiendelee na ule mchezo mchafu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunakuwa na huruma na watu ambao hawana huruma na watoto. Leo hii fikiria una mtoto, wengi hapa mna watoto wadogo, sasa fikiria kama ungemkuta yule mtu anamfanyia mtoto wako kitendo hicho wewe ungefanya nini? Ungemshika hapa umpeleke Polisi? Naamini wengi hapa ungemnyonga pale pale, ungemmaliza. Sasa kwa sababu kunyonga wanasema sijui haki za binadamu basi wahasiwe, vyombo viko hapa wanawakamata wanawahasi huko huko kimya kimya au wanaweka wadudu wa kifafa waendelee ili wasiwe katika dunia hii. Hata hivyo, tukiendelea hivyo hawa watoto wanafanyiwa toka wakiwa wadogo, basi kundi la mashoga litaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, wako baadhi ya Viongozi sijui ni wapagani, sijui wana dini gani? Ndani ya Makanisa watu wanatetea ushoga, Serikali wanawaangalia tu, kweli jamani? Clip zinatoka mtu anatetea ushoga, anasema kwani ushoga ni nini? Si mtu unaamua mwenyewe? Serikali iko kimya, huyu wangemchukua kabisa hapo Madhabahuni anakohubiri ushoga wangemchukua wakamfanyia hicho kitu… (Makofi)

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

T A A R I F A

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumpa taarifa mchangiaji kwamba sio sahihi kwamba hakuna hatua zilizochukuliwa. Watu ambao wamefanya hiyo tayari wameshachukuliwa hatua na sheria inachukua mkondo wake na Serikali haitaendelea kuvumilia aina yoyote ya uvunjifu wa sheria za nchi hii. Kwa hiyo naomba nimpe taarifa hiyo.

NAIBU SPIKA: Daktari, taarifa hiyo Waziri mhusika amekupa.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri Masauni mimi nakuheshimu sana, sheria hizo zipo, hizo sheria zipo lakini bado siyo kali, ndiyo maana wanaendelea kufanya hayo madudu, leteni sheria tukifanya kwa watu watano, kwanza ukiwahasi unafikiri watatangaza kwamba mimi wamenihasi? Hawawezi! Leteni hapa tutaweka hiyo sheria, kwa nini mnatetea Mheshimiwa Masauni, hivi kweli hawa watoto tunaowazaa kwa uchungu vile wanafanyiwa hivyo? Hapana, hebu tujipange. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni kuhusu ndoa za utotoni. Leo hii mimi huwa nashangaa sana, tunakaa hapa ndani ya Bunge tunasema ndoa za utotoni hazifai, ndoa za utotoni hazifai halafu tunajichanganya wenyewe tunasema eti mtoto akishapevuka anaweza akaolewa wakati wowote.

Mheshimiwa Naibu Spika, watoto wa siku hizi wasichana wanapevuka kati ya miaka tisa na miaka kumi. Fikiria una binti yako ana miaka kumi, eti unaenda kumuoza kwa sababu amepevuka, unaenda kumuoza kwa mwanaume mwenyewe ni giant natamani kutaja hata majina ya mfano, kweli. (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba unilinde mtoto ana miaka kumi, kumi na moja, kumi na mbili kumi na tatu, kumi na nne, unaenda kumuoza kwa mwanamme, mtu kama Festo Sanga. (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, huo ni mfano, huyu mtoto anapokwenda pale anaenda kuolewa, anaenda kubakwa? Huyu mtoto si atajeruhiwa tu? Zamani watu wanashangaa wanasema zamani…

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba utulivu.

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa.

NAIBU SPIKA: Taarifa.

T A A R I F A

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Napenda kumpa taarifa Mama yangu pale. Mdogo wangu Festo yupo under forty ni mdogo, nadhani ana miaka sijui 32 kwa hiyo huo ni mwili tu usije ukaogopa. (Kicheko)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa endelea.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, zamani Mama zetu walikuwa wanaolewa wakimaliza Darasa la Saba. Ni kweli wanaolewa miaka 16, miaka 17, miaka 18 lakini lazima tujue kwamba walikuwa wanamaliza Darasa la Saba au Darasa la Nne hana pa kwenda. Hakuna VETA, hakuna shule za sekondari, leo hii kuna shule za sekondari kibao, kuna VETA, watoto wamalize Darasa la Saba waendelee na masomo. Niwaambie ukweli hata wale wazazi wetu walivyokuwa wanaolewa zamani wakiwa wadogo wengi wao ukiwauliza wanasema mwanangu tulikuwa tunaolewa ni mateso matupu, wala tulikuwa hatufaidi hayo maisha ya ndoa, kwa sababu kibinti kinaolewa kidogo kwa hiyo kinakwenda pale kinanyanyasika, kilichokuwa kinatokea pale ni sexual abuse! Sasa wewe leo unasimama mahali unahutubu unasema eti mtoto akishapevuka akaolewe!

