Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Ally Anyigulile Jumbe (17 total)

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020
MHE. ALLY A. J. MLAGHILA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pia naomba nami niungane na wenzangu kumshukuru sana Mwenyezi Mungu ambaye ametujaalia tumepata nafasi ya kuwatumikia Watanzania tukiwa wamoja katika Bunge hili Tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kumshukuru pia Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli. Huyu Rais amejidhihirisha hasa kuanzia kwenye uchaguzi wetu ambapo alihakikisha hata sisi wanyonge tunapata nafasi ya kufika hapa kupitia Chama Cha Mapinduzi ambacho anakiongoza kama Mwenyekiti wa Chama.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nidhahiri maneno mengi yanaweza yakasemwa juu ya huyu Rais, lakini nataka niwaambie Watanzania wote na Bunge hili Tukufu kuna wakati na mimi sitaki tufike huko tutakuja tujilaumu na kusema tunge, haya yasingetokea. Naomba tusifike huko tukafikia kwenye maneno ambayo Wanyakyusa wanasema pride comes after a fall. Naomba Watanzania na Bunge hili lifike wakati lijitathmini juu ya huyu Rais na ikiwezekana Wabunge tuungane, tufikie wakati tutoe tamko. Sio kwamba Rwanda ni wajinga walipofikia pale, sio kwamba Wachina ni wajinga walipofikia pale. Niwaombe Bunge hili, najua maneno haya wengi hawayapendi, lakini naomba tusifikie wakati wa kujilaumu tukasema tungelifanya hivi kwa huyu Rais basi Tanzania ingefika hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015 imemfanya Rais wetuna Chama Cha Mapinduzi kufikisha asilimia 84.4. Ilani bora ya sasahivi ya Chama Cha Mapinduzi, naomba sasa ifikishe Rais huyu kuzidi miaka mitano ijayo.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie hotuba hii na kuunga mkono kwenye maeneo machache. Naomba nifike kwenye eneo la kilimo ambapo zao la cocoa ambapo ukiitaja cocoa unaisema Kyela moja kwa moja, ni zao ambalo limetufikisha hatua ya kujiona na sisi tuna dhahabu. Hata hivyo, zao hili kwa sasahivi halimnufaishi mkulima kupitia kitu kinachoitwa stakabadhi ghalani. Wataalam wetu hawajatufikirisha vizuri, wamelichukua desa lao kama lilivyo wamelihamisha. Wamedesa mfumo unaotumika kwenye mazao ya msimu wameleta kwenye mazao ya muda wote.Cocoa sio zao la msimu ni zao ambalo lipo muda wote wa mwaka na zao hili sio zao ambalo linalimwa kwenye mashamba makubwa, ni vivuli kwenye nyumba za watu. Watu wanaokota kilo moja moja, kilo tano tano. Sasa huyu mtu ukidesa mfumo wa korosho au kahawa ukauleta kwenye mfumo wa zao kama hili, unafeli nahapo ndiyo unapofeli mfumo huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye zao la cocoa sasahivi mtu anashindwa kusubiri siku nane za kuvundika cocoa ndipo akauze anaamua kuuza kwa Sh.2,500, wakati yule anayenunua mtu wa kati anapata zaidi ya Sh.5,000. Kwa kweli hili suala naomba kusema halijatusaidia wana Kyela na ni lazima tukae chini wataalam waishauri Serikali vizuri tuweze kutatua hili tatizo ili mnufaika awe ni yule aliyelengwa na ushirika ili suala la kumfanya apate faida yeye sio mtu wa kati.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kyela pia tunalima mpunga. Ni bahati mbaya sana, sasahivi kuna maneno yanaenea kwamba mchele wa Kyela umepungua ladha! Sio kweli. Ladha ya mchele wa Kyela ni ile ile ilakuna watu wanauza mchele wao kwa kutumia jina hilo. Naomba Wabunge na Watanzania wote waelewe mchele wa Kyela ni ule ule. Tunachoomba kwa Serikali sasa ni kwamba tuna mito minne mikubwa, sasa tunahitaji skimu za umwagiliaji ili tuwaoneshe mpunga wetu ulivyo bora ukiwa mwingi zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la maji ni tatizo kubwa sana, lakini naomba hebu tujikite pia kwenye sera zetu. Sera ya Maji inasema mtu asitembee zaidi ya mita 400, lakini kwenye kituo kimojawachote watu 250. Maana yake ninini? Maana yake nikwamba kwenye saa 12 ina maana wanatakiwa kuchoka watu 20 kila saa moja na kila dakika tatu achote mtu mmoja na hapo ni kwamba maji yachuruzike muda wote. Sasa naomba hili suala liangaliwe na wataalam ili kuweza kuweka vizuri na takwimu zetu zikae vizuri tofauti na zilivyo kwa sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara zetu sasahivi zinatia aibu. Mheshimiwa Rais anajitahidi kujenga barabara nzuri, lakini ndani ya muda mchache zinaharibika na tatizo lingine linaloharibu barabara ni kwamba viwango vyetu bado hatujaviweka vizuri, lakini bado tuna matatizo ya matuta barabarani. Hebu tujiulize, je mpaka sasa tunaingia kwenye uchumi wa kati tunahitaji matuta kudhibiti spidi? Matuta haya yanaharibu barabara lakini kwa uchumi wetu sio mazuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana niunge mkono hoja ya Mheshimiwa Rais kwa kusema Wabunge tujitathmini, sisi ndiyo walinzi wa Rais wetu. Ahsante sana. (Makofi)
Azimio la Bunge Kuhusu Mapendekezo ya Kurejea Katiba ya Tume ya Usafiri wa Anga ya Afrika ya Mwaka 2009
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia kulishawishi Bunge liridhie na kuunga mkono Katiba ya Tume hii ya African Civil Aviation Commission.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania sio kisiwa, hatuwezi tukaishi kama kisiwa na tukajifanya na sisi tunao uwezo wa kuwa na mabavu tukiwa peke yetu. Lazima tuungane na Nchi Wanachama wa AU (Umoja wa Afrika) ambao wameridhia pamoja na Tanzania kwenye Katiba ya Tume hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, industry ya usafiri wa anga kwa sasa inakua sana. Vile vile, Tanzania tumeanza kuingia huko kwa nguvu kubwa sana. Tunapokwenda kwa nguvu ni lazima tujue na tuungane na wenzetu ambao wako kwenye industry hiyo ili twende tukapate uzoefu na manufaa makubwa ambayo yanatokana na usafiri wa anga.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwa nini turidhie? Kwanza, tayari nchi nyingine zimekwisharidhia. Pili, hivi tunavyoongea Tanzania inalipa ada bila kuridhia. Tunalipa ada ambayo haitakuwa na manufaa, lakini tukiwa tunalipa ada tukapa manufaa itasaidia zaidi. Hivi tunavyoongea mpaka mwaka 2023 Tanzania imekwishalipa dola 45,230 karibu milioni 108. Hizi pesa hatuwezi tukakubali ziende bure. Kwa maana hiyo, naomba na nilishawishi Bunge twende huko turidhie Katiba hii ambayo itakuwa ni silaha kubwa ya sisi kujinufaisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunakwenda kupata ajira kwa vijana wetu, tunakwenda kupata ajira kwa watu wetu kuingia kwenye eneo hilo, lakini pia tutafaidika na Sheria nyingi na mabadiliko yanayotokea ya ICAO

Mheshimiwa Naibu Spika, tukikaa huko ndani, tuna fursa kubwa ya kueneza lugha yetu ya Kiswahili na tutaweza kutumia fursa zote zinazopatikana ili kuwafanya wenzetu waone umuhimu wa Kiswahili ambacho tunakitumia kama lugha bora kabisa na ambayo inashika nafasi kubwa Afrika na duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Watanzania tumelelewa vizuri sana na Baba wa Taifa. Vile vile, Baba wa Taifa alikuwepo kwenye kuanzisha Umoja wa Afrika (OAU) mwaka 1963. Tulipoanzisha Umoja wa Afrika (AU) ndipo mabadiliko yalipotokea. Pia huko nyuma tulikuwepo na tulikuwa tumeunga mkono Katiba ya Umoja huu. Baada ya mabadiliko mwaka 2009, ndipo tulipokuwa nyuma. sasa niliombe Bunge hili tuungane kwa pamoja turidhie na sisi tuangalie faida tunazozipata ambazo ni kubwa na ni nyingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii na naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Dunia na Afrika nzima inashangaa na kustaajabu ukuu wa Mungu ambao amebariki Taifa hili mpaka sasa hatujaingia kwenye lockdown na tunakaa kwenye Bunge hili. Naomba tuendelee kumshukuru Mungu na sifa na utukufu vimwendee yeye. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nawaomba Watanzania na Wabunge wote tusijisahau, haya yanayotokea ni kwa sababu ya mtu mmoja tu, Mungu huwa anamwangalia mzawa wa kwanza wa familia, matendo yake ndiyo yanayoshuka chini. Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli alimwamini Mungu, alisema Watanzania hatuna haja ya kuingia kwenye lockdown hata kama Mataifa mengine yanaingia twende tumuamini Mungu na yale maneno naomba tuendelee kuyaishi ndiyo yaliyotufikisha hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu zangu haya yote pia Rais Dkt. John Pombe Magufuli hakufanya yeye peke yake, alikuwa na msaidizi wake ambaye alikuwa pia anamuonesha na kushauriana naye, naye si mwingine, ni mama yetu kipenzi, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan. Huyu mama ndiye yule ambaye aliahidiwa kwamba atampokea kijiti Mussa, sasa Mussa amebaki yeye anaendelea na ndiyo maana naomba leo niwasalimie kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

WABUNGE FULANI: Kazi iendelee.

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue nafasi hii kumshukuru sana Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Waziri Mkuu anafanya kazi kubwa sana na anachapa kazi usiku na mchana. Ndiyo maana katika yote niseme naunga mkono hoja hii ya Waziri Mkuu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijaendelea, nilipenda niongelee mambo mengi sana lakini nimejikuta nipo kwenye masikitiko makubwa sana. Kata kumi za Wilaya ya Kyela leo ni siku ya tatu wananchi wako kwenye maji, wako kwenye mafuriko. Naomba nichukue nafasi hii kuwapa pole, lakini naomba sasa hata kama taarifa hazijafika basi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kitengo cha Maafa kiiangalie Wilaya ya Kyela kwa jicho la huruma. Wilaya ya Kyela Kata kumi za Katumbasongwe, Bujonde, Kajunjumele, Matema, Isaki, Mwaya, Ikama, Ipinda na Makwale. Kata hizi zote wananchi wametoka kwenye nyumba zao, hawana chakula wala mahali pa kulala wako nje na mpaka barabara zote hata barabara yetu ya lami ipo kwenye maji sasa hivi na kuna sehemu imeanza kubomoka.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana naomba nichukue nafasi hii kusema kwamba Ofisi ya Waziri Mkuu kuna haja ya kuipendelea Wilaya ya Kyela kwa namna moja au nyingine kwa sababu moja tu. Wilaya ya Kyela ndiyo iko chini kabisa kwenye uwanda, iko mita 450; mvua zote zinazonyesha Ileje, Songwe, Rungwe na Busokelo matokeo yote mabaya yanaelekea Kyela. Hata barabara zilizoko Kyela sasa hivi zimegeuka kuwa mito.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kyela bado haijapata pesa za development kwenye barabara zake. Miaka mitano iliyopita mpaka mwaka huu hakuna pesa hiyo. Naomba sasa Serikali iiangalie Kyela tofauti na sehemu zingine kwani yenyewe iko tofauti na sehemu zingine, iko chini mno. Kwa hiyo, naomba Serikali iangalie suala hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee suala dogo tu ambalo ni la Kimungu. Kuna watu wanashangaa kwa nini Tanzania hiko hivi? Viongozi wote wanafanya vizuri. Nataka niseme, ndugu zangu, kila Rais aliyetokea Tanzania alikuja kwa mkono wa Mungu na kwa kazi yake maalum. Hakuna Rais aliyekuja kivyake vyake kwa sababu nchi hii imebarikiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Rais wa Kwanza alikuja kwa ajili ya Uhuru na kutuunganisha Watanzania wote ili tuwe kitu kimoja. Akafuata Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi; baada ya kuungana Watanzania wote, Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi aliona Watanzania mmoja mmoja, hawana uchumi wa kutosha, akatufungua wote, tukapata fedha, tukajifunza kutumia fedha. Nakumbuka kwetu ndiyo wakati ambao watu walianza kujifunza kuvaa viatu, tulikuwa tunaviita Ahsante Salim.

