Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Questions to the Prime Minister from Hon. Edward Olelekaita Kisau (2 total)

MHE. EDWARD K. OLELEKAITA Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Jimbo la Kiteto?
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edward Kisau Olelekaita, Mbunge wa Kiteto, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na mpango wa kujenga vyuo vya ufundi stadi ikiwa na lengo la kuwa na Chuo cha Ufundi Stadi katika kila mkoa na kila wilaya. Kwa mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, ilitenga jumla ya shilingi bilioni 48.6 kwa ajili ya kujenga vyuo 29 vya VETA katika ngazi za wilaya ambavyo kwa sasa viko katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutafuta vyanzo mbalimbali vya fedha ili kuendelea kutekeleza azma yake ya kuwa na chuo cha ufundi stadi katika kila mkoa na wilaya nchini ikiwemo Wilaya ya Kiteto. Aidha, endapo Halmashauri ya Kiteto inayo majengo ambayo yanakidhi vigezo vya kutumika kwa VETA, Wizara yangu itakuwa tayari kununua vifaa kwa ajili ya kuwezesha majengo hayo kuanza kutumika mara moja. Ahsante.
MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kwa kuwa viboko hivi vinaleta taharuki kubwa sana kwa nini msilete mwongozo tu aidha tukafuta kabisa ama walau kutoka nne iwe moja? Ahsante.
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Olelekaita, Mbunge wa Kiteto kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Olelekaita ametoa ushauri; na kwa kuwa hii ilikuwa ni kanuni zilizokuwa zimewekwa na zikatolewa na waraka kutoka Wizara ya Elimu na Utamaduni, basi kwa ushairi huo tunauzingatia tutaona kama inawezekana, wadau watahusishwa, wataangalia mwenendo wa nidhamu, matatizo ya nidhamu yaliyopo nchini na pia wakati tulionao, ambao ndio unaowezesha. Hata sisi Wabunge kubadilisha sheria moja na kuifanyia maboresho inatokana na wakati. Kwa hiyo nalo pia tutaliangalia kama wakati unaruhusu kuondoa viboko vinne mpaka kimoja au kuondoa kabisa basi wadau watatushauri, na Serikali tupo tayari kutekeleza pale ambako inaonekana wadau watakubaliana na hilo, ahsante sana.