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbunge muda wako umekwisha.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo ninakushukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nakushukuru, nitakwenda kwa haraka sana. Naomba Mheshimiwa Waziri awe makini wachukue hizi point, najua watazidadavua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nipongeze Wizara kwa mipango yenye kuleta tija, tunatumaini italeta tija. Lakini nimwambie Mheshimiwa Waziri, jana nilikuwepo pale jioni wakati Mheshimiwa Waziri Mkuu anatoa yale maagizo. Yale maagizo maana yake ni kwamba, bado tunahitaji utambuzi na ufatiliaji wa mifugo, hapa hatuwezi kukwepa; na alitoa yale maagizo ili ukayafanyie kazi ubaki kwenye hicho kiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado ufugaji katika nchi yetu ni kama adhabu. Ni kama adhabu kwa sababu kuna mambo bado tunahitaji tulete mabadiliko ndani ya sekta hii ya mifugo. Nchi imesema ina ng’ombe milioni 36 lakini bado wafugaji wale hawana access kwenye elimu ya mifugo, hawana access kwenye afya za mifugo yao, hawana access kwenye kujua malisho, hawana access hata ya elimu inayotolewa kwenye ufugaji wenyewe. Sasa hayo ni mambo ambayo Mheshimiwa Waziri wanatakiwa wayafanyie kazi; na wanaweza tu kuyafanyia kazi ikiwa kuna ufatiliaji, na ndani ya ufatiliaji ndipo tunapata hizo research, ndiyo maana ya research. Kwa hiyo hapo ndio utapata tafiti za kujua kwamba wafugaji wangu wana elimu, wanafaidika kweli, hawa wafugaji wangu wanajua afya za mifugo yao, magonjwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kuna haya mabadiliko ya tabianchi. Mabadiliko ya tabianchi yanaingia katika kila sekta. Kwa hiyo mfugaji asipokuwa na elimu ya mifugo, elimu ya aina ya maradhi yanayokuja au magonjwa hatufiki huko. Kwa hiyo suala la ufatiliaji, suala la kutambua mifugo ni muhimu, hilo ninamwambia Mheshimiwa Waziri asilipindishe na alifanye kwa uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nini tukifanye sasa hivi, tukishafanya huo utambuzi maeneo muhimu ya malisho hayo wanayoyasema ya chakula yatajulikana, upatikanaji wa masoko pia utajulikana. Lakini pia tutaweza kuzuia ulaghai wa kuingiza wanyama kutoka nje ya nchi pamoja na ulaghai wa kuuza nyama isiyokuwa na ubora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakwenda haraka, na sasa ninakwenda kwenye hiyo Wizara yenyewe ya Mifugo. Nimuombe, nilizungumza kipindi kilichopita, katika Wizara ambazo zinaweza kusaidia, kama alivyosema Mheshimiwa Mhagama, Wizara zinazoweza kusaidia kuleta ajira hii ya kwake ni mojawapo, wasikwepe. Ile program ya BBT ije kwake kama BBT2 na ile ya kilimo ya Bashe iwe one. Yeye alete BBT2 atafanikiwa. Ni lazima wafungue hiyo ili wahitumu hawa wapate maeneo ya kupata ajira. Kwa hiyo atakapokuja kwenye speech yake ya mwisho aweke mikakati yako tuone kama hili ameliweka, litakuongezea; na hilo ndilo linaweza kusababisha kuongezwa kwa bajeti, wakaona kwamba huyu ana mpango wa BBT2 kwa vijana. Kwa hiyo hapo anaweza akaongezewa hata bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye suala la uvuvi. Wenzangu wamesema, tuna Bahari na maziwa lakini pato linalotokana na huo uvuvi ni 1.7%, hiyo ni ndogo sana. Sasa mimi nataka nitoe ushauri kwenye eneo la uzalishaji wa vifaranga vya Samaki, anzeni kufatilia pale SUA. Kile chuo ukienda pale na mitambo yao utafurahi; sijui kama amewahi kutembelea pale, waende wakaone, wanazalisha vifaranga vya Samaki. Sasa wao wakiwasaidia, wakaungana, kwa sababu chuo ni cha Wizara ya Elimu lakini wale Samaki na mifugo iliyopo SUA ni vya kwake yeye. Waende wakaungane na chuo waone ni namna gani wanaweza kujaribu kutengeneza vifaranga vingi vikasambaza si Morogoro tu vikaenda mpaka mikoa mingine kwa sababu hawa walisema wanazalisha wanasambaza pale Morogoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ile ni project kubwa, kwa hiyo wao wawasaidie ili iwe project ambayo ni kubwa zaidi, maana nasikia nchi hii kuna sehemu mbili tu wanazalisha vifaranga vya Samaki. Sasa kile chuo pia kitawasaidia kuwainua wao. Kwamba wanatumia vyuo vyetu, lakini pia hata kile chuo chenyewe kinaweza kikasaidika na kufanya mradi wake ukue zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi baada ya kusema hayo niseme nampongeza, lakini ili bajeti yake iongezeke achukue hii ya BBT2 atakuja kunikumbuka siku moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza kabisa, nami nipongeze sana kwa kazi nzuri inayofanywa katika Wizara ya Elimu. Nampongeza Mheshimiwa Rais kwa kuyatenda hayo, nampongeza Waziri na watendaji wote na hasa Wakurugenzi wa taasisi mbalimbali katika Wizara ya Elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi zangu zinakwenda kwa sababu sasa hivi tunaona vyuo vya ufundi vinajengwa vya kutosha halafu kuna hii project ya HEET imesaidia sana katika kuboresha mitaala na pia ujenzi wa mashule. Pia hii bodi ya mikopo tulianza na shilingi bilioni 450, leo hii shilingi bilioni 654 ndiyo zimepelekwa kwa wanafunzi. Hili jambo Waheshimiwa Wabunge wenzangu limeleta utulivu mkubwa sana katika vyuo vyetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba tu hapo kwenye HEET, Mheshimiwa Waziri ananisikia, mmetoa mgawanyo mzuri sana wa Universities hizi za Serikali, sasa tupate hata mgawanyo wa fedha za HEET katika universities zile za binafsi, tunaziita private universities; ule mgawanyo mnasema kwamba wao wamepewa fedha kwa ajili ya kuwasomesha, lakini tupate mgawanyo unaoonesha kwamba, je, universities zitapata mgawanyo wa walimu wangapi kwenda kusoma, ili na wao watulie? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwa hawa watendaji wa kati. Watendaji wa kati ndio msingi mkubwa sana wa kuchochea maendeleo hasa kwenye uchumi. Vyuo vyetu vitano kama unakumbuka; DIT, MUST, ATC, NIT na kile Chuo cha Maji viliondoa kabisa malengo yake ya zamani. Yale malengo yaliondoka kabisa, kwa sababu vyuo hivi vyote sasa vilijikita katika kutoa shahada. Siyo vibaya, lakini naomba sasa vyuo hivi virudi kwenye malengo yake ya zamani, ndiyo tutapata hao mafundi tunaowaita mafundi mchundo na wahandisi. Wajikite pia katika yale malengo ya zamani kama nilivyosema. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kozi za kati kwa sasa hivi kwa wasichana ni asilimia 25 tu kwa taarifa, sasa tuangalie, tuongeze juhudi za kuona wasichana pia wanajiunga katika hizo kozi za kati.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Tanzania uwiano wa watendakazi kwa sasa, nina maana ya mhandisi, fundi mchundo na mafundi stadi ni kumi kwa tisa kwa saba (10:9:7). Sasa hii haikubaliki, tumegeuza. Sasa muundo au uwiano unaotakiwa kidunia au kiulimwengu ni moja kwa tano kwa ishirini na tano (1:5:25). Yaani unapokuwa na mhandisi mmoja, basi uwe na hao mafundi mchundo watano, uwe na mafundi stadi Shirini na tano, lakini sisi tunafanya vice versa na ndiyo maana tunapata shida sana katika watendaji hawa mafundi mchundo na hawa mafundi stadi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tumegeuza ndiyo, tunazalisha shahada, siyo mbaya, lakini sasa tuone, kama nilivyosema, ukuaji wetu wa uchumi sasa hivi tujipange kuona kwamba hawa mafundi watendaji kazi wanakuwa wakubwa zaidi na namba yao inaongezeka zaidi. Sisemi kwamba shahada tuziondoe, Hapana, la hasha, lakini nasema tujipange kuona kwamba uwiano huu twende kidunia zaidi, ndiyo tunaweza kufanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na Serikali sasa kuongeza hiyo bajeti ya mikopo, wastani wa asilimia 70 mpaka 80 zinakwenda kwa wanafunzi wale wanaochukua masomo ya arts, hiyo ndiyo taarifa. Yaani wa masomo ya arts asilimia 70 mpaka 80 ndiyo zinakwenda kwao, ukiangalia hii bajeti ya mikopo. Sasa ukiangalia wanafunzi wanapomaliza masomo, wengi wao wanakaa muda mrefu sana bila kupata ajira, lakini ndio wamechukua hiyo asilimia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni vyema sasa tuanze kujitafakari, yaani hiyo iwe katika mpango, akilini mwetu, tuanze kujipanga sasa. Je, watoto hawa wanaomaliza Kidato cha Nne na cha Sita, siyo vema wakaanza kupata mikopo ili waweze kujiunga na kusomea ujuzi uwasaidie kujiajiri? Hilo mliweke yaani kama mpango wa baadaye, muanze kulifikiria sasa hivi. Maana yake tunapompa mkopo huyu mtoto anayemaliza Chuo Kikuu halafu unakuta hata ajira hana, amesoma tu shahada, ajira hana. Inaleta shida na wakati mwingine kumwongezea mzigo wa umasikini. Kwa hiyo, tujipange kwenye eneo hilo tuione kama sasa tunaweza kufanya, akimaliza form four au form six, anapata mkopo, anakwenda kwenye fani za ujuzi na kuweza kujiajiri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwenye ujenzi wa vyuo vikuu. Hili nalisema kwa masikitiko makubwa sana. Mkoa wa Mtwara na Ruvuma, yaani hata ukiangali vile vyuo vikuu vya private vingi vimekufa. Nilikuwa nafikiria, hivi Serikali, haiwezi kusaidia? Kwa mfano, tulikuwa na chuo cha udaktari pale Peramiho, kikafungwa, wale wanafunzi wakapelekwa Mbeya. Yale majengo yako pale, wananchi wa kuzunguka yale maeneo ya Peramiho waliwekeza sana katika majumba na mashamba, lakini sasa hivi wamebaki pale hakuna kitu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukafikiria wakati mwingine tukasikia kuna chuo Tunduru, Branch ya SUA. Ghafla tukaona ile SUA imekwenda Katavi. Siwaonei wivu, wala sikatai, lakini pale ambapo wazo la Tunduru lilianza, kwa nini halikuendelezwa, badala yake sasa nguvu ziko Katavi? Sasa wanasema huenda kikaendelezwa. Naomba Mheshimiwa Waziri Chuo cha Tunduru pale branch ya SUA, nguvu mnazozipeleka kule Katavi zianze pale kwanza, kwa sababu Katavi ilikuwa ni ya pili. Kule hatuna mradi mkubwa, nikwambie ukweli. Hatuna mradi mkubwa wowote Ruvuma wala huko Mtwara. Miradi mikubwa na sisi tunaipenda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati mnafikiria kujenga Chuo Kikuu sijui cha IT Dodoma, niliwaza sana. Kwa nini hamkukipeleka Ruvuma? Dodoma kuna hii UDOM ambayo sasa hivi imekuwa kubwa na ina changamoto za kutosha. Kwa nini hiyo IT mnayosema chuo kikubwa kinajengwa hapa Dodoma kisijengwe hata kule kusini tukawa na sisi na mradi mkubwa? Miradi mikubwa nasema hata ya maji, hatuna, Ruvuma na Mtwara ni shida. Kwa hiyo hii ya vyuo, niwaombe sana msaidie kama ambavyo Mheshimiwa Mkapa alivyosaidia ile Muslim University ya pale Morogoro, walikuwa na changamoto ya majengo, akawasaidia akawapa majengo. Serikali ulizeni hivi vyuo, kwa nini hiki chuo cha udaktari pale Peramiho kimekufa? Kwa nini kile chuo kingine cha St. Joseph, Ruhuiko kinakufa na ninyi mpo? Hebu wasaidieni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hivyo vyuo vikuu, nirudi tena. Kila siku tunaongea hapa, Chuo cha UDOM ni Chuo Kikubwa Afrika Mashariki. Nenda pale, utashangaa. Yale majengo yanaporomoka, roof inaanza kudondoka, vigae chini vimepasuka, na mabomba ya maji yamepasuka. Nimekwenda pale nikaingia kwenye vyoo vya kule UDOM, yaani mpaka unaona aibu. Kuna mlipuko utatokea. Maji yanapotea pale kwa sababu mabomba yote yamepasuka. Wana upungufu wa maji karibu lita milioni 1.1, Serikali mpo. Sitaki Mheshimiwa Waziri tuongozane, nenda ukaone UDOM, hali ni mbaya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, halafu pale pale UDOM kuna jengo la Chimwaga. Ule ni ukumbusho mkubwa sana. Sasa tuangalie, Chimwaga tunaiacha hivi hivi? Tuliingia mle ndani wakati tunafanya lile kongamano, yaani unaingia mle ndani unafurahi. Ni ukumbi mkubwa mno, lakini angalia nje. Ynatakiwa ukarabati ufanyike, tena kwa kumuenzi Mwalimu Nyerere na kwa kuenzi Makao Makuu ya hapa Dodoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie kwa kuzungumzia shule kongwe. Kuna shule kongwe zimesahaulika kabisa. Kuna shule kongwe ambayo Mheshimiwa Mkapa amesoma huko, Marehemu Mheshimiwa Profesa Mbilinyi alisoma huko, inaitwa Shule ya Kigonsera, hakuna maktaba, you can’t imagine. Kuna form five, pale wapewe maktaba, na watoto wajifunze kujisomea, ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi nianze kwa kupongeza Wizara na hasa Waziri Gwajima na Naibu wake angalau tunaanza kusikia wizara wanasema inawaka waka, kuna amsha amsha ndani ya wizara, hata hivyo ni bado muendelee.