Mheshimiwa Naibu Spika, alipokuja Mheshimiwa Hayati Benjamin Mkapa, akaona kwamba nchi haina fedha, lazima nchi ijikamilishe, Serikali iwe tajiri. Akaifanya Serikali ya Tanzania ikaanza kuwa na uchumi wake na kulipa madeni. Akaja Rais Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete akaifanya Tanzania ijulikane nje. Hiyo ni kazi ya Mungu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna watu walikuwa hawajui hata kwamba Mlima Kilimanjaro uko Tanzania. Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete alitufanya watu wa nje wajue Mlima Kilimanjaro uko Tanzania. Likaja Bulldozer ambalo kazi yake ilikuwa ni kuifanya Tanzania ijitegemee na hapa ndipo tulipofika. Haya hayajafika kwa kudra tu, ni Mungu aliyapanga kwamba yatakuwa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana nataka kukishukuru sana Chama cha Mapinduzi. Chama hiki ni chama ambacho Mungu alikibariki, kwa sababu ni chama pekee ambacho kinafuata mifumo ya vitabu vya Mungu. Nimesoma kwenye Biblia; Kutoka 18:21-23 ndiko zilikoanzia nyumba kumi kumi. Maana alisema watu waongozwe na nyumba kumi kumi, elfu elfu na hamsini hamsini.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue nafasi hii kukushukuru sana. Ahsanteni sana kwa kunisikiliza. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 na Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025
MHE. ALLY A. M. JUMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata nafasi hii, lakini kabla ya yote naomba nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutufikisha siku ya leo ambapo tunazungumzia mambo makubwa ya Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa moyo wa dhati kabisa, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa anayoifanya kwa ustawi na maendeleo ya nchi hii na pia hasa katika utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo tunaweza tukajisahau nini kinaendelea. Unapomwona Rais wa IPU ni matunda ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ndiye ambaye amefanya kwa sasa tuwe na Rais huyo. Kwa hiyo, hiyo ni kazi kubwa, lakini pia ushawishi mkubwa alionao kwenye mataifa ya nje na jinsi ambavyo watu wanavyomheshimu yeye na kuliheshimu Taifa hili. Kwa kweli tunamshukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, nitakuwa mnyimi wa fadhila nisipowashukuru hawa Mawaziri wawili Dkt. Mwigulu Nchemba na Profesa Kitila Mkumbo. Wamefanya kazi kubwa na wametuletea Mpango mzuri sana ambao kwayo utaleta mambo makubwa na maendeleo makubwa kwa Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hawa Mawaziri wawili tu, naomba nikiri wazi kwamba, nimekaa hapa kwa hii miaka mitatu, nimefuatilia Mawaziri wetu wanavyofanya kazi. Naomba niwashukuru hawa Mawaziri. Wanasema mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Hawa Mawaziri hawalali usingizi. Kuna watu nimewahi kuongea nao wananiambia wengine wanalala wanapigiwa simu mpaka usiku kwa ajili ya kunusuru Taifa hili ili liweze kuendelea. Waheshimiwa Mawaziri, watembee kifua mbele na wao ndiyo Askari wa Mwamvuli wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan. Pia, mambo yote yanayotendeka pamoja na watendaji wenu ninyi ndiyo mnaoyafanya. Nawashukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mpango wote na mambo yote tunayoyazungumza hapa leo na hata tangu tumeanza, lengo letu kubwa ni ustawi wa jamii zetu na ustawi wa wananchi walioko kule chini. Vile vile, tunapoyafanya haya tunafanya mambo makubwa. Mheshimiwa Rais amejitolea moyo wake wote kwa dhati kuhakikisha mambo mengi yanakwenda kule chini na sasa tunatembea kifua mbele. Kila tunachokiomba kwa Mheshimiwa Rais kwa kweli kinafanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo madogo sana ambayo ningeomba tushauriane vizuri sana tena kwa maneno ya staha sana na ndugu zetu wanaoshiriki katika mipango hii. Mambo hayo ni yale ambayo yanawahusu wananchi hasa kwenye sehemu zile ambazo niseme zinaleta kero kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kero ndogo ndogo ambazo kwa kweli wakati mwingine siyo za lazima. Kwa mfano, kule kwangu kuna malalamiko ya Wastaafu hasa wanajeshi. Wanaambiwa waende kuhakikisha taarifa zao, watoke vijijini kwa nauli zao waende Mbeya kilomita 118 na unapanda milima, kwenda na kurudi bila kula ni zaidi ya shilingi 25,000. Sasa hao watu walilitumikia Taifa, walipigana vita na tayari wamekwishazeeka. Hili la kuhakiki badala ya kuweka centers kwenye wilaya, wanawaambia waende mikoani ndiko wakahakiki taarifa zao. Ndiyo nasema hivi ni vitu ambavyo huwa vinahitaji kurekebishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la TASAF; TASAF imekuja kuwakomboa watu maskini, lakini kuna malalamiko makubwa sana huko kwamba, wanaopewa siyo wale ambao walistahili na mfumo unaotumika ni mfumo wa kisomi. Sasa, wale wazee wetu walioko huko chini ukiwaletea mfumo wa kisomi unakuwa ni shida. Maswali wanayoulizwa na majibu yanayoingia kwenye Computer ili computer ichague, hayaendani na uhalisia. Mtu mwingine hata umri wake haujui, hata kwamba anapata shilingi ngapi kwa siku hajui. Sasa, unapomwingiza kwenye computer ndiyo achague kwa kweli inakuwa ni ngumu. Ningeomba ifanyike kama ilivyokuwa ikifanyika zamani. Wananchi wenyewe ndiyo watoe majina ya hao watu. Pia wakitoa kusiwe na haja ya mfumo kuchambua tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni Serikali kulipa madeni ya wakandarasi lakini na haya madeni madogo madogo yanayohusu wananchi. Kwa mfano, kuna sehemu zinapitishwa barabara, mpaka mnakwenda mnagombana na wananchi kwa kitu ambacho hakina maana ambapo tayari tulikuwa tumekwishapanga barabara ipite.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mfano mmoja kwenye barabara ya Ibanda – Itungi port. Tunaishukuru sana Serikali inajenga barabara ile lakini tangu wananchi wake wamefanyiwa assessment mpaka leo hawajalipwa fedha zao na barabara inaendelea kujengwa. Kwa hiyo, vitu kama hivi huwa vinawaudhi sana wananchi, ningeomba Serikali inapopanga mipango, ipange na mipango ambayo itakuwa inaondoa hizo kero ndogo ndogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kero kubwa kubwa pia. Leo tunapozungumza kulikuwa kuna kero za wananchi kupigwa, wananchi kufanywa nini na TANAPA. Mimi ni shahidi, nilibahatika kuwa kwenye timu ya kamapeni kule Mbarali. Wakati wa ufungaji wa kampeni kule Mbarali pamoja na kata nane nilizozunguka, nilipangiwa Kata ya Madibila kwenye Vijiji vya Ifuchilo na Ukwavila. Hata hivyo tulipowambia Mheshimiwa Rais na Makamu kupitia Chama Cha Mapinduzi wamesema, wananchi sasa wataendelea kulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, walinivuta vijana wachache walikuwa kama mia moja hivi pembeni hivi baada ya mkutano, wakaniambia Mheshimiwa Mbunge tumekubaliana na wewe, sisi kura kwa CCM tutatoa lakini suala la kwamba tuende tukalime, hatuwezi kwenda kule tumepoteza ndugu zetu, tumepoteza vifaa vyetu vya kulimia, labda aje yeye mwenyewe aje atupeleke kule, otherwise tunapigwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo lingine nataka nisistize, wataalam wetu hebu wachague moja kuishauri Serikali kwa weledi, wenzetu walioko Ulaya wamekuwa na ubunifu mkubwa sana kwa sababu ya matatizo. Leo sisi tuna matatizo kwa mfano kule Mbarali, kuna tatizo la ardhi, kuna matatizo ya maeneo oevu, mimi naona hakuna haja ya kuanza kupigana kikubwa ni kwamba, Serikali wataalam washauri ni jinsi gani tunaweza tukatokana na hilo wakiwashirikisha wananchi. Kuna mambo mengine yanafanyika bila kushirikisha wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi hii ni nchi ambayo ni ya umoja hebu tuende tuwe tunawashirikisha wananchi katika mambo mengine ambayo yanafanyika. Kwa hiyo mimi naomba wataalam wetu waishauri vizuri Serikali kule chini Mbarali watu wanasema achana na kitu chochote kile sisi ni ardhi. Kwa hiyo watu wabuni ni jinsi gani tutatumia ardhi pamoja na kuhifadhi mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kule Kyela kuna suala la cocoa, kuna matatizo pamoja na Serikali yetu na Mkuu wetu wa Mkoa kujitahidi kwa dhati ya moyo wake kuhakikisha anaondoa matatizo yanayotokea, lakini imekua ni ngumu kwa sababu ya nature ya zao lenyewe lilivyo. Kwa hiyo mimi ningeomba kuna vitu vingine ambavyo hakuna haja ya kuingizia kwenye mfumo wa stakabadhi ghalani, kwa sababu lile zao ni zao ambalo haliwezi kumnufaisha mkulima, kwanza ni zao la wazee, ni zao ambalo watu wanalima kwenye nyumba zao. Kwa hiyo inakuwa ni ngumu sana kulifanya liingie kwenye stakabadhi ghalani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ili tuendelee tunahitaji sana nishati, kuna miradi mingi ambayo inahitajika ili kuweka nishati vizuri. Tusitegemee Bwawa la Mwalimu Nyerere tu, kule kwetu Mbeya kuna mradi wa River Songwe Basin mara nyingi hauongelewi lakini ni mradi ambao unakuja na Megawatt 90 za umeme ukikamilika. Mimi ningeomba sasa iwe ni wakati sahihi Serikali kuanza kuutekeleza huo mradi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Kiwila Coal Mine kuna megawati 200 ambazo zingefanyiwa kazi saa hizi tungekuwa tunapata umeme na tayari tusingekuwa kwenye matatizo haya ambayo Kyela kila siku ni giza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mengine nitachangia kwa maandishi lakini kuna Kiwanda cha Urafiki ni aibu tena ni kwa Mheshimiwa Kitila Mkumbo kule.

MWENYEKITI: Ahsante, Mheshimiwa kengele ya pili.

MHE. ALLY A. M. JUMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Urafiki pale imekuwa ni sehemu ya kupangisha badala ya kutengeneza nguo ambazo tulinuia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono, hoja ahsante sana kwa nafasi.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, timu bora sana duniani zinazocheza mpira zina mifumo ya uchezaji mpira na mfumo mmojawapo ni 4-4-2 lakini ipo na mifumo mingine ambayo wanaibadilisha inakuwa 4-3-3 na sisi katika kujenga vijana wetu, wakina mama pamoja na walemavu tulichagua mfumo bora kabisa ambao unashinda mfumo wa 4-4-2. Mimi leo nataka nishangae wakati tunataka kushinda tunaletewa mfumo wa 5-2-2-1 mfumo huu ni wa ku-defend haujawahi kushinda hata siku moja. Maana yake ni kwamba, nasema hivi turudi kwenye mfumo wetu ambao umekuwa ukitushindia ambao umekifanya Chama cha Mapinduzi kiweze kushinda, ambao tuliwaahidi wananchi wetu kwamba tutafanya hivi ili waweze kushinda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka kusema hivi asilimia 10 ninataka nilishawishi Bunge ibaki kama ilivyo, lakini tunasema asilimia tano iende eti ikajenge miundombinu, miundombinu ipi? Miundombinu ambayo tunataka kuijenga haijatolewa ufafanuzi, lakini hata tukijenga miundombinu hivi ni lini mmachinga yaani huyu mmachinga ambaye tunamuangalia akafanya biashara ya kukaa badala ya kwenda kutembea kuuza bidhaa zake? Mimi nasema hapana, hili tuliangalie vizuri.

Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa kazi nzuri inayofanywa na Waziri wetu, kwa kuhakikisha sasa hivi tunapata fedha za kulipa elimu bure kuanzia shule ya awali mpaka Kidato cha Sita. Hivi tunapofanya haya tumewafikiria watoto wa kike ambao tunataka kesho wawe wakina Mama Samia, kesho wawe wakina Tulia, kesho wawe wakina Mama Abdallah tumewafikiria ni watoto wangapi hawaendi shule kwa kukosa taulo zao za kike? Mimi nilitaka nilishawishi Bunge hili kwamba tuoneshe mfano, kwa mara ya kwanza tusimchoshe mama yetu Samia Suluhu Hassan hebu twende tuongeze katika hii asilimia 10 hata iwe asilimia 12 au asilimia 11. Asilimia moja itolewe ruzuku kila shule watoto wa kike wapate mataulo ya kike.

