Contributions by Hon. Ahmed Yahya Abdulwakil (6 total)
Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022
MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Natumia fursa hii kukushukuru wewe binafsi na kumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye amenijalia mara yangu ya kwanza kusimama katika Bunge lako hili tukufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapohapo nawashukuru sana wananchi wa Jimbo la Kwahani kule Zanzibar ambao kwa imani moja wamenileta hapa niwe mwakilishi wao. Walikuwa na simanzi kwa vile wanaona kama wameondokewa na Mbunge mwaminifu, mtiifu na mwenye bidii, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Nawahakikishia kwa nafsi yangu kwamba mimi naweza na nitawapa utumishi uliotukuka na kufuta machozi madogo madogo ambayo walikuwa wanayatoa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Miundombinu na Mawasiliano na kwa kiasi fulani nitajikita zaidi katika kuuchangia Mpango huu wa Miaka Mitano. Nchi yetu kama hii kwa kitendo cha Rais wetu mpendwa kuanzisha reli iendayo kasi kwa kutumia fedha zetu za ndani kwa kipindi hiki ni suala la kumpongeza na kumtakia mafanikio mema katika safari hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilibahatika kidogo kusafiri (mtundu wa kusafiri), ninakona reli kama hii ya Shirika la Reli la Marekani linaitwa Acela inayochukua abiria na mizigo kutoka Washington DC mpaka New York kwa mwendo wa saa nne na nilipanda shirika hilo. Leo nchi kama yetu ya Tanzania hili ni jambo la mfano, Rais wetu mpendwa ameidhinisha zaidi ya shilingi trilioni saba na kuendelea na reli inaendelea. Kwa hiyo, hili ni jambo la kuigwa na huyu ni Rais wa kuombewa dua kila siku kwa madhehebu yote ili aweze kuishi na aweze kutufikisha salama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile napenda kuchangia kuhusu Shirika la Ndege la ATC. Shirika la Ndege la ATC kila mmoja leo anaona mafanikio yake na limeweza kwa mara ya kwanza katika utawala wa Dkt. John Pombe Magufuli kutoa gawio (dividend) kwa Serikali. Kwa hiyo, hili ni jambo la mfano; amefufua shirika hili na leo lina ndege zaidi ya tisa na nyingine za mizigo ziko mbioni zinakuja. Kwa hiyo, hili ni jambo la mfano katika nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni ilivyoingia COVID tumeona deterioration ya bidhaa kuja kwetu Tanzania. Shirika la Ndege la Ethiopia limetumia nafasi ya kuchukua mizigo ya wafanyabiashara kuleta Tanzania. Ni jambo la faraja kusikia kwamba ndege ya mizigo inakuja na iko njiani. Kwa hiyo, uchumi wetu utazidi kuhuika kwa kuwa sasa hivi tunatumia ndege yetu wenyewe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini si hivyo tu, nadokeza kwamba hivi karibuni shirika hili baada ya hii COVID kuondoka, lina mpango wa kuazisha safari za kuelekea Gatwick pamoja na London, Heathrow. Kwa hiyo, Watanzania hapa watakuwa wanapanda direct flight kutoka Julius Kambarage Nyerere Airport mpaka Gatwick. Kwa hiyo, hili ni jambo la mfano kwa Shirika la Ndege na hizi zote ni juhudi za Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli; hongera sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho katika uchangiaji wangu, natoa ushauri kwamba uvuvi wa Bahari Kuu ambao unachochea uchumi wetu uangalie ofisi za Zanzibar. Hapa katikati utoaji wa leseni ulisababisha ofisi ya Zanzibar kidogo kutikisika. Wavuvi wenye meli walikuwa wengi lakini alibakia mvuvi mmoja tu ndiye aliyepewa leseni. Kwa hiyo, zipo dalili za kuwasaili ikiwa hali imetengemaa na wakati wa utoaji wa leseni za meli za uvuvi wakaangalie kwa makini sana kutoa leseni kwa wakati na fair ili kusudi ile shake ya ofisi isije ikatokea tena.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa jumla mimi naunga mkono mpango huu kwa asilimia 100 ili mambo yaende.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)
Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026
MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii ya kuchangia Mpango huu ambao ni dira kubwa, mimi naita ni jahazi litakalotuvusha kama kuna upepo au hakuna upepo kama alivyosema Rais wetu mpendwa, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Wabunge wengi walipokuwa wanachangia walizungumzia habari za markets yaani masoko, kwamba uzalishaji ni mkubwa lakini tuna upungufu wa masoko katika kuuza bidhaa zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri ndugu yangu Mheshimiwa Mwigulu pamoja na Naibu kwamba duniani au Serikali ya Marekani imetoa fursa kwa nchi za kiafrika ambao Mpango huu unaoitwa AGOA (African Growth and Opportunity Act)nadhani katika utawala wa Bush ameamua Afrika iweze kuuza bidhaa zaidi bila ushuru wa aina yoyote. Sasa ni vema zaidi tukajikita na masoko ya nje, nchi yetu ina utajiri wa bidhaa mbalimbali tunazalisha, kuna maparachichi, kuna aina ya bidhaa mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nikifuatilia kwa karibu sana, kila Mbunge anayesimama anasema kwamba soko hatuna bidhaa zinaharibika, kwa hiyo naishauri Serikali kwamba soko la AGOA nalo likapiga hodi Marekani. Hili ni soko zuri na halina ushuru maadamu tu ile bidhaa iliyozalishwa iwe brand yake made in Tanzania na iko katika hali ya ubora. Tusiwe waoga, wakati umefika tutumie fursa za ulimwengu, tutumie madirisha ya ulimwengu kusudi na sisi tuweze kuuza bidhaa zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hayo machache, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja, ipite. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira
MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, asubuhi ya leo baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye tupo katika mfungo, mimi naheshimu sana heshima hii ya kupewa kuwa mchangiaji wa mwanzo katika wizara hii ambayo ni ya uhai wa maisha yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kikawaida sina uchangiaji mkubwa sana maisha yote na nitatumia haitozidi dakika tatu, nne mpaka tano. Kwa hiyo nitasevu muda kusudu ajaye apate nafasi ya kuongea zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nitaongea upande wa Mazingira (Environment). Katika hotuba ya Mheshimiwa Rais, hapa alitumia dakika tatu, jinsi anavyojali na kuthamini mazingira. Kwa njia hii alipitia kiatu hiki kabla ya leo kufikia kuwa Rais wa Tanzania, kwa hiyo tumpongeze sana. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa ufadhili hapa kidogo ndiyo nataka Mheshimiwa Waziri atakapokuja ku-wind up hotuba yake, dunia imekuwa sana katika upande wa mazingira na mikutano mbalimbali inafanyika ulimwenguni kwa sababu ya kuhifadhi mazingira. Kwa hiyo, kwa upande wa Zanzibar kuna PECCA ukanda wa PECCA ni ukanda mali sana huu, ambao kwa namna moja au nyingine umeingia katika ramani ya dunia pamoja na kisiwa cha Misali. Misali kuna kisiwa, kuna bahari na kuna bustani chini ya ulimwengu ambayo si nchi nyingine ni natural. Sasa lazima yalindwe kimazingira kwa hiyo tulikuwa na wasiwasi kama nchi kwamba vipi hali ya ufadhili wa kimazingira katika hizo sehemu ambazo kubwa zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ukiangalia katika uchumi, Tanzania tunakusudia kununua meli nane (8) za uvuvi; meli nne (4) Tanzania Bara na nne(4) Tanzania Visiwani.
