Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Venant Daud Protas (34 total)

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri Nishati lakini nina swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, halmashauri ya Wilaya ya Uyui hasa Jimbo la Igalula tuko nyuma sana katika kuunganishiwa nishati ya umeme. Wakati wa kampeni Mheshimiwa Waziri alikuja tukazindua mradi mkubwa lakini mara baada ya kuondoka yule mkandarasi hakuendelea na kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kupeleka umeme kwenye kata zaidi ya sita zilizoko katika Jimbo la Igalula na vijiji vyake? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa umeme jazilizi katika vijiji vya kata ya Goeko Msasani, Igalula Stesheni na Kigwa Majengo Mapya?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Protas Venant wa Jimbo la Igalula, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyotangulia kujibu kwenye jibu la msingi kwamba vijiji vyote 46 vilivyobaki katika Jimbo la Igalula vitapatiwa umeme kuanzia mwezi Februari kwa miezi 18 kwenye mradi wa REA III mzunguko wa pili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali la pili ambalo nadhani ndilo la nyongeza alikuwa anasema kwamba mwaka jana Mheshimiwa Waziri alizindua mradi wa umeme jazilizi (Densification) awamu ya pili, Densification 2A.

Mheshimiwa Naibu Spika,Jimbo la Igalula, Mkoa wa Tabora ni mojawapo ya mikoa 9 inayonufaika na Densification 2A ambayo ilianza mwaka jana na tayari ilishazinduliwa kwa Mkoa wa Tabora. Mkandarasi anayefanya kazi katika Mkoa wa Tabora anayo Lot moja ambayo ina mikoa miwili; Tabora na Singida na atafanyakazi hiyo kwa shilingi bilioni 9.7. Tayari mobilization imeshaanza, ameshafanya survey katika Jimbo la Igalula na amekamilisha na tunatarajia muda wowote kufikia mwezi wa nne atakuwa tayari ameanza kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge kwamba amekuwa akifuatilia hata ofisini kuulizia Densification 2A itaanza lini kwenye Jimbo lake, tunamhakikishia kabla ya mwezi Aprili upelekaji wa umeme kwenye vitongoji vilivyoko katika Jimbo la Igalula utakuwa umeanza.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Matatizo ya Jimbo la Mbogwe yanafanana vile vile na matatizo ya Jimbo la Igalula. Tuna Mradi wa Ziwa Victoria katika Jimbo la Igalula, lakini mradi ule mpaka sasa hivi umesimama:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa kupeleka maji katika Kata za Goweko, Igalula, Kigwa na Nsololo ili wananchi waanze kutumia maji ya Ziwa Victoria? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mradi ambao tayari utekelezaji wake umeanza ni lazima ukamilike. Sisi Wizara ya Maji tunapoanza kazi ni lazima zikamilike. Kwa mradi huu ambao umesimama napenda nikutoe hofu Mheshimiwa Mbunge, tuonane baada ya hapa, lakini vile vile wiki ijayo tutaangalia fungu la kupeleka fedha ili pale kazi iliposimama, utekelezaji uendelee na tutahakikisha mradi huu unaisha ndani ya wakati ili maji yaweze kupatikana Igalula. (Makofi)
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba nitoe taarifa, katika Jimbo la Igalula kuna watoa huduma wamekwishafika baadhi ya maeneo ambayo wamekwishasainiana mikataba ikiwemo Maguliathi, Migongwa, Makoyesengi na Mbulumbulu lakini wameondoka mpaka sasa hivi hawajui nini hatima ya maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niulize maswali mawili ya nyongeza, Jimbo la Igalula ni miongoni mwa majimbo yenye changamoto kubwa ya mawasiliano na vijiji vingi vimekua, wananchi wana simu lakini hawana mawasiliano hasa katika Vijiji vya Songambele, Kawekapina, Nyauwanga na Simbozamalu. Sasa ni lini Serikali itaiwekea mpango wa kupelekea minara hasa vijiji hivi vilivyokuwa katika Jimbo la Igalula? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; tuna huduma ya mawasiliano katika kata alizozitoa katika jibu la msingi lakini, huduma hizi zimekuja miaka mingi iliyopita, sasa mitandao imekuwa ikisumbua na wananchi hawapati huduma. Je, ni lini Serikali itakwenda kwa watoa huduma kukagua kwa sababu idadi ya watu imekuwa kubwa, wananchi ikifika jioni haipatikani simu na huduma haipatikani. Serikali ina kauli gani kwa watoa huduma ili waweze kwenda kuipitia minara hii ili iweze kutoa huduma nzuri kwa wananchi? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Protas Daudi, Mbunge wa Igalula kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kwanza ameongelea kuhusu watoa huduma ambao wamefika na kuanza kufanya utafiti ili waweze kuweka minara. Kwanza naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi ambayo anaifanya kwa niaba ya wananchi wake wa Jimbo la Igalula. Mheshimiwa Mbunge alishafika katika ofisi zetu na akatuomba tuweze kuhakikisha kwamba mawasiliano katika Jimbo lake yanapatikana na ndio maana mpaka sasa amesema kwamba, kuna watoa huduma tayari wameshafika katika eneo lake. Hii ni kwa sababu, Serikali imeenda kutekeleza ombi la Mheshimiwa Mbunge. Pia tufahamu kwamba, mikataba tunayowapatia watoa huduma ni mikataba ambayo inachukua takribani miezi tisa katika utekelezaji wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kama ambavyo amesema hatua ya kwanza watoa huduma wanayoifanya, ni kwenda kupata ile lease agreement pale ambapo mnara unatakiwa kwenda kujengwa. Hatua ya pili mtoa huduma anatakiwa kwenda kutafuta aviation permit ili aweze kuruhusiwa kujenga mnara. Hatua ya tatu ni kwenda kutafuta environmental impact assessment permit ili aweze kuruhusiwa na ndugu zetu wa mazingira. Baada ya hapo ndipo sasa apate building permit.

Mheshimiwa Naibu Spika, hizi process zote ni sequential process ambazo hatua moja ikitokea ndio inatoa nafasi ya hatua ya pili kufanyika. Kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge baada ya kukamilika kwa huu mchakato mzima wa kupata hivi vibali, basi utekelezaji wa ujenzi wa minara hii katika Jimbo lake utatekelezwa bila kuwa na changamoto yoyote.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna suala la pili ambalo ameongelea kwamba, kuna minara ambayo ipo lakini haitoi huduma stahiki. Ni kweli kabisa tunatambua kwamba kuna minara mingine ambayo ilijengwa miaka ya nyuma ambapo population ya eneo husika ilikuwa kidogo, iliweza kuhudumia wananchi waliokuwepo kwa kipindi hicho, lakini kwa sababu wananchi wanaendelea kuongezeka maana yake sasa minara hii inaanza kuzidiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo tumeshaelekeza watoa huduma wetu waende kufanya tathmini, ili wajiridhishe tatizo halisi ni lipi, kwa sababu kuna matatizo mengine ambayo yatahitaji kufanya treating tu ya antenna. Mengine itabidi kuongeza capacity, tatizo lingine itabidi kuongeza nguvu ya transmitter na tatizo lingine ambalo litatufanya tukaongeze antenna zingine ili ziweze kuhudumia wananchi wa eneo husika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, haya yote ni lazima tathmini ifanyike kwa kina na kuna mengine ambayo yana budget implication, lakini kuna mengine ambayo ni matatizo ya kiufundi peke yake, tayari watoa huduma tumeshawaelekeza na tayari wameshaanza kufanya tathmini katika maeneo yote nchini ili kujiridhisha kwamba tatizo linalolalamikiwa linahusiana na nini hasa. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante; pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, barabara hii ambayo inatoka Wilaya ya Igunga kuja Loya mpaka Magulyati ni barabara muhimu kwenye uchumi wa wananchi wa Jimbo la Igalula, lakini barabara hii ina mito zaidi ya tisa, kwa tafiti ya mkandarasi inasema kila mto mmoja kwa kujenga box culvert inagharimu takribani shilingi milioni 100. Leo Waziri ananiambia ametenga milioni 200 maana ma-box culvert mawili tu hela itakuwa imekwisha.