Mheshimiwa Spika, yaliyopo huko vijijini ni mengi unajua sisi hapa Wabunge wako tunaongea mambo yaliyoko site hatuongei mambo yaliyoko Mjini, huko site watoto wa kike hawaendi shule wengine wanafikia hatua ya kuweka mawe kwa sababu wamekosa fedha. Kwa hiyo, ninaomba hili lifanyiwe kazi na Wizara yetu ninajua ni sikivu inataka Bunge hili litoke na vitu vipya kama inavyofanya sasa. Nashukuru sana kwa usikivu huu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunapoongelea mambo ya site ni mengi sana katika vitu ambavyo ni muhimu kwa nchi yetu pia ni viongozi wetu. Usalama wa viongozi wetu ni kitu muhimu sana, lakini tunapozungumza usalama wa viongozi wetu kuna sehemu ambapo wananchi wetu tunawakwaza. Kiongozi wetu anaposafiri au anapita sehemu utakuta atapita Saa Tano, lakini magari yanaanza kufungiwa kuanzia saa 12 asubuhi! Hili halikubaliki katika teknolojia ya sasa, hivi ni nani amewahi kufanya utafiti wa madhara yanayotokea? Kwa mfano, mtu alikuwa anakwenda Mahakamani halafu akafungiwa mnajua ni watu wangapi ambao wameshindwa kufika Mahakamani? Mimi ninaomba tutumie njia rahisi sana, kuna mambo mengi viongozi wetu wanaweza wakaenda kwa helikopta. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hapa majuzi Mheshimiwa Nape alikwenda kwa helikopta well done! lakini viongozi wetu sisi tunao uwezo wa kufanya TEHAMA nzuri kabisa na sasa hivi kwenye mitandao tunao uwezo wa kufikia, kwa nini hazitolewi taarifa kwamba leo barabara fulani na barabara fulani hazitapitika, ili kama mtu unawahi basi mtu uanze saa 10 uwahi sehemu unayokwenda ili ikiwezekana hata wale ambao wanataka kusafiri wajiandae.

Mheshimiwa Spika, katika uchumi tunaokwenda nao, uchumi huu tunaoujenga muda ni kitu muhimu sana tusiuchezee muda. Hapa majuzi mimi nimeshuhudia tumesimamishwa round about hapo tunakuja Bungeni, tumekaa dakika 40 halafu hakuna kiongozi aliyepita magari yakaruhusiwa kweli hii ni haki? Hii siyo nchi ya kujenga uchumi ambao ni wa blabla! tujenge uchumi uliokamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na mambo mazuri sana yaliyopo kwenye bajeti hii, pamoja na hotuba nzuri sana, lakini kuna suala la pendekezo la kufuta baadhi ya vifungu vinavyoiwezesha TCRA kusimamia baadhi ya huduma na miundombinu. Hivi kwa nini tuna-rush sana kwenda huko kitu gani kinachotukimbiza mpaka tukahangaike na kubadilisha kanuni sasa? Hata ambao tunasimamia Wizara hiyo hata hatujui hivi vifungu vina-conflict gani, vina faida gani na wala hatujui ni sababu gani ambazo zinatupelekea twende tuvibadilishe. Kazi kubwa ya TBS ni ku-formulate, mimi nilidhani sasa hivi tunatakiwa tuiwezeshe TBS ilete viwango vya ujenzi wa nyumba zetu. Sasa hivi tunatumia viwango vya watu wa Ulaya, kwa mfano standard temperature ni 20 je, Tanzania standard temperature ni 20? Hivi utafiti umefanyika? ndiyo kazi ya TBS! TBS kuna sehemu tumewahi kufeli, tuliwapa wakague magari Japan hivi hilo limefika wapi? Matokeo yake Serikali imepata hasara sasa. Mimi ningeomba tusikimbilie huko Mheshimiwa Waziri, tuende tufanye mijadala ya kina na kuangalia kwa kina zaidi kuna mambo mengi. Haya mambo tunayokwenda kuyafuta ni globally harmonized, ni mambo ya Kimataifa. Wizara yetu ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imeingia mikataba ya Kimataifa kwa ajili ya kusimamia haya. Mimi ningeomba hili tuachane nalo tulifanyie utafiti wa kina ili lilete tija kwa nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna suala la kubana matumizi limeongelewa sana hapa, mimi nitakuwa kinyume sana na kubana matumizi mpaka kufikia eti vikao na semina vifanyike kwa sinema Hapana! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nchi yetu uchumi wake unategemea fedha za Serikali na jinsi tunavyokula maisha ndivyo mzunguko wa fedha unavyozunguka kuwafikia kila mtu. Tukisema tubane hilo Wakurugenzi wakae huko eti aje huku hatutafika popote. Haya mahoteli tunayojenga sasa hivi ambayo ndiyo uchumi lakini uchumi wa Dodoma utakufa, wanaoleta fedha ni hao ambao tunataka tuwabanie tuwaangalie kwa sinema. Lakini exposure tu DED akitoka huko anakutana na mwenzie, akifika hapa anabadilishana mawazo, anakuwa na mawazo mapya lakini pia ana-refresh. Mimi nataka kusema mlowee kwa kubana matumizi ya kuangalia semina kwenye ving’amuzi hapana, tusifike huko, tunaharibu nchi! acha watu wale maisha wapate fedha Mama amefungua zipu. Jambo kubwa hapa tumsaidie Waziri atafute vyanzo vizuri vya mapato na kuna wakati waliwahi kusema uchumi tunao lakini tumeukalia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninakushukuru ulituruhusu Kamati yetu tukaiangalie barabara bora kabisa inayotoka Njombe kwenda Ludewa mpaka Manda kilomita zaidi ya 200 inayojengwa kwa zege. Barabara ile tukifikia hatua ya kwamba tunataka tuache kubana matumizi watu wale maisha nataka niseme ile barabara acha tuimalizie sasa. Ile barabara ikifika Manda itaunganisha na Itungi Port ambapo meli zikibeba makaa yatafika pale Itungi Port mpaka Manda. Manda yatabebwa kwa magari kwa barabara bora nzuri sana kabisa, lakini kule ndiko Mchuchuma na Liganga iliko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa nini leo hii tuache kuvuna yale makaa sasa, ndiyo uchumi ambao tunasema hebu tuende tujielekeze huko, tutafute vyanzo vizuri vya uchumi tuache haya mambo ya kubana bana matumizi madogo madogo haya ambayo hayana maana kwa kweli. Fedha yetu tunayohitaji ni kubwa matumizi tunayobana ni kidogo sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna suala la kilimo tumefanya kazi nzuri sana na Waziri amefanya kazi nzuri sana, lakini tunakwenda kutoa zaidi ya Bilioni 900 Je, tumewaangalia Maafisa kilimo waliopo huko wanafanya kazi gani? Hivi ninavyosema inawezekana tunakwenda kutoa ruzuku kwenye mbolea lakini hata idadi (database) ya wakulima hapa hatuna! Ni sababu gani? hatujawaangalia Maafisa Kilimo waliopo mimi nataka kusema tuweke maafisa kilimo walio bora ili waweze hata kusimamia haya tunayoyasema yaweze kufanyiwa kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka nitoe mfano mwingine, kuna suala la kilimo cha umwagiliaji hapa tumezungumza lakini kuna mradi mkubwa ambao siuoni popote. Wizara ya Mambo ya Nje siuoni, Wizara ya Fedha siuoni, Wizara ya Kilimo siuoni, Wizara ya Maji siuoni ni ule wa Songwe River Basin ambao unakwenda kufanya kazi kubwa. Nataka niseme Mheshimiwa Waziri hebu liangalie hili ni Dola Milioni 577 zinahitajika, ili watu wa Kyela walime mpunga kwa kumwagilia ili kule kuwepo na mambo ya umwagiliaji mazuri.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii, naunga hoja mkono. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kwa utangulizi nikushukuru sana wewe mwenyewe, Naibu Waziri wa Maji na Mheshimiwa Suma Fyandomo na Bahati kwa kwenda kuwaona wahanga wa mafuriko kule Ipinda. Wanawashukuru sana. Mlichokifanya ni kitendo cha utu Mungu aendelee kuwabariki. Ahsante sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba nikushukuru kwa utangulizi ulioanza nao na ninaomba hata katika hotuba yangu basi haya mambo yaingizwe moja kwa moja kwamba nami nayasema kama ulivyoyasema. Kitendo cha ugawanyaji rasilimali yetu, kufuatana na umuhimu wa sehemu ambapo barabara na sehemu za uchukuzi unaenda ni kitendo ambacho kinatakiwa kizingatiwe sana na Wizara yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimejipanga nizungumzie mambo machache. La kwanza, ni suala la Serikali yetu kutimiza wajibu wake. Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi nataka nikiri inatimiza wajibu wake ipasavyo. Hata hivyo: Je, watendaji wetu wanafanya kazi zinazotakiwa? Hapana. Maana Serikali yetu inatoa fedha za matengenezo ya barabara kupitia Mfuko wa Barabara na kwa kweli zinatoka vizuri, lakini wenzetu wanaoenda kuzitumia hizi fedha wanafanya kazi ambayo kwa kweli wanaiaibisha taaluma ya Uhandisi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, zipo barabara nyingi, lakini nitatolea mfano barabara chache tu. Haiingii akilini, barabara inafanyiwa matengenezo, hapa kiraka kinachimbwa, wanatengeneza, lakini ukikaa siku mbili, ukirudi tena hapo hapo unakuta shimo. Naomba tujiulize, tatizo liko wapi? Haya yanapoteza rasilimali zetu sehemu moja kutengenezwa mara mbili.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, utakuta sehemu iliyotengenezwa ni hiyo hiyo, sehemu inayofuata nayo inaharibika hakuna hata mita moja, sentimita mbili hapo hapo shimo linatokea. Hii barabara tunayoipita ya kutoka Dodoma kuelekea Iringa, kwa kweli wakati mwingine hatutakiwi kuwasimulia hata watoto wadogo, watatushangaa kabisa. Namwomba Mheshimiwa Dkt. Chamuriho, Waziri wetu haya matatizo myaangalie yasiendelee tena.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, ni suala la ubora wa barabara zetu ambazo zinajengwa. Unashangaa kuna barabara zimejengwa hazina hata miaka kumi, lakini wameshaanza kuweka viraka. Tatizo liko wapi ndugu zangu? Tunapofeli ni wapi? Hivi ma-engineer wetu wako wapi? Tatizo kubwa tunaanza kusingizia eti Mkandarasi ndiye anafanya hivyo. Siyo kweli. Naomba hapa Bunge hili tuelewane vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, anayefanya barabara yetu idumu na iwe nzuri ijengwe kwa viwango siyo mkandarasi, ni msimamizi (consultant). Hao wanaajiriwa na Serikali yetu na wanasimama upande wa Serikali. Sasa nani alaumiwe hapa? Naomba sana, kuanzia sasa nashauri tuwe na standard za ujenzi wa barabara za Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama tunashindwa kuweka standards zetu basi tudese. Tufanye tutengeneze desa, nami hilo desa ninalo Mheshimiwa Waziri. Desa lenyewe ni barabara ya kutoka Uyole kwenda Kasumuru. Kwa nini tusichukue kama mfano? Kwa nini tusichukue nyaraka zao tukazitumia kama standard ya ujenzi wa barabara za Tanzania? Barabara ile ndugu zangu imejengwa mimi nina ndevu moja; ipo. Mpaka nimefikisha ndevu nne, naiona, miaka zaidi ya thelathini ipo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya kutoka Iringa kwenda Igawa sasa hivi ina vipara na haitadumu zaidi hata ya miaka kumi ijayo. Naomba tutengeneze standard zetu. Barabara ile ndugu zangu ya Uyole Kasumulu, ikitengenezwa vizuri, ikisimamiwa vizuri ina uwezo wa kuishi miaka mingine kumi. Walijenga SOGEA nina uhakika nyaraka za barabara ile zipo, twendeni tuzichukue, tutengeneze, tuziweke vizuri, iwe ni reference ya ujenzi wa barabara zetu, kila nchi duniani ina reference ya ujenzi wa barabara zake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee masuala ambayo yanaharibu barabara, mojawapo ni matuta, matuta barabarani yanaharibu barabara zetu. Ndio maana hata ukiangalia matuta yenyewe hayana hata standard, mengine yamekaa kama vichuguu, mengine yamekaa utafikiri ni matuta ya mbatata sasa, tuelewe lipi na ndio maana nataka niseme barabara zetu matuta yanaziharibu. Kwa nini tusifanye utaratibu mwingine? Matuta yana athari nyingi sana kwa uchumi wa nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, linapokuwepo tuta ni lazima mtu akamate breki, vipuri vile vya breki hatutengenezi hapa nchini vinatoka nje tunatumia pesa zetu kununua vitu nje ya nchi. Uchumi wetu unapungua. Kila unaposimama ukikanyaga breki unapoanza kuendesha gari, gari linakula mafuta mara ishirini ya lilivyokuwa linatembea. Mafuta hatuna hapa, lakini kitaalam ile lami haiwezi ikastahimili mzigo unaosimama, inastahimili mzigo unaodundadunda. Kwa hiyo, naomba hebu tuachane na haya tutafute njia nyingine ya kuweka hata box cover tu watu wapite chini barabara ipite juu haitasumbua hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, naomba nisemee kidogo barabara moja ambayo inatoka Ibanda kwenda Itungi Port. Meli zimejengwa tunaishukuru Serikali, lakini mpaka sasa meli zinashindwa kupata hata mafuta. Tarehe 13 -17 Aprili, gari la kupeleka mafuta kwenye meli limeshindwa kupita, kwa sababu barabara ni mbovu na barabara hii tangu mwezi wa Disemba, 2019 iko mezani kwa Mtendaji Mkuu atoe kibali.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sasa hivi inaenda kutengenezwa, naomba niishukuru Serikali, lakini zaidi ya yote naomba pia Serikali itusaidie watu wanaotembea na vimulimuli wameweka kwenye magari mbele pale kama vile na wao ni rider, jamani tunashindwa kutembea vizuri barabarani, tunaomba Serikali itoe tamko katika hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kupata nafasi hii mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni ume-set standards na sisi ni wanafunzi wako na hata tunapochangia tunajua tuko na mlinzi wetu ambaye ni wewe na sisi tutakulinda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sitachangia kwa hasira kama alivyofanya Mheshimiwa Mlugo na Mheshimiwa Tabasamu na wengine kwa sababu ninataka leo liwe ni fundisho tujifunze tusome tujue vizuri maeneo yetu tunakotoka.

