Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Prof. Shukrani Elisha Manya (1 total)

MHE. PROF. SHUKRANI E. MANYA: Mheshimwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Janejelly Ntate, nipende kuuliza swali la nyongeza – na kwanza ninashukuru kwa majibu ya Serikali – kwamba sasa baada ya kukamilisha kituo hicho, ni lini sasa watumishi wataletwa ili kuimarisha hali ya usalama katika maeneo hayo?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru baada ya kituo hiki kukamilishwa nampa assurance Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya Mheshimiwa Janejelly kwamba Serikali kupitia Jeshi la Polisi Kanda Maalum Mkoa wa Dar es Salaam na Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, mara moja watapelekwa Askari kwa ajili ya kuanza kutoa huduma. Ikumbukwe kwamba sasa hivi tunao Askari mpaka ngazi ya Kata na eneo hili lipo kwenye utawala wa Kata na Inspectors wameshapangwa kule wameshapangwa kule kwa ajili ya kutoa huduma za ulinzi. Kituo kikikamilika tutapeleka askari wa kutosha ili kutekeleza majukumu ya usalama kwenye eneo hilo. (Makofi)