Je, Serikali haioni haja ya kuitilia kipaumbele kuiongezea fedha hii barabara ili wananchi waweze kupita masaa yote? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili, barabara hii ina vigezo na imekidhi vigezo vya kupandishwa hadhi ihudumiwe na TANROADS kwa sababu inaunganisha Wilaya mbili ya Igunga na Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, lakini vilevile inaunganisha na Mkoa wa Tabora na Singida. Kwa nini Serikali isipitie mchakato kuipandisha hadhi iweze kuhudumiwa na TANROADS ili kuepuka bajeti ndogo ya TARURA? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Venant Daudi Protas, Mbunge wa Igalula kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba barabara hii ni muhimu sana kwa uchumi wa wananchi wa Igalula na barabara hii imepitiwa na mito mingi na kama ambavyo nimeongea kwenye jibu langu la msingi, Serikali imetenga zaidi ya shilingi milioni 600 katika mwaka wa fedha 2021 tunaomaliza lakini katika mwaka wa fedha unaokuja. Jumla ya shilingi milioni 600 kwa ajili ya kutambua umuhimu wa barabara hii.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie pamoja na ma-culvert ambayo tumeendelea kujenga lakini tathmini itafanyika katika maeneo mengine yote ya barabara ile ambayo yanahitaji kujengewa ma-culvert lakini pia na madaraja ili fedha iweze kutafutwa na iweze kutengwa kwa ajili ya kujenga madaraja hayo kwa awamu.

Mheshimiwa Spika, barabara zote ambazo zinahitaji kupandishwa hadhi kwenda kuwa barabara za TANROADS utaratibu upo wazi unaanza katika ngazi ya Halmashauri husika DCC tunakwenda RCC na baadae unawasilishwa katika Wizara za TAMISEMI na Ujenzi.

Kwa hiyo, naomba nimshauri Mheshimiwa Mbunge kwamba wafuate utaratibu huo ili tuweze kuona kama inakidhi vigezo iweze kupata hadhi inayotakiwa, nashukuru sana.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri lakini nilitaka kuongeza kwenye majibu yake kwa mara ya kwanza Serikali imesikia kilio cha Waheshimiwa Wabunge kwa sababu fedha za TARURA zilikuwa zinatoka katika Mfuko wa Barabara, kwa mara ya kwanza tumepata fedha shilingi bilioni 172 kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu fedha hizi tumezipata haraka haraka na bajeti zilishapitishwa na Kamati za Halmashauri, kwa hiyo tumetumia maamuzi ya jumla kila Jimbo tunapeleka shilingi milioni 500 TARURA kwa ajili ya ujenzi wa barabara. (Makofi)

Kwa hiyo, Halmashauri au Waheshimiwa Wabunge mtaamua milioni 500 kujenga kilometa moja ya barabara ya lami au milioni hiyo 500 kujenga kilometa 10 kupandisha barabara ya udongo kuwa ya changarawe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tumeiweka hii chini ya uamuzi wa Mabaraza ya Madiwani kuamua milioni hii 500 kwa kila Jimbo sio kwa kila Halmashauri. Kwa hiyo, kama Halmashauri ina Majimbo matatu kila Halmashauri itapata milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa barabara. Na hii ndiyo kazi ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amesikia kilio chenu Waheshimiwa Wabunge na Waziri wa Fedha ananiambia bado wanaangaliaangalia kwa hiyo mambo yanaweza yakawa mazuri zaidi. (Makofi)
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante; pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, barabara hii ambayo inatoka Wilaya ya Igunga kuja Loya mpaka Magulyati ni barabara muhimu kwenye uchumi wa wananchi wa Jimbo la Igalula, lakini barabara hii ina mito zaidi ya tisa, kwa tafiti ya mkandarasi inasema kila mto mmoja kwa kujenga box culvert inagharimu takribani shilingi milioni 100. Leo Waziri ananiambia ametenga milioni 200 maana ma-box culvert mawili tu hela itakuwa imekwisha.

Je, Serikali haioni haja ya kuitilia kipaumbele kuiongezea fedha hii barabara ili wananchi waweze kupita masaa yote? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili, barabara hii ina vigezo na imekidhi vigezo vya kupandishwa hadhi ihudumiwe na TANROADS kwa sababu inaunganisha Wilaya mbili ya Igunga na Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, lakini vilevile inaunganisha na Mkoa wa Tabora na Singida. Kwa nini Serikali isipitie mchakato kuipandisha hadhi iweze kuhudumiwa na TANROADS ili kuepuka bajeti ndogo ya TARURA? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Venant Daudi Protas, Mbunge wa Igalula kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba barabara hii ni muhimu sana kwa uchumi wa wananchi wa Igalula na barabara hii imepitiwa na mito mingi na kama ambavyo nimeongea kwenye jibu langu la msingi, Serikali imetenga zaidi ya shilingi milioni 600 katika mwaka wa fedha 2021 tunaomaliza lakini katika mwaka wa fedha unaokuja. Jumla ya shilingi milioni 600 kwa ajili ya kutambua umuhimu wa barabara hii.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie pamoja na ma-culvert ambayo tumeendelea kujenga lakini tathmini itafanyika katika maeneo mengine yote ya barabara ile ambayo yanahitaji kujengewa ma-culvert lakini pia na madaraja ili fedha iweze kutafutwa na iweze kutengwa kwa ajili ya kujenga madaraja hayo kwa awamu.

Mheshimiwa Spika, barabara zote ambazo zinahitaji kupandishwa hadhi kwenda kuwa barabara za TANROADS utaratibu upo wazi unaanza katika ngazi ya Halmashauri husika DCC tunakwenda RCC na baadae unawasilishwa katika Wizara za TAMISEMI na Ujenzi.

Kwa hiyo, naomba nimshauri Mheshimiwa Mbunge kwamba wafuate utaratibu huo ili tuweze kuona kama inakidhi vigezo iweze kupata hadhi inayotakiwa, nashukuru sana.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Serikali ulikuwa wananchi wa Kata za Goweko, Kigwa, Nsololo na Igalula kupata maji Desemba, 2021 lakini majibu ya Serikali yamekwenda tena Juni, 2022. Lakini utekelezaji wake mpaka sasa hivi umefikia asilimia 10.