Mheshimiwa Spika, nitaongelea mfumo wa pili aliousema mchangiaji wa kwanza Mheshimiwa Mhagama mfumo wa Stakabadhi Ghalani na nitahusianisha mfumo huu na zao lililoko Kyela zao la kokoa ambalo ni zao kati ya mazao muhimu yaliyowekwa katika mfumo wetu wa mazao saba Tanzania hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mfumo huu pia hata ulivyoingizwa Wilayani Kyela uliingizwa kwa ubabe hakuna aliyefanya utafiti hakuna aliyezungumza na mkulima kilichofanyika ni kwamba leo tunazungumza kesho makampuni yote yasinunue kokoa. Ilikuwa ni kitendo cha ukatili na kuna makampuni yalipoteza pesa zao. Ukiuliza wanakwambia Serikali imesema Serikali ni nani kama siyo sisi wananchi? Ndugu zangu hili lilifikia hatua ya kutuparang’anya wana Kyela tulifikia hatua ya kuanza kuichukia Serikali lakini ilikuwa ni kwa sababu ya watu wachache.

Mheshimiwa Spika, cocoa ni zao ambalo ni tofauti na mazao mengine yaliyoko Mtwara kama korosho ambayo yanalimwa kwa msimu. Kokoa inalimwa kwenye vivuli sisi Wanyakyusa zao la cocoa ni zao la heshima kuwepo nyumbani kwako. Zao lile hatulimi porini maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba huwezi ukachukua mfumo unaotumika kwenye zao la korosho ambalo ni la msimu ukaja kwenye mfumo huo ukauleta kwenye cocoa ambayo inachumwa kila siku kwa msimu na kila mtu anaokota kidogo kidogo.

Mheshimiwa Spika, kilichotokea mfumo wa korosho ukahamishiwa kwenye mfumo wa cocoa matokeo yake ni kwamba wale wote waliokuwa wananunua cocoa makampuni yote yalipoteza pesa zao na hata walipokubali kilichofuata ni kwamba wale wote ambao walikuwa wananunua cocoa hizo walishindwa kuendelea na biashara kwasababu wengi pia walifikia kufilisika na kampuni mojawapo ni Baoland ambao mpaka sasa hivi hawanunui kokoa Kyela.

Mheshimiwa Spika, hili zao kwetu huwezi ukamfanya mtu asubiri kila mtu anachuma siyo zaidi ya kilo tano kwa wiki ukisema huyu mtu anayechuma kilo moja asubiri aziandae cocoa ndani ya siku tano kama kuna jua lakini apeleke mnadani akishapeleka mnadani anatakiwa kusubiri mwezi mzima ndipo apate pesa sasa wewe elfu 30 unaisubiri mwezi mzima kwa kweli haiingii akilini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa kinachotokea hawa watu wanashindwa kusubiri tumetengeneza tabaka la wanunuzi wa kati ambalo limejitengeneza automatically kwenye mfumo badala ya kununua kuuza hizo cocoa kwa shilingi elfu nne watu wanauza cocoa hizo kwa shilingi elfu tatu, na ni kwanini kwa sababu cocoa yao siyo cocoa kwa ajili ya kupata utajiri cocoa ya Kyela ni kwa ajili ya matumizi ya kila siku mtu anataka auze cocoa akamtibu mtoto, mtu anataka kuuza cocoa apeleke school fees kwa mtoto, anataka auze cocoa abadilishe mboga halafu auze cocoa angalau jioni akakae na wenzie anywe bia ndiyo kazi ya cocoa sasa leo unapomwambia mtu asubiri inashindikana.

Mheshimiwa Spika, sasa ninaomba niseme mambo machache ambayo ninaomba sana Serikali inisikilize hili zao katika dunia hii kokoa iliyopo Kyela ndiyo hamira ya cocoa inayotoka Ivory Coast, cocoa inayotoka Ghana kwa ubora kokoa yetu inaongoza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na kuna fununu…

SPIKA: Dakika moja ya kumalizia

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Naunga mkono hoja.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022
MHE. ALLY A. J. MLAGHILA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, tarehe 30 machi, nilimuandikia message ndugu yangu Mwigulu Nchemba nikimuombea kwamba ikitokea baada ya kuchukuliwa Mheshimwa Mpango kuwa Makamu Rais basi nikasema naomba Mheshimiwa Rais ikimpendeza uwe Waziri wa Fedha; na bahati nzuri yale maombi yalitokea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilifanya hivyo kumuombea kwa sababu nilijua uwezo wake na nilijua uzalendo wake alionao kwa nchi hii ya Tanzania. Sasa tumeshakupata Mwigulu Nchemba na baada ya kukupata tumeshaanza kuona matunda yako pamoja na ya Naibu Waziri wako. Matunda haya hayajajificha, tumeanza kuyapata kwa kuyashika mkononi. Katika hili naomba nimshukuru sana Mama yetu, Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Ingekuwa tupo mtaani ningesema ameupiga mwingi kukupata wewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tunaona matunda ya kupata shilingi milioni 500. Kwa jimbo langu mimi Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwa pesa hiyo tunakwenda kujenga kilometa 2.5 za lami mjini. Hii itakuwa ni alama kubwa sana ya kazi kubwa uliyoanza nayo kuifanya. Maana yake ni nini? Kama naweza kujenga kwa milioni 500 kilometa 2.5 kwa kujiongeza ninaomba niiongezee shilingi zingine milioni 500 niende vijijini nikapige kazi ya mara mbili ya hiyo pesa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ninaomba niseme, sifa zangu zitakuwa nyingi sana baada ya kuona matunda mengine yajayo, hasa kwenye eneo la jinsi utakavyogawanya hizi pesa zilizopo kwenye bajeti. Huko nyuma tumekuwa tukiona wakati mwingine sehemu nyingine hazifikiwi ilhali ni sehemu muhimu.

Ninaomba kama ni ma-flyover basi hata Tunduru kule, hata Iringa wayaone, siyo Dar es Salaam tu. Kama ni flyover pale Mbeya napo nani amewaambia hai-fit? Inakaa vizuri, tena inapendeza; ninaomba twende huko. Lakini hebu tupeleke akili sehemu zote za Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tunapozungumza watu ambao wanastahili kupata hata ile reli ya SGR TAZARA inastahili ifike hapo, tusirudi tu huku kwenye mpya, tukitengeza TAZARA, nataka nikuhakikishie, uchumi wetu utapanda zaidi ya ulivyo sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tunapotoa hizi rasilimali Mheshimiwa Mwigulu, wakati mwingine inasikitisha. Kyela ni sehemu ambayo inapata magonjwa mengi kwa sababu ya jiografia yake. Hata hivyo tangu mwaka jana hospitali imeungua wodi zimeungua pesa leo ndiyo zinapelekwa milioni 500 tu ilhali tuliomba na kwenye bajeti ilitengwa 1.3 billion, lakini sehemu zingine utakuta pesa zimeenda na wala hawakuunguliwa. Mimi ningeomba Mheshimiwa Waziri, hebu iangalieni Kyela kwa jicho tofauti na sehemu zingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ile ndiyo inayopokea masalia yote ya maji yanayotoka milimani, Ileje, Rungwe na Busekelo. Sasa miundombinu yake yote imeharibika kiasi kwamba hata kupeleka wagonjwa hospitalini ni ngumu, watu wanakufa vijijini kwa sababu hawawezi kufika haraka sehemu za kutolea huduma za afya. Kwa hiyo ningeomba hili tuliangalie si kwa Kyela tu lakini kwa Tanzania nzima. Twende tuangalie maeneo ambayo yapo prone namna hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ni suala la takwimu. Katika kitu muhimu kuliko vyote kwenye uchumi ni takwimu sahihi. Leo kwenye bajeti tumetenga fedha kwa ajili ya kufanya sensa ya wananchi wa Tanzania, lakini hivi tunahitaji kutenga hizo fedha? Mimi kwa mawazo yangu, nilitaka nishauri kwamba inawezekana hatukuwa na haja hiyo iwapo tungetumia vizuri sana rasilimali watu tulionayo; na nina uhakika wala tusingekuwa tunakisia idadi ya Watanzania, tungekuwa tunasema kwa uhuru tena kwa uhakika; kwamba leo hii tumeamka asubuhi tupo na watu kiasi fulani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini tusiwatumie hata mabalozi kwamba watoe taarifa za kila siku watu wapo wangapi hapo kwake Inawezekana ikaenda kwa mwenyekiti wa kitongoji tukatengeneza system nzuri ya mtandao. Tunaweza tukawa na computer zikaa pale kila siku au hata kwa wiki zikawa zinatolewa taarifa za idadi ya watu waliopo hapo. Mimi nafikiri kiasi hiki kisingefikiwa tungefanyia kazi nyingine. Ninaomba sana hebu twende tuangalie takwimu zetu za kila siku.

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi za Ulaya zimefanikiwa sana. Hakuna mtu anayelala nchini au kwenye nyumba ya mtu asijulikane yupo hapo na ameingia lini na anaondoka lini; na hata kwa usalama wa nchi itatusaidia sana. Zamani ilifanikiwa sana, hata kwa mabalozi, balozi alikuwa anajua ni nani ameingia kwenye eneo hilo na anatoa taarifa kwa nini haya tumeyaacha. Hivi, vyama vingi ndivyo vinatakiwa kuondoa hayo? Mimi ningeomba turudi huko tufanye mambo makubwa nchi yetu ipo kwenye eneo zuri na inaenda kuzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho ni kwenye mapato ya simu. Tumesema sana na Serikali inategemea kupata kama 1.2 trillion kutoka kweney simu. Mimi ningeomba Mheshimiwa Waziri, hebu kaa na watoa huduma wa simu wakuhakikishie uwezekano wa kupata kiasi hiki. Kwa sababu kuna sehemu kuna kuwa kama inaonekana haiwezekani ikapatikana hii. Sasa ili kuweka vizuri mimi nikuombe hebu fanya utafiti zaidi ili pesa hiyo ipatikane. Maana katika utafiti wangu nimegundua kwenye GSM na kwenye M-Pesa au Tigo Pesa pato lote la wao ni takriban bilioni 700. Sasa je, sisi tunaendaje hapo juu? Mimi ningeomba Mheshimiwa Waziri lifuatilie hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie suala la polisi. Tunahitaji kuwatunza sana polisi. Kuna sehemu tunasahau kuwasemea, na bahati nzuri Mheshimiwa Mwigulu na Mheshimiwa Masauni wote mmepita huko. Ninawaomba nendeni mkawaboreshee mafao hawa, hawa jamaa ndugu zetu wanalala nje kila siku na tunawategemea sana.