Katika uvuvi, kuna siri kubwa sana ya kupata harvest yaani mavuno kwa kutumia matumbawe. Haya kama hayakuhifadhiwa kimazingira, mara nyingi samaki wanahama na kutakuwa hakuna pia samaki wenyewe tunaokusudia, meli itakuja na hatutavua. Sasa napenda kujua wakati Mheshimiwa Waziri akija ku-wind up, atueleze hali ya kimazingira ya matumbawe, nchi zote baina ya Zanzibar na Tanzania Bara ikoje kusudi tuweze kufaidi neema hii. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nyuma kuna mfuko ukiitwa, Mfuko wa Kusaidia Nchi Masikini katika Kuokoa Mazingira (LDCF). Sasa wakubwa duniani wana hiari yao kutusaidia au kutosaidia hali ikoje katika kupambana na hali hii na ufadhili, ili kusudi tuweze kuishi katika ustahi mazingira mazuri kwa nchi yetu? Ahsante sana. (Makofi)
SPIKA: Ahsante sana Ahmed, lakini jina lako huwa linanipa tabu kidogo, unauhusiano gani na Mzee Abdulwakil?
MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Mheshimiwa Spika, jina langu kamilifu naitwa Ahmed Yahya Abdulwakil Mbunge wa Kohani. Tunao uhusiano wa kijomba wa huko nyumbani. (Makofi/Kicheko)
SPIKA: Ahsante sana Ahmed.
MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Sikutaka kuweka sawa ehe! Kusudi watu wakatishika, hamna! (Kicheko)
SPIKA: Kiti changu kimekuwa kikipata tabu kidogo. Nashukuru kwa ufafanuzi huo, Ndugu yangu Ahmed.
Muswada wa Sheria ya Uwekezaji Tanzania wa Mwaka 2022
MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii jioni ya leo na mimi nikiwa ni miongoni mwa wachangiaji wa sheria hii.
Kwanza niseme tu mimi ni miongoni mwa Wajumbe wa Kamati ambao tulijadili kwa kina huu Muswada wa Ulinzi wa Taarifa Binafsi. Mimi nasema hatujachelewa, tumekuja muda mzuri na muda muafaka kwa ajili ya kujadili na kupitisha sheria hii. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hakika sheria hii tulipata wadau wengi kwa mara ya kwanza, walifurika kwenye chumba chetu na kwa muda wote kulikuwa hakuna mizozo ya kisheria na kanuni na miongozo yao, walitukubalia na sisi tukawakubalia, lakini katika kujadili suala hili kuna neno lilijitokeza, kuongezwa neno faragha ili kutia nyama kwenye sheria hii na ndio maana wajumbe wengi ukiona waliosimama hapa kitu faragha imo, ingawa muswada ndani yake humo ndani kuna neno linaitwa faragha.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mimi nakubaliana na neno faragha na liangaliwe vizuri kwenye kamusi ya Kiswahili ya Oxford, lina maana yake. Kamusi ya Kiswahili ya Oxford neno faragha lina maana yake, sitaki kuendelea sana, lakini nasema kwamba sheria hii ikipitishwa itajenge utu wetu, heshima yetu na faragha yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ndogo, ahsante. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi wa Mwaka 2022
MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii jioni ya leo na mimi nikiwa ni miongoni mwa wachangiaji wa sheria hii.