Je, Serikali haioni kuusogeza karibu mradi huu uweze kutekelezeka kwa kasi ili wananchi wa kata hizo waweze kupata maji? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Jimbo la Igalula lina changamoto sana ya upatikanaji wa maji, ndiyo maana tunaelekeza Serikali iwekeze katika uchimbaji wa mabwawa. Niiombe Serikali haioni haja ya uharakishaji wa haraka wa usanifu wa uchimbaji wa mabwawa hasa hili Bwawa la Kizengi? (Makofi)
WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Igalula kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya. Ni Mbunge mfuatiliaji, mpambanaji hususan katika suala zima la wananchi wake waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa miradi ya maji unategemeana na fedha. Nitoe shukrani kwa Bunge lako tukufu kwa kutuidhinishia fedha zaidi ya bilioni 680 lakini Mheshimiwa Rais naye ametupatia fedha ya nyongeza zaidi ya bilioni 207. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge maeneo ambayo tutayapa kipaumbele na kuyapa fedha za kutosha ili kukamilisha mradi ule ni eneo la mradi huu wa Igalula kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na wananchi wake wanapata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Wizara yetu ya maji tumeboresha Kitengo chetu cha Uchimbaji wa Mabwawa. Tunaona kabisa yapo maeneo ambayo hayana fursa ya uchimbaji wa visima. Tunataka maji ya mvua isiwe laana, tunataka tuyavune kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa ili Watanzania waweze kunufaika na uvunaji wa maji ya mvua waweze kupata huduma ya maji.

Kwa hiyo, mkakati uliokuwepo tunakwenda kununua seti ya ujenzi wa mabwawa kwa maana ya vitendea kazi ili kazi hii ianze na Watanzania waweze kunufaika na ujenzi wa mabwawa. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nataka niulize maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na miongozo yote ambayo ameitoa hapa swali langu lilikuwa ni ahadi ya Viongozi Wakuu, hayati Dkt. Benjamini Mkapa, Rais wa Awamu ya Tatu ambaye alikuja katika jimbo la Igalula, Kata ya Igalula mwaka 2002 na akatangaza Tarafa ya Kizenji ambapo ilikuwa na Kata Kizengi, Tula na Loya. Tulisimama kufuata miongozo hii kwa sababu Rais alikuwa kashatamka. Sasa, je kama Serikali wana utaratibu gani wa kufuatilia kauli za Rais na kuzifanyia kazi ili tusiweze kuleta mikanganyiko ya kuwa tunaomba mara mbili mbili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Jimbo la Igalula pamoja na mambo mengine ni kubwa sana na jiografia yake ni kubwa sana. Je, ni nini mkakati wa Serikali kutoa utaratibu wa kuanzisha na kutoa maagizo ya kuanzisha maeneo ya utawala mengine, maombi mapya ili tuweze kuleta hasa maombi ya halmashauri?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MITAA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa David Protas Venant, Mbunge wa Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba halmashauri ya Igalula kwa maana ya Jimbo la Igalula linahitaji kupata Tarafa ya Kizenga, lakini pamoja na maelezo ya Mheshimiwa Mbunge kwamba ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais, Serikali inatekeleza ahadi za viongozi wa kitaifa kwa utaratibu na kwa wakati, lakini kuna miongozo ambayo ni muhimu iweze kufuatwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na ahadi ya Mheshimiwa Rais ambayo Serikali inaitambua na tutaifanyia kazi, lakini watendaji wameelekezwa kufuata mwongozo kwa maana kuanzishwa vikao ngazi ya vijiji, kata, wilaya na mkoa ili sasa wawasilishe maombi hayo Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa kadri ya mwongozo na maamuzi yaweze kufanyika. Kwa hiyo, naomba kumhakikishia Mheshimiwa kwamba wakiwasilisha mambo hayo mamlaka husika itafanya tathmini na kufanya maamuzi kama tunaweza kuanzisha tarafa hiyo au viginevyo na taarifa rasmi zitapelekwa katika wilaya hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili; utaratibu huu wa kuanzisha maeneo mapya ya utawala kama nilivyotangulia kujibu kwenye swali la msingi, unaongozwa kwa miongozo ambayo ipo rasmi. Kwa hiyo kama kuna uhitaji wowote wa kuanzisha halmashauri mpya ni lazima tufuate miongozo ile. Kwa hivyo nimpe rai Mheshimiwa Mbunge na viongozi wa halmashauri husika wakafanye utaratibu wa vikao hivyo na kuleta maombi yao level ya Wizara. Ahsante.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto la Jimbo la Sengerema ni sawa sawa na Jimbo la Igalula.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Igalula hatuna shule ya kidato cha tano na sita, lakini baada ya kutambua hayo wadau na wanachi tumeweza kujikongoja na tumepata mabweni na miundombinu salama ya kuweza kupokea wanafunzi wa kidato cha tano na sita.

Je, lini Serikali itaitambua shule ya Sekondari ya Tula ili iweze kupokea wanafunzi wa kidato cha tano na sita ili kupunguza uhaba wa shule katika nchi hii?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MITAA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Venant Mbunge wa Jimbo la Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika swali la msingi kwamba katika maeneo yale ambayo yanahitajika kuanzishwa kidato cha tano na cha sita ni lazima halmashauri husika kupitia Ofisi za Elimu pamoja na watu wa Udhibiti Ubora wanakwenda katika eneo husika wanakagua ile shule, wanatuletea hayo mapendekezo tunaona kama ina meet vile vigezo.

Kwa hiyo, kama inafikisha vile vigezo basi sisi tutakuwa tayari kuongeza fedha na baadhi ya miundombinu ili kuhakikisha tunaisajili na kupokea. Kwa hiyo, na yeye Mheshimiwa Mbunge ni kwamba tutawaagiza watu katika halmashauri yake watatuletea hiyo taarifa na baada ya hiyo taarifa maana yake tutaleta majibu ya msingi kama inakidhi kupandishwa au itasubiri katika mwaka mwingine wa fedha. Ahsante sana.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza mimi nimpongeza Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri na tunakiri kabisa kwamba wameleta fedha.

Nina maswali mawili ya nyongeza; la kwanza, mwaka 2017 Mheshimiwa Waziri Mkuu alikuja katika Kata ya Goweko, Kijiji cha Imalakaseko kulikuwa na wodi ambayo walianzisha wananchi, aliahidi ataleta shilingi milioni 80 tangu mwaka 2017 mpaka leo hazijafika? Lakini vilevile aliyekuwa Waziri wa TAMISEMI Selemani Jaffo mwaka 2019 alikuja katika Kata ya Igalula wodi ipo pale wananchi walianzisha aliahidi ataleta fedha mpaka leo, halikadhalika na kata zingine.

Mheshimiwa Spika, nataka nijue nini kauli ya Serikali kulinda ahadi za viongozi endapo wanatoa ahadi na hazitekelezeki kwa wakati?