Naomba sana polisi tuwaangalie kwa jicho linguine. Lakini pia ningeomba nikutafutie chanzo kingine ambacho kinaweza kikawa ni privilege, lakini pia inaweza ikaonyesha uzalendo hata kwa Wabunge hapa hapa. Hebu tengeneza plate number za Wabunge halafu wawe wanalipia kidogo kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, plate number za Wabunge tu zinaweza zikalipa. Hebu angalia hata huko kwenye Serikali sehemu ambazo tunaweza tukatafuta, zikawa na Karangi kazuri kabendera yetu, tukawa tunalipia kwa mwezi au kwa mwaka itakwa vizuri zaidi na tutaongeza mapato. Unapokuwa Dodoma huwezi kupeperusha bendera, lakini ili ujulikane huyu ni Mbunge usijifiche ile plate number inaweza ikakusaidia, lakini iende kwa uchumi wa nchi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho naomba kusema nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ninawaombe tu viongozi wetu wote wa Tanzania waendelee kumuenzi Mungu na waendelee kumkumbuka Mungu, kwamba tupo hapa kwa sababu Mungu ameichagua Tanzania kuwa Paradiso yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 30 Septemba, 2020, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alikwenda kuomba kura pale Mbeya; na alisema maneno makuu matatu ambayo Wanambeya wanayakumbuka. Jambo la kwanza alisema naomba wanambeya mnichagulie Wabunge wote wa Mkoa wa Mbeya waingie Bungeni, Wanambeya wakafanya, ahsante Wanambeya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili alisema, naomba Wanambeya nichagulieni Tulia, roho yangu itulie. Sasa kama huko alipo anatusikia tunamwambia roho yake itulie sana, Tulia alichaguliwa na sasa ndiyo Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pia tunataka tumwambie aliyemuachia kazi Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kazi yake anaiendeleza na anaupiga mwingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu alilolisema, alisema nataka niifanye Mbeya iwe ni kitovu cha biashara kwa Nchi za Kusini mwa Afrika na SADC kwa ujumla. Ili mambo haya yatimie, kuna mambo muhimu ni lazima yawepo hasa ya miundombinu; na jambo la kwanza ni uwanja wa Mbeya ambao tayari unaendelea vizuri. tunaishukuru sana Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni barabara; barabara ya TANZAM, barabara muhimu kuliko zote na nataka niseme katika barabara ambazo kwa sasa zimesuswa ni hii barabara. Sasa naiomba Serikali kama kweli lengo lipo vilevile halijabadilika, ni lazima sasa Serikali yetu ihakikishe inakwenda kuijenga barabara hii kwa viwango sahihi. Sasa hivi ajali za magari zinatokea kila sehemu, ukitoka Mbeya kilomita 70 ni kila siku kuna ajali, barabara imeharibika na hii barabara ndiyo inayounganisha SADC, ndiyo inayounganisha magari yote na mizigo yote inayokwenda Malawi, Zambia, Congo mpaka Zimbambwe. Kuisusia barabara hii ni kuisusa Tanzania kiuchumi na kuharibu bandari zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unapofika Mbeya, ukifika pale katikati hapapitiki, barabara haipitiki, pamejaa vibajaji, daladala na kadhalika. Tunaomba Serikali sasa ichukue hatua za haraka ijenge barabara ile kwa njia mbili nina uhakika itatusaidia wakati huo tunafikiria kujenga bypass. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la tatu, ili kuhakikisha ile ndogo ya Mheshimiwa Rais inatimia ni lazima TAZARA ifanye kazi. Naomba katika jambo la TAZARA Bunge hili livae meno ya chuma, tuache kuvaa meno ya plastiki kwa sasa. Naomba hili suala siyo la mchezo, safari hii tumekubaliana na Zambia tubadilishe mikataba, mkataba uwe mzuri, lakini tutunge sheria ya maana. Upande wa Tanzania mambo yamekwenda vizuri, leo naambiwa eti Zambia hawana Bodi ya Wakurugenzi mpaka watakapounda Bodi ya Wakurugenzi ndipo hizo Kanuni na Sheria zipitishwe, tunakwenda wapi? Ni lazima sasa tutoe tamko lenye maana. Naiomba Serikali; katika hili Serikali tuwe wakali, mkataba huu unaiangusha nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge, ili lengo hili litimie ni lazima Mbeya kuwe na Bandari ya Nchi kavu pale Inyala. Vyombo vyote vya usafiri vikiishia pale Inyala na nchi za SADC kule Kusini zikachukua mizigo pale uchumi huu utakwenda na Serikali itaona bandari yetu itakavyofanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, tazama ramani utaona nchi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi nzuri kuliko zote duniani ni Tanzania; na si kwamba, ni Tanzania tu ambayo imejaliwa, Tanzania hiyo ni Tanzania ambayo inatoa mwanamke bora sana duniani anaitwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini si hivyo tu...

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MWENYEKITI: Nani, Mheshimiwa Jumbe kuna Taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Hamisi Taletale.

T A A R I F A

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, alipoimba nilikuwa nataka kuingia chini ya meza. Kwa hiyo, nimuombe asirudie tena kuimba nyimbo nzuri akiwa anatutisha, ahsante. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa…

MHE. ALLY J. MLAGHILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napokea Taarifa hiyo kwa sababu yeye ni talented sina haja ya kumbishia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka tu kusisitiza kwamba, Tanzania hii ni nchi ambayo imebarikiwa sana. Inatoa mwanamke bora kabisa ambaye anaitwa Samia Suluhu Hassan ambaye ndiye Rais wa nchi hii. Ni nchi hii duniani ambayo inatoa Spika bora kabisa, a super woman, anaitwa Tulia Ackson. Ni nchi hii inatoa Mawaziri bora kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninataka tu niseme katika hali ya nchi kama hii ni lazima tufike wakati tujue kwamba, sisi tunaangaliwa na dunia nzima. Na tunapoangaliwa na dunia nzima ni lazima tuwe tunakubaliana kwamba, tumekuja hapa Bungeni kwa ajili ya hoja na si kutakiana ajali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme hili kwa masikitiko makubwa. Jana mchangiaji Mheshimiwa Festo Sanga amechangia vizuri sana kuhusu suala la kuwatetea wananchi juu ya mambo ambayo yanaendelea Mbarali lakini matokeo yake imeonekana yeye hayupo kwa ajili ya kutetea wananchi bali ana maslahi yake. Sisi hapa tumekuja kwa ajili ya kuwatetea wananchi, hatujaja kwa ajili ya kufurahisha watu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ameongea hapa Mheshimiwa Saashisha kuhusiana na suala la kutokutumia wataalam vizuri, tunatafutiana ajira. Nina mfano mmoja mzuri naomba niuweke hapa. Pale Bandari ya Tanga tulipokuwa tunasomewa taarifa hapa kulionekana kulikuwa kuna baadhi ya vitu ambavyo hazikuwa sawa. Aliyeibua mambo hayo nataka nikwambie, yupo mfanyakazi aliibua mambo hayo mpaka sasahivi hayupo kazini, alifukuzwa na hakuna mtu anayetaka kumjadili wala kuona kwamba anafaa kuendeleza bandari n ani mtaalam. Kuna jamaa mmoja anaitwa salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeamua kumtaja jina kwa sababu, namfahamu na yeye ndiye aliyeibua uozo, walipoona anaibua uozo huo wamemfukuza kazi. Ninaomba wanaohusika wawatafute hao watu watatusaidia kwa mengi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunaongelea mambo ya kuanzisha Bandari ya Bagamoyo. Hivi bandari tulizonazo tumezitumia kwa uhakika?

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA
UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ally Mlagila Jumbe kuna Taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora.

T A A R I F A

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Serikali yetu inathamini sana misingi ya utawala bora, na kwa kuwa Serikali yetu imejipambanua kuhakikisha wkamba, inapambana na rushwa na inasimamia haki kwa watumishi wote wa umma ambao wamekuwa ni chanzo cha utendaji kazi bora, matumizi bora ya fedha na suala zima la maadili katika utendaji wa kila siku wa wawatumishi; kwa hiyo, kwa kuwa Serikali imejipambanua hivyo ninaomba tu nimpe taarifa Mheshimiwa Mbunge tuko tayari kumfahamu mtumishi huyo na kufuatilia kama iko misingi ya utawala bora imevunjwa kwa uadilifu na utendaji kazi uliotukuka kwa mtumishi huyo, Serikali itachukua hatua zaidi. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Waziri. Mheshimiwa Ally Mlaghila Jumbe unapokea Taarifa hiyo kutoka kwa Mheshimiwa Waziri?

MHE. ALLY J. MLAGHILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napokea Taarifa hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bandari ya Bagamoyo tunaisema sana hapa. Je, hivi Bandari ya Tanga tayari tumeshamaliza kazi zote zilizotakiwa pale, ili iweze kupokea mzigo? Ni kweli Bandari ya Dar es Salaam inafika wakati inaelemewa. Je, Bandari ya Mtwara ambayo ina kina ambacho ni natural, ambayo iko vizuri, Je, tumeitumia ipasavyo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ningeomba Bandari ya Bagamoyo tusiiseme kama bandari. Tukisema industrial park itakuwa ni nzuri zaidi, lakini tukisema juu ya bandari ninaomba bandari tulizonazo tuweze kuzitumia ipasavyo, ili...

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Jumbe inaonekana watu wameupenda sana uchangiaji wako. Kuna Taarifa kutika kwa Mheshimiwa Soud.

T A A R I F A

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba tu kumpa Taarifa mchangiaji kwamba, wakati tukiongelea kuhusu networking ya bandari, basi pia tuiweke pia Bandari ya Zanzibar umuhimu wake kwa sababu nayo pia ni sehemu ya nchi ya Tanzania. Na huduma itakapotoa itatoa kwa ajili ya nchi nzima. Ahsante sana. (Makofi)

MWENYEKITI: Sawa. Mchangiaji anaweza akaweka huo mchango, lakini tusije tukachanganya mambo, tukaanza mambo ya muungano hapa halafu tukawa tumezalisha jambo lingine zito.

Mheshimiwa Ally Mlaghila Jumbe.

MHE. ALLY J. MLAGHILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la bandari ninaomba likae hivyo, lakini naomba nijielekeze pia kwenye barabara na mchango ambao tunachukua kwenye mafuta wa road toll. Tunakoelekea sasahivi ni kwamba tunaenda kwenye magari nyanayotumia gesi; na hapa yupo Dangote anatumia gesi. Tunakoelekea itatokea wakati huo mfuko ambayo tunatoa kwenye mafuta tutashindwa kuufikisha na utashindwa kutusaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba wataalamu watusaidie, nchi zote sasa hivi zimeacha ku-charge kwenye mafuta, tutumie teknolojia, tuangalie ni namna ambavyo tunaweza tukapata hiyo kodi kwenye magari baada ya kwenye mafuta. Kwa mfano, kuna Road Toll; tunao uwezo wa kutumia teknolojia, Wajerumani wame- advance sana, wana kitu kinaitwa MOT, gari linahesabika kwa jinsi linavyotembea barabarani ndivyo linavyolipa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii mkulima ambaye analima kwa trekta, anatembea shambani, diesel anayonunua analipa Road Toll, mchenjuaji ambaye yuko kule porini anatumia diesel kuendesha mtambo wake, analipa Road Toll kwa kununua mafuta. Hii siyo haki. Hebu tutafute njia sahihi ambayo itahakikisha kila mmoja analipa kwa haki. Gari lililobeba mafuta, limelipa Road Toll, halafu mtu anayeenda kutumia shambani, analipa Road Toll. Hata kuendeleza kilimo inakuwa ni shida sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba, hebu tukae na wataalam wanaotakiwa, ambao wanaweza wakafanya haya mambo vizuri, watuhakikishie na watuongoze. Sasa hivi zipo taxi pale mjini, zote zimehamia kwenye gesi, hazilipi. Hakuna anayelipa tena mafuta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, naomba hebu tunapozungumza mipango hii twende kwenye irrigation. Tuna irrigation ambazo ni muhimu sana; kuna irrigation ambayo iko sehemu ya pale Malawi na Tanzania ambayo inasisitizwa lakini leo sioni Mpango ukiongelea hiyo, ambayo ni Songwe River Basin.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Haya, ahsante sana.

MHE. ALLY J. MLAGHILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba niunge mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza niendelee kuishukuru Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kwa kazi nzuri sana zinazofanyika chini ya jemadari wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze moja kwa moja na wenzetu wa TARURA, kuna vitu ambavyo vinashangaza sana. TARURA na TANROADS wanaishi kama watoto ambao hawajatoka baba mmoja, mama mmoja, kuna tatizo kubwa sana. Nimeshuhudia kwenye wilaya kwenye Jimbo la Kyela, wakati tuna matatizo ya madaraja, wananchi wanatembea kilomita 30 kwenda kulikuta daraja, barabara mpya ilipojengwa, madaraja mawili makubwa yamepotea wakati kuna uhitaji wa zaidi ya madaraja nane kwenye Wilaya ya Kyela. Sasa unajiuliza hivi TARURA na TANROADS ni watoto wa nani? Je, wanafanya kazi wanafanya kazi ambazo zinaendaje? Mwisho wa siku, mpaka naamini kwamba inawezekana kanuni iliyounda TARURA kuna sehemu haikuwa sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani leo, TANROADS, wako hapo hapo lakini wanabeba daraja kwa sababu tu eti hiyo barabara ambayo daraja hilo lingefaa wanaoshughulikia ni TARURA. Sasa ningeomba kuwe na coordination nzuri kati ya TANROADS na TARURA, mambo yote yataenda sawa. Kwa sababu mama ameamua kupeleka na kufungua pochi yake kwa ajili ya wananchi walioko huko vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo yote, kipindi kilichopita nilisema hapa katika wilaya zinazopata mvua kwa wingi, lakini wilaya ambayo iko chini mno, ambayo inapokea mvua zote na maji ya mvua zote kutoka milimani ni Kyela, maana yake nini? Maana yake ni kwamba, kama Kyela ipo chini madhara makubwa yapo kwenye miundombinu iliyoko kule. Sasa matokeo yake Kyela huu ni mwaka wa sita haijawahi kupata fedha za development kwenye miundombinu. Hii maana yake nini? Maana yake ni kwamba kila barabara iliyopo kule imegeuka kuwa ni sehemu ya kupitisha maji, imegeuka kuwa mto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe mwenyewe ni shahidi, unapita mara nyingi, mafuriko yakitokea unatuma kule vijana wako wa Red Cross, wewe unajua. Unapoenda kule Bwato, hakuna barabara, kuna daraja limejengwa pale Ngorwa, limeishia ukingoni, barabara hakuna na daraja lingine la kumalizia hakuna. Sasa ningeomba niseme hivi, nataka kujua sababu ni kwa nini Kyela imenyimwa siku zote hizo fedha za development.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwahidi Mheshimiwa Waziri, kama hajawahi kushikiwa shilingi yake, basi kesho nisipopata majibu sahihi, nitashika shilingi kwenye mshahara wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye fedha za UVIKO, Wabunge hapa watashangaa kama hawajawahi kushangaa sasa hivi watashangaa. Tulipopata fedha za kujenga madarasa 67 nilitafuta mdau ambaye alikuwa tayari kutoa bilioni 1.1 kuongeza kwenye fedha hizo kumuunga mkono Mheshimiwa Mama Suluhu Hassan. Kilichotokea mpaka leo hizo fedha mhisani ameondoka nazo na hazijafanya kazi kwa sababu ya coordination, watu kutafuta umwamba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme, tumefika mahali ambapo mtu anakuwa anaamua badala ya wananchi kuamua nini wanakitaka. Nataka kusema hata kama ni fedha ambayo haifai, lakini kwa vile nilikuwa najenga madarasa, mhisani alisema mnajenga 67, hizo fedha leteni tuchanganye, nitajenga madarasa 154, mwisho wa siku tumeishia 67 tu, sasa hili linasikitisha sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili lazima nimshukuru sana ndugu yangu Naibu Waziri wa TAMISEMI alishughulisha sana walihangaika, lakini yule mhisani yupo anaendelea kusaidia sehemu zingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kitu kimetokea hapa, katika ujenzi huu nataka nijifunze kutoka TAMISEMI, nani alisema cement inayotakiwa kutumika ni ile ya 42.5? Kila sehemu nani amewaambia? Nimejaribu kupekua kila literature kujua kuna tofauti gani, kwa nini utumie hii 42 badala ya 32? Kila sehemu unaambiwa ya 42 inatumika kwenye structural elements kama beam, lakini hili limetumika kama kivuli cha kuiba fedha. Fedha mama Samia alizitoa ili zikasaidie na wananchi, lakini nawaambia hapa ndugu zangu reflection ya fedha zile kwa wananchi haziko, walikuwa wanachukua wanapeleka kwenye makampuni, badala ya kununua kwa wazubuni walioko hapa.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Mlaghila, muda wako umekwisha, tunakushukuru sana kwa mchango wako.