Kwanza niseme tu mimi ni miongoni mwa Wajumbe wa Kamati ambao tulijadili kwa kina huu Muswada wa Ulinzi wa Taarifa Binafsi. Mimi nasema hatujachelewa, tumekuja muda mzuri na muda muafaka kwa ajili ya kujadili na kupitisha sheria hii. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hakika sheria hii tulipata wadau wengi kwa mara ya kwanza, walifurika kwenye chumba chetu na kwa muda wote kulikuwa hakuna mizozo ya kisheria na kanuni na miongozo yao, walitukubalia na sisi tukawakubalia, lakini katika kujadili suala hili kuna neno lilijitokeza, kuongezwa neno faragha ili kutia nyama kwenye sheria hii na ndio maana wajumbe wengi ukiona waliosimama hapa kitu faragha imo, ingawa muswada ndani yake humo ndani kuna neno linaitwa faragha.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mimi nakubaliana na neno faragha na liangaliwe vizuri kwenye kamusi ya Kiswahili ya Oxford, lina maana yake. Kamusi ya Kiswahili ya Oxford neno faragha lina maana yake, sitaki kuendelea sana, lakini nasema kwamba sheria hii ikipitishwa itajenge utu wetu, heshima yetu na faragha yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ndogo, ahsante. (Makofi)
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022
MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii asubuhi ili nami niweze kuchangia bajeti hii ya Serikali, ambayo mimi ninaiita bajeti mkombozi na ufunguzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu, kwanza inafurahisha mno, kwamba bajeti hii ina malengo mazuri ya kututoa hapa tulipo na kwenda katika hatua nyingine, hili ni jambo la kupongezwa. Vijana wetu, Mawaziri wote, Naibu Waziri pamoja na timu yote imefanya kazi kubwa sana kuandaa bajeti hii ambayo leo mmetuletea mbele yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukuza uchumi lazima kuwe na vichocheo vya uchumi ambavyo vitaufanya uchumi ule ustawi na uendelee. Dalili zinaonesha kwamba katika kipindi kifupi tu cha mama yetu Pato la Taifa limekuwa na mama yetu ameweza kujiamini kwa kutoa fedha nyingi katika miradi mikubwa ya uchumi, ambayo italeta ufufuaji wa uchumi mzuri zaidi katika siku za usoni, hongera sana, hongera sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi na-declare interest kama ni mfanyabiashara na muwekezaji, na kwa bahati niliwahi kuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi kwenye sekta ya biashara, viwanda na kilimo. Ni ukweli usio wazi, na niko tayari hata na Naibu Waziri kwenda kuangalia ripoti ya fedha ya urari wa biashara baina ya Bara na Zanzibar kuwa ni mbovu mno! mbovu mno! Na niko tayari wowote kwenda, kwamba asilimia 75 ya biashara iliyokuwa ikifanywa baina ya Bara, imepungua mpaka asilimia 15 na imeweza kuathiri bajeti ya SMZ kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo, hiyo iko wazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na ndugu yangu tunapendana sana, Mheshimiwa Naibu Waziri tunaweza tukaenda tukaangalia namna hali ilivyoathiri biashara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa nini basi, Tanzania Bara wana-influence kubwa ya kuuza bidhaa kwetu Zanzibar; kwa mfano mbao, nondo, maji, cement na biashara nyingine zozote; hiyo ni free na hiyo ni free trade markets. Nchi ndogo kama yetu, ya Zanzibar yenye population ya watu 1,500,000 tu, sisi ukitaka tusitake tunategemea soko la Tanzania Bara. Na ukiangalia kwa upevu niliokuwa nao kwamba, hata miaka 100 nyuma, Zanzibar ilikuwa inategemea biashara (trade).
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hii bajeti iliyokuja ya kuondoa ondoa vikwazo vidogo vidogo tumeifurahia na tunaipongeza. Lakini la msingi, Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri naomba na hapa kidogo unitolee macho. Umefika wakati kwa makusudi na kwa malengo mazuri, iundwe tume ya fedha ya pamoja, jambo ambalo mama nalo amelisisitiza hilo. Hii yote itaondoa minong’ono midogo midogo baina ya Zanzibar na Tanzania Bara, na unalijua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, basi mimi kwa jumla naunga mkono. Lakini la mwisho ni kwamba, katika ufanyaji wa biashara, nchi yoyote duniani haiogopi wafanyabiashara. Kwa mfano kampuni kubwa za Marekani kama vile Amazon, Boeing na nyingine zote, hizi zote zipo karibu na nchi au Serikali husika. Muhimu tu zile kodi zinalipwa na wale watu wathaminiwe, pasiwe na woga baina ya wafanyabiashara na Serikali, hawa ndio wenye engine ya uchumi wa nchi husika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hayo machache mimi naunga mkono hoja kwa asilimia 100. Mama amejizatiti na yuko kazini, na yote haya yatafanikiwa ikiwa tutakuwa tuna umoja na umoja wetu inshallah, Mwenyezi Mungu ataujaalia udumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)