Swali langu la pili ni mkakati gani Serikali sasa itatoa kumaliza maboma yote ili kuwatia nguvu na moyo wananchi ambao wamejitoa kuisaidia Serikali? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Daud Protas Venant, Mbunge wa Jimbo la Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kauli ya Serikali ni kwamba ahadi zote za Viongozi wetu wa Kitaifa ni lazima zitatekelezwa na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi hii ya milioni 80 ya Mheshimiwa Waziri Mkuu tutapeleka fedha hizi kabla ya mwisho wa mwaka wa fedha 2021/2022. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu na suala la mkakati wa umaliziwaji wa maboma katika jibu langu la msingi nimeeleza namna ambavyo Serikali kwanza imepeleka fedha nyingi kwenye maboma, lakini kuyatambua maboma yote zaidi ya 1700. Lakini tatu tunatafuta fedha na kupeleka kwa awamu kwa ajili ya kukamilisha maboma hayo.

Mheshimiwa spika, kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote kwamba mkakati wa Serikali uko thabiti na tutaendelea kuyakamilisha maboma hayo kupitia mapato ya ndani na mapato ya Serikali Kuu. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kumekuwa na changamoto ya katikakatika ya umeme katika Jimbo la Igalula lakini ukiuliza, unaambiwa changamoto hiyo inasababishwa na kusafiri kwa umbali mrefu wa nishati hii ya umeme: Je, Serikali haioni haja ya kujenga vituo vya kupoozea umeme katika Kata ya Kigwa na Kizengi ili kupunguza adha ya kusafiri umeme na kupunguza changamoto ya katikakatika hii ya umeme?

Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant, Mbunge wa Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika huu mpango wa grid stabilization project kwa mwaka huu wa fedha, Tabora inavyo vituo viwili vya kupooza umeme ambacho kitajengwa pale Uhuru katika Wilaya ya Urambo na kingine kitajengwa Ipole katika Wilaya ya Sikonge. Kwa Mheshimiwa Venant kule Igalula nitaenda kuangalia kwenye mpango wetu wa ujenzi wa vituo vya kupooza umeme katika wilaya zenye mahitaji na nitamfahamisha ni lini Serikali imejipanga kukijenga katika eneo lake. (Makofi)
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Ni kweli majengo yameshaanza kujengwa katika kituo cha Itobo pamoja na kuendeleza; Serikali imekuwa ikipeleka fedha na kujenga majengo nusu baadhi ya vituo, kikiwemo Kituo cha Igalula, jengo la OPD halijajengwa, Kituo cha Lutete majengo hayajakamilika: -

Je, nini mikakati ya Serikali kupeleka fedha kumalizia vituo vya afya vyote ili wananchi waendelee kupata huduma? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikijenga vituo vya afya kwa awamu kwa kupeleka fedha awamu ya kwanza kujenga majengo ya awali na awamu ya pili kumalizia majengo yaliyobaki.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge, kuna baadhi ya vituo vya afya vimepata awamu ya kwanza Shilingi milioni 250, vitapelekewa awamu ya pili Shilingi milioni 250 kutimiza Shilingi milioni 500. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba vituo vya afya ambavyo bado havijakamilishwa, fedha itapelekwa awamu ya pili ili kukamilisha majengo yale na vituo vianze kutoa huduma kwa wananchi. Ahsante sana.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Serikali ambayo yatakwenda kuzua mgogoro mwingine; katika vijiji alivyovitaja hapo ni kijiji kimoja tu ambacho kipo kwenye Jimbo la Igalula. Kuna Kamati ya Mawaziri nane ilikuja kule na ikatoa maelekezo kuwa itaenda kugawa maeneo katika maeneo haya, lakini katika jibu lake wanasema hawaoni haja.

Je, Serikali haioni sasa kuweka kauli inayoeleweka kwa wananchi ili waweze kutoa mkanganyiko ambao unajitokeza?

Swali la pili, Jimbo la Igalula limezungukwa na vijiji vingi vyenye mgogoro kama huu hasa katika Kata ya Miswaki, Loya, Igudi, Mwamabondo na vijiji vingine. Je, Serikali haioni haja ya kwenda kupitia mipaka upya ili kila mwananchi ajue ni wapi anaishia na hifadhi inaishia wapi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu kauli ya Serikali iweke kauli sahihi kuhusiana na vijiji vilivyotajwa; kuna mapori matatu yapo ndani katika Jimbo la Igalula, kuna Pori la Iwembele, Uyui, Kigwa, Lubuga, kuna Nyahua.

Mheshimiwa Spika, swali la Mheshimiwa Mbunge la msingi halikuhainisha ni vijiji gani hasa ambavyo analenga. Lakini nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba eneo la Igalula kwa maana ya Jimbo la Igalula kuna vijiji ambavyo vinaenda kunufaika na Kamati hii ya Mawaziri nane, kuna kijiji cha Miswaki, Igudi, Mwamdalaigwe, Loya na Mwamabondo, vijiji hivi vinatoka katika Jimbo la Igalula na vitaenda kunufaika na kumegewa kwa maamuzi ya Kamati ya Mawaziri nane.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuonesha mipaka, niwatoe wasiwasi Wabunge pamoja na Mbunge aliyeuliza swali kwamba kwa utaratibu tulionao sasa ni kuhakikisha kwamba yale mapori mapya ambayo tutayapa GN mpya tutaweza kushirikisha wananchi namna ya kutambua mipaka mipya na yale ambayo yatatangazwa na Serikali kwamba haya sasa ni mapori halali basi wananchi watafahamu mipaka yao ili iwe rahisi kutoingiliana tena na kuanzisha migogoro mipya.

SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Ardhi.

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa namna alivyojibu swali la Mheshimiwa.

Mheshimiwa Spika, labda nijibu kwa ujumla kulingana na changamoto iliyokuwepo katika maeneo ambayo Mheshimiwa Rais ameridhia kati ya vijiji 975, vijiji 920 wamekubaliwa kubaki kwenye maeneo yao. Kitakachofanyika ili kuondoa hizi changamoto ni ushirikishaji wa wananchi katika maeneo watashirikishwa wote na wataalam wote watakuwepo na katika maeneo ambayo tumekwishapita tayari wapo ili kuweza kubaini mipaka kwa pamoja. Na hii inafanyika hivyo ili baadae kusijekutokea lawama pengine kwamba hawakushirikishwa katika kubainisha mipaka mipya.

Kwa hiyo, tunaimani maeneo ambayo Mheshimiwa Rais ameridhia na ameongeza hata pale ambapo alikuwa amesema kwamba wangeishia, imewapa pia fursa ya kuwa na maeneo ya akiba ya wao pia kuweza kuyawekea mpango wa matumizi ambao Serikali itafanya kwa kushirikiana na wao ili basi wasiendelee kuwa na ugomvi na hifadhi ambazo ziko zimetengwa kwa kazi maalum.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Wananchi wa Kata ya Tula na Goweko wameanza ujenzi wa vituo vya afya. Ni lini Serikali itapeleka fedha kuungana na wananchi kumalizia vituo hivyo?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tutafanya tathimini ya kuangalia kiwango cha ujenzi uliofikiwa ili kuona kiasi cha fedha ambazo zinahitajika kumalizia ujenzi wa kituo hicho, na gharama zitakapojulikana zitajumuishwa kwenye mapango wetu wa umaliziaji wa vituo vya polisi vikiwemo hivyo vya Goweko na Igalula.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante, Kituo cha Afya cha Igalula katika bajeti tulikitengea milioni 450 na tumekwisha pokea milioni 450 lakini cha ajabu TAMISEMI mmeleta barua ya kugawa zile fedha kwenye vituo vitatu.