Mheshimiwa Spika, nitazungumzia hili suala sasa hivi limeota mizizi na hasa kwa wazazi ambao ni baba na walimu. Hawa walimu tuna wakabidhi watoto lakini sasa hivi limeibuka kweli hili wimbi walimu wakabidhiwa watoto ili wakawafundishe lakini imetokea walimu hao ndiyo wanawabaka watoto, walimu wana wabaka wanafunzi.

Mheshimiwa Spika, kuanzia mwezi wa tatu mpaka wa nne kuna kesi sita za walimu wanawabaka wanafunzi, sasa wazazi wanajiwaza hivi hao watoto tunawapeleka wapi? Ukienda makanisani shida, misikitini shida hata shuleni. Kwa hiyo, suala la wazazi na hasa baba, baba mzazi wa mtoto kujiusisha kumbaka mtoto mpaka anampa mimba hili suala limekuwa ni zito sasa nini nataka kusema hapo?

Mheshimiwa Spika, ifikie wakati sasa na ndiyo maana Waziri wa Katiba alijibu hapa ilifikie wakati kama alivyosema Mheshimiwa Mwantumu, suala hili la ubakaji na ulawiti hawa watu wasipewe kabisa dhamana, hawa watu wasipewe dhamana waendelee kukaa ndani hata kama hizo kesi zinakaa muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimpongeze sana Hakimu wa Kilolo aliyemfunga yule mwanamme aliye mbaka mtoto wa dada yake kifungo cha Maisha. Lakini kifungo cha maisha hakitoshi yule alitakiwa anapoingia gerezani atandikwe viboko kumi na mbili halafu ndiyo aingie huko lakini kule bado mwili wake haujajeruhiwa ndiyo maana tunasema hawa watu wapewe adhabu kali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niliwauliza baadhi ya Wabunge mistari kama mitatu hivi hapa nyuma nikasema hebu chagueni adhabu kati ya kunyongwa au kuasiwa? Wakasema afadhali kunyongwa sasa inamaana hao wanapenda sana waendelee kubaka au kulawiti. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, chakufanya hapa bora hawa wahasiwe ile wanayoikataa ndiyo tuiweke huko, wakihasiwa hili janga litapungua na wale wa sheria hao mnapoenda kujadili mmeniahidi kwamba mtaleta mswada. Tunaomba mlete muswada wa sheria kali, sisi tunaogopa nini? Mbona wenzetu wanawanyonga kabisa ni aibu, ni aibu sana maana yake tunalisema, tunalisema lakini watu wanaendelea tu, kila siku unapata hizi kesi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hilo nimelisema kwa uchungu na tuanze na hawa walimu wanao lawiti watoto. Hawa ndiyo wawe mfano kwenye hizi adhabu kali, ni mwalimu lakini kwa hilo nasema tuanze na walimu na baba wazazi wanaofanya hicho kitendo leteni huo mswada haraka sana ili turekebishe hayo mambo, dhamana isiwepo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, bahati mbaya sana wakitoka nje kama wamepewa dhamana wanaenda kushirikiana na ndugu hata wazazi wanakaa pamoja, kesi ile inafutika, tume ziwe zinaundwa kucheki…

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara, kuna taarifa, sijajua ni wapi?

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Spika, inatoka hapa kwa Mheshimiwa Ramadhan.

SPIKA: Ahaa jirani yako. Mheshimiwa, haya kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Ramadhan Ramadhan.

TAARIFA

MHE. RAMADHAN SULEIMAN. RAMADHAN: Mheshimiwa Spika, nataka nimpe taarifa kwa ruska yako mzungumzaji kabla ya mwaka 2018 Zanzibar kwenye Sheria yake ya Penal Code (Kanuni za Adhabu) makosa ambayo yalikuwa na dhamana yalikuwa matano tu.

Mheshimiwa Spika, baada ya 2018 tukafanya marekebisho ya sheria yakaongezwa kutoka matano mpaka kumi na moja kwenye Sheria za Mwenendo wa Adhabu (Criminal Procedure) za Zanzibar. Miongoni mwa makosa ambayo yaliwekwa yasiwe na dhamani ni makosa ambayo mchangiaji anayasema. Kwa kiasi kikubwa hii taarifa imsadie kwa kiasi kikubwa tumepunguza wimbi la makosa haya kwa sababu ya ukali wa washeria zetu zilizoko Zanzibar. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara, unapokea taarifa hiyo?

