Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Mohammed Maulid Ali (2 total)

MHE. MOHAMMED MAULID ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nilitaka kumwuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mpango gani wa Serikali katika bajeti ijayo kuhusu suala zima la kutoa maji kwenye maziwa na kupeleka kwa wananchi? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mohamed Maulid Ali kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Wizara, nimesema katika jibu langu la msingi, ni kuona kwamba tunakwenda kutumia vyanzo vya uhakika, ikiwemo maji ya maziwa makuu. Hivyo tuko kwenye mpango huo, lazima tutatekeleza. (Makofi)
MHE. MAULID ALI MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri naomba kumpa ushauri mmoja. Kituo hiki ni kituo chetu cha Wilaya na bahati mbaya sana kipindi cha mvua askari wetu wanalazimika kuhama kule juu kwa sababu kumekuwa na bwawa. Sasa pamoja na hiyo program ya kutengeneza nyumba zote za polisi lakini ningeomba kitu kimoja. Kama kuna uwezekano wa lile paa lifanyiwe dharura halafu masuala mengine yatafuata baadaye, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napokea ushauri wake tutaufanyia kazi na mara nitakapopata nafasi ya kuja Kiembe Samaki tutapata nafasi pia ya kushauriana Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.