Je, kwa nini Serikali isione haja ya kukimaliza kabisa Kituo cha Afya cha Igalula katika vifaa tiba na kiendelee kutoa huduma stahiki? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant David Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inapopeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya kwanza dhamira ya kwanza ni kuhakikisha kwamba vituo vile vinakamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi mara moja.

Naomba sasa niichukue hoja ya Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imepeleka shilingi milioni 450 lakini kuna maelekezo ya kuzigawa fedha hizo katika vituo vitatu, nikitoka hapa nikaa na Mheshimiwa Mbunge lakini nifuatilie kuona sababu za msingi za kufanya hivyo na kama hakuna sababu tutakubaliana tukamilishe Kituo cha Afya cha Igalula na hatimaye tuendelee na vituo vingine kwa mujibu wa utaratibu, ahsante. (Makofi)
MHE. DAUD P. VENANT: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri yametia moyo kwa wana Igalula. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwanza, tulishafanya mchakato mara kwanza tukapitia mchakato wote kama alivyoutaja, tulivyofika kwenye hatua ya mwisho kwenye kikao cha RCC, walisema mchakato huo bado. Lakini sasa unavyosema tumepita kwenye mchakato huo huo na tayari document zimetayarishwa kwa ajili ya vikao hivyo, sasa Serikali kupitia kwako Waziri hauoni haja ya kutoa maelekezo kwenye RCC wao sio hatua ya mwisho kutoa maamuzi waziachie document zije Wizara ili ziendelee na machakato mwingine?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, ni kubwa sana na jiografia yake ni kila unapokwenda unaikuta Uyui. Sasa hamuoni kama Serikali kutoa maelekezo ya kina kwa zile halmashauri ambazo ni zenye competition ili kuweza kuzigawa ili kurahisisha huduma bora kwa wananchi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Daud Protas Venant, Mbunge wa Jimbo la Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema katika swali lake, kwamba walifanya mchakato wa awali, lakini kwa namna moja ama nyingine haukukidhi vigezo lakini wamefanya mchakato wa pili ambao uko ngazi ya mkoa, kwa maana ya kufanya RCC. Sasa tunaelekeza, Mkoa wa Tabora kutekeleza wajibu wao kutimiza sheria hii, kwa maana ya kufanya vikao vya RCC, ili kupitia maombi hayo na baadaye kuwasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kwa kadri ya mwongozo.

Mheshimiwa Spika, lakini pili, kuhusiana na maelekezo ya kugawa halmashauri hii kwa sababu ni kubwa itakuja kulingana na tathmini ambayo itafanyika baada ya RCC kuwasilisha maombi hayo ofisi ya Rais TAMISEMI. Ahsante.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kumekuwa na mrundikano sana wa abiria katika stesheni ya Tabora Mjini na Stesheni zinazofuata za Goweko, Tula na Malongwe wakienda pale wanakosa tiketi au tatizo la mfumo. Je, Serikali haioni haja ya kuongeza mabehewa ili wananchi wanapokwenda kupata huduma hiyo waweze kupata huduma na seat ili waweze kusafiri?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kumekuwa na changamoto ya mfumo wakienda pale mfumo ukiwa chini hawawezi kupata tiketi na wakipanda kwenye treni wanapigwa faini asilimia 100. Je, Serikali haioni haja ya kuboresha hii mifumo ili abiria akienda pale asipate usumbufu wa kupata tiketi?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Igagula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia masuala haya ya mifumo pamoja na Wabunge wote wa Mkoa wa Tabora. Hata hivyo ameomba suala zima la kuongezewa mabehewa ili kuweza kuwa na route nyingi katika kusafirisha wananchi ama abiria kutoka Tabora mpaka Dar es Salaam, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan tayari alishatoa idhini na tulishasaini mkataba wa ununuzi wa mabehewa mengine mapya 22 yenye thamani ya Dola za Kimarekani Milioni 14, lakini pamoja na hilo tutakarabati behewa 37 ili kuongeza safari za kutoka Tabora kuja Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, anasema changamoto za mfumo; ni kweli wakati mwingine kunakuwa kuna changamoto za mfumo kwa sababu ya internet. Nilishatoa maelekezo kwa uongozi wa TRC kwamba sasa wafikiri nje ya mfumo huu ili watumie mfumo unaoitwa USSD kwa maana ni Unstructured Supplementary Service Data ili kuweza kupatikana mfumo wakati wote, lakini hata hivyo mfumo tulionao unaruhusu kufanyakazi kwa njia ya offline mode.

Mheshimiwa Spika, nitoe maelekezo na maagizo kwa Ma- TT pamoja na wote wanaohusika na masuala ya booking clerk kwamba wahakikishe tiketi zinapatikana hata kama mfumo haupatikani kwa sababu unaruhusu mfumo wa offline mode.

Mheshimiwa Spika, ahsante.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, Serikali haioni haja ya kuondoa matumizi ya Kitambulisho cha Taifa wakati Serikali haijajipanga kuwapa wananchi wake vitambulisho na kuondoa usumbufu unaowapata wananchi wake?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant Daud kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hoja anayojaribu kuihoji inatokana tu na changamoto tulizozipata. Jambo linalotia faraja ni kwamba katika bajeti hii tunayoendelea kuitekeleza, Serikali imeweza kutoa fedha zote zaidi ya Bilioni 40 zilizokuwa zinahitajika ili kumlipa Mkandarasi na hatimaye aweze kuzalisha vitambulisho.

Mheshimiwa Spika, nimpe assurance Mheshimiwa Mbunge kwamba mara vitambulisho vitakapozalishwa Watanzania wote ambao walikuwa wako kwenye backlog hawajapata vitambulisho watapata vitambulisho vyao. Ninakushukuru.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Uchache wa mawakala ulileta usumbufu wa upatikanaji wa mbolea kwa msimu uliopita. Je, Serikali haioni haja ya kupeleka mawakala angalau kwa kila kijiji ili wasiendelee na usumbufu walioupata wakulima kwa msimu uliopita? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya changamoto ambazo pia tulizibaini wakati wa msimu uliopita ilikuwa ni hiyo ya uchache wa mawakala. Tumeshatoa maelekezo kupitia TFRA kuongeza idadi ya usajili wa Mawakala ili wakulima wapate mbolea katika maeneo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, tumeamua kuyatumia maghala yote makubwa ya Serikali kwa ajili ya uhifadhi na kupeleka mbolea karibu na wakulima; na tatu, tumeruhusu Vyama vya Ushirika pia kuwa sehemu ya Mawakala ili kufanya huduma hii ifike kwa ukaribu zaidi kwa wakulima.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Timu ya Mawaziri Nane ilikuja katika Kata ya Kigwa na kutuahidi kutupa eneo katika Kigwa Rubuga. Je, ni lini Serikali itaweka mipaka mipya katika maeneo hayo ili wananchi wajue mipaka yao?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika,
ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tulikuwa na kazi ya kufanya tathmini, kamati hii iliandaliwa na Kamati ya Mawaziri Nane na tayari wengi wameshamaliza kazi yake. Kazi inayofanyika sasa hivi ni kuainisha mipaka na kuweka vigingi. Hivyo, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Igalula kwamba wakati wowote tutaendelea kufanya kazi ya kuweka vigingi.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Kawekapina, Ipululu na Vumilia Kata ya Igalula wanacheleweshewa kupata umeme kwa sababu ya mgogoro wa TANESCO, TRC na REA: -