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nilipokuwa najiandaa kuchangia nilikuwa na mlolongo mrefu sana wa pongezi na shukrani. Nilitaka nianze na Waziri nikimlinganisha na msemo usemao wembamba wa reli unapitisha gari moshi, lakini nikarudi kwamba yupo Kasekenya yupo Atupele Mwakibete, wao wana uwezo pia wa kuongeza kidogo huku kwa Mheshimiwa Waziri. Nikataka niende kwa ma–DG ndugu zetu akina Kadogosa, akina Mbosa, akina Matibila mpaka kwa Meneja wangu wa TANROADS, Engineer Masige.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mwisho wa siku nimejikuta pongezi hizi nazijumuisha sehemu moja tu kwa yule ambaye alipewa jicho na Mwenyezi Mungu la kuwatambua vipaji vya hawa watu na kuwapa kuendesha Serikali hii, naye siyo mwingine anaitwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Pongezi nyingi sana na shukrani kwake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, shukrani hizi zinakuja pia kutoka kwa Wanakyela. Ni hapa juzi tu tulipata janga la kukatika daraja pale Nsesi. Nilipopiga simu moja tu kwa Mheshimiwa Waziri daraja pale tayari. Mheshimiwa Waziri nataka nikwambie daraja liko tayari Engineer Masige ameshafanya mambo, daraja lile mpaka wiki ijayo litakuwa limeanza kupitika, ahsante sana. Wananchi wa Ngonga, Katumba Songwe, na Ikolo wanakushukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na haya ni lazima nitoe shukrani kwa mambo makubwa yaliyofanyika Kyela. Barabara ya Ibanda - Itungi Port kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania, imekuwa kuwekewa saini pale Kyela, na ndipo tulipoanzia. Hii ni historia kubwa Kyela kuanzisha na haya ni mapenzi ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu kumtuma Waziri kuja hapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo mengi yanayoenda kufanyika. Tunaanza kujenga barabara ya Katumba – Songwe – Ileje ambayo tayari imeshaanzia upande wa Ileje inarudi huku; hii ni heshima kubwa. Vilevile kuna madaraja makubwa kama Daraja la Ipyana, Daraja la Bujonde pamoja na Daraja la Irondo; haya ni mambo makubwa ambayo tunafanyiwa shukrani nyingi sana. Pamoja na hayo nimeona leo nitoe pongezi kwa Waziri na Wizara yake kwamba kwa mara ya kwanza sasa nchi yetu inaanzisha mfumo mzuri sana wa ujenzi wa barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo nimeona leo nitoe pongezi kwa Waziri na Wizara yake kwamba, kwa mara ya kwanza sasa nchi yetu inaanzisha mfumo mzuri sana wa ujenzi wa barabara pamoja na sehemu nyingine za bandarini. Haya yote yanatokea kwenye mfumo wa PPP. Ningeomba hata hii EPC + Finance bado tuiache nyuma tukimbilie kwenye PPP, kwa sababu moja tu kwamba, huu ndio mfumo ambao uko duniani kote, yaani habari ya mjini, habari ya dunia ni PPP. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpe Mheshimiwa Waziri mfano mmoja, Bandari ya Hamburg, Wajerumani wanaita Hamburg Hafen, ni bandari ambayo wao wenyewe kwa heshima wanaiita Das Tor zur Zukunft, maana yake ni lango la kwenda to the future, a door to the future. Pale yupo mtu mmoja anayeitwa CSCO (Chinese Shipping Company), wanaendesha terminal ya container pale, lakini ukienda Rotterdam pale CSCO wapo. Wajerumani walikuwa wanajiuliza hivi tumeuza bandari hii kwa Wachina?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ujerumani wamesema hapana. Mfumo wa sasa ni wa kuendesha kwa pamoja Serikali na wawekezaji. Nataka nimwambie Waziri tunampigia makofi kwa kuingia kwenye mfumo huu, ataitoa Tanzania ilipo kwenda mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunataka tutoke kwenye bandari twende kwenye barabara. Mfumo wa sasa wa ujenzi wa barabara kwa pesa tulizonazo hatutaweza kusonga mbele kwa kutumia pesa za nchi hii, ni lazima tuweke uwekezaji na tunashukuru tayari umeshaanza. pongezi nyingi sana kwa Mheshimiwa Waziri. Pamoja na pongezi hizi naomba sana baadhi ya mambo yafanyike kwa ufanisi na tuendelee kuwekeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Mbeya ni Mkoa mkubwa sana, lakini ni Mkoa ambao mazingira yake ni tofauti kabisa na mikoa mingine. Ninachokiomba ni kwamba, tunapojadili na Mheshimiwa Waziri anapofikiria juu ya kutoa bajeti kwa Mkoa wa Mbeya, kwa barabara za Mkoa wa Mbeya, asiwaze jinsi ya kugawa, hebu afikirie mambo mawili tu makubwa, aangalie jiografia, lakini angalia terrain ya Mkoa wa Mbeya. Ukishuka kule Kyela, Kyela iko chini ya maji, ili ujenge barabara unahitaji ujaze mita mbili ndipo barabara ipitike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitoka Kyela kilometa 50 tu, ukipandisha Rungwe, ukifika Mbeya, barabara inahitaji ukate milima mita sita, haya hayatokei mahali pengine, yanatokea Mbeya na ndio maana nataka nimwombe Mheshimiwa Waziri, leo hii barabara imeshindwa kutoka Matema kwenda Ikombe na niliwahi kusema hapa, watu walishangaa kwamba, hii ni Tanzania au uongo na kuna watu walinifuata wakaniuliza unachokisema ni kweli?

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliwaambia Kijiji cha Ikombe tangu kuumbwa kwa dunia hawajawahi kuona gari, watu wakashangaa. Nataka niseme ni kweli hakuna gari, lakini kibaya zaidi tangu tumeanzisha dunia hii kila Mbunge anayeenda kule analiliwa kilio akifika, mimi naanza kuogopa kwenda; nimeenda mwezi juzi, wananchi badala ya kunipokea wakaanzisha misiba, hiyo misiba ni ya nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni misiba ya akinamama ambao walishindwa kujifungua kwa sababu Ziwa lilichafuka wakashindwa kuja Matema, akinamama wamefariki na mimba. Hii ni nchi ya Tanzania ambayo inaendeshwa na mwanamke mwenye uchungu. Nataka niombe, Barabara ya kutoka Matema kwenda Ikombe, tafadhali sana wananchi wamelia wamechoka, hatutaki tuendelee na misiba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ninayoyasema wananchi wanayasikia na Tanzania sasa iangalie. Kuna sehemu ambazo ni lazima ziwe za kipaumbele pamoja na kwamba, bajeti ni finyu, lakini wapo wananchi ambao wanahitaji huduma hii kwa umuhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naomba kuunga mkono hoja hii. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
MHE. ALLY A. J. MLAGHILA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Hapa juzi tumeshuhudia utiaji wa saini wa minara 758 ambayo inakwenda kujengwa kwenye maeneo ambayo ni ya wananchi wa kawaida sana. Hii imetokea ni kwa mkupuo mmoja kwa mwaka mmoja. Huko nyuma tangu uwepo wa Tanzania imekuwepo minara 1383 tu. Jambo kama hili linatokea kipindi hiki cha Mheshimiwa wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan, haijawahi kutokea kipindi chochote kile. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili nataka nisema sisi Wabunge kama wawakilishi wa wananchi hatutakiwi kuona haya wala soni kumshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Waswahili wanasema mtu husifia chake hasa kinapompendeza. Mheshimiwa Rais, anatupendezesha Tanzania inang’ara. Ahsante sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, haya yote yanayofanyika lengo lake kubwa ni kuhakikisha ufanisi wa mawasiliano, data lakini pia kumpunguzia mzigo wa gharama za bundle mtanzania aliyeko huko chini. Pia, haya yatawezekana iwapo kila unapokwenda mnara REA watapeleka umeme na umeme utarahisisha uendeshaji wa minara hiyo badala ya sasa ambapo minara inazungushiwa mafuta ya diesel kila siku, inaongeza gharama kubwa

Mheshimiwa Naibu Spika, kubwa kuliko zote, pamoja na minara yote hiyo ubora wa mawasiliano, ubora wa usikivu usipoboreshwa tutaendelea kuliwa. Na nataka niseme, katika hili kuna mahali mimi ninaamini sisi hatuko vizuri katika Tanzania na hasa katika vertical modulation. Namuona Mheshimiwa Waziri anacheka, ni kwa sababu nimekuwa nikiwaambia siku zote. Hawa Mawaziri wako vizuri sana na nataka niseme ingekuwa ni kipindi kile ndio tunaoita wanajeshi wa mwamvuli lakini katika hili la vertical modulation.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania tumefeli hata ukisafiri kidogo ukipanda kakichuguu tu mawasiliano yanakatika na yanapokatika hela yetu inaliwa huko ndiko tunakowaibia wananchi

Mheshimiwa Naibu Spika, nina mfano mmoja, ukitoka Kasumuru kwenda Blantyre, Malawi ni kilomita zaidi ya 1300. Ukitoka pale, kama unaongea na simu unauwezo wa kuongea na simu isikatike unapanfa milima unashuka milima mpaka unafika Blantyre. Tanzania nini kinashindikana? Ninaiomba Serikali yangu iangalie ubora wa mitandao ili wananchi wapate ile quality inayotakiwa kwenye usikivu na pia hata kwenye pesa yao wanayoitumia.

Mheshimiwa Naibu Spika, siyo usikivu tu, hata hapahapa ukimpigia mtu simu ukiongea dakika moja hujamalizia hata ya pili itakuta mikwaruzo imeshaingia kwenye simu. Sasa hapo ubora unakuwa wapi ningeomba hili liangaliwe sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili niipongeze Serikali, imenunua mtambo wa kuchapa hapa kwa wenzetu wa TSN, lakini pamoja na juhudi zote hizi iwapo Serikali na Mawaziri hamtasisitiza wadaiwa wa taasisi hizi pamoja na taasisi zingine, hasa Serikali na Wizara kutokulipa madeni tutakuwa tunaua kabisa. Hata tununue mitambo gani msipolipa madeni mtakuwa mnaua kabisa haya mashirika yetu. Tunaomba mlipe madeni mnayodaiwa. Na mnapolipa madeni msiwape hawa wanao simamia wakaanza kuota mnvi kwa sababu inaonekana wao hawadai wakati ni ninyi hamlipi. Kuna wakati mtu unaweza ukadai ukashindwa; sasa naomba tuwasimamie hawa wenzetu wapate pesa zao ni pamoja na TTCL wapewe pesa zao wanazodai kwenye Mashirika, Posta vivyo hivyo Serikali isimamie.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu ni kuhusu hawa vijana wanaoanza kwenye TEHAMA. Nashukuru sana wapo startups wanakuwa wanalelewa. Wapo Watanzania wazuri hata ukienda kule kwangu Kyela ukienda Mbeya, wana uwezo wa kutengeneza mifumo yote katika Serikali hii e-GA kwa nini inang’ang’ania kutengeneza mifumo wakati wapo vijana ambao kwa kuwapa kazi tungetoa ajira lakini pia tungepata kodi? e-GA ambacho wanatakiwa kufanya ni kusimamia ubora na kuangalia uendeshaji wa mifumo hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, ni kuhusu suala la anuani za makazi. Imekuwa kama watu wamerusha tu hili jambo linafanyika. Hivi kweli Tanzania tumekosa majina? Mtu anasema Barabara ya Shule, Barabara ya Church, Barabara ya Msikiti, Barabara ya Mosque. Kweli hakuna majina kabisa Tanzania? Tumeshindwa hata kutoa majina hata ya Wanyama? Haiwezekani, tusijidharirishe, unapoandika anuani hii ni ya kimataifa, unapo mwambia mtu alieko Marekani mimi naishi kwenye barabara ya school anakushangaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na naomba kuunga mkono hoja, ahsante sana.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata nafasi hii muhimu na adhimu sana. Ni kama mwaka mmoja na nusu nilisimama hapa na nikasema juu ya mambo muhimu ambayo marehemu Hayati Baba yetu Dkt. Magufuli aliyasema kwa ajili ya kufanya Mji wa Mbeya na Mbeya nzima kuwa ni hub ya uchumi kwa nchi za Kusini mwa Afrika na katika mambo hayo nilitaja TAZARA, nilitaja Bandari ya Nchi Kavu Inyala lakini nikasema pia juu ya barabara.


Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ninafurahi kusema kwamba ninawashukuru sana waliomshauri Mheshimiwa Rais kubuni mfumo wa EPC+F; na hao sio wengine ni Waziri wa Fedha ambaye anajua hizi ni kodi za wananchi ambazo zinaenda kulipa, nakushukuru sana Mheshimiwa Waziri. Pia ninamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kulipokea hili. Leo Mbeya tunaenda kujivunia barabara ya njia nne, mbili mbili kutoka Igawa mpaka Tunduma, hili si jambo dogo. Ukilisema kwa maneno mepesi ni dogo lakini kwa kweli nataka niseme, Mheshimiwa Rais ametuheshimisha sana Mbeye, ahsante sana Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Mwenyekiti, si hivyo tu, tunaenda kupata bypass ambayo ina kilometa 48. Ndugu zangu, Tanzania tulizoea ni barabara moja inatoka huko mpaka inakoishia. Sasa kwa mfano mpya tutapata barabara mbili mbili kila upande kilometa 218. Mimi ni nani leo nisimshukuru Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan? Nitakuwa nimekosa kibali mbele ya Mwenyezi Mungu. Na mimi nataka niseme, kama kuna watu wataendelea kushukuru kama kuna watu wataendelea kupiga magoti basi mimi nitaendelea. Kama kuna watu wana wivu nikimshukuru Mheshimiwa Rais basi wanywe sumu wajinyonge, sisi tutaendelea kumshukuru. Haiwezekani leo unafanyiwa mambo makubwa kama haya kwa muda mfupi halafu usishukuru, kwani kuna tatizo gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mimi nataka niseme, pamoja na haya mambo yote ambayo yamefanyika, nataka nikumbushe baadhi ya mambo katika hizo barabara. Barabara zetu zina matatizo makubwa sana, hasa kwa hawa wanaofanya usanifu. Kwanza ni wakatili wakubwa, wanawakatili walemavu, hawataki walemavu watumie barabara. Ninaomba kwenye barabara hizi zinazojengwa waache mambo ya kujenga vighorofa vya kupandia sehemu ambazo ambazo kunatokea overpass. Kwa nini msijenge subway ambapo hata mlemavu anao uwezo wa kupita, mtu anayetembea kwa mguu atapita? Mnapojenga vile vidude vya kupanda juu zile ngazi mlemavu hawezi kupanda, tuache ukatili. Ninaomba Mheshimiwa Waziri walisimamie hili, fedha ni za wananchi, walemavu ni walipa kodi pia, wapate ku-enjoy kwenye barabara hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, inapoijengwa ile barabara, kuna barabara ambayo itakatisha inatoka Uyole kuelekea Kasumulu, tunaenda kufungua bandari. Wewe ni shahidi na wewe umeshuhudia kwamba sasa bandari yetu inaenda kufunguka. Malawi wataitumia sana, hawataenda tena Kusini kule Beila, wataitumia bandari yetu kwa sababu itakuwa attractive. Ninachoomba, tunapojenga hizi barabara tukumbuke kwamba kuna barabara inayotoka Uyole kuelekea Kasumulu ni muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo ninaomba niseme jambo moja ambalo ni muhimu. Jambo hili ni la pongezi nyingi kwa Serikali kwa sababu Serikali hii imekuwa Sikivu. Na leo nataka niwasifu Waheshimiwa Mawaziri wawili na niwashukuru. Mheshimiwa Bashe, Waziri wa Kilimo na Mheshimiwa Ashatu Kijaji Waziri wa Viwanda na Biashara. Nawashukuru kwa sababu wamesikia kilio cha Wanakyela kwa kwenda kukomboa soko la zao la cocoa; ninawashukuru sana. Mmefanya kitu kikubwa na wananchi wa Kyela wanamshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuwakomboa kwa sababu leo wanatoka kwenye utumwa na fedha zinaenda kukaa mifukoni mwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu malipo ya wafanyakazi wa Kiwira Coal Mine. Ninaomba nikumbushe, Mheshimiwa Rais tarehe 7 Agosti, 2022 alipofika Kyela mliahidi kuwalipa. Ninaomba hili lishikiliwe katika kipindi hiki. Hawa wananchi, hadi wengine wamefariki hawajapata hizo fedha. Wameahidiwa muda mrefu zaidi ya miaka 12. Ninaomba wananchi hawa wapate fedha zao na walipwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kule Kyela kuna eneo linaitwa Ikombe ninaomba, hata kama kwenye bajeti hakuna fedha, hata tunapojenga haya mambo ya barabara kubwa, trilioni 5.7 ni fedha nyingi mno kwa mwaka mmoja. Nimeangalia nchi nyingi nimefunua hakuna nchi ambayo imesaini mikataba na kujenga kilometa 2,035 kwa mpigo, hata Ulaya hakuna. Wakisaini sana ni kilometa 500. Sisi Samia amesaini 2,035; hii ni ajabu, na ukitaka kuweka kwenye maajabu ya dunia hili ni ajabu mojawapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapofanya haya ninaomba tusiwasahau wale waliopo kule chini. Kuna watu wilayani kwangu Mheshimiwa Waziri hawajawahi kuona barabara wala kuona gari, Kijiji cha Ikombe, wananchi kule wanakufa. Nimesema hapa mara nyingi, sio utani. Mheshimiwa Waziri nilikubeba hapa tukaenda; niliwahi kumbeba Mheshimiwa Mwenyekiti pale, alishuhudia kilio cha wananchi wa Ikombe wakitulilia. Ninakuomba Waziri, niko chini ya miguu yako, ninapiga magoti, twende tuwakomboe wananchi wa Ikombe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine nataka nichangie ni juu ya mambo ambayo yanahusu mikanganyiko ya wafanyabiashara. Ninakuomba sana wafanyabiashara kukitokea tatizo tusiingie kwenye kutoa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Hitimisha hoja yako Mheshimiwa.

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba dakika nane zimeisha? Hapana ni dakika tatu hizi. Mimi nimehesabu dakika tatu hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumzie suala la ETS. Ninaomba sana hili suala ni muhimu hatutakiwi kuliacha, kinachotakiwa ni kuongeza wigo wa kwenda sehemu zingine. Lakini kwa mambo ambayo yanawaudhi wafanyabiashara ninaomba Serikali wafanyabiashara na watoa huduma mkae pamoja muyafanyie kazi haya mambo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ninaomba niishukuru Serikali na Mheshimiwa Waziri kwa kunipa shilingi bilioni moja kujenga Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, halmashauri ambayo ilikuwa inakaa kwenye majengo ya mkuu wa wilaya, sasa tunaenda kujenga ofisi nashukuru sana Mungu awabariki sana na kwa maneno haya naomba niunge mkono hoja ahsante sana. (Makofi)
Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa nafasi hii, lakini naomba sana nimshukuru Mwenyezi Mungu kwamba ametufikisha leo siku ambayo tunaenda kuijenga nchi yetu kwa kuitengenezea uchumi thabiti. Uchumi thabiti wa nchi hii unategemea sana miundombinu ambayo leo ndio tunaijadili kwa ajili ya mwaka ujao wa fedha.

Mheshimiwa Spika, ili Tanzania iendelee na ili uchumi wa Kyela ukue kuna vitu ambavyo tunavihitaji; kitu cha kwanza ni kuhakikisha barabara yetu ya kutoka Ibanda kuelekea Itungi ports inakamilika kikamilifu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, barabara hii najua imetangazwa lakini naomba sana Serikali ihakikishe inafanya haraka kwasababu tayari bandari yetu na meli zetu zimekamilika na zipo tayari kwa ajili ya kufanya kazi pale Itungi port. Hii barabara isipokamilika zile meli hazitafanya kazi.

Mheshimiwa Spika, uchumi wa Kyela pia unategemea sana Bandari ya Dar es Salaam. Bandari ya Dar es Salaam ndio inayopeleka mizigo yote inayokwenda Malawi na pia kuelekea hadi Zimbabwe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, bandari yetu vyovyote vile ninajua sisi hapa tulipo tulikuwa tunajitahidi kuona ni jinsi gani ambavyo nchi yetu inajikwamua kiuchumi kupita bandari, tunajua nchi nyingi Malaysia wamekuwa matajiri wanaenda kwa sababu ya bandari, sasa nataka tu niwahakikishie Watanzania na niseme mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Miundombinu nataka nilihakikishie Bunge; katika kipindi ambacho watanzania na Bunge hili linatakiwa kujivunia ni kipindi hiki, bandari yetu inakoelekea ndugu zangu tunakwenda mahali pazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, takwimu ndiye msema kweli, leo mzigo wa pale bandarini umeongezeka kwa asilimia 21 sio kitu cha mchezo, na katika hili tusipoipongeza Serikali na katika hili tusipompongeza Rais kwa kumuona Erick na kumfanya awe ni DG pale tutakuwa tunafanya makosa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna wakati tunafanya vikao kwenye Kamati unaambiwa DG wa bandari hayupo, ukiuliza yupo wapi wanakwambia yupo Rwanda, yupo Congo, DG anajibeba kwenda ku-negotiated, kutafuta masoko hiki kitu hakikuwahi kutokea huko nyuma, leo hii tusipompa nguvu huyu Erick, tusipomsifia, tusipompa nguvu na kumpa ari, nafikiri tutakuwa tunafanya makosa makubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimesema bandari hii ndio kioo chetu na ndio sehemu yetu ya uchumi magari yote yanayotoka bandarini yanapita barabara ya TANZAM kuelekea Malawi. Nataka tu nisisitize ninaomba sana pale Inyara nafikiri ni Mbeya, lakini nataka niseme pale Inyara ni lazima tujenge bandari ya nchi kavu, Wamalawi, Wazambia na nchi zote za SADC ni lazima zije zichukue pale mzigo ndipo tutakapokuwa tumerahisisha kazi na tutakuwa tumejenga uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niongelee TRC kuhusu ujenzi wa reli ya kisasa; ni kweli wananchi nataka niseme ndugu zangu sisi Bunge hili tulikuwa tunategewa sana mwaka 2025 tuchekwe, watu walijiandaa watucheke, lakini nataka nishukuru kwamba safari hii vicheko vinarudi kwetu, kilio kinarudi kwao, kwa sababu mambo yanayoendelea kwenye reli yetu, kwenye SGR ni mambo ambayo wengi hawakuyategemea, walidhani yatasimama, lakini sasa yanasonga mbele na katika hili nataka nimpongeze sana Mtendaji Mkuu wa TCR na nafikiri kupongeza ni sahihi, lakini tumpongeze pale ambapo amefanya kazi nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna jambo ambalo huwa wakati mwingine tunaliangalia kijuu juu, leo hii ujenzi wa reli Tanzania ni ujenzi ambao ni the cheapest duniani, tunajenga kilometa moja kwa wastani yaani ukichanganya zote halafu ukapata wastani kwa dola milioni 3.8 hii ni kiwango ambacho kipo chini ukilinganisha mpaka na nchi zetu jirani ambao wamejenga SGR lakini siyo ya umeme. Wenzetu wengi wamefika kwenye sita wanaenda mpaka nane. Mimi nataka niseme Tanzania ni lazima tutembee kifua mbele kujivunia kwamba tuna watendaji wazuri ambao wapo wa kizalendo kwa ajili ya kuisaidia nchi yao. Yanaweza yakazungumzwa maneno mengi kwamba mara wanafanya hivi wanafanya hivi. Ndugu zangu palipo na mambo mema ni lazima pawe na maneno mabaya ili kutukatisha tamaa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa ninawaomba tusikatishwe tamaa na maneno, tukianza kukatishwa tamaa na maneno hatutafika mbali. Mimi nawaomba watendaji waendelee na kazi wafanye kazi na tupo na Mheshimiwa Kakoso Mwenyekiti wa Kamati yetu anajua kutupanga na kutuambia mambo yote ambayo yanafanyika, tunataka tukushukuru sana Mheshimiwa Kakoso kwa kuhakikisha unawalinda hata hawa ndugu zetu wanaofanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba tu nishauri kwenye SGR, kuna kipande pale cha Kilosa kwenda Mikumi kile kipande naomba kiunganishwe, lakini kwa nini naomba kiunganishwe? Kwa sababu pale ndipo ambapo SGR ina uwezo wa kuungana na TAZARA na TAZARA ikiungana na SGR mizigo ni rahisi kupelekwa kila sehemu mzigo unaotoka TAZARA ukaja SGR na unaotoka SGR ukaingia TAZARA sasa nataka niseme pamoja na hayo niombe tu barabara yetu ya kutoka pale Iringa ilivyojengwa imeshaanza kuharibika na kama inaharibika najua tatizo liko wapi.