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, naipokea ahsante sana, ahsante sana Mheshimiwa Ramadhan. Sasa nilikuwa nasema kuna ndugu akienda kuambiwa huyo mtoto wako, tukae chini tulimalize hili wanakubali. Ndugu na wale watumishi na polisi wanaohusika katika kuhakikisha kwamba kesi hizi zinaishia huko mitaani nao waingizwe kwenye hiyo adhabu wafungwe maisha na wao wahasiwe pia tukifanya hivyo watajua hee sasa hivi hali mbaya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nije kwenye hili suala la elimu ya jamii, kwa kingereza wanaita sociology of education. Mambo yanayofundishwa au niseme haya mambo yanayaofundishwa kwenye sociology of education vyanzo vyake ili mtoto aelewe, apate hiyo elimu ya jamii, anaipata kwenye familia, anapata shuleni, anapata kwenye rika, anapata kwenye media, anapata kwenye NGO, anapata kwenye vyombo vya dini.

Mheshimiwa Spika, sasa hivi, vyombo hivi, hivi vyanzo hivi vikitoa elimu potofu au vikitoa elimu mbaya inamuathiri mtoto kwenye jamii wakitoa elimu nzuri inamsadia mtoto kwenye jamii.

Mheshimiwa Spika, sasa kwa sasa hivi, katika hivi nilivyovitaja hivi vyanzo, media ikitoa kitu kibaya mnasikia hata Bunge tunakemea. Lakini leo hii naomba niliseme kwa faida ya watoto wetu. Kuna wakati mwingine elimu inayotolewa kwenye hizi dini zetu ni elimu ya uongo tunasika, vyombo vya dola wapo, Wizara ya elimu ipo, maendeleo ya jamii wapo. Watu wanafundishwa kwamba mtu unaenda mbinguni unaoana na Mungu. Watu wanafundishwa kwenye madhehebu kwamba humu ndani kuna mtu alikufa sasa hivi amefufuka yuko kwenye hiki chumba, kwa nini polisi wasiende kumtoa huyo mtu aliyekufa kwenye hicho chumba? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa tunafundishwa vitu vya uongo watu wanavichukua na wakati mwingine mimi naona kama ni ujambazi na kupora fedha za watu. Suala hili tuliangalie; kutangaza elimu za uongo kwa kutumia madhehebu ya dini lazima Serikali tukae macho.

Mheshimiwa Spika, nasema hivi kwa sababu gani? haya yanayotokea nchi za jirani tukae chonjo, yanayotokea nchi za jirani yanaweza yakatokea hata Tanzania. Nasema tujipange, Wizara zinazohusika zihakikishe elimu zinazotolewa kwenye hivi vyanzo ziwe elimu za ukweli.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, naomba nimalize dakika mbili tu, please!

