Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Hon. Maulid Saleh Ali (2 total)

MHE. MAULID SALEH ALI aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuzuia Hati za kusafiria kwa Wakandarasi wanaoingia nchini kutekeleza miradi mbalimbali?
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maulid Saleh Ali, Mbunge wa Welezo, kama ifuatavyo: -

Mheshimwa Spika, Serikali haina mkakati wa kuzuia hati za kusafiria kwa Wakandarasi wanaoingia nchini kutekeleza miradi mbalimbali isipokuwa inafanya hivyo kwa mujibu wa sheria pale inapohitajika. Serikali kupitia Sheria ya Uhamiaji Sura Na. 54 rejeo la mwaka 2016, imeipa mamlaka Idara ya Uhamiaji kuweza kushikilia au kuzuia kitu chochote ikiwa ni pamoja na nyaraka yoyote ambayo inaweza kuonyesha au kuthibitisha uvunjifu wa sheria.
MHE. MAULID SALEH ALI aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti utapeli unaofanywa kwa kutumia namba za simu za nje?
NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maulid Saleh Ali, Mbunge wa Jimbo la Welezo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, utapeli ama kwa lugha nyingine ni udanganyifu unaofanywa kwa kutumia simu za nje hudhibitiwa kwa kushirikisha Mamlaka za Udhibiti kwenye nchi ambako namba zinazotumika zimegawiwa. Mamlaka hizo huchukua hatua stahiki kwa kadri wanavyopokea taarifa zinazohusiana na utapeli huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ni Mwanachama wa Jumuiya za Kikanda na Kimataifa kama vile ATU, EACO, CRASA, CTO, ITU, UPU, PAPU na kadhalika. Ushirikiano uliopo kupitia Jumuiya hizi husaidia sana kwenye utatuzi wa masuala mengi yakiwemo yanayohusu utapeli unaofanyika kwenye mitandao ya simu.