Je, ni lini mtaumaliza mgogoro huu wa kuvusha nyaya kwenda kwenye vijiji hivyo ili wananchi wapate umeme kwa wakati?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant, Mbunge wa Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, TANESCO na REA wako tayari na wanayo fedha kwa ajili ya kuvusha umeme kwenye line ya SGR lakini wenzetu wa Wizara ya Uchukuzi walikuwa hawajajua eneo gani watuoneshe kwa ajili ya kupitisha njia na sisi tusingependa tutumie pesa nyingi kupisha eneo temporary halafu baadae kidogo tuhamishie kwingine. Tumekaa pamoja na wenzetu wa TRC watatuonesha sehemu ambayo ni ya kudumu tutakayopitisha miundo mbinu hiyo ili wananchi waweze kupata umeme katika maeneo hayo. Kwa hiyo nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba tunalifatilia na tutalikamilisha kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma.
MHE. DAUD P. VENANT: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza nipongeze Serikali kwa majibu mazuri. Wilaya ya Uyuwi ina upungufu ya watumishi zaidi ya 2,000 lakini pamoja na upungufu huo Serikali imebadilisha utaratibu wa watumishi hasa walimu na madaktari kuwa wakandarasi. Yuko darasani anaambiwa huku mfuko wa simenti umepotea huku anatibu anaambiwa vibarua hawajalipwa.

Je, Serikali haioni haja ya kubadilisha mfumo ili hawa ambao tunao pamoja na upungufu wao wafanye kazi kikamilifu?

Swali la pili, Jimbo la Igaula hatukuwa na shule ya five na six, nashukuru Serikali imetuletea, lakini shule ile ina mchepuo wa sayansi hatuna walimu wa sayansi.

Je, kwenye ajira hizi hauoni unipe upendeleo maalum kwenye ile shule ili iweze kufanya vizuri kwa sababu imeshaanza kufundisha?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa
Spika, swali lake la kwanza hili la nyongeza analo sema kwamba walimu sasa au watumishi kwa ujumla wamegeuka kuwa wakandarasi na kuacha kufanya kazi zao; naomba nimkumbushe Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine humu ndani, kwamba wale wakuu wa shule na walimu wakuu ni nafasi za madaraka. Hivyo wao ndio accounting officers katika zile shule zao. Ni kama mtu anapokuwa Katibu Mkuu wa Wizara, anapokuwa Katibu Tawala wa Mkoa, yeye ndiye accounting office. Zile pesa zinaingia kwenye account ya shule husika kwenye mradi. Sasa ni wajibu wao kuhakikisha matumizi ya zile fedha yanakuwa ni mazuri na ya uwajibikaji. Sasa nitolee kwa ujumla kwamba halmashauri bado ina mkono kuhakikisha zile kamati za manunuzi kwenye force account, kamati ya mapokezi na kadhalika zinafanya kazi kwa miongozo na wataalam wa halmashauri kusimamia; lakini bado ni wajibu wa Mkuu wa Shule, ni wajibu wa Mwalimu Mkuu kuhakikisha matumizi ya zile fedha yanakuwa mazuri.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la walimu wa sayansi kupatikana katika hii shule ambayo tayari imeshafanywa kuwa A-level ndani ya halmashauri yake. Nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge. Ninyi wote ni mashahidi, katika kipindi kifupi cha uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, maeneo yote yamepata watumishi wa kutosha katika kipindi cha miaka hii miwili; na tayari kuna ajira hizi ambazo zimetangazwa. Kwa hiyo nikutoe mashaka Mheshimiwa Mbunge kwamba katika hizi ajira zilizotangazwa tutahakikisha pia na wewe kule katika shule uliyoitaja mnapata walimu.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, Kata ya Lutende ambayo unasema mmetenga shilingi milioni 300 ambayo itaenda kumalizia kituo cha afya, fedha hiyo haijaenda mpaka siku ya leo; je, ni lini fedha hiyo itakwenda kumalizia Kituo cha Afya cha Kata ya Lutende?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Wananchi wa Kata ya Igalula wamejenga boma la wodi ya kulazia wagonjwa na Serikali imeleta fedha nyingi na tumenunua vitanda, hakuna sehemu ya kuvipeleka; je, Serikali haioni haja ya kupeleka fedha kumalizia wodi hiyo kwa sababu operation mpaka sasa hivi ni 27 hakuna sehemu ya kuwalaza? Nakushukuru.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Venant, la kwanza fedha hii shilingi milioni 300 katika Kituo cha Afya Lutende, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi kwamba ilikuwa ni kwenye mwaka wa fedha ambao umepita, sasa nitakaa na Mheshimiwa Mbunge tuweze kuona nini kilitokea hata fedha hii mpaka sasa haijafika, na kama kuna mkwamo wowote, basi tutashirikiana kwa pamoja kuhakikisha kwamba fedha hii inafika katika Kituo cha Afya cha Lutende.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili la Igalula, fedha ya kukamilisha wodi. Serikali itaendelea kutoa fedha kadiri ya upatikanaji ili kukamilisha majengo mbalimbali kwenye vituo vya afya, zahanati na hospitali za wilaya kote nchini. Kwa hiyo, fedha itakapopatikana, basi tutahakikisha Kituo cha Afya Igalula nacho kinapata fedha.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Tabora Mjini lina kata za mjini na vijini, lakini licha ya kuwa na Hospitali ya Rufaa ya Kitete na hospitali ya wilaya kumekuwa na mrundikano mkubwa wa wagonjwa. Je, nini mikakati ya Serikali kuzisaidia kata za vijijini kupata vituo vya afya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, Sera ya Serikali ni kujenga vituo vya afya kwa kila kata lakini mwaka 2021 Waziri wa TAMISEMI, wakati huo Mheshimiwa Ummy Mwalimu alituletea Wabunge kuandika kata za kimakakati ambazo katika Jimbo la Igalula tuliandika Kata ya Goeko, kizengi na Miswaki.