Mheshimiwa Spika, tatizo lipo kwa wasimamizi wetu, sasa naomba tunapojenga kuanzia Igawa kuelekea Mbeya hadi Songwe isiwe hivyo tena, tujenge barabara ya maana ambayo itakuwa imestahimili na inaweza pia kupitisha mzigo mkubwa.

Mheshimiwa Spika, mimi naomba tu niseme tumefika hatua ambayo tunahitaji kuijenga nchi yetu kizalendo na kuipigania, tukiacha kuipigania nchi yetu hakuna mtu mwingine ambaye atasimama kuipigania nchi hii, nchi hii ni yetu sisi sote na Tanzania ni yetu wote na Rais ni wetu wote. Tumuunge mkono Mheshimiwa Rais, tumefikia hatua pia ya kuhakikisha kwamba Mbeya yetu inakwenda kuwa ya kisasa. Tunaenda kujenga barabara ya njia mbili pale mjini sasa nikuhakikishie tu kama tulikuwa tuna wasiwasi tayari imeshawekwa kwenye bajeti ya mwaka kuu na inakwenda kujengwa na tayari Waziri ameshathibitisha hawezi kutuangusha, ninakuombea Waziri wetu na ninataka niseme mimi nitalinda shilingi yako mpaka tuhakikishe barabara zile zinajengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi hii Mungu akubariki sana na naunga nkono hoja. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Uwekezaji Tanzania wa Mwaka 2022
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kupata fursa hii ili na mimi niweze kuchangia machache kwenye Muswada huu wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi.

Mheshimiwa Spika, naomba tu niseme kama kuna kipindi ambacho Tanzania inaenda kujijengea heshima Kimataifa pamoja na mambo yote ambayo yamefanyika, basi kwa kupitisha sheria hii tunaenda kuingia kwenye hanga za juu sana na tutakuwa tumejitengenezea heshima kubwa Duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Bunge lako linaenda kuingia kwenye vitabu vya kutunga sheria ambayo kila mtu alikuwa anaisubiri. Wananchi wengi na wadau wameipongeza sana Serikali. Wamekupongeza sana kwa kukubali kuleta Muswada wa Sheria hii.

Mheshimiwa Spika, sina haja ya kuelezea manufaa ya Sheria hii kwa sababau kila mmoja ameeleza na kila mmoja anajua, ninachotaka kusisistiza ni kwamba taarifa zetu binafsi ni biashara, huko Duniani na huko kwenye hanga taarifa zetu ni biashara, zitaenda kutumika kibiashara. Katika kutumika kibiashara ni lazima tuhakikishe taarifa zetu ni sahihi na zinalindwa, kulindwa kwake kunakuja na sheria hii. Ndiyo maana katika kulinda haya maslahi kuna kitu tumekisema kwa juu juu sana, ni kwenye jina la Sheria hii, tunaposema tu Ulinzi wa Taarifa Binafsi mimi nafikiri kuna kitu kinapungua.

Mheshimiwa Spika, hii sheria ikiongezewa faragha mbele, ulinzi wa Taarifa Binafsi na Faragha italeta uzito sana, kuna nchi tayari wameishafanya hivyo New Zealand wanasema Data Protections and Privacy na hapa jirani Uganda wanataja hivyohivyo, Tanzania tunapata wapi kigugumizi kuweka hiyo privacy. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niseme machache kwenye privacy. Tukiacha Sheria ikawa hivi, kuna mtu mwingine atakuja hadharani ataanza kukuuliza wewe unaitwa nani? Ulizaliwa lini? Jina la Baba yako ni lipi? Kwa sababu hatujaweka privacy, privacy ni jinsi pia ya kuchukua hizo data, mkakae pembeni kwa siri na huyo mchukua data, mchukua taarifa, sasa tusipoilinda hiyo nafikiri tutakuwa bado hatujajenga msingi ambao utakuwa imara sana.

Mheshimiwa Spika, kule Wanyakyusa mtoto wa kike hawezi kutaja jina la Baba Mkwe. Sasa ukilifanya hili liwe peupe kuna mtu atahukumiwa kwa kutaja jina la Baba Mkwe wake, usije ukafikiri kwa mfano sisi ng’ombe kama mkwe hawezi kusema kusema ng’ombe atasema hata linaloelekeana atasema ngwafi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo mimi ninaomba hebu hili neno la faragha liingizwe ili taarifa zetu tunapozitoa pia ziwe ni siri. Mtu unaumwa magonjwa makubwa ambayo hutaki watu wengine wajue, huwezi ukasema na mwingine anasikia ni lazima kuwe na utaratibu wa privacy, utaratibu wa faragha kama neno faragha siyo zuri kwa Kiswahili tutafute neno lingine kuweka uzito, naomba sana hili neno liongezwe.

Mheshimiwa Spika, vilevile kuna vitu pamoja na uzuri wa sheria hii, kuna mtu ambae tumemsahau, wakati wote sisi ni marehemu watarajiwa ukifa taarifa zako zinabaki kwenye vyombo. Je, kuna sehemu gani ambapo huyo marehemu ataenda kulindwa na taarifa hizo? Ninaomba tuweke taarifa za marehemu ni jinsi gani zitakavyolindwa na ni nani atayezisimamia? Kuacha hivi hivi, mimi Baba yangu alifariki, wengine hapa Baba zao wamefariki data zao tuna uhakika gani kwamba zitalindwa na sheria hii? Ninaomba hilo kama siyo sasa basi kwenye Kanuni liangaliwe vizuri.

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho Sheria yeyote inayotungwa ili iwe nzuri, inatakiwa ilete manufaa na isiwe mzigo kwa wananchi, isiwe mzigo. Tumetunga sheria hii vizuri sana, sheria hii inaenda kusimamiwa na Tume lakini Tume itasimamiwa na Bodi, hawa ni watu wengi sana na hawa watu wengi watahitaji rasilimali fedha, woga wangu na baridi ninayoipata nikwamba mbona vyanzo vya pesa bado hatujaviweka vizuri. Sheria yetu haijawa wazi, inasema tu Bunge litapitisha, Bunge litapitisha kwa Bajeti ipi? Kwa nini wasitengeneze na wao vyanzo vyao? Ninaomba tunapoelekea huko mbele tuangalie jinsi ya kupata vyanzo ambavyo vitaelezwa EWURA, walipokuwa wanatunga Sheria walisema watatoa wapi pesa. Sisi kwenye sheria hii tumesema kiujumla mno, ningeomba tuweke vizuri kwenye Muswada huu, tujue ni jinsi gani tunaenda kupata pesa.

Mheshimiwa Spika, zaidi ya yote sidhani kama kuna Mtanzania ambaye anaipenda Tanzania hatatupongeza kwa kupitisha Sheria hii, na mimi ninasema tuungane wote Wabunge hapa, tuipitishe Sheria hii kwa manufaa na mustakabali wa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga hoja mkono, ahsante sana. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi wa Mwaka 2022
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kupata fursa hii ili na mimi niweze kuchangia machache kwenye Muswada huu wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi.

Mheshimiwa Spika, naomba tu niseme kama kuna kipindi ambacho Tanzania inaenda kujijengea heshima Kimataifa pamoja na mambo yote ambayo yamefanyika, basi kwa kupitisha sheria hii tunaenda kuingia kwenye hanga za juu sana na tutakuwa tumejitengenezea heshima kubwa Duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Bunge lako linaenda kuingia kwenye vitabu vya kutunga sheria ambayo kila mtu alikuwa anaisubiri. Wananchi wengi na wadau wameipongeza sana Serikali. Wamekupongeza sana kwa kukubali kuleta Muswada wa Sheria hii.

Mheshimiwa Spika, sina haja ya kuelezea manufaa ya Sheria hii kwa sababau kila mmoja ameeleza na kila mmoja anajua, ninachotaka kusisistiza ni kwamba taarifa zetu binafsi ni biashara, huko Duniani na huko kwenye hanga taarifa zetu ni biashara, zitaenda kutumika kibiashara. Katika kutumika kibiashara ni lazima tuhakikishe taarifa zetu ni sahihi na zinalindwa, kulindwa kwake kunakuja na sheria hii. Ndiyo maana katika kulinda haya maslahi kuna kitu tumekisema kwa juu juu sana, ni kwenye jina la Sheria hii, tunaposema tu Ulinzi wa Taarifa Binafsi mimi nafikiri kuna kitu kinapungua.

Mheshimiwa Spika, hii sheria ikiongezewa faragha mbele, ulinzi wa Taarifa Binafsi na Faragha italeta uzito sana, kuna nchi tayari wameishafanya hivyo New Zealand wanasema Data Protections and Privacy na hapa jirani Uganda wanataja hivyohivyo, Tanzania tunapata wapi kigugumizi kuweka hiyo privacy. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niseme machache kwenye privacy. Tukiacha Sheria ikawa hivi, kuna mtu mwingine atakuja hadharani ataanza kukuuliza wewe unaitwa nani? Ulizaliwa lini? Jina la Baba yako ni lipi? Kwa sababu hatujaweka privacy, privacy ni jinsi pia ya kuchukua hizo data, mkakae pembeni kwa siri na huyo mchukua data, mchukua taarifa, sasa tusipoilinda hiyo nafikiri tutakuwa bado hatujajenga msingi ambao utakuwa imara sana.

Mheshimiwa Spika, kule Wanyakyusa mtoto wa kike hawezi kutaja jina la Baba Mkwe. Sasa ukilifanya hili liwe peupe kuna mtu atahukumiwa kwa kutaja jina la Baba Mkwe wake, usije ukafikiri kwa mfano sisi ng’ombe kama mkwe hawezi kusema kusema ng’ombe atasema hata linaloelekeana atasema ngwafi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo mimi ninaomba hebu hili neno la faragha liingizwe ili taarifa zetu tunapozitoa pia ziwe ni siri. Mtu unaumwa magonjwa makubwa ambayo hutaki watu wengine wajue, huwezi ukasema na mwingine anasikia ni lazima kuwe na utaratibu wa privacy, utaratibu wa faragha kama neno faragha siyo zuri kwa Kiswahili tutafute neno lingine kuweka uzito, naomba sana hili neno liongezwe.

Mheshimiwa Spika, vilevile kuna vitu pamoja na uzuri wa sheria hii, kuna mtu ambae tumemsahau, wakati wote sisi ni marehemu watarajiwa ukifa taarifa zako zinabaki kwenye vyombo. Je, kuna sehemu gani ambapo huyo marehemu ataenda kulindwa na taarifa hizo? Ninaomba tuweke taarifa za marehemu ni jinsi gani zitakavyolindwa na ni nani atayezisimamia? Kuacha hivi hivi, mimi Baba yangu alifariki, wengine hapa Baba zao wamefariki data zao tuna uhakika gani kwamba zitalindwa na sheria hii? Ninaomba hilo kama siyo sasa basi kwenye Kanuni liangaliwe vizuri.

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho Sheria yeyote inayotungwa ili iwe nzuri, inatakiwa ilete manufaa na isiwe mzigo kwa wananchi, isiwe mzigo. Tumetunga sheria hii vizuri sana, sheria hii inaenda kusimamiwa na Tume lakini Tume itasimamiwa na Bodi, hawa ni watu wengi sana na hawa watu wengi watahitaji rasilimali fedha, woga wangu na baridi ninayoipata nikwamba mbona vyanzo vya pesa bado hatujaviweka vizuri. Sheria yetu haijawa wazi, inasema tu Bunge litapitisha, Bunge litapitisha kwa Bajeti ipi? Kwa nini wasitengeneze na wao vyanzo vyao? Ninaomba tunapoelekea huko mbele tuangalie jinsi ya kupata vyanzo ambavyo vitaelezwa EWURA, walipokuwa wanatunga Sheria walisema watatoa wapi pesa. Sisi kwenye sheria hii tumesema kiujumla mno, ningeomba tuweke vizuri kwenye Muswada huu, tujue ni jinsi gani tunaenda kupata pesa.

Mheshimiwa Spika, zaidi ya yote sidhani kama kuna Mtanzania ambaye anaipenda Tanzania hatatupongeza kwa kupitisha Sheria hii, na mimi ninasema tuungane wote Wabunge hapa, tuipitishe Sheria hii kwa manufaa na mustakabali wa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga hoja mkono, ahsante sana. (Makofi)