Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Maryam Omar Said (1 total)

MHE. MARYAM OMAR SAID: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na ufinyu na uchakavu wa ofisi za Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, Mkoa wa Kaskazini Pemba. Je, ni lini Serikali itaanzisha ujenzi mpya kwa ajili ya ofisi hizi katika Mkoa huu?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunao mpango wa kujenga ofisi zote za Makao Makuu ya Polisi ngazi ya Mkoa. Kwa hiyo, tumeanza na Kusini Pemba, hatua itakayofuata ni Kaskazini Pemba ili Mikoa yote iweze kupata vituo vya Polisi vyenye ngazi ya Mkoa kwa maana ya Daraja A. Kwa hiyo, uwe na subira katika miaka miwili ijayo kituo hicho pia kitakuwa kimejengwa.