SPIKA: Dakika moja malizia.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, dakika moja. Niwaombe Wizara hebu angalieni sheria ya jamii inasemaje kuhusu watoto wadogo wanaoajiriwa majumbani. Inasemaje sheria? Wanapataje haki zao au wanastahili kweli kuajiriwa wakiwa watoto wadogo? Na sheria za wafanyakazi wa majumbani bado. Ongea na Wizara ya Kazi na Ajira, mjipange muone kwamba hakuna unyanyasaji kwa watoto wanaoajiriwa wakiwa wadogo.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Leo nitaanza kwa maeneo machache sana kwenye elimu kwa sababu mengi wameyafanya. Kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza sana Serikali ya Awamu ya Sita. Mambo mengi sana yanayohusu elimu hasa ya vyuo vikuu yametekelezwa lakini niseme tu machache. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaja kwako katika kuchangia, Mheshimiwa Waziri wa Elimu kuna mambo fulani inabidi umuone huyu Mheshimiwa Waziri wa Fedha. Kwanza niseme ukweli Waziri wa Fedha pamoja na msaidizi wake mmekuwa ni watu mnaoweza kufikika, hakuna ubaguzi ninyi ni kati ya wale Mawaziri ambao ni rahisi sana kufikika, nyie wenyewe mnajua jamani Waheshimiwa Wabunge, Wizara ya Fedha tumekuwa na Mawaziri ambao unaogopa hata kumkaribia lakini Mheshimiwa Dkt. Mwigulu nikupongeze kwa hilo na hasa kwa kujali makundi yote ya Wabunge wanafika kwako unawasikiliza. Wakati mwingine ndiyo hapa ndani lazima utibuliwe wewe ni Waziri wa Fedha lakini huna hasira, huna chuki wala huweki kinyongo. Endelea na hivyo and that is leadership. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niseme suala la mikopo nikuombe sana sana Waziri hivi vyuo vya kati vipewe mikopo ikiwemo vyuo vya maendeleo ya jamii. Nimeona wakati Waziri wa Elimu anajibu anasema ooh, vyuo vya kati sijui VETA na nini tunaangalia. Tukiaza hivyo lazima kutakuwa na malalamiko. Kama tumesema vyuo vya kati vipewe mikopo ni vyuo vyote vya kati ili isilete shida. Hawa watu wataleta shida tu, tutapata tena message mimi nimechaguliwa chuo cha kati sijapata mkopo. Kwa hiyo, hakikisha wewe ni mjanja tafuta fedha ili kama kuongeza muweze kuongeza ili fedha hizo hata hivi vyuo vya kati vyote vipate mikopo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije jingine naomba tu kukumbusha kwamba kwenye ile fedha ya HEET nimepata tetesi mnafanya allocation. Fedha za HEET ni kwa ajili ya universities. Mnafanya allocation sasa kama mnafanya hakikisheni kwamba hata Chuo cha Mwalimu Nyerere wanapata kwa sababu wana miundombinu ambayo inabidi waitengeneze lakini pia kuna branch yao kule Pemba. Kwa hiyo, kama mtafanya allocation kwenye HEET fanyeni allocation hiyo muhakikishe hiki chuo kinapata fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kwenye elimu, Waziri wa Elimu aliahidi kwamba mishahara ya Wakuu wa Vyuo itafanyiwa kazi, mpaka leo kimya. Nimuombe Mheshimiwa Mkenda aje aonane na Mheshimiwa Waziri wa Fedha, aonane na Mheshimiwa Simbachawene wa Utumishi mlimalize hili limechukua muda mrefu. Mkuu wa Chuo anapata mshahara sawa na lecturer wa kawaida, jamani inatoka wapi hiyo? Hebu tulimalize hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemaliza huko. Nakuja kwenye Wizara hii ya Maendeleo ya Jamii. Nashukuru kwamba walitengewa shilingi bilioni 40 Bajeti iliyopita, sasa hivi wana shilingi bilioni 71 ni vizuri ongezeko ni zuri lakini niseme bado ni kidogo mno. Hii Wizara ina madudu mengi mengi, maadili, ukatili wa kijinsia, ubakaji, ulawiti, vipigo, ukeketaji ambao unaendelea ingawa Waziri alisema eti amemfunga ngariba mmoja. Ngariba mmoja unamfunga halafu unakuja kutuambia hapa kwenye Bunge kweli? Wakati mangariba wako kibao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ulawiti unaendelea, ndoa za utototni. Kwa hiyo hii Wizara ina mambo mengi mengi. Nimuombe Waziri wa Fedha sasa nikuombe. Hizo fedha za kodi unazokusanya hizo naomba uzitenge nyingine kwa ajili ya ulinzi wa watoto. Hapa kuna fedha zinatengwa kwa ajili ya ulinzi hata sisi hapa tunalindwa, hakuna mtu anayeweza kuingia humu akatufanyia mambo yale mabaya lakini ulinzi wa watoto bado. Mheshimiwa Dkt. Mwigulu nakuomba halafu wewe unapenda sana watoto. Sijawahi kuona Mbunge yeyote au mwanaume yeyote wa Kitanzania anabeba mtoto mgongoni. Wewe unapenda watoto. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hili ulifanyie kazi. Kwenye hizo fedha unazokusanya za kodi hakikisha tunapata ulinzi wa watoto. Mpe fedha Mheshimiwa Masauni, mpe fedha Mheshimiwa Gwajima, mpe fedha Mheshimiwa Simbachawene, fanyeni kazi kwenye ulinzi wa watoto nimesema tafuteni dawa. Tafuteni dawa kwa wanaume wabakaji wote na walawiti na fedha hizo unaweza ukazipata. Tukifanya hivyo nakwambia mambo haya yatapungua tu. Nimeshasema mara nyingi hapa hivi mnaona tabu gani kuwa hasi hao? Na wao hawawezi kuwa hasi mpaka wewe utoe fedha ili hao Mawaziri wengine wenye hizi sekta waweze kusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisema jambo la ndoa za utotoni. Yaani mpaka wakati mwingine nashindwa kuelewa. Tunaomba Mheshimiwa Waziri wa Katiba alimhakikishia Mheshimiwa Spika ndani ya Bunge hili kwamba ataleta muswada hapa tukapitisha sheria. Sasa nasikia pembeni pembeni vinakuja vikundi mbalimbali eti ndoa za utotoni ziendelee. Nimesema mara nyingi jamani mtoto wa miaka 12 anaolewa anakwenda kufanya nini huko? Mbona hatuna uchungu na mabinti na haya mambo yote yanayohusu watoto wa kike, yanayohusu wanawake hayafanyiwi kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wangekuwa wanakeketwa wanaume ukeketaji ungeisha, wangekuwa wanaolewa wanaume wadogo, ndoa za utotoni zingeisha lakini mambo yanayohusu wanawake kwa nini Serikali hamtaki kuifanyia kazi? Watoto wana keketwa kila siku, Serikali mpo, vyombo vya dola vipo eti mnasema hamuwezi kujua wanafanya kwa siri, nchi hii tunashindwa kulikomesha hilo? Mbona la ualbino tulilikomesha kwa sababu gani la ualibino lilikwisha? Kwa sababu waliokuwa wanaathirika ni watu wenye ualbino wanaume na watu wenye ualbino wanawake na ndiyo maana lilipungua na likaisha. Leo hii kwa sababu wanaokeketwa ni wanawake Serikali mko wapi? Mheshimiwa Waziri wa Fedha toa fedha zikafanye kazi kwenye maeneo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatutaki hiyo ya ukeketaji wala hatutaki hiyo ya ndoa za utotoni. Mnatuletea hapa taratibu za ajabu eti watu wanasema sheria, sijui utamaduni. Mbunge gani hapa atatoa mtoto wake wa miaka 12 akaolewe? Nani atatoa mtoto wake wa miaka 10 akaolewe? Wanasema tu pembeni huko, wawalete watoto wao hapa ili wakaolewe kwa miaka hiyo 12. That is uncouth, inasikitisha. Wanawake tusimame ndani ya Bunge hili tukatae. Leta Muswada hapa tujadili msiufiche fiche huko kwa kusikiliza vikundi vya watu wachache. Tamaduni zilizopitwa na wakati ziondoke ili mwanamke huyu akombolewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nimekupa kazi na sisi tunasimamia Serikali kwa hiyo mimi nakusimamia leo Mheshimiwa Mwigulu toa fedha, utoe fedha za kuwatunza watoto. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nikushukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nianze kwa kuipongeza Wizara ikiongozwa na Dkt. Mabula na Mheshimiwa Ridhiwani. Pia niwapongeze watendaji waliopo kwenye hiyo Wizara Katibu Mkuu akiwa ndiye kiongozi. Sasa licha ya changamoto nyingi ambazo zimesemwa bado wanajitahidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitajikita sana kwenye vyuo hivi vinavyohusiana na ardhi. Tuna Chuo cha Ardhi Tabora, kuna hiki Chuo kikubwa cha Ardhi hapo Dar es Salaam, kuna Nelson Mandela, kuna chuo kinaitwa UDSM, hivi vyuo vyote vinajihusisha moja kwa moja na ardhi. Sasa niseme hivi Serikali, niliongea wakati fulani, hivi Serikali wanaonaje wavitumie hivi vyuo katika kufanya research na kazi zinazohusiana na ardhi ili kupunguza upungufu huu wa wafanyakazi. Hivi vyuo vipo hapo lakini havitumiwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilizungumza mwaka jana, ni kiongozi mmoja tu anaitwa Mheshimiwa Sagini wakati akiwa RAS, nami nikiwa RAS Tabora, alikuwa ndiyo anatumia kile Chuo cha Tabora kufanya kazi zake kule Simiyu. Leo hii mikoa ina changamoto nyingi lakini unakuta hivi vyuo hawavitumii; mpaka nikajiuliza au kuna kitu hawakiweki vizuri ndiyo maana hawawatumii hawa watu. Hebu watumie hawa wa Chuo cha Ardhi, MUST, Tabora, UDSM na Nelson Mandela, hasa katika maeneo ya IT kule Nelson. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije niseme jambo lingine, niiombe Wizara ya Ardhi, wasaidiane au washirikiane na Wizara ya Fedha, Wizara ya Elimu na Ofisi ya Waziri Mkuu, kuona namna gani wataongeza bajeti hasa katika hiki Chuo cha Ardhi kwenye research. Sasa kutokana na idadi ya wanafunzi waliopata mikopo kuwa wengi na lilikuwa ni jambo zuri sana, kwa hiyo fedha za research zikapungua sana, hivyo, unakuta hawa wanafunzi wa Chuo cha Ardhi wanakwenda kwenye research wanafanya research kwa wiki moja; hivi kuna research kweli ya wiki moja kwa mwanafunzi. Kinachotokea ni nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba unisikilize, kinachotokea unajua ni nini? Watoto wale wana-copy au wanagushi researches za kwenye mitandao, hawawezi kufanya research zilizokamilika; kwa hiyo, forgery inaanzia kwenye vyuo; ndiyo maana wakienda field kwenye halmashauri zetu, mahali panahitajika nondo 10, wanaandika nondo mbili. Forgery inaanzia chuoni, tumeshindwa kuwafanya hawa watoto wakafanya researches za uhakika kwa hiyo, wana-copy tunapata degree fake, halafu baadaye tunalaumu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sana, sasa tuangalie namna gani tunaweza kutumia mifuko katika kuongeza bajeti ya research kwa hao wanafunzi, hivihivi tunapoteana. Hao watu wathaminishaji, tunapata watu wa procurement, Engineers, sijui wengine wanawaita Valuers nasema wote hawa wanahitaji kufanya researches za kutosha. Sasa ardhi kuna hilo tatizo na naomba Mheshimiwa Waziri alichukue hilo. Vijana wanakwenda wanafanya research wiki moja kweli! Hili litatuangusha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo nije kwenye National Housing. National Housing Corporation wanafanya kazi vizuri sana, tulikagua hata wakati ule wamekwenda kufanya marekebisho kwenye sekondari, walijitahidi sana wakati tulilinganisha na lile Shirika lingine, walijitahidi sana. Hata hivyo, niseme, hizi nyumba za National Housing, mimi ni mdau nina nyumba pale Tabora, nikishuka pale nataka kuingia naangalia kushoto na kulia, nani ananiangalia naingia kwenye hii nyumba, yaani unaweza kusema ni magofu. Ukiangalia vijana wanaohusika kwenye National Housing hawafanani na hizo nyumba. Mheshimiwa Msechu, kuna kina Merkio, akina Deo, sijui akina Elias ni vijana ambao ukiwaangalia hawafanani na zile nyumba za National Housing.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa wakaangalie ni namna gani watazifanyia ukarabati na kazi hiyo wanaiweza akina Msechu, hebu wazibadilishe; tunataka wawe na uniqueness ya National Housing na wanaweza kufanya hivyo. Mandhari yake nyingine hapa zipo Iyumbu zinaitwa Satellite, waende wakaziangalie, tunataka zilete mandhari, zioneshe kabisa kwamba hizi nyumba zinasimamiwa na vijana wasomi na wanaoweza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, niende kwa wafanyakazi wa National Housing na hasa vibarua. Wananiambia vijana wale, wanafanya kazi, lakini Mkurugenzi akaangalie wakifanya kazi wapate malipo kwa wakati. Akifanya hivyo kila mtu atasema hivyo sasa kweli tumempata Msechu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nikushukuru sana. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nami nianze kwa kuwapongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu na Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii, hongereni sana kwa hotuba zenu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kwanza kabisa kwa sababu nachangia kwenye elimu, niwapongeze sana sana watumishi wote ambao wameonesha hamasa kubwa ya kusoma kujiendeleza na hasa Wabunge wengi ambao safari hii wameingia katika kujiendeleza, wasikatishwe tamaa na watu ambao mara nyingi wanakwenda kubeza wasomi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakwenda kwenye suala la mikopo. Suala la mikopo niipongeze sana Serikali imejitahidi kutoa mikopo lakini hasa kwa upande wa vyuo vya kati. Safari hii vyuo vya kati vinavyoingia kwenye yale madaraja sita wanafunzi wote wa Diploma watapata mikopo, hata hivyo, inaonyesha kabisa kwamba bado kuna kundi ambalo halitapata mikopo. Kwa mfano, wale wanaochukua Diploma za Utumishi na sehemu nyingine hawako kwenye hii list.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nitakuja kwa upande mwingine zaidi kwenye suala la mikopo, kama Serikali imejitahidi kutoa mikopo kwa maeneo haya sita ambayo ni afya na sayansi, elimu ya ualimu, usafiri na usafirishaji, uhandisi wa nishati, madini na sayansi ya ardhi, kilimo na mifugo ina maana Serikali hapo imejitahidi na hawa ndiyo watakaofanya kazi katika maeneo yetu ya kati, kwa kufanya hivyo tutapunguza ule upungufu wa wafanyakazi katika zahanati zetu, katika afya, maafisa wa maendeleo na watu wa manunuzi, hao wote wanaingia huko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niseme hizi fedha ingawa zimetolewa hazitoshi, kitu kingine kinachotufanya bado tukalalamika kwamba wanafunzi wetu wanahitaji mikopo hasa hawa wa kati ni kwa sababu wale waliopata mikopo hawalipi mikopo yao. Niombe sana Serikali sasa ijipange watu waliokopeshwa wamesoma, wamemaliza na wengine wapo kwenye ofisi, kwenye taasisi mbalimbali walipe ile mikopo ili hawa watoto wengine wote wapate mikopo, wakifanya hivyo hatutakuwa tena na makundi kwamba hili kundi ndiyo lipate mikopo, watoto wote watapata mikopo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wengine wako humu ndani, tumalize kulipa mikopo ili watoto wetu wote wapate mikopo. Tena kuna wengine marafiki zangu nawafahamu, sasa tukifanya hivi, mimi nawaambia tukifanya hivi hatutapata tena shida ya watoto kusema aah! Mimi sijui sina mkopo, diploma hii ipate mikopo, hii isipate mikopo kwa sababu wote watapata mikopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali na Bodi ya Mikopo ninawapongeza sana wameanza kampeni inaitwa “Fichua” hiyo kampeni inafichua wale wote wenye madeni hawataki kulipa mikopo. Kwa hiyo, usishangae utakapoona na mimi nipo kwenye hiyo Kamati ya fichua, mimi nina maeneo yangu na mimi nimepangiwa huko. Niwaombe tuwe wazalendo, tulipe madeni ili tusilalamike ili hawa watoto wetu wote wapate kusoma. Kama wewe umesomeshwa na hii mikopo kwa nini usiwalipie watoto na wengine wazazi wana uwezo walipieni vijana mikopo yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hivyo basi nije kwenye hizi taasisi mbili nitazungumzia. COSTECH pamoja na Elimu ya Watu Wazima. Tulitembelea pale COSTECH mimi nilishaangaa, wale watu wanafanya utafiti na ubunifu, kuna ubunifu unaoshangaza na unaofurahisha lakini COSTECH tatizo hawajitangazi wako pale. Tulikuta vijana wamebuni utengenezaji wa mbolea kiasi kwamba wakati mwingine unaweza ukasamehe hii mbolea ya Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Bashe. Wanatengeneza mbolea ya asili inafungwa kabisa safi, haina chumvi chumvi wala nini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa COSTECH nao wana tatizo moja, niombe Serikali iwasimamie COSTECH, kwanza waorodheshe wabunifu wote katika vyuo vyote. Namba mbili, wabunifu wote waliopo kwenye jamii, wako vijana huko wanabuni vitu vya ajabu vinavyofurahisha lakini wamekaa pale ukiwauliza naomba list ya wabunifu katika vyuo, hawana! Naomba list ya wabunifu mtaani, hawana! Wabunifu wapo ili hawa wabunifu waweze kuwekwa vizuri, wapewe mipango na hao wabunifu watawezakujitegemea vizuri zaidi kiuchumi. Kwa hiyo, hii COSTECH bado haijajitangaza lakini wajipange vizuri ili tujue hawa vijana huu ubunifu tumefikia kiasi gani. Siyo wanakuja tu kwenye maonesho pale uwanjani, wanatuonyesha ubunifu tunashangaa shangaa hatuelewi kinachoendelea, tunataka wale wabunifu waje wawe matajiri, ubunifu wao uwasaidie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye elimu ya watu wazima. Hiyo elimu ya watu wazima kwenye miaka ya 1980 mpaka 1990 sisi tukiwa tunakua tulikuwa tunaisikia elimu ya watu wazima, elimu ya watu wazima leo hii ni kama haipo. Elimu ya Watu Wazima nao wana tatizo, wajitangaze hawa kama walivyosema wenzangu. Kuna watoto wale ambao wengine wanaona aibu wale ambao walitoka walishindwa kuendelea na masomo Mheshimiwa Rais akasema waingie na wao wasome. Sasa kuna wengine wanajinyanyapaa wanasikia aibu kwenda kwenye haya madarasa ya kawaida, haya ya sekondari ya kawaida lakini Elimu ya Watu Wazima ina vituo inaweza ikawachukua wao, hapa nyuma ya VETA wapo wanafunzi wanaosoma elimu hii ya sekondari kupitia elimu ya watu wazima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Elimu ya Watu Wazima ijipange kila Mkoa ikusanye, isaidiane na sekondari za kawaida, wajipange wakusanye watoto waingie wasome. Kwa kufanya hivyo tutasaidia sana kupata idadi kabisa ya wanafunzi wetu walioko nje ya mfumo wa kawaida ambao wamerudi katika madarasa. Nimesema hivyo kwa sababu gani? Elimu ya Watu Wazima wajitangaze kwa nini?

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, muda umeisha?

MWENYEKITI: Muda umeisha Dkt. Thea.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipe dakika moja tu nimalizie.

MWENYEKITI: Mheshimiwa malizia kwa sekunde 30.

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, haya, hawa Elimu ya Watu Wazima wenzao walikuwa wanatangaza zamani, tulikuwa na Redio Tanzania tu lakini ilisikika, leo tuna social media kibao, Elimu ya Watu Wazima wajipange wafanye kazi yao tuwasikie. Ahsante sana. (Makofi)