Je, ni lini mtatekeleza yale maagizo ya kata za kimkakati ili tuweze kujenga vituo vya afya na kusogeza huduma za wananchi katika maeneo hayo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali lake la kwanza la utofauti wa Mjini na vijijini katika Jimbo la Tabora Mjini na Serikali kusaidia. Serikali itaendelea kutenga fedha kadri ya bajeti ambavyo inaruhusu kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu ikiwemo Jimbo la Tabora Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali la pili la nyongeza la Kata za Goeko, Kizengi na nyinginezo katika Jimbo la Igalula. Serikali itajenga vituo hivi vya afya vya kimkakati kadri ya upatikanaji wa fedha.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika pamoja na majibu mazuri ya Waziri barabara hii ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya 2020/2025 na huenda pia kwenye Bajeti iliyopita Waziri aliliahidi Bunge hili kuwa atatenga fedha kwenda kuanza usanifu katika barabara hii;

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha ili wananchi hao waanze kufanyiwa usanifu ili barabara yao ijengwe?

Mheshimwa Naibu Spika, swali langu la pili, barabara ya Chaya – Nyaua, Chanya – Manyoni – Tabora yenye kilomita zaidi ya 200, sasa kumekuwa na msongamano wa magari mengi. Tuliomba pendekezo la kuiweka bypass ya Kigwa – Magili;

Je, ni lini Serikali itaanza usanifu wa kuiweka barabara ya Kigwa- Magili ili iweze kupata kiwango cha lami? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika kama nilivyosema, barabara hii ya Chimo – Simbo hadi Puge ilikuwa haijafanyiwa usanifu; na tayari tumeshaanza kufanya usanifu. Wakati wa Bajeti ni kweli Waziri aliahidi kwamba tutaanza kujenga kilomita 10 kwa kiwango cha lami, lakini kilomita hizi zitaanza kujengwa pale tu ambapo usanifu utakuwa umekamilika, hizo kilomita za awali kilomita 10. Barabara ya pili Serikali inaendelea kutafuta fedha ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami kama alivyoomba Mheshimiwa Mbunge. Ahsante.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwapongeze Serikali kwa majibu mazuri. Ni kweli Wilaya ya Uyuwi tumepata chuo cha VETA, lakini kutokana na jiografia ya Wilaya ya Uyuwi na kuwepo kwa majimbo mawili, wananchi wa Jimbo la Igalula kwenda kuifata VETA ni zaidi ya kilometa 200.

Je, Serikali haioni haja sasa ya kunipatia upendeleo maalum wa kunipatia angalau hata shule ya ufundi ili niweze kuwa na shule ya ufundi na wanachi wa Jimbo la Igalula wakanufaika na matunda ya Mama Samia Suluhu Hassan?
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant Mbunge wa Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti,kama nilivyoeleza kwenye majibu ya swali la msingi kwamba ni azma ya Serikali kujenga vyuo hivi katika wilaya zote ikiwemo Wilaya ya Uyuwi, hivyo nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali wakati inajenga miundombinu hii vile vile tunatoa huduma za mabweni pamoja na zile za kutwa. Lakini vile vile tunafahamu, inawezekana huduma hizi za mabweni kwa wale wanafunzi wanaotoka mbali zinaweza zikawa sio toshelezi. Serikali vile vile inatambua kwamba kuna Wilaya ambazo ni kubwa na jiografia yake ni kubwa na zina majimbo zaidi ya moja. Nitoe tu mfano wa hiyo Wilaya ya Uyuwi lakini tuna Wilaya ya Bagamoyo, tuna Wilaya ya Lindi kuna Wilaya ya Bariadi kwa hiyo kuna Wilaya nyingi ambazo zinachangamoto aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, tunauchukua ushauri wake. Serikali ina mipango mingi endelevu na Serikali hii ya Mama Samia tunakwenda kufanya mambo makubwa kwa lengo la kusogeza huduma za elimu pamoja na elimu ya ufundi karibu. Kwa hiyo andaa tu eneo kwa ajili ya ujenzi wa hiyo shule uliyozungumza na Serikali ya Mama Samia ni sikivu. Tuna amini baada ya kukamilisha ujenzi wa vyuo hivi tunakwenda sasa katika ujenzi wa shule hizi za ufundi katika maeneo ambayo yamekosa vyuo vya VETA, nakushukuru sana.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kumekuwa na migogoro mingi sana katika maeneo mbalimbali ya Kata kwa Kata, Kijiji kwa Kijiji, Mkoa kwa Mkoa, Wilaya kwa Wilaya. Sasa na wataalam wetu wamekuwa wakisoma hizi ramani kwa muda mrefu sana.

Je, kupitia Wizara yako hauoni kutoa maagizo mahsusi kwa wahusika wakamalize migogoro hii kwa haraka?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili. Kwa kuwa, mgogoro huu mahsusi wa Kata ya Tura na Wilaya ya Singida (Ikungi). Je, hauoni haja ya mimi na wewe Naibu Waziri tukaenda tukaumaliza ili sasa wananchi wabaki na amani na wajue nini wanachotakiwa kuenda na wapi ni mpaka wao? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Venant Protas, Mbunge wa Igalula:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna mgogoro wa muda mrefu katika eneo hili ambalo Mheshimiwa Mbunge amelizungumzia na hasa kuna vijiji viwili vya Makene ambayo ipo katika Kata ya Iyumbu, Wilayani Ikungi na Kijiji cha Nkongwa kilichopo Kata ya Tura, Wilayani Uyui. Tayari jitihada za Serikali kupitia Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya hizi mbili ya Uyui na Ikungi, vilevile Mikoa hii miwili zimekuwa zikifanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba nitumie Bunge lako Tukufu hili kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuwaelekeza, Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya wa Wilaya hizi mbili kukutana mara moja wiki hii, kwa ajili ya kupata suluhu ya mgogoro huu na kufanya majadiliano haya yafike mwisho ili mipaka ya Mikoa hii miwili iweze kujulikana na wananchi wajue wanapata huduma kutoka upande gani wa maeneo haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, mimi nipo tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge kadri tutakapopata tu taarifa ya Kamati za Ulinzi na Usalama hizi mbili za Wilaya ya Ikungi na Uyui, nitaongozana na Mheshimiwa Mbunge ambae amekuwa mstari wa mbele katika kuwapigania wananchi wake wa Uyui. Nitaongozana nae kwenda kuhakikisha tunafanya mkutano na wananchi hawa na kuwaeleza mipaka iliyopo kwa mujibu wa GN.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante katika vijiji vipya ambavyo mnapeleka umeme, kumekuwa na tatizo la Mkandarasi kufunga vifaa vilivyoko chini ya viwango na kusababisha umeme kukatikakatika na kukosa umeme zaidi ya siku 40.

Je, nini usimamizi wa Serikali kusababisha hili tatizo kutokuwepo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, vifaa ambavyo tunavifunga kule tunavihakiki kabla ya kuvilipa, inawezekana labda ni matumizi vimefika muda wake lakini nimwombe Mheshimiwa Mbunge tutashirikiana kuhakikisha kwamba tunahakiki tatizo hasa ni nini kama ni vifaa mbavyo havikidhi basi tuviondoe na mkandarasi arekebishe tatizo hilo.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nikiri wazi kweli wataalam wako katika Kata ya Loya, wanafanya usanifu.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika maswali yangu mawili ya nyongeza la kwanza, tarehe 17 Mei, Mheshimiwa Rais alipokuwa Mkoa wa Tabora nilimfikishia kero hii ya wananchi wa Loya na akamuagiza Waziri wa Ujenzi aweze kushughulikia daraja hilo.

Je, Serikali kupitia Wizara ya TAMISEMI, hamuoni kuharakisha huo usanifu ili mpeleke Wizara ya Ujenzi ili muweze kusaidia kujenga daraja hili?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili, kwa kuwa daraja hili litachukua muda mrefu kukamilika na wananchi wanaendelea kupoteza maisha, hamuwezi kuona uharaka kwa kujenga daraja la watembea kwa miguu ili wananchi wasiendelee kupoteza maisha? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Igalula kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu ambacho nina uhakika nacho ni kwamba tuko katika hatua za mwisho za kukamilisha usanifu ambao mpaka sasa hivi tumebakiza kama wiki tatu tu kukamilika. Kwa hiyo, mara baada ya kukamilika basi tutakabidhi kwa wataalam kwa ajili ya hizo fedha ili sasa zipatikane na ujenzi wa daraja uanze. Kwa hiyo, uharaka wa kujenga daraja la miguu kwa sababu hizi kazi zinaenda sambamba, nimhakikishie tu kwamba tutafanya haya yote kwa pamoja kuhakikisha kwamba wananchi wale wanapata huduma, ahsante.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Lutende, mwaka 2019 walipeleka shilingi bilioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya na jengo la OPD limekamilika. Palikuwa pana ongezeko la milioni 300 lakini kata hiyo haijapelekewa fedha hiyo. Je, ni lini watapeleka fedha hiyo ili tuweze kumaliza Kituo cha Afya cha Kata ya Lutende?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nnaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kituo hiki kilipelekewa milioni 200 na kama ilivyo kwa vituo vyote ambavyo vilipelekewa milioni 200 au milioni 250, awamu inayofuata wanapewa milioni 300 au milioni 250 kukamilisha milioni 500 ili kukamilisha vituo vya afya. Kwa hiyo, fedha hiyo itapelekwa kwenye kituo hicho cha afya. Ahsante.

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu ya Serikali naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Kumekuwa na wimbi kubwa la tembo kuvamia makazi ya watu na mashamba, lakini kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kuna askari wanatokea Ngara. Tumekuwa tukitoa taarifa ya uvamizi wa tembo huwa inachukuwa zaidi ya siku mbili mpaka nne kwenda kutatua tatizo hilo.

Mheshimiwa Spika, je, Serikali mtanipa lini askari watakao kaa katika Jimbo la Igalula siyo hao wa Ngara na siwajui na sijawahi kuwaona?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, tumekuwa na uvamizi na uharibifu wa mali za wananchi na mwaka jana tulikwenda kufanya tathmini wananchi zaidi ya hao 17 walivamiwa na uharibifu mkubwa. Lini mtawalipa fidia wananchi waliopata athari hizo? Nakushukuru sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli nchi yetu imekuwa na wimbi kubwa la matukio ya wanyama wakali na waharibifu kushambulia maeneo ya wananchi wetu. Serikali imekuwa ikijitahidi kuhakikisha kwamba pale tunapopata taarifa tunawatuma askari wetu kwa haraka kwenda kusaidia kukabiliana na changamoto hizi.

Mheshimiwa Spika, sasa tathmini iliyokuwa imefanyika ilionekana kabisa askari hawa tuliokuwa nao kwenye eneo lile wana uwezo wa kushughulikia jambo hili, lakini kwa sababu ya concern ya Mheshimiwa Mbunge baada ya kikao hiki cha leo nitakaa nae tuweze kuona ni jinsi gani tunaweza kushirikiana na halmashauri kutoa mafunzo kwa maafisa wanyama pori wa vijiji ili waweze kushirikiana na wale wa Serikali kuondokana na changamoto iliyopo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuwalipa hawa wananchi ambao wamepata madhara haya kama nilivyosema kwenye jibu la msingi tuko kwenye hatua za mwisho za kufanya tathmini ili tuweze kuwalipa. Tathmini hii ikikamilika nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wale watakaostahili kulipwa watapata malipo yao kwa wakati.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza niwapongeze Serikali kwa kujenga reli ya kisasa ambayo ya SGR kutoka Makutupora Tabora. Reli ile mpaka sasa hivi wamefukua makaburi ya watu wa Igalula, watu wa Goweko, Tula hamjawalipa mpaka leo. Je, ni lini mtawalipa fedha ambazo mliwarudishia msiba mpaka leo hamjawalipa kwa sababu reli inataka ipite?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, hii hoja ya Mheshimiwa Venant naomba niichukue tuifatilie halafu tuifanyie kazi baada ya kupata taarifa zake za kina.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya kuendelea kuboresha mahakama zetu hapa nchini na hii itatusaidia hata ukienda kuhukumiwa kule uende vizuri vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina swali moja tu la nyongeza. Kwa kuwa Serikali ina mpango wa kujenga mahakama ikiwemo hiyo ya Urambo aliyojibu, lakini Halmashauri ya Wilaya ya Uyui mpaka leo tunatumia majengo ya Mkuu wa Wilaya: Je, ni lini Halmashauri ya Wilaya ya Uyui nayo itajengewa Mahakama ya Wilaya? Nashukuru.
NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Venant Daud, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Venant Daud, Mbunge wa Uyui pamoja na Mheshimiwa Almas Maige, wamekuwa wakifatilia ujenzi wa mahakama katika Wilaya yao ya Uyui. Pia nampongeza Mheshimiwa DC kwa kutupatia ofisi yake na majengo ili kazi za mahakama ziendelee. Nimjulishe Mheshimiwa Venant kwamba tunajenga Mahakama ya Uyui mwaka huu wa fedha, na tayari utaratibu unaendelea kumpata mkandarasi.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza niwapongeze Serikali kwa kujenga reli ya kisasa ambayo ya SGR kutoka Makutupora Tabora. Reli ile mpaka sasa hivi wamefukua makaburi ya watu wa Igalula, watu wa Goweko, Tula hamjawalipa mpaka leo. Je, ni lini mtawalipa fedha ambazo mliwarudishia msiba mpaka leo hamjawalipa kwa sababu reli inataka ipite?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, hii hoja ya Mheshimiwa Venant naomba niichukue tuifatilie halafu tuifanyie kazi baada ya kupata taarifa zake za kina.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Tarehe 29 mwaka 2021 niliuliza swali la msingi juu ya mradi ya Ziwa Victoria wa kwenda Kata za Goweko, Igalula na Nsololo na majibu ya Serikali hadi kufikia Juni, 2022, utakuwa umekamilika, lakini mradi huu upo asilimia 30. Nataka kauli ya Serikali, je, mradi huu utakamilika lini na wananchi wa Kata za Kigwa, Goweko na Nsololo wataweza kupata maji ya Ziwa Victoria?
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant Protas, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mheshimiwa Mbunge amekuwa akifuatilia sana huu mradi, lakini changamoto za kiufundi ndizo zilizopelekea mradi huu kusuasua na sasa hivi ufumbuzi umeshapatikana. Mheshimiwa Mbunge kama tulivyoongea avute subira tunakwenda kukamilisha mradi huu na lengo ni kuona wananchi wanapata maji safi, salama na ya kutosha tena bombani.