Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Prof. Shukrani Elisha Manya (2 total)

MHE. PROF. SHUKRANI E. MANYA: Mheshimwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Janejelly Ntate, nipende kuuliza swali la nyongeza – na kwanza ninashukuru kwa majibu ya Serikali – kwamba sasa baada ya kukamilisha kituo hicho, ni lini sasa watumishi wataletwa ili kuimarisha hali ya usalama katika maeneo hayo?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru baada ya kituo hiki kukamilishwa nampa assurance Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya Mheshimiwa Janejelly kwamba Serikali kupitia Jeshi la Polisi Kanda Maalum Mkoa wa Dar es Salaam na Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, mara moja watapelekwa Askari kwa ajili ya kuanza kutoa huduma. Ikumbukwe kwamba sasa hivi tunao Askari mpaka ngazi ya Kata na eneo hili lipo kwenye utawala wa Kata na Inspectors wameshapangwa kule wameshapangwa kule kwa ajili ya kutoa huduma za ulinzi. Kituo kikikamilika tutapeleka askari wa kutosha ili kutekeleza majukumu ya usalama kwenye eneo hilo. (Makofi)
MHE. PROF. SHUKRANI E. MANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kukamilika na kuanza kutumika kwa jengo hilo kunaifanya Hospitali ya Kanda ya Mbeya kuongeza uwezo na ufanisi hata hivyo kuongeza pia viatanda kutoka 600 hadi 800.

Je, ni lini Serikali itakapoifanya Hospitali ya Kanda ya Mbeya kupata hadhi ya taasisi kama ilivyo MOI, JKCI na nyinginezo?
NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba mchakato huo unaendelea wa kuifanya hospitali hiyo kuwa taasisi na bado tunaendelea mjadala, Wizara ya Afya, Wizara ya Fedha na Utumishi kuona namna gani tunaweza kufikia hatua hiyo, ili nayo Mbeya iweze kuwa taasisi kama ambavyo hospitali nyingine za Kanda zinakuwa